Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni Upendo wa Aina Gani Wenye Kuleta Furaha ya Kweli?

Ni Upendo wa Aina Gani Wenye Kuleta Furaha ya Kweli?

“Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova!”​—ZAB. 144:15.

NYIMBO: 111, 109

1. Tunaishi katika kipindi cha pekee, sababu gani?

TUNAISHI katika kipindi cha pekee cha historia ya wanadamu. Kama vile Biblia ilitabiri, Yehova anaendelea kukusanya ‘umati [ao, mukutano] mukubwa . . . kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga.’ Wale wenye kukusanywa wanafanyiza “taifa lenye nguvu” la watu zaidi ya milioni munane wenye furaha wenye ‘wanamutolea [Mungu] utumishi mutakatifu muchana na usiku.’ (Ufu. 7:9, 15; Isa. 60:22) Hakujakuwa hata kidogo hesabu kubwa kama hiyo ya watu wenye wanamupenda Mungu na wanadamu wenzao.

2. Watu wenye hawamutumikie Mungu wanaonyesha upendo wa aina gani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

2 Lakini, Maandiko yenye kuongozwa na roho ya Mungu yalitabiri pia kama katika siku zetu, kungekuwa upendo mwengine wenye haufae, upendo wenye uchoyo. Watu wenye hawamutumikie Mungu wangeonyesha upendo huo. Mutume Paulo aliandika hivi: ‘katika siku za mwisho . . . , watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa [feza], . . . wanaopenda raha badala ya kumupenda Mungu.’ (2 Tim. 3:1-4) Kujipenda mwenyewe ni tofauti na upendo wa Kikristo, kunapingana kabisa na upendo huo. Kufuatia miradi yenye uchoyo hakuletee watu furaha yenye wanatazamia. Kwa kweli, upendo kama huo unatokeza ulimwengu wenye kujipenda wenyewe wenye kuwa ‘mugumu kushugulika nao.’

3. Tutazungumuzia nini katika habari hii, na sababu gani?

3 Paulo alijua kama tabia hiyo yenye kuenea, ni kusema, upendo wenye uchoyo, ingekuwa hatari kwa Wakristo. Kwa hiyo, aliwaonya ‘wageukie mbali’ ao waepuke wale wenye kuonyesha upendo wenye haufae. (2 Tim. 3:5) Lakini, hatuwezi kuepuka kabisa-kabisa watu hao. Kwa hiyo, namna gani tunaweza kuepuka mawazo ya watu wa ulimwengu wenye kutuzunguka na kujikaza kumupendeza Yehova, Mungu mwenye upendo? Tuzungumuzie basi tofauti yenye kuwa kati ya upendo wa kweli na upendo wenye kuzungumuziwa katika 2 Timotheo 3:2-4. Kufanya hivyo kutatusaidia kuchunguza na kukomalisha zaidi aina ya upendo wenye tunaonyesha, upendo wenye kutuletea furaha ya kweli na kutosheka.

UNAMUPENDA MUNGU AO UNAJIPENDA MWENYEWE?

4. Sababu gani haiko mubaya kujipenda mwenyewe kwa njia yenye kufaa?

4 Mutume Paulo aliongozwa na roho ya Mungu ili kuandika kama “watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe.” Ni mubaya kujipenda mwenyewe? Hapana, ni jambo la kawaida, na hata ni lazima kujipenda kwa njia yenye kufaa. Ni hivyo Yehova alituumba. Yesu alisema hivi: ‘Mupende jirani yako kama wewe mwenyewe.’ (Mk. 12:31) Ikiwa hatujipende wenyewe, hatuwezi kupenda jirani yetu. Biblia inasema pia hivi: ‘Wanaume wanapaswa kuwa wakiwapenda wake [ao, bibi] zao kama miili yao wenyewe. Yeye anayemupenda muke wake anajipenda mwenyewe, kwa maana hakuna mutu anayeuchukia mwili wake kwa vyovyote; bali anaukulisha na kuutunza.’ (Efe. 5:28, 29) Kwa hiyo, ni muzuri kujipenda wenyewe kwa njia yenye kufaa.

5. Watu wenye kujipenda wenyewe kupita mipaka wako namna gani? Eleza.

5 Upendo wenye kuzungumuziwa katika 2 Timotheo 3:2 haiko upendo wa kawaida, ao wenye kufaa. Ni upendo wenye haufae, ni upendo wenye uchoyo. Watu wenye kujipenda wenyewe kupita mipaka wanajifikiria sana kuliko namna wanapaswa kujifikiria. (Soma Waroma 12:3.) Wanajiona kuwa wa maana zaidi katika maisha yao. Hawahangaikie wengine. Wakati mambo hayaendeke muzuri wanapenda kulaumu wengine kuliko kukubali matokeo ya makosa yao. Kitabu kimoja chenye kutoa maelezo juu ya Biblia kinalinganisha watu wenye kujipenda wenyewe na munyama mumoja mwenye kuitwa nungunungu. Wakati anajikunja kama kabumbu, anaweka sehemu ya manyoya yake ya teketeke yenye joto kwa ajili yake mwenyewe na kuonyesha wengine sehemu yenye kuwa na miiba. Watu hao wenye kujipenda wenyewe hawana furaha kabisa.

6. Kumupenda Mungu kunaleta matokeo gani?

6 Watu wenye elimu ya Biblia wanasema kama kati ya tabia za mubaya zenye Paulo alitaja zenye watu wangeonyesha katika siku za mwisho, tabia ya watu ya kujipenda wenyewe inatajwa kwanza, kwa sababu tabia zingine zote zinatokana na tabia hiyo. Kwa upande mwengine, watu wenye kumupenda Mungu wanaonyesha sifa zenye kuwa tofauti sana. Biblia inaonyesha kama upendo wenye Mungu anapenda tuonyeshe unatusaidia kuwa na sifa kama vile furaha, amani, ustahimilivu, fazili, wema, imani, upole, na kujizuia. (Gal. 5:22, 23) Muandikaji mumoja wa zaburi aliandika hivi: “Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova!” (Zab. 144:15) Yehova ni Mungu mwenye furaha, na watu wake wanaonyesha sifa hiyo. Zaidi ya hilo, tofauti na wale wenye kujipenda wenyewe na wenye kufurahia kupokea tu, watumishi wa Yehova wanapata furaha kwa kujitoa ili kusaidia wengine.​—Mdo. 20:35.

Namna gani tunaweza kuepuka kujipenda wenyewe? (Picha hizi zinapatana na fungu la 7)

7. Ni maulizo gani yenye yatatusaidia kujichunguza ili kuona ikiwa tunamupenda Mungu?

7 Namna gani tunaweza kujua kama tumeanza kujipenda sana wenyewe kuliko kumupenda Mungu? Fikiria shauri lenye kupatikana kwenye Wafilipi 2:3, 4 lenye kusema hivi: ‘Bila kufanya jambo lolote kwa ugomvi ao kwa kujisifu, bali kwa unyenyekevu wa akili mukiwaona wengine kuwa ni bora [wazuri zaidi] kuliko ninyi, mukiendelea kuangalia, si faida za kibinafsi za mambo yenu wenyewe tu, bali pia faida za kibinafsi za wengine.’ Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Ninatumikisha shauri hilo katika maisha yangu? Ninajikaza kabisa kufanya mapenzi ya Mungu? Niko tayari kusaidia wengine, katika kutaniko na katika kazi ya kuhubiri?’ Haiko mwepesi kujitoa sikuzote. Inaomba kujikaza sana na kujinyima. Lakini hakuna jambo lingine lenye linaweza kutuletea furaha zaidi kuliko kujua kama tunakubaliwa na Mutawala Mukubwa wa ulimwengu wote.

8. Kumupenda Mungu kumechochea watu fulani wafanye nini?

8 Kumupenda Mungu kumechochea watu fulani waache kazi zenye kuonekana kuwa za muzuri ili wafanye mengi katika kazi ya Yehova. Ericka, mwenye kuishi katika inchi ya Amerika, ni munganga. Lakini, kuliko kufuatia kazi yenye kuwa na mushahara muzuri katika mambo ya kinganga, akakuwa painia wa kawaida na ametumikia katika inchi mbalimbali pamoja na bwana yake. Wakati anakumbuka, anasema hivi: “Mambo mengi yenye tumejionea kwa kuhubiria katika eneo lenye kutumia luga ya kigeni, na marafiki wenye tumepata, vimetuletea kabisa furaha katika maisha. Ninaendelea kufanya kazi ya kinganga, lakini kutumia wakati wangu mwingi na nguvu zangu ili kusaidia watu wapone kiroho na kusaidia ndugu na dada kunaniletea furaha na ninajisikia kuwa mwenye kutosheka.”

UNAJIKUSANYIA UTAJIRI MBINGUNI AO DUNIANI?

9. Sababu gani kupenda feza hakulete furaha?

9 Mutume Paulo aliandika kama watu wangekuwa “wenye kupenda pesa.” Miaka fulani yenye imepita, painia mumoja katika inchi ya Irelandi alizungumuza na mwanaume mumoja juu ya Mungu. Mwanaume huyo alikamata mufuko wake mudogo wa kuwekea feza, akatosha ndani feza fulani, na akasema hivi kwa majivuno: “Ona mungu wangu!” Hata kama watu wengi hawaseme hivyo waziwazi, dunia inajaa watu wenye kupenda feza na vitu vyenye zinaweza kuuza. Lakini, Biblia inatuonya hivi: ‘Anayependa feza hatatosheka na feza, wala anayependa mali hatatosheka na mapato.’ (Mhu. 5:10) Watu kama hao wanapenda sikuzote kupata feza zaidi, na wakati wanajikaza kuwa na feza nyingi zaidi, wanajiletea wenyewe “maumivu mengi.”​—1 Tim. 6:9, 10.

10. Biblia inasema nini juu ya utajiri na umaskini?

10 Kwa kweli, sisi wote tuko na lazima ya feza. Zinatutolea ulinzi kwa kadiri fulani. (Mhu. 7:12) Lakini mutu anaweza kuwa na furaha kabisa ikiwa iko tu na feza za kutosha ili kutimiza mambo yake ya lazima? Ndiyo kabisa! (Soma Mhubiri 5:12.) Aguri mwana wa Yake aliandika hivi: ‘Usinipe umaskini wala utajiri. Acha nikule chakula nilichoamuriwa.’ Tunaweza kuelewa kabisa sababu gani hakupenda akuwe maskini sana. Kama vile alifikia kueleza, hakupenda akuwe katika jaribu la kuiba kwa sababu kuiba kunamuvunjia Mungu heshima. Lakini sababu gani alisali asipate utajiri? Aliandika hivi: “Nisije nikashiba nikakukana, nikasema: ‘Yehova ni nani?’” (Met. 30:8, 9) Pengine unajua watu wenye kutumainia mali yao kuliko kumutumainia Mungu.

11. Yesu alitoa shauri gani juu ya feza?

11 Wale wenye kupenda feza hawawezi kumupendeza Mungu. Yesu alisema hivi: ‘Hakuna anayeweza kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana ama atamuchukia mumoja na kumupenda yule mwingine, ama atashikamana na mumoja na kumuzarau yule mwingine. Hamuwezi kutumikia Mungu na Utajiri.’ Mbele ya kusema maneno hayo, alikuwa amesema kwanza hivi: ‘Muache kujiwekea hazina duniani, ambako nondo na kutu wanakula, na ambako wezi wanavunja na kuiba. Badala yake, mujiwekee hazina mbinguni, ambako nondo na kutu havikule, na ambako wezi hawavunje na kuiba.’​—Mt. 6:19, 20, 24.

12. Namna gani kufanya maisha yetu yakuwe mepesi kunatusaidia kumutumikia Mungu? Toa mufano.

12 Wengi wametambua kama kuishi maisha mepesi kunawaletea furaha, lakini pia kunawatolea wakati mwingi zaidi wa kumutumikia Yehova. Jack, mwenye kuishi Amerika, aliuzisha nyumba yake kubwa na biashara yake kwa sababu alijua kama kufanya hivyo kungemusaidia yeye pia akuwe painia kama bibi yake. Anaeleza hivi: “Ilikuwa vigumu kuacha nyumba yetu yenye kupendeza na kiwanja chetu chenye kilikuwa mbali na muji. Lakini, kwa miaka mingi, nilikuwa ninarudia nyumbani nikiwa mwenye kuchoka akili kwa sababu ya matatizo kwenye kazi. Bibi yangu mwenye alikuwa painia wa kawaida, alikuwa na furaha sikuzote. Alikuwa anasema, ‘Ninatumikia mukubwa wa kazi muzuri zaidi!’ Kwa sababu sasa mimi pia ninafanya kazi ya upainia, sisi wawili tunatumikia Mutu uleule, ni kusema, Yehova.”

Namna gani tunaweza kuepuka kupenda feza? (Picha hizi zinapatana na fungu la 13)

13. Namna gani tunaweza kuchunguza mawazo yetu juu ya feza?

13 Ili kuchunguza mawazo yetu juu ya feza, tunaweza kufikiria kabisa namna tunaweza kujibia maulizo haya: ‘Ninaamini kabisa na kuishi kulingana na mambo yenye Biblia inasema juu ya feza? Kutafuta feza ndilo jambo la maana zaidi katika maisha yangu? Ninaona kuwa vitu vya kimwili ni vya maana zaidi kuliko urafiki wangu pamoja na Yehova na watu wengine? Ninaamini kabisa kwamba Yehova atanitimizia mahitaji yangu?’ Tunaweza kuwa hakika kama hataachilia hata kidogo wale wenye kumutumainia.​—Mt. 6:33.

UNAMUPENDA YEHOVA AO UNAPENDA RAHA?

14. Tunapaswa kuwa na mawazo gani juu ya mambo ya kujifurahisha?

14 Kama vile ilitabiriwa watu wengi leo ni watu “wanaopenda raha.” Kama vile haiko mubaya kuwa na mawazo yenye kusawazika juu yetu sisi wenyewe na juu ya feza, haiko mubaya pia kuwa na mawazo yenye kusawazika juu ya mambo ya kujifurahisha. Yehova hapendi tujinyime kupita mipaka ao kuepuka mambo ya muzuri ya kujifurahisha yenye kuleta furaha. Biblia inatia moyo watumishi waaminifu wa Mungu hivi: ‘Enda, ukule chakula chako kwa kushangilia na kunywa divai yako kwa moyo muchangamufu.’​—Mhu. 9:7.

15. Andiko la 2 Timotheo 3:4 linazungumuzia raha ya aina gani?

15 Andiko la 2 Timotheo 3:4 linazungumuzia wale wenye kufuatia raha ao mambo ya kujifurahisha na kumusahau Mungu. Ona kwamba mustari huo hauseme kama watu wangependa raha zaidi kuliko Mungu, ili kuonyesha kama wanamupenda Mungu kwa kadiri fulani. Mustari huo unasema ‘badala ya Mungu.’ Mutu mumoja mwenye kuwa na elimu ya Biblia aliandika hivi: “[Mustari] huu haumaanishe hata kidogo kuwa wanamupenda Mungu kwa kadiri fulani. Unamaanisha kuwa hawamupendi Mungu hata kidogo.” Hilo ni onyo kubwa kwa wale wenye wanaendelea kupenda mambo ya kujifurahisha kupita mipaka! Maneno “wanaopenda raha” yanazungumuzia kabisa wale wenye “kuchukuliwa . . . na raha za maisha haya.”​—Lu. 8:14.

16, 17. Yesu alituachia mufano gani juu ya mambo ya kujifurahisha?

16 Yesu alionyesha kwa ukamilifu mawazo yenye kusawazika juu ya mambo ya kujifurahisha. Alienda kwenye “karamu ya ndoa” na kwenye “karamu kubwa.” (Yoh. 2:1-10; Lu. 5:29) Kwenye karamu ya ndoa, aligeuza maji kuwa divai kwa njia ya muujiza, ili kuongezea divai yenye ilikuwa imeisha. Na wakati mwingine, alikataa kabisa mawazo ya watu wenye walijiona kuwa wenye haki wenye walimuchambua kwa sababu alikula na kunywa.​—Lu. 7:33-36.

17 Lakini, Yesu hakuona kuwa mambo ya kujifurahisha ndiyo ya maana katika maisha yake. Alitia Yehova pa nafasi ya kwanza na alijitoa sana kwa ajili ya wengine. Ili watu wengi wapate uzima, alikuwa tayari kuvumilia kifo chenye maumivu makali kwenye muti wa mateso. Ili kuzungumuzia wale wenye wangefuata mufano wake, Yesu alisema hivi: ‘Wenye furaha ni ninyi wakati watu wanapowashutumu na kuwatesa na kusema kwa uwongo kila namna ya jambo mbaya juu yenu kwa ajili yangu. Mushangilie na kuruka kwa shangwe, kwa kuwa sawabu [ao, malipo] yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana hivyo ndivyo walivyowatesa manabii waliokuwa kabla yenu.’​—Mt. 5:11, 12.

Namna gani tunaweza kuepuka kupenda raha? (Picha hizi zinapatana na fungu la 18)

18. Tunaweza kujiuliza maulizo gani ili kujichunguza ikiwa tunapenda sana mambo ya kujifurahisha?

18 Namna gani tunaweza kujichunguza ikiwa tunapenda sana mambo ya kujifurahisha? Ni muzuri tujiulize hivi: ‘Ninatia mambo ya kujifurahisha pa nafasi ya kwanza kuliko mikutano na kazi ya kuhubiri? Niko tayari kujinyima kwa sababu ninapenda kumutumikia Mungu? Wakati ninatafuta mambo ya kujifurahisha, ninafikiria namna gani Yehova ataona mambo yenye ninachagua?’ Ikiwa tunamupenda kabisa Mungu, tutakuwa waangalifu ili kuepuka mambo yenye tunajua kuwa yanamuchukiza Mungu, lakini pia mambo yenye tunafikiri kuwa yanaweza kumuchukiza.​—Soma Mathayo 22:37, 38.

NAMNA YA KUPATA FURAHA

19. Ni nani wenye hawawezi kupata furaha ya kweli hata kidogo?

19 Kisha wanadamu kuteseka kwa miaka 6000 hivi, ulimwengu wa Shetani unakaribia mwisho wake. Dunia inajaa watu wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, na wenye kupenda raha. Wanafikiria mambo yenye wanaweza kupata na wanafanya tamaa zao kuwa jambo la maana zaidi katika maisha yao. Watu kama hao hawawezi kuwa na furaha ya kweli hata kidogo. Lakini, Biblia inasema hivi: ‘Mwenye furaha ni yule ambaye Mungu wa Yakobo ni musaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yehova Mungu wake.’​—Zab. 146:5.

20. Namna gani kumupenda Mungu kumekuletea furaha?

20 Watu wa Yehova wanaendelea kumupenda, na hesabu yetu inaendelea kuongezeka kila mwaka. Huo ni ushuhuda wenye kuonyesha kama Ufalme wa Mungu unatawala, na kama hivi karibuni utaleta baraka za ajabu duniani. Kufanya mapenzi ya Mungu ndiyo kunaleta furaha ya kweli na yenye kuendelea, kwa sababu tunajua kama tunamupendeza Ule Mwenye Kuwa Juu Zaidi. Na wale wenye kumupenda Yehova watakuwa na furaha milele! Katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia tabia mbalimbali zenye kuletwa na upendo wenye uchoyo na tutaona namna gani tabia hizo ni tofauti na sifa zenye watu wa Yehova wanaonyesha.