Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unaona tofauti yenye kuwa kati ya watu?

Unaona tofauti yenye kuwa kati ya watu?

‘Mutaona . . . tofauti kati ya muadilifu na muovu.’​—MAL. 3:18.

NYIMBO: 127, 101

1, 2. Watu wa Mungu wanapambana na magumu gani leo? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

WANGANGA wengi wanatunza watu wenye kuwa na magonjwa yenye kuambukiza. Wanahangaikia wagonjwa kwa sababu wanapenda kuwasaidia. Lakini, wakati wanafanya hivyo, wanapaswa kujilinda ili wao pia wasiambukizwe na ugonjwa wenye wanapenda kutunza. Vilevile, wengi kati yetu wanaishi na wanatumika pamoja na watu wenye kuwa na mawazo na tabia zenye kupingana na sifa zenye Mungu anapenda tuonyeshe. Hilo linatuletea magumu.

2 Katika siku hizi za mwisho watu wako na mwenendo mubaya sana. Barua ya pili yenye mutume Paulo alimuandikia Timotheo inaeleza tabia mbalimbali za watu wenye hawamutumikie Mungu, zenye zitaendelea kuonekana zaidi kadiri mwisho unakaribia. (Soma 2 Timotheo 3:1-5, 13.) Hata kama tunaweza kuhuzunika sana kuona namna tabia hizo zinaenea, tunaweza kuchochewa na tabia ao mawazo ya watu wenye kuonyesha tabia hizo. (Met. 13:20) Katika habari hii, tutazungumuzia namna gani tabia zenye watu wanaonyesha katika siku za mwisho ziko tofauti na sifa zenye watu wa Mungu wanaonyesha. Tutaona pia namna gani tunaweza kujilinda ili tusiambukizwe na tabia hizo za mubaya wakati tunaendelea kusaidia wengine kiroho.

3. Tabia zenye kutajwa katika 2 Timotheo 3:2-5 zinahusu nani?

3 Mutume Paulo aliandika kama “siku za mwisho” zingeleta ‘nyakati za hatari zilizo ngumu kushugulika nazo.’ Kisha alitaja tabia za mubaya 19, zenye watu wangeonyesha katika siku hizi. Tabia zenye alitaja zinafanana na zile zenye kutajwa kwenye Waroma 1:29-31, lakini tabia zenye Paulo anataja katika barua ya pili kwa Timotheo zinatia ndani tabia zingine zenye hazipatikane nafasi ingine yoyote katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Paulo anaanza kutaja tabia hizo za mubaya kwa kusema maneno, “kwa maana watu watakuwa . . .” Lakini, haiko watu wote ndio wanaonyesha tabia hizo. Wakristo wanaonyesha sifa zenye kuwa tofauti sana na hizo.​—Soma Malaki 3:18.

NAMNA TUNAJIONA SISI WENYEWE

4. Kulingana na mawazo yako, kujivuna kwa kiburi maana yake nini?

4 Kisha kusema kama watu wengi wangekuwa wenye kujipenda wenyewe na wenye kupenda feza, Paulo aliandika kama watu wangekuwa pia wenye kujidai ao wenye kujiwazia, wenye majivuno, na wenye kujivuna kwa kiburi. Mara nyingi tabia hizo zinaonyesha kuwa mutu anajiona kuwa wa maana zaidi kuliko wengine kwa sababu ya uwezo wake, sura yake, utajiri, ao cheo chake. Watu wenye kuonyesha tabia kama hizo, wanapenda sana watu wawafurahie na kuwasifu. Mutu mumoja mwenye elimu aliandika hivi juu ya mutu mwenye kuwa na majivuno sana: “Katika moyo wake kuko mazabahu ndogo kwenye anajiinamia yeye mwenyewe.” Watu fulani wamesema kuwa majivuno ya kupita mipaka ni yenye kuchukiza sana mupaka hata watu wenye kuwa na majivuno kama hayo wanachukia wakati wengine wanaonyesha tabia hiyo.

5. Namna gani hata watumishi waaminifu wa Mungu wameambukizwa na majivuno?

5 Yehova anachukia kabisa majivuno. Anachukia “macho ya majivuno.” (Met. 6:16, 17) Majivuno yanazuia mutu kumukaribia Mungu. (Zab. 10:4) Hiyo ni tabia ya Shetani. (1 Tim. 3:6) Lakini, jambo la kuhuzunisha ni kwamba, watumishi fulani washikamanifu wa Yehova wameambukizwa na majivuno. Mufalme Uzia wa Yuda alikuwa muaminifu kwa miaka mingi. Biblia inasema hivi: ‘Hata hivyo, mara tu alipopata nguvu, moyo wake ukakuwa na majivuno hata kufikia hatua ya kusababisha [kuleta] uharibifu, hivi kwamba akatenda kwa ukosefu wa uaminifu kwa Yehova Mungu wake, akaingia katika hekalu la Yehova ili kufukiza [kuchoma] uvumba juu ya mazabahu ya uvumba.’ Kisha, Mufalme Hezekia pia alifikia kuwa na majivuno, lakini kwa muda mufupi tu.​—2 Nya. 26:16; 32:25, 26.

6. Ni nini ingemufanya Daudi akuwe na majivuno, lakini sababu gani hakukuwa na majivuno?

6 Watu fulani wanakuwa na majivuno kwa sababu wako na sura ya muzuri, wanajulikana, wako na uwezo fulani katika mambo ya muziki, wako na uwezo fulani wa kimwili, ao cheo cha juu. Daudi alikuwa na mambo hayo yote, lakini aliendelea kuwa munyenyekevu katika maisha yake yote. Kisha kumuua Goliathi na kupewa mutoto wa Mufalme Sauli akuwe bibi yake, Daudi alisema hivi: ‘Mimi ni nani na watu wa ukoo wangu ni nani, familia ya baba yangu, katika Israeli, hata nikuwe mwana-mukwe wa mufalme?’ (1 Sam. 18:18) Ni nini ilimusaidia Daudi aendelee kuwa munyenyekevu? Daudi alikuwa na sifa, uwezo, na mapendeleo mbalimbali kwa sababu Mungu ‘alijishusha,’ ao kujinyenyekeza ili kumufikiria sana. (Zab. 113:5-8) Daudi alijua kama mambo yote ya muzuri yenye alikuwa nayo yalitoka kwa Yehova.​—Linganisha na 1 Wakorintho 4:7.

7. Ni nini itatusaidia tuonyeshe unyenyekevu?

7 Kama Daudi, watu wa Yehova leo wanajikaza kuonyesha unyenyekevu. Tunashangaa kujua kama Yehova, Mutu mukubwa zaidi katika ulimwengu, anaonyesha sifa yenye kupendeza ya unyenyekevu. (Zab. 18:35) Tunatii shauri hili lenye liliongozwa na roho yake: ‘Mujivike [muvae] upendo mwororo wenye huruma, fazili, unyenyekevu wa akili, upole, na ustahimilivu [uvumilivu].’ (Kol. 3:12) Tunajua pia kama upendo ‘haujigambe, haujivune.’ (1 Kor. 13:4) Wakati tunaonyesha unyenyekevu, tunaweza kusaidia watu wamukaribie Yehova. Kama vile bwana wanaweza kuvutwa na mwenendo wa bibi zao bila maneno, wengine wanaweza kumukaribia Mungu wakati wanaona namna watu wake wanaonyesha unyenyekevu.​—1 Pet. 3:1.

NAMNA TUNATENDEA WENGINE

8. (a) Leo, watu fulani wako na mawazo gani juu ya tabia ya kukosa kutii wazazi? (b) Maandiko yanatolea watoto shauri gani?

8 Paulo alieleza namna watu wenye kuishi katika siku za mwisho wangetendea wengine. Aliandika kama katika siku za mwisho watoto wangekuwa wasiotii wazazi. Hata kama wakati fulani vitabu, filme, na programu za televizyo zinakubali na kuchochea tabia hiyo leo, kukosa utii katika familia kunafanya familia, yenye kuwa musingi wenye kufanyiza vikundi vya watu, ikuwe zaifu. Wanadamu wanajua jambo hilo tangu zamani. Kwa mufano, katika Ugiriki ya zamani ikiwa mutu angepiga wazazi wake angepoteza haki zake zote za raia; na sheria ya Roma pia ilionyesha kama kupiga baba ilikuwa kosa kubwa kama vile kuua mutu. Maandiko ya Kiebrania na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yanashauria watoto kuheshimia wazazi wao.​—Kut. 20:12; Efe. 6:1-3.

9. Ni nini inaweza kusaidia vijana watii wazazi wao?

9 Watoto wanaweza kujilinda ili wasiambukizwe na tabia ya kukosa kutii kwa kufikiria mambo yenye wazazi wao wamekwisha kuwafanyia. Pia vijana wanapaswa kuelewa kuwa Mungu, Baba yetu sisi wote, anawaomba watii wazazi wao, hilo linaweza kuwachochea wakuwe wenye shukrani. Wakati vijana wanasema muzuri juu ya wazazi wao, wanaweza kusaidia vijana wengine waheshimie wazazi wao pia. Kwa kweli, ikiwa wazazi hawana upendo wa asili juu ya watoto wao, inaweza kuwa vigumu kwa watoto kuwatii kwa moyo wote. Kwa upande mwingine, wakati mutoto anaona namna wazazi wake wanamupenda kabisa, hilo linamuchochea kuwafurahisha hata wakati iko katika jaribu la kukosa kutii. Austin anasema hivi: “Hata kama mara nyingi nilikuwa ninataka kufanya mambo ya mubaya, wazazi wangu waliweka sheria zenye kuwa na usawaziko, walinifasiria sababu gani waliweka sheria hizo, na waliendelea kuzungumuza na mimi kwa ukawaida. Hilo lilinisaidia kuwatii. Niliona kuwa wananihangaikia, na hilo lilinichochea kuwafurahisha.”

10, 11. (a) Ni tabia gani za mubaya zenye kuonyesha kuwa watu hawapendane? (b) Wakristo wa kweli wanapenda wanadamu wenzao kwa kadiri gani?

10 Paulo alitaja tabia zingine za mubaya zenye kuonyesha kama watu hawapendane. Kisha kutaja “wasiotii wazazi” mutume Paulo anataja wasio na shukrani. Hilo linafaa kwa sababu hiyo ni tabia ya watu wenye hawana shukrani juu ya wema wenye wengine wanawafanyia. Pia watu wangekuwa wasio washikamanifu. Wangekuwa wasiotaka makubaliano yoyote, wenye hawapendi kupatana na watu wengine. Wangekuwa wakufuru na wasaliti, wenye kutukana ao kusema maneno ya mubaya juu ya wanadamu na hata juu ya Mungu. Na wangekuwa pia wachongezi, watu wenye kusema mambo ya mubaya juu ya wengine ili kuwaharibishia sifa. *

11 Tofauti na watu wenye kuonyesha tabia ya kukosa upendo yenye kuenea leo, wale wenye kumuabudu Yehova wanaonyesha wanadamu wenzao upendo wa kweli. Ni hivyo tangu zamani. Yesu alisema kama kisha amri ya kwanza ya maana zaidi ya kupenda Mungu, kupenda jirani, aina a·gaʹpe, ndiyo ilikuwa amri ya pili ya maana zaidi katika Sheria ya Musa. (Mt. 22:38, 39) Yesu alisema pia kwamba kupendana ndiyo sifa yenye ingetambulisha Wakristo wa kweli. (Soma Yohana 13:34, 35.) Wakristo wangepaswa hata kupenda maadui wao.​—Mt. 5:43, 44.

12. Namna gani Yesu alionyesha upendo kwa wengine?

12 Yesu alionyesha upendo mukubwa kwa wengine. Alienda katika miji mbalimbali ili kuhubiria watu habari njema ya Ufalme wa Mungu. Aliponyesha vipofu, walemavu, wenye kuwa na ukoma, na viziwi. Alifufua wafu. (Lu. 7:22) Yesu alitoa hata uzima wake kwa ajili ya wanadamu, hata kama wengi walimuchukia. Upendo wa Yesu ulionyesha kwa ukamilifu upendo wenye Baba yake anaonyesha. Katika dunia yote, Mashahidi wa Yehova wanaonyesha upendo kwa wengine.

13. Namna gani upendo wenye tunaonyesha wengine unaweza kuwasaidia wamukaribie Yehova?

13 Upendo wenye tunaonyesha unafanya watu wamukaribie Baba yetu wa mbinguni. Kwa mufano, mwanaume mumoja katika inchi ya Thailandi, aliguswa moyo na upendo wenye ndugu na dada walionyeshana kwenye mukusanyiko mumoja wa eneo. Kisha kurudia nyumbani, aliomba kujifunza Biblia mara mbili katika juma. Alihubiria watu wote wa jamaa yake, na miezi sita kisha mukusanyiko huo, alifanya usomaji wake wa Biblia wa kwanza kwenye Jumba la Ufalme. Ili kuchunguza ikiwa tunaonyesha kabisa wengine upendo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Ninajikaza kusaidia wengine katika familia yangu, katika kutaniko langu, na katika mahubiri? Ninajikaza kuona wengine namna Yehova anawaona?’

IMBWA-MWITU NA WANA-KONDOO

14, 15. Watu wanaonyesha tabia gani zenye kufanana na za wanyama, lakini namna gani wamoja wamebadilika na kuwa watu wazuri?

14 Tabia zingine zenye watu wanaonyesha katika siku za mwisho, zinapatia Wakristo sababu zingine za kuepuka watu kama hao. Watu wenye hawamuogope Mungu wangekuwa wasiopenda wema. Tafsiri zingine zinatafsiri maneno hayo kuwa, “wenye kuchukia mema” ao “wenye kupinga sana mambo yote mema.” Wangekuwa wasiojizuia, na wakali. Wengine wangekuwa wenye vichwa vigumu, ao wenye kutenda haraka bila kufikiri na bila kuhangaika ikiwa matendo yao yanaweza kuumiza wengine ao hapana.

15 Watu wengi wenye walikuwa zamani na tabia hizo kama za wanyama wamebadilika na kuwa watu wazuri. Mabadiliko hayo yalitabiriwa kabisa katika unabii fulani wa Biblia. (Soma Isaya 11:6, 7.) Unabii huo unaonyesha kama wanyama wa pori kama vile imbwa-mwitu na simba wanaishi kwa amani pamoja na wanyama wa nyumbani kama vile wana-kondoo na wana-mbuzi. Kwa kweli hali hiyo ya amani itaendelea ‘kwa maana dunia hakika itajawa na kumujua Yehova.’ (Isa. 11:9) Kwa sababu wanyama hawawezi kujifunza juu ya Yehova, utimizo wa kiroho wa unabii huo unahusu wanadamu.

Kutumikisha kanuni za Biblia kunabadilisha maisha ya watu! (Picha hizi zinapatana na fungu la 16)

16. Namna gani Biblia imesaidia watu kubadilisha maisha yao?

16 Kuko watu wengi wenye zamani walikuwa wakali kama imbwa-mwitu lakini sasa wanaishi kwa amani pamoja na wengine. Unaweza kusoma mifano fulani juu ya watu hao katika habari zenye kichwa “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu,” zenye kupatikana kwenye jw.org. Wale wenye wamefikia kumujua Yehova hawako kama wale wenye kuwa na namna ya ujitoaji-kimungu ao ya kushikamana na Mungu lakini wanazikana nguvu zake, wanajifanya kama vile wanamutumikia Mungu lakini matendo yao hayaonyeshe kabisa jambo hilo. Lakini, watu wenye walikuwa wakali zamani ‘wamevaa utu mupya ulioumbwa kulingana na mapenzi ya Mungu katika uadilifu wa kweli na ushikamanifu.’ (Efe. 4:23, 24) Wakati watu wanaendelea kujifunza juu ya Mungu, wanaona kwamba kuishi kulingana na kanuni zake ni jambo la lazima. Kisha, wanachochewa kubadilisha mambo yenye walikuwa wanaamini, mawazo yao, na matendo yao. Haiko mwepesi kufanya mabadiliko hayo; lakini inawezekana kwa sababu roho ya Mungu itasaidia wale wenye wanapenda kabisa kufanya mapenzi ya Mungu.

“GEUKIA MBALI KUTOKA KWA HAO”

17. Namna gani tunaweza kuepuka kuchochewa na watu wenye kuwa na tabia za mubaya?

17 Tofauti yenye kuwa kati ya wale wenye kumutumikia Mungu na wale wenye hawamutumikie inaendelea kuonekana wazi. Sisi wenye kumutumikia Yehova tunapaswa kuwa waangalifu ili tusiambukizwe na tabia za mubaya za wengine. Ni jambo la hekima kutii shauri lenye kuongozwa na roho lenye kutuomba tugeukie mbali kutoka kwa wale wenye kuzungumuziwa katika 2 Timotheo 3:2-5. Ni kweli kwamba hatuwezi kuepuka kabisa-kabisa watu wenye kuwa na tabia za mubaya. Pengine tunalazimika kutumika pamoja nao, kusoma pamoja nao, ao kuishi pamoja nao. Lakini, tunaweza kuepuka kuiga mawazo yao na tabia zao. Ili kufanya hivyo, tunapaswa kutia nguvu hali yetu ya kiroho kwa kujifunza Biblia na kujiunga kabisa na wale wenye wanaazimia kumutumikia Yehova.

18. Namna gani maneno na matendo yetu yanaweza kusaidia wengine wamujue Yehova?

18 Tunapaswa pia kujikaza kusaidia wengine ili wamujue Yehova. Tafuta nafasi za kuhubiria wengine, na kumuomba Yehova akusaidie useme mambo yenye kufaa kwa wakati wenye kufaa. Tunapaswa kujulisha wengine kama sisi ni Mashahidi wa Yehova. Ikiwa tunafanya hivyo, mwenendo wetu wa muzuri hautatuletea sisi utukufu, lakini utamuletea Mungu utukufu. Tumezoezwa ‘kukataa kabisa kutomuogopa Mungu na tamaa za ulimwengu na tuishi kwa utimamu wa akili [akili nzuri] na uadilifu na ujitoaji-kimungu katikati ya mufumo wa mambo wa sasa.’ (Tito 2:11-14) Ikiwa tuko na mwenendo muzuri, wengine wataona jambo hilo, na wamoja wanaweza kusema hivi: ‘Tutaenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia ya kuwa Mungu yupo pamoja nanyi.’​—Zek. 8:23.

^ fu. 10 Neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa ‘muchongezi’ ao ‘mushitaki’ ni di·aʹbo·los, neno lenye kutumiwa katika Biblia ili kuonyesha jina la Shetani, muchongezi muovu wa Mungu.