Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Anamupatia Nguvu Mutu Aliyechoka’

‘Anamupatia Nguvu Mutu Aliyechoka’

Andiko letu la mwaka wa 2018: Wale wanaomutumaini Yehova watapata nguvu mupya.’​ISA. 40:31.

NYIMBO: 3, 47

1. Tunapambana na magumu gani, lakini sababu gani Yehova anapendezwa na watumishi wake waaminifu? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

KAMA vile unajua maisha katika ulimwengu huu muovu yanajaa magumu. Wengi kati yenu ndugu na dada wapendwa munapambana na magonjwa hatari. Na wengine, hata kama wamekwisha kukomaa sana, wanahangaikia watu wa jamaa zao wenye kuzeeka. Tena, wengine wanajikaza sana ili kutimizia watu wa familia yao mahitaji ya lazima. Na tunajua kama wengi hawapambane na tatizo moja tu, lakini wanapambana na matatizo mengi kama hayo kwa wakati mumoja! Hilo linaomba kutumia wakati mwingi, kutumikisha sana akili, na hata feza nyingi. Hata hivyo, munaendelea kuwa hakika kabisa katika ahadi za Mungu; imani yenu juu ya wakati muzuri zaidi wenye kuja iko nguvu kabisa. Yehova anapendezwa sana na jambo hilo!

2. Andiko la Isaya 40:29 linatutia moyo namna gani, lakini ni kosa gani kubwa lenye tunaweza kufanya?

2 Lakini, wakati fulani unajisikia kuwa hauwezi tena kuvumilia? Ikiwa ni hivyo, haiko wewe peke yako. Biblia inasema kama mara nyingi watumishi wa zamani wa Mungu walijisikia kama hawawezi tena kuvumilia hali fulani. (1 Fal. 19:4; Ayu. 7:7) Hata hivyo, kuliko kuvunjika moyo, walitegemea Yehova ili awapatie nguvu. Biblia inasema kama Yehova ‘anamupatia nguvu mutu aliyechoka.’ (Isa. 40:29) Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, watumishi fulani wa Mungu katika siku zetu wamefikia kuona kuwa njia ya muzuri zaidi ya kupambana na magumu ya maisha ni ‘kuacha kwanza kweli,’ ni kama vile wanaona kuwa kumutumikia Yehova ni muzigo muzito kuliko kuwa baraka. Kwa hiyo, wanaacha kusoma neno la Mungu, kuenda kwenye mikutano ya kutaniko na kuenda katika kazi ya kuhubiri; kama vile Shetani anapenda wafanye.

3. (a) Namna gani tunaweza kuzuia mupango wa Shetani wa kutufanya tupunguze bidii yetu? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

3 Shetani anajua muzuri kama ikiwa tunafanya mengi katika kazi ya Yehova, hilo linaweza kututia nguvu, na hapendi tukuwe na nguvu. Wakati unajisikia kuwa mwenye kuchoka kimwili na kiakili, usiache kumutumikia Yehova. Umukaribie zaidi kwa sababu ‘atakufanya kuwa imara, atakufanya kuwa mwenye nguvu.’ (1 Pet. 5:10; Yak. 4:8) Katika habari hii, tutazungumuzia hali mbili zenye zinaweza kutufanya tupunguze bidii yetu katika utumishi wetu kwa Mungu na tutazungumuzia pia namna gani kutumikisha kanuni za Biblia kunaweza kutusaidia kupambana na hali hizo. Lakini, kwanza, tuzungumuzie uwezo wa Yehova wa kutupatia nguvu kama vile andiko la Isaya 40:26-31 linaonyesha.

WALE WENYE KUTUMAINIA YEHOVA WATAPATA NGUVU MUPYA

4. Andiko la Isaya 40:26 linaweza kutufundisha nini?

4 Soma Isaya 40:26. Hakuna mutu mwenye ameweza kuhesabia nyota zote zenye kuwa katika ulimwengu. Wanasayansi wanaamini kuwa galaksi yetu yenyewe inaweza kuwa na nyota miliare 400. Lakini, Yehova anazipatia zote majina ao utambulisho. Hilo linatufundisha nini? Ikiwa Yehova anahangaikia viumbe vyake vyenye havina uzima, wazia namna gani anakuona wewe mwenye kumutumikia kwa sababu unamupenda, lakini haiko kwa sababu umepangwa kufanya hivyo! (Zab. 19:1, 3, 14) Baba yetu mupendwa anakujua muzuri sana. Biblia inasema hivi: “Nywele zenyewe za kichwa chenu zimehesabiwa zote” naye. (Mt. 10:30) Na muandikaji mumoja wa zaburi anatuhakikishia jambo hili: “Yehova anazijua siku za watu wasio na kosa.” (Zab. 37:18) Ndiyo, anajua magumu yenye unapambana nayo, na anaweza kukupatia nguvu ya kuvumilia magumu hayo yote.

5. Sababu gani tunapaswa kuwa hakika kama Yehova iko na uwezo wa kutupatia nguvu?

5 Soma Isaya 40:28. Yehova ndiye Chanzo cha nguvu yote. Kwa mufano, fikiria nguvu yenye anapatia jua letu lenyewe. Muandikaji wa sayansi David Bodanis alisema kama nguvu yenye jua letu linatoa katika anga kila segonde, iko sawa na nguvu ya mamiliare ya bombe za atomu. Mutu mwingine mwenye kutafuta habari alifanya hesabu kuwa nguvu yenye jua linatoa katika segonde moja inatosha kabisa ili kutolea wanadamu wote umeme kwa miaka 200 000! Tunaweza kuwa hakika kama Yehova mwenye anapatia jua “nguvu” anaweza kutupatia nguvu zenye tuko nazo lazima ili kupambana na magumu yoyote yenye tunapata.

6. Ni katika njia gani nira ya Yesu ni laini, na kujua hilo kunapaswa kuwa na matokeo gani juu yetu?

6 Soma Isaya 40:29. Kumutumikia Yehova kunaleta furaha nyingi. Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: ‘Muchukue nira [kipande cha muti cha kutumia ili kubeba muzigo] yangu.’ Na aliongezea hivi: ‘Nanyi mutapata burudisho [ao, kitulizo] kwa ajili ya nafsi zenu. Kwa maana nira yangu ni laini na muzigo wangu ni mwepesi.’ (Mt. 11:28-30) Maneno hayo ni ya kweli kabisa! Wakati fulani, tunaweza kujisikia kuwa tumechoka sana wakati tunatoka nyumbani ili kuenda kwenye mikutano ao katika kazi ya kuhubiri. Lakini tunajisikia namna gani wakati tunarudia? Tunajisikia kuwa wenye nguvu na wenye kuwa tayari kabisa kupambana na magumu ya maisha. Kwa kweli, nira ya Yesu ni laini!

7. Toa mufano wenye kuonyesha kama maneno ya Mathayo 11:28-30 ni ya kweli.

7 Dada mumoja mwenye tunaweza kuita Kayla amepambana na ugonjwa wa kuchoka kila wakati, kushuka moyo, na kichwa kuuma sana. Ndiyo sababu, wakati fulani ameona kuwa vigumu kuhuzuria mikutano ya kutaniko. Lakini, kisha kujikaza sana ili kuhuzuria mukutano mumoja wa watu wote, aliandika hivi: “Hotuba ilizungumuzia kuvunjika moyo. Habari ilitolewa katika njia yenye kutia moyo na yenye kuonyesha huruma mupaka nikatokwa machozi. Nilikumbushwa kama ninapaswa kuwa kwenye mikutano.” Alifurahi sana kwa sababu alijikaza kuhuzuria!

8, 9. Mutume Paulo alipenda kusema nini wakati aliandika: ‘Ninapokuwa zaifu, ndipo ninapokuwa mwenye nguvu’?

8 Soma Isaya 40:30. Hata kama tunaweza kuwa na uwezo gani, kuko mambo yenye hatuwezi kufanya kwa nguvu yetu wenyewe. Sisi wote tunapaswa kujua jambo hilo. Hata kama alikuwa mwanaume mwenye nguvu, mutume Paulo hakukuwa na uwezo wa kufanya mambo yote yenye alipenda kufanya. Wakati alimuambia Mungu mambo yenye yalikuwa yanamuhangaisha, Mungu alimuambia hivi: ‘Nguvu zangu zinakamilishwa katika uzaifu.’ Paulo alielewa jambo hilo. Kwa hiyo alisema hivi: ‘Ninapokuwa zaifu, ndipo ninapokuwa mwenye nguvu.’ (2 Kor. 12:7-10) Paulo alipenda kusema nini?

9 Paulo alijua kama hangeweza kufanya mambo mengi bila musaada kutoka kwa ule mwenye kuwa na nguvu zaidi. Roho takatifu ya Mungu ingemupatia Paulo nguvu zenye alikuwa nazo lazima. Zaidi ya hilo, roho ya Mungu ingemupatia Paulo nguvu za kufanya kazi zenye hangeweza kufanya hata kidogo kwa nguvu zake mwenyewe. Ni hivyo pia kwetu. Ikiwa Yehova anatupatia roho yake takatifu, kwa kweli tutakuwa na nguvu!

10. Namna gani Yehova alimusaidia Daudi kupambana na magumu yake?

10 Daudi, muandikaji mumoja wa zaburi, alijionea mara nyingi namna nguvu ya roho takatifu ya Mungu inatenda. Aliimba hivi: ‘Kwa musaada wako ninaweza kukimbiza kikundi cha waporaji; na kwa musaada wa Mungu wangu ninaweza kuupanda ukuta.’ (Zab. 18:29) Kuko kuta fulani, ni kusema, magumu fulani yenye hatuwezi “kupanda” ao kupambana nayo kwa nguvu zetu wenyewe; tuko na lazima ya nguvu kutoka kwa Yehova.

11. Namna gani roho takatifu inatusaidia kupambana na magumu yetu?

11 Soma Isaya 40:31. Ndege mumoja mwenye kuitwa tai hatumie nguvu zake mwenyewe ili kuruka juu sana na kuenda mbali sana. Hewa yenye joto inasaidia tai kupanda juu, na hilo linamufanya asitumie nguvu nyingi. Kwa hiyo, wakati unapambana na tatizo kubwa, ukumbuke tai. Umuombe Yehova “akupandishe” kupitia ‘musaidizi, roho takatifu.’ (Yoh. 14:26) Jambo la kufurahisha ni kwamba, tunaweza kupata roho takatifu wakati wowote tuko na lazima ya roho hiyo. Pia, tunaweza kuwa na lazima kabisa ya musaada wa Mungu wakati tuko na tatizo la kukosa kuelewana na ndugu ao dada fulani katika kutaniko. Lakini, sababu gani matatizo hayo yanatokea?

12, 13. (a) Sababu gani kukosa kuelewana kunatokea kati ya Wakristo? (b) Habari ya Yosefu inatufundisha nini juu ya Yehova?

12 Kukosa kuelewana kunatokea kwa sababu sisi wote hatukamilike. Kwa hiyo, wakati fulani maneno ao matendo ya Wakristo wenzetu yanaweza kutukasirisha ao wao pia wanaweza kukwazika kwa sababu ya maneno ao matendo yetu. Hilo linaweza kuwa jaribu kali. Kama vile anafanya wakati tunapata majaribu mengine, Yehova anatuacha tuonyeshe ushikamanifu wetu kwa kujifunza kutumika katika umoja pamoja na wanaume na wanawake wenye wamejitoa kwake wenye anapenda hata kama wako na uzaifu fulani.

Yehova hakumuacha Yosefu; hatakuacha wewe pia (Picha hii inapatana na fungu la 13)

13 Yehova hazuie watumishi wake kupata majaribu kama vile habari juu ya Yosefu inaonyesha. Wakati Yosefu alikuwa kijana, ndugu zake walimusikilia wivu na wakamuuzisha ili akuwe mutumwa na akapelekwa Misri. (Mwa. 37:28) Yehova aliona mambo yenye yalikuwa yanatendeka na kwa kweli, alihuzunika kuona namna rafiki yake, Yosefu, mutu mwenye haki, alikuwa anatendewa mubaya. Lakini, hakumusaidia palepale. Kisha, wakati Yosefu alishitakiwa kuwa alijaribu kulala kinguvu bibi ya Potifa na kufungwa katika gereza, tena Yehova hakutenda palepale. Lakini, Mungu alikuwa amemuacha Yosefu? Hapana. Tofauti na hilo: “Yale aliyokuwa akifanya [Yosefu] Yehova aliyafanikisha.”​—Mwa. 39:21-23.

14. ‘Kuacha’ hasira kunaweza kutuletea faida gani za kiroho na za kimwili?

14 Kuko mufano mwingine. Ni hesabu kidogo ya watu ndio wametendewa mubaya kama vile Daudi alitendewa. Lakini, rafiki huyo wa Mungu hakuruhusu kinyongo kiendelee kumusumbua. Hata hivyo, aliandika hivi: ‘Acha hasira na uache gazabu; usijionyeshe umewaka hasira ili tu kufanya uovu.’ (Zab. 37:8) Jambo la maana zaidi lenye kutuchochea ‘kuacha’ hasira ni kwamba tunapenda kumuiga Yehova, mwenye ‘hakututendea kulingana na zambi zetu.’ (Zab. 103:10) Lakini, tunaweza kupata faida zingine wakati ‘tunaacha’ hasira. Hasira inaweza kuleta matatizo ya afya kama vile kupanda kwa nguvu yenye kusukuma damu katika mwili na matatizo ya kupumua. Inaweza kuleta matatizo ya kusaga chakula, matatizo ya maini, na matatizo ya kongosho (mufuko mudogo wenye kuwa na maji-maji yenye kusaidia kusaga chakula). Wakati tuko na hasira, mara nyingi hatufikiri tena muzuri. Na wakati fulani hasira kali inaweza kufanya mutu ashuke moyo kwa muda murefu. Kwa upande mwingine, Biblia inasema hivi: ‘Moyo mutulivu ni uzima wa mwili.’ (Met. 14:30) Kwa hiyo, namna gani tunaweza kupambana na hasira na kufanya amani pamoja na ndugu ao dada yetu? Tunaweza kufanya hivyo kwa kutumia mashauri yenye hekima yenye kupatikana katika Biblia.

WAKATI WAKRISTO WENZETU WANATUVUNJA MOYO

15, 16. Namna gani tunaweza kuzungumuza na mutu mwenye ametukwaza?

15 Soma Waefeso 4:26. Hatushangae wakati watu wa ulimwengu wanatutendea mubaya. Lakini, wakati Mukristo mwenzetu ao mutu wa familia yetu anasema ao kufanya jambo fulani lenye kutuumiza sana, tunaweza kuvunjika moyo sana. Tutafanya nini ikiwa hatuwezi kusahau tu jambo hilo? Tutaacha kinyongo kiendelee kwa miaka mingi katika moyo wetu? Ao tutafuata shauri la Biblia lenye hekima la kumaliza matatizo haraka? Kama tunaacha muda murefu upite bila kumaliza matatizo, itakuwa vigumu sana kwetu kufanya amani na ndugu ao dada yetu.

16 Tuseme nini ikiwa ndugu ao dada fulani amekukwaza na hauwezi kuachilia jambo hilo. Ni hatua gani zenye kufaa zenye unaweza kukamata ili kufanya amani? Kwanza, usali kwa Yehova kwa moyo wako wote. Umuombe akusaidie ufanye mazungumuzo yenye kujenga pamoja na ndugu ao dada yako. Ukumbuke kama yeye pia ni rafiki ya Yehova. (Zab. 25:14) Mungu anamupenda. Yehova anatendea marafiki wake kwa upole, na anapenda sisi pia tufanye hivyo. (Met. 15:23; Mt. 7:12; Kol. 4:6) Kisha, urudilie katika akili yako mambo yenye utasema. Usifikiri kuwa ndugu ao dada yako alipenda tu kukuumiza; ujikaze kuelewa sababu gani alifanya hivyo. Na ukuwe tayari kukubali kama pengine wewe pia ulifanya jambo fulani lenye lilitokeza tatizo hilo. Unaweza kuanza mazungumuzo kwa kusema maneno kama haya: “Pengine niko mwenye kuchokozeka haraka, lakini wakati ulizungumuza na miye jana, nilijisikia . . .” Ikiwa mazungumuzo hayo hayalete matokeo ya muzuri kama vile ulipenda, utafute wakati mwingine wa kufanya amani. Na wakati huohuo usali kwa ajili ya ndugu yako; umuombe Yehova amubariki. Umuombe Mungu akusaidie ukaze akili yako juu ya sifa za muzuri za ndugu ao dada yako. Hata upate matokeo gani, unaweza kuwa hakika kama Yehova atafurahia bidii yenye unafanya kwa moyo wako wote ili kufanya amani pamoja na ndugu ao dada yako, rafiki ya Mungu.

WAKATI TUNAJILAUMU KWA SABABU YA ZAMBI ZETU ZA ZAMANI

17. Ni njia gani zenye Yehova anaweza kutumia ili kutusaidia wakati tumefanya zambi, na sababu gani tunapaswa kutumia mupango huo?

17 Watu fulani wanajiona kuwa hawastahili kumutumikia Yehova kwa sababu wamefanya zambi nzito. Kujilaumu kunaweza kutufanya tupoteze amani, furaha, na nguvu yetu. Mufalme Daudi, mwenye alisumbuliwa sana na tatizo la kujilaumu, alisema hivi: ‘Nilipokaa kimya mifupa yangu ilichakaa [kuwa zaifu] kwa sababu ya kuugua kwangu muchana kutwa. Kwa maana mukono wako ulikuwa muzito juu yangu muchana na usiku.’ Jambo la kufurahisha ni kwamba, Daudi alishugulikia tatizo hilo kama mwanaume, ni kusema, mwanaume mwenye kukomaa kiroho. Aliandika hivi: ‘Mwishowe niliungama zambi yangu kwako, nawe mwenyewe ukanisamehe kosa la zambi zangu.’ (Zab. 32:3-5) Ikiwa umefanya zambi nzito, Yehova iko tayari kukusaidia ukuwe tena na urafiki wa muzuri pamoja naye. Lakini unapaswa kukubali musaada wenye anatoa kupita kutaniko. (Met. 24:16; Yak. 5:13-15) Usikawie, uzima wako wa milele unategemea jambo hilo! Lakini tuseme nini ikiwa zamiri yako ingali inakusumbua kwa sababu ya makosa yenye ulifanya zamani hata kama yalisamehewa kumepita muda murefu?

18. Namna gani mufano wa Paulo unaweza kusaidia wale wenye kujisikia kuwa hawastahili?

18 Kwa kweli wakati fulani mutume Paulo alijilaumu juu ya makosa yake ya zamani. Alisema waziwazi hivi: ‘Mimi ni mudogo zaidi kati ya mitume, nami sifae kuitwa mutume, kwa sababu nililitesa kutaniko la Mungu.’ Hata hivyo, Paulo aliongeza hivi: ‘Lakini kwa fazili zisizostahiliwa za Mungu mimi niko kama nilivyo.’ (1 Kor. 15:9, 10) Yehova alimukubali Paulo hata kama alifanya makosa zamani, na alipenda Paulo aelewe jambo hilo juu yake mwenyewe. Ikiwa umetubu kwelikweli zambi zako za zamani na umefanya hivyo kwa kadiri inaombwa kabisa, unaweza kuwa hakika kuwa Yehova atakuonyesha rehema. Kwa hiyo, ukuwe hakika kuwa Yehova amekusamehe, na ukubali musamaha wake!​—Isa. 55:6, 7.

19. Andiko letu la mwaka wa 2018 ni gani, na sababu gani linafaa?

19 Kadiri mwisho wa ulimwengu huu muovu unakaribia, tunatazamia kwamba magumu ya maisha yataongezeka. Lakini, ukuwe hakika kama, Yehova mwenye ‘kupatia nguvu mutu aliyechoka’ na ‘kujaza nguvu kamili kwa mutu asiye na nguvu’ anaweza kukupatia mambo yoyote yenye uko nayo lazima ili kuvumilia. (Isa. 40:29; Zab. 55:22; 68:19) Katika mwaka wa 2018, tutakumbuka kweli hiyo ya maana kila wakati tunahuzuria mikutano katika Jumba la Ufalme na kuona maneno haya ya andiko letu la mwaka: ‘Wale wanaomutumaini Yehova watapata nguvu mupya.’​Isa. 40:31.