Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sababu Gani Umutolee Ule Mwenye Kuwa na Kila Kitu?

Sababu Gani Umutolee Ule Mwenye Kuwa na Kila Kitu?

Ee Mungu wetu, tunakushukuru na kulisifu jina lako nzuri.’​1 NYA. 29:13.

NYIMBO: 80, 50

1, 2. Namna gani Yehova anatumia kwa ukarimu mali yake ya kimwili?

YEHOVA ni Mungu mwenye kuonyesha ukarimu. Kila kitu chenye tuko nacho kinatoka kwake. Zahabu yote na feza na mali yote ya asili ya dunia ni vya Yehova, na anavitumia ili kutoa mambo yenye kuhitajiwa ili kutegemeza uzima. (Zab. 104:13-15; Hag. 2:8) Biblia iko na habari nyingi zenye kuzungumuzia namna Yehova alitumia mali yake kwa muujiza ili kutegemeza watu wake.

2 Kwa miaka 40, Yehova alitolea taifa la Israeli mana na maji wakati walikuwa katika jangwa. (Kut. 16:35) Kwa hiyo, “hawakukosa chochote.” (Neh. 9:20, 21) Kupitia nabii Elisha, Yehova alifanya muujiza kwa kuzidisha mafuta kidogo ya mujane mumoja muaminifu. Zawadi hiyo yenye kutoka kwa Mungu ilimusaidia kulipa madeni yake na alibakia na feza za kumusaidia yeye na watoto wake wanaume waendelee kuishi. (2 Fal. 4:1-7) Kwa musaada wa Yehova, Yesu alitoa kwa muujiza chakula na hata feza wakati ilikuwa lazima kufanya hivyo.​—Mt. 15:35-38; 17:27.

3. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

3 Yehova anaweza kutumia mambo yote yenye anapenda ili kutegemeza viumbe vyenye kuwa duniani. Hata hivyo, anaomba watumishi wake watumie vitu vyao vya kimwili ili kutegemeza kazi ya tengenezo lake. (Kut. 36:3-7; soma Methali 3:9.) Sababu gani Yehova anapenda tutumie vitu vyetu vya maana ili kumutolea? Namna gani watumishi waaminifu wa zamani walitumia feza zao ili kutegemeza kazi za wale wenye Yehova alitumia ili kuongoza? Namna gani tengenezo linatumia michango ya feza zenye kutolewa leo? Tutapata majibu ya maulizo hayo katika habari hii.

SABABU GANI TUNAMUTOLEA YEHOVA?

4. Wakati tunategemeza kazi ya Yehova tunamuonyesha nini?

4 Tunamutolea Yehova kwa sababu tunamupenda na tunapenda kumuonyesha shukrani. Tunaguswa moyo sana wakati tunafikiria mambo yote yenye Yehova ametufanyia. Wakati alizungumuzia mambo yenye walikuwa nayo lazima ili kujenga hekalu, Mufalme Daudi alisema waziwazi kuwa kila kitu chenye tuko nacho kinatoka kwa Yehova na kama kila kitu chenye tunamupatia kinatoka katika vitu vyenye amekwisha kutupatia.​—Soma 1 Mambo ya Nyakati 29:11-14.

5. Namna gani Maandiko yanaonyesha kama kutoa bila uchoyo ni sehemu ya maana ya ibada ya kweli?

5 Kutoa pia ni sehemu ya ibada yetu kwa Yehova. Katika maono fulani, mutume Yohana alisikia watumishi wa Yehova huko mbinguni wanasema hivi: “Unastahili, Ee Yehova, naam, Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako navyo vikaumbwa.” (Ufu. 4:11) Kwa kweli, unakubali kama Yehova anastahili utukufu wote na nguvu zote na heshima yote yenye tunaweza kumutolea wakati tunamupatia mambo ya muzuri zaidi yenye tuko nayo. Kupitia Musa, Yehova aliamuru Waisraeli wakusanyike mbele za Yehova mara tatu katika mwaka ili kufanya sikukuu. Kwa sababu kutoa ilikuwa sehemu ya ibada yao kwenye sikukuu hizo, Waisraeli hawakupaswa ‘kuonekana mbele za Yehova mikono mitupu.’ (Kum. 16:16) Vilevile leo, kutoa bila uchoyo ili kuonyesha shukrani na kutegemeza sehemu ya duniani ya tengenezo la Yehova, ni sehemu ya maana ya ibada yetu.

6. Sababu gani ni muzuri kutolea wengine? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

6 Kutoa kunatuleta faida. Ni muzuri tukuwe wenye kutolea wengine kwa ukarimu kuliko kuwa tu wenye kupokea. (Soma Methali 29:21.) Kwa mufano, mutoto anaweza kupatia wazazi wake zawadi fulani kwa kutumia feza kidogo zenye wamemupatia. Wazazi wanaweza kufurahia sana zawadi hiyo! Ao, mutoto mwenye kufanya kazi ya upainia na mwenye kuishi nyumbani anaweza kuwapatia wazazi feza fulani ili kuwasaidia kutimiza mahitaji yao. Hata kama wazazi hawamuombe kufanya hivyo, wanaweza kukubali zawadi hizo kwa sababu mutoto anatumia njia hiyo ili kuonyesha shukrani yake kwa ajili ya mambo yote yenye wanamufanyia. Vilevile, Yehova anajua kama wakati tunamutolea vitu vyetu vya lazima hilo linatuletea faida.

NAMNA WATUMISHI WA YEHOVA WALITOA ZAMANI

7, 8. Namna gani watumishi wa zamani wa Yehova walituachia mufano wa kutoa michango (a) kwa ajili ya kazi fulani za pekee? (b) kwa ajili ya kutegemeza kazi?

7 Maandiko yanazungumuzia namna watu wa Yehova walitoa michango ili kutegemeza kazi yake. Wakati fulani, watu wa Yehova walitoa michango kwa ajili ya kazi fulani za pekee. Kwa mufano, Musa aliomba michango kwa ajili ya kujenga tabenakulo; na Mufalme Daudi pia aliomba michango kwa ajili ya kujenga hekalu. (Kut. 35:5; 1 Nya. 29:5-9) Wakati wa Mufalme Yehoashi, makuhani walitumia michango ya feza zenye zilitolewa ili kutengeneza upya nyumba ya Yehova. (2 Fal. 12:4, 5) Wakati wa mitume ndugu na dada waliambiwa kama kulikuwa uhitaji kwa sababu ya njaa yenye ilitokea Yudea. Kwa hiyo, “wakaamua, kila mumoja kwa kadiri ambayo yeyote angeweza kutoa, wafanye huduma ya kupeleka misaada kwa akina ndugu waliokuwa wakikaa Yudea.”​—Mdo. 11:27-30.

8 Wakati mwingine, watu wa Yehova walitoa michango ili kutegemeza wale wenye walikuwa wanaongoza kazi. Wakati wa Sheria ya Musa, Walawi hawakupewa uriti kama makabila mengine. Lakini, Waisraeli waliwapatia sehemu ya kumi, na hilo lilisaidia Walawi wakaze akili zao juu ya kazi yao ya kutumika kwenye tabenakulo. (Hes. 18:21) Vilevile, Yesu na mitume wake walifaidika na ukarimu wa wanawake wenye ‘walikuwa wakiwahudumia [ao, kuwasaidia] kwa mali zao.’​—Lu. 8:1-3.

9. Namna gani watu wa zamani walipata michango yenye walitoa?

9 Kwa kweli, michango hiyo ilipatikana kwa njia mbalimbali. Wakati Waisraeli walifanya michango kwa ajili ya kujenga tabenakulo katika jangwa, inawezakana kuwa vitu vyenye walitosha katika inchi ya Misri vilikuwa kati ya michango hiyo. (Kut. 3:21, 22; 35:22-24) Wakati wa mitume, Wakristo fulani waliuzisha vitu vyao, kama vile mashamba ao nyumba zao, na kuleta feza hizo kwa mitume. Mitume waligawia feza hizo wale wenye walikuwa na lazima ya musaada. (Mdo. 4:34, 35) Wengine waliweka pembeni feza na kutoa michango kwa ukawaida ili kutegemeza kazi. (1 Kor. 16:2) Kwa hiyo, watu wa hali zote, ni kusema, wale wenye walikuwa matajiri sana ao wenye walikuwa maskini sana, wote walitoa michango.​—Lu. 21:1-4.

NAMNA TUNATOA MICHANGO LEO

10, 11. (a) Namna gani tunaweza kuiga ukarimu wa watumishi wa Yehova wa wakati wa zamani? (b) Unajisikia namna gani juu ya pendeleo lenye uko nalo la kutegemeza kazi ya Ufalme?

10 Leo, sisi pia tunaweza kuombwa michango kwa ajili ya kazi fulani ya pekee. Kwa mufano, pengine kuko mupango wa kujenga Jumba la mupya la Ufalme lenye kutaniko lako litatumia. Ao pengine Jumba la Ufalme lenu la sasa linatengenezwa upya. Tunaweza kujulishwa kama kuko mahitaji ya feza kwa ajili ya kutengeneza upya biro ya tawi ya eneo letu, kwa ajili mukusanyiko wenye tunahuzuria, ao ili kusaidia ndugu na dada zetu kisha musiba wa asili kutokea. Tunatoa michango ili kutegemeza pia wale wenye kufanya kazi kwenye makao yetu makubwa na kwenye biro zetu za tawi katika dunia yote. Tena, michango yetu inategemeza wamisionere, mapainia wa pekee, na wale wenye kufanya kazi ya muzunguko. Kwa kweli, kutaniko lenu limefanya pia azimio la kutoa feza fulani ili kutegemeza programu ya ujenzi wa Majumba ya Mikusanyiko na Majumba ya Ufalme katika dunia yote, kwa ajili ya ndugu na dada.

11 Sisi wote tunaweza kutoa michango ili kutegemeza kazi yenye Yehova anatimiza katika siku hizi za mwisho. Michango mingi inatolewa na watu wenye hawataje majina yao. Tunatia kwa siri michango yetu katika visanduku vya michango kwenye Jumba la Ufalme, ao tunaweza kutoa michango yetu kupitia Internete kwenye jw.org. Tunaweza kuona kuwa michango yetu kidogo haina faida hata kidogo. Lakini, michango mingi yenye kutolewa leo inatolewa kupitia zawadi nyingi ndogo-ndogo kuliko zawadi kidogo kubwa-kubwa. Ndugu na dada zetu, hata wale wenye kuwa maskini, wako kama vile Wakristo wa Makedonia wenye walikuwa na ‘umaskini mukubwa’ lakini waliomba ili wapewe pendeleo la kutoa na walifanya hivyo kwa ukarimu.​—2 Kor. 8:1-4.

12. Namna gani tengenezo linajikaza sana kutumia muzuri michango yenye kutolewa?

12 Ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza wanasali ili watumie feza za tengenezo kwa uaminifu na busara. (Mt. 24:45) Michango yenye kutolewa inapangiwa muzuri na kutumiwa kulingana na mahitaji. (Lu. 14:28) Zamani, watu wenye walikuwa wanasimamia michango yenye ilitolewa walihakikisha kuwa michango hiyo inatumiwa tu kwa ajili ya ibada ya Yehova. Kwa mufano, Ezra alifanya safari ya kurudia Yerusalemu na michango ya vitu vyenye Mufalme wa Perse alimupatia, kama vile, zahabu, feza, na vitu vingine vya bei sana vyenye kulingana leo na dola za Amerika zaidi ya milioni 100. Ezra aliona michango hiyo ya kujipendea kuwa yenye kutolewa kwa Yehova na alitoa maagizo mbalimbali ili michango hiyo ichungwe muzuri wakati walifanya safari ya kupita katika eneo lenye kuwa hatari. (Ezra 8:24-34) Mutume Paulo alikusanya michango yenye ilitolewa ili kusaidia ndugu na dada katika Yudea. Alikamata hatua ili kuhakikisha kama wale wenye walipeleka michango hiyo walifanya mambo yote kwa “unyoofu [ao, uaminifu], si machoni pa Yehova tu, bali pia machoni pa wanadamu.” (Soma 2 Wakorintho 8:18-21.) Kwa kuiga mufano wa Ezra na Paulo, tengenezo letu linafuata maagizo yenye kuwa wazi juu ya namna ya kutumia michango kwa uangalifu.

13. Sababu gani tengenezo lilifanya mabadiliko fulani hivi karibuni?

13 Watu wa familia wanaweza kufanya mabadiliko wakati wanapenda kuwa na usawaziko juu ya namna ya kutumia feza zenye wanapata. Ao wakati wanafikiria namna ya kufanya maisha yao yakuwe mepesi na kuepuka kutumia feza nyingi ili wafanye mengi katika kazi ya Yehova. Tengenezo la Yehova linafanya hivyo pia. Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa mipango mingi ya mupya yenye kufurahisha. Wakati fulani, hilo limefanya tutumie feza nyingi kuliko zile zenye tunapata kwa kipindi fulani. Kwa hiyo, tengenezo linatafuta njia za kupunguza garama na kufanya kazi ikuwe mwepesi ili liweze kufanya mengi zaidi kwa kutumia michango yenye munatoa kwa ukarimu.

FAIDA ZENYE MICHANGO YENU INALETA

Michango yenye unatoa kwa ukarimu inategemeza kazi yetu katika dunia yote (Picha hizi zinapatana na fungu la 14-16)

14-16. (a) Michango yako yenye unatoa inatimiza mambo gani fulani? (b) Namna gani umefaidika na mambo hayo?

14 Watumishi wa Yehova wenye wamemutumikia kwa miaka mingi wanasema kama hawajaona wakati kama huu wenye kuwa na chakula kingi cha kiroho. Fikiria jambo hili! Katika miaka ya hivi karibuni, tumekuwa na jw.org na JW Télédiffusion. Biblia Takatifu​—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inachapishwa katika luga nyingi zaidi. Katika mwaka wa 2014 na 2015, katika viwanja fulani kubwa-kubwa 14 katika dunia yote, kulifanyika Mikusanyiko ya Kimataifa ya siku tatu yenye kichwa ‘Muendelee Kutafuta Kwanza Ufalme wa Mungu!’ Wale wenye walihuzuria mikusanyiko hiyo walifurahi sana.

15 Wengi wameonyesha shukrani yao juu ya faida nyingi za ajabu zenye wanapata katika tengenezo. Kwa mufano, juu ya mupango JW Télédiffusion, bibi na bwana fulani wenye kutumikia katika inchi moja ya Asia waliandika hivi: “Mugawo wetu uko katika muji mudogo. Kwa hiyo, wakati fulani tunajisikia kama tuko peke yetu, na tunasahau haraka kuwa kazi ya Yehova ni kubwa. Lakini wakati tunaangalia programu mbalimbali za JW Télédiffusion, tunakumbuka kama tuko sehemu ya familia ya ndugu na dada ya duniani pote. Ndugu na dada zetu wapendwa wa eneo hili wanafurahia sana programu za JW Télédiffusion. Kila mara tunasikia wanasema kama kisha kuangalia programu ya kila mwezi, wanajisikia kama wako karibu na ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza. Sasa wanajivunia sana kuwa katika tengenezo la Mungu.”

16 Katika dunia yote, karibu Majumba ya Ufalme 2500 yako yanajengwa ao kutengenezwa upya. Kisha kuanza kutumia Jumba lao mupya la Ufalme, ndugu na dada wa kutaniko moja katika inchi ya Hondura waliandika hivi: “Tunafurahi sana kuwa katika familia ya Yehova ya ulimwenguni pote na tunafurahia kuwa kati ya ndugu na dada wa duniani pote, wote walisaidia kufanya ndoto yetu ya kuwa na Jumba la Ufalme katika eneo letu ikuwe kweli.” Wengi wanasema maneno kama hayo yenye kuonyesha shukrani kisha kupata Biblia na vichapo vingine vyenye kutafsiriwa katika luga zao, kisha kupata musaada fulani, ao kisha kuona katika maeneo yao matokeo ya kuhubiri katika miji mikubwa-mikubwa na mahali pa watu wengi kwa kutumia vyombo vya kuwekea vichapo.

17. Nini inaonyesha kama Yehova anaendelea kutegemeza tengenezo lake?

17 Watu wenye hawako Mashahidi hawaelewe namna gani tunaweza kutimiza kazi hizo zote kupitia tu michango ya kujipendea. Kisha kutembelea moja kati ya majengo yenye tunatumia ili kuchapisha vichapo, musimamizi mumoja wa kompanyi kubwa alishangaa kusikia kuwa kazi hiyo yote inafanywa na watu wenye kujitolea na kupitia michango ya kujipendea, na bila kufanya biashara fulani ao kufanya kampanye fulani ili kukusanya feza. Alisema kama haiwezekane kufanya mambo yenye tunafanya. Tunakubaliana naye! Tunajua kama inawezakana tu kwa sababu Yehova anategemeza kazi hii.​—Ayu. 42:2.

BARAKA ZENYE TUNAPATA WAKATI TUNAMUTOLEA YEHOVA

18. (a) Tunapata baraka gani wakati tunatoa michango ili kutegemeza kazi ya Ufalme? (b) Namna gani tunaweza kuzoeza watoto wetu na wapya juu ya kutoa michango?

18 Yehova anatupatia pendeleo la kutegemeza kazi kubwa yenye kufanywa leo. Anaahidi kama atatubariki wakati tunategemeza kazi ya Ufalme. (Mal. 3:10) Yehova anaahidi kama ule mwenye kutoa kwa ukarimu atapata faida sana. (Soma Methali 11:24, 25.) Kutoa pia kunatuletea furaha kwa sababu “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Mdo. 20:35) Kupitia maneno na mufano wetu, tuko na pendeleo la kuzoeza watoto wetu na wapya wafikirie namna wanaweza kutoa michango, na wakati wanafanya hivyo wao pia wanaweza kupata baraka nyingi.

19. Habari hii imekutia moyo namna gani?

19 Kila kitu chenye tuko nacho kinatoka kwa Yehova. Wakati tunamutolea tunaonyesha kama tunamupenda na tuko wenye shukrani juu ya mambo yote yenye ametufanyia. (1 Nya. 29:17) Wakati walitoa michango kwa ajili ya kujenga hekalu, watu ‘walishangilia kutokana na matoleo yao ya hiari [ao, ya kujipendea] waliyotoa, kwa maana walimutolea Yehova matoleo ya hiari kwa moyo kamili.’ (1 Nya. 29:9) Basi sisi pia tuendelee kupata furaha na kutosheka wakati tunamutolea Yehova vitu vyenye vimetoka katika mukono wake mwenyewe.