Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna Gani Unaweza Kuzoea Kutaniko Lako la Mupya?

Namna Gani Unaweza Kuzoea Kutaniko Lako la Mupya?

ALLEN * anasema hivi: “Nilikuwa na wasiwasi juu ya kuhamia hapa. Sikujua ikiwa ningeweza kufanya marafiki ao kukaribishwa.” Allen anajikaza kuzoea kutaniko la mupya lenye kupatikana kwenye umbali wa kilometre zaidi ya 1400 kutoka nyumbani kwao.

Ikiwa umehamia katika kutaniko lingine, wewe pia unaweza kuwa na wasiwasi. Ni nini inaweza kukusaidia uzoee? Unaweza kufanya nini ikiwa inakuwa vigumu kuzoea kuliko namna uliwazia? Kwa upande mwengine, namna gani wewe unaweza kusaidia watu wenye kuhamia katika kutaniko lako wazoee?

NAMNA GANI TUNAWEZA KUZOEA NA KUFANYA MAENDELEO?

Fikiria mufano huu: Wakati miti inaongolewa na kuenda kupandwa nafasi ingine, inakuwa katika hali ngumu. Wakati muti unaongolewa katika udongo, kwa kawaida mutu anakata mizizi yake mingi ili ikuwe mwepesi kuubeba. Kisha tu kupandwa tena, muti unapaswa kuanza mara moja kutosha mizizi ya mupya. Vilevile, pengine kuhamia katika kutaniko lingine kulikufanya ukuwe na wasiwasi. Katika kutaniko lako la zamani, ulikuwa umeota mizizi ni kusema, ulikuwa na marafiki wengi wenye ulipenda na ulikuwa na programu ya kawaida ya kumutumikia Yehova. Sasa unapaswa kutoa mizizi ya mupya ili ufanye maendeleo katika eneo hilo la mupya. Ni nini itakusaidia kufanya hivyo? Utumikishe kanuni za Maandiko. Tuzungumuzie basi kanuni fulani.

Mutu mwenye kusoma kwa ukawaida Neno la Mungu iko ‘kama muti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao unatoa matunda yake katika majira yake na ambao majani yake hayanyauke [yakauke], na kila jambo analofanya litafanikiwa.’​Zab. 1:1-3.

Kama vile muti uko na lazima ya kupata maji kwa ukawaida ili uendelee kuwa na afya ya muzuri, Mukristo anapaswa kula kwa ukawaida chakula cha Neno la Mungu ili aendelee kuwa na urafiki wenye nguvu pamoja na Mungu. Kwa hiyo, uendelee kusoma Biblia kila siku, na kuhuzuria kwa ukawaida mikutano ya kutaniko. Uendelee kuwa na programu ya muzuri ya kufanya ibada ya familia na funzo la pekee. Unapaswa kuendelea kufanya mambo yote yenye ulikuwa unafanya katika kutaniko la zamani ili kufanya urafiki wako pamoja na Yehova uendelee kuwa nguvu.

Anayenywesha wengine kwa ukarimu yeye mwenyewe pia atanyweshwa kwa ukarimu.”​Met. 11:25.

Utakuwa nguvu na kuzoea haraka ikiwa unafanya kazi ya kuhubiri kwa ukawaida. Muzee mumoja wa kutaniko mwenye kuitwa Kevin, anasema hivi: “Jambo lenye lilinisaidia zaidi mimi na bibi yangu ni kuwa mapainia wasaidizi kisha tu kufika katika kutaniko letu la mupya. Bila kukawia tulifikia kujua ndugu, mapainia, na eneo.” Roger, mwenye alihamia katika eneo lenye kuwa kwenye umbali wa kilometre zaidi ya 1600 kutoka mahali alikuwa anaishi, anasema hivi: “Njia ya muzuri zaidi ya kukusaidia kuzoea kutaniko la mupya ni kuenda kwa ukawaida katika kazi ya kuhubiri kwa kadiri inawezekana. Pia, ujikaze kujulisha wazee kuwa uko tayari kujitolea kusaidia katika njia yoyote, pengine kwa kusafisha Jumba la Ufalme, kutoa sehemu fulani ya mutu mwenye haiko tayari ao hakufika kwenye mikutano, ao kusaidia mutu fulani kuenda kwenye mikutano. Wakati ndugu na dada wanaona mutu fulani mwenye kuwa mupya iko na roho ya kujitolea wanakuwa tayari kufanya urafiki pamoja naye.”

‘Mupanuke.’​2 Kor. 6:13.

Upanuke katika upendo wako wa kindugu. Kisha Melissa na watu wa familia yake kuhamia katika kutaniko la mupya, walikaza akili zao juu ya kufanya marafiki wapya. Anasema hivi: “Tulipitisha wakati pamoja na wengine kwenye Jumba la Ufalme mbele na kisha mikutano. Hilo lilitutolea wakati wa kuzungumuza mambo mengi zaidi nao kuliko kuwasalimia tu.” Hilo lilisaidia pia familia hiyo kujua majina ya ndugu na dada bila kukawia. Zaidi ya hilo, walionyesha sana ukaribishaji-wageni, na hilo liliwasaidia watie nguvu urafiki wenye walikuwa wameanzisha na ndugu na dada. Aliongezea hivi: “Tulipatiana namba za telefone, ili waweze kutupata na kutualika ili tujiunge nao katika mambo mbalimbali ya kutaniko na mambo mengine.”

Ikiwa unajisikia kuwa haiko rahisi kwako kuzungumuza na wapya, unaweza kuanza kwa kufanya mambo madogo-madogo. Kwa mufano, unaweza kuonyesha sura ya kicheko, hata kama mwanzoni haujisikie kufanya hivyo. Kuonyesha sura ya kicheko kutafanya wengine wajisikie huru kukukaribia. Kwa kweli, ‘Kungaa kwa macho kunafanya moyo ushangilie.’ (Met. 15:30) Rachel mwenye alihamia mbali sana na mahali penye alikomalia, anasema hivi: “Kwa kawaida mimi ni mutu mwenye haya sana. Wakati fulani ninapaswa kujikaza sana kuzungumuza na ndugu na dada katika kutaniko langu la mupya. Ninatafuta mutu mwenye kukaa yeye mwenyewe katika Jumba la Ufalme, mwenye haiko anazungumuza na mutu yeyote. Mutu huyo anaweza kuwa mutu mwenye haya kama mimi.” Unaweza kujiwekea muradi wa kuzungumuza na mutu mumoja mbele ao kisha mikutano.

Kwa upande mwingine, unaweza kuwa na furaha ya kukutana na wapya kwa majuma kidogo ya kwanza-kwanza. Lakini hali ya kujisikia kuwa wa mupya inaweza kupunguka kadiri wakati unapita. Wakati huo, unapaswa kujikaza sana ili kuendelea kufanya marafiki wapya.

Miti yenye kuongolewa inakuwa katika hali ngumu, lakini wakati inapandwa tena nafasi ingine, inatoa mizizi ya mupya

UJIPATIE WAKATI WA KUZOEA

Miti fulani inakamata wakati murefu ili ikuwe na mizizi yenye kukaza kabisa katika eneo la mupya. Vilevile, watu fulani wako na lazima ya kipindi fulani cha wakati ili wazoee kutaniko la mupya. Ikiwa umehama kumepita wakati fulani lakini ni vigumu kwako kuzoea, kutumikisha kanuni hizi za Biblia kunaweza kukusaidia:

‘Na tusife moyo katika kufanya yaliyo mema, kwa maana katika majira yanayofaa tutavuna ikiwa hatuchoke kabisa.’​Gal. 6:9.

Ujipatie wakati zaidi ili kuzoea kuliko namna uliwazia. Kwa mufano, wamisionere wengi wenye wamepata mazoezi kwenye Masomo ya Gileadi wanabakia miaka fulani katika migawo yao katika inchi zingine mbele ya kuenda kutembelea tena inchi zao. Kufanya hivyo kunawasaidia wazoee ndugu na dada na kuzoea desturi ya mupya.

Alejandro, mwenye amehama mara nyingi, anajua kuwa kuzoea haiko hatua ya kufanya haraka-haraka. Anasema hivi: “Kisha kuhama kwetu kwa mara ya mwisho, bibi yangu alisema hivi: ‘Marafiki wangu wote wako katika kutaniko letu la zamani!’” Alimukumbusha kuwa alikuwa amesema maneno hayohayo tena miaka mbili yenye ilikuwa imepita, kisha kuhama kwao mara ingine. Lakini kwa muda wa miaka mbili, alionyesha kuwa anahangaikia wengine na watu wenye hakukuwa anajua zamani wakakuwa marafiki wake wa sana.

“Usiseme: ‘Kwa nini siku za zamani zilikuwa bora kuliko hizi?’ kwa maana haukuuliza hilo kwa hekima.”​Mhu. 7:10.

Uepuke kulinganisha kutaniko lako la mupya na kutaniko lako la zamani. Kwa mufano, ndugu na dada wa kutaniko lako la mupya wanaweza kuwa watu wa kimya-kimya ao wenye kuzungumuza sana kuliko namna unazoea. Ukaze akili yako juu ya sifa zao za muzuri, kama vile tu unapenda wakufanyie. Watu fulani wenye kuhamia katika kutaniko lingine wanafikia kushangaa wakati wanaelewa kwamba kuhama kwao kumewalazimisha kujiuliza hivi: ‘Ninapenda kabisa “ushirika muzima wa akina ndugu”?’​—1 Pet. 2:17.

‘Muendelee kuomba, nanyi mutapewa.’​Lu. 11:9.

Uendelee kuomba musaada katika sala. Muzee mumoja wenye kuitwa David alisema hivi: “Usitegemee uwezo wako mwenyewe katika hali hiyo. Tunaweza kufanya mambo mengi kwa musaada wa Yehova tu. Usali kwa ajili ya jambo hilo!” Rachel, mwenye tulizungumuzia mwanzoni, anakubaliana na jambo hilo. Alisema hivi: “Wakati mimi na bwana yangu tunajisikia kwa kadiri fulani kuwa hatuko sehemu ya kutaniko, tunasali hivi kwa Yehova juu ya jambo hilo, ‘Tafazali utusaidie kujua ikiwa tuko tunafanya jambo fulani lenye liko linazuia wengine kutukaribia.’ Kisha tunajikaza kupitisha wakati mwingi zaidi pamoja na ndugu na dada.”

Wazazi, ikiwa watoto wenu wanapambana na tatizo la kuzoea kutaniko la mupya, mukamate wakati wa kusali pamoja nao kwa ajili ya jambo hilo. Muwasaidie wafanye marafiki wapya kwa kutokeza nafasi za kufanya urafiki wenye kujenga.

SAIDIA WAPYA WAJISIKIE KUWA WANAKARIBISHWA

Unaweza kufanya nini ili kusaidia wapya wenye wamehamia katika kutaniko lenu? Ujikaze kuwa rafiki wa kweli tangu mwanzo. Ili kufanya hivyo, ujikaze kuwazia ni mambo gani yenye ungependa wakufanyie ikiwa wewe ndiye ulikuwa mugeni, na kisha uwafanyie mambo hayo. (Mt. 7:12) Unaweza kualika wapya wajiunge na ninyi kwenye ibada ya familia ao kuangalia programu ya kila mwezi ya JW Télédiffusion? Unaweza kuwaalika waende pamoja na wewe katika mahubiri? Ikiwa unawaalika ili kula chakula pamoja nao, hawatasahau ukaribishaji wako. Ni mambo gani mengi yenye kufaa yenye unaweza kufanyia wapya?

Carlos anasema hivi: “Wakati tulifika katika kutaniko letu la mupya, dada fulani alitupatia liste ya duka zenye kuwa na vitu vya bei chini. Hilo lilitusaidia sana.” Wale yenye kufika kutoka katika maeneo yenye kuwa na hali ingine ya hewa wanaweza kuwa wenye shukrani ikiwa munawaonyesha namna ya kuvaa katika kipindi cha joto, baridi ao wakati wa mvua. Unaweza pia kuwasaidia kupata matokeo ya muzuri katika kazi ya kuhubiri kwa kuwaelezea historia ya watu wenye kuishi katika eneo ao kwa kuwaelezea mafundisho ya dini yenye wanaamini.

KUZOEA KUNALETA MATOKEO YA MUZURI

Allen, mwenye tulizungumuzia mwanzoni, amekuwa katika kutaniko la mupya kwa zaidi ya mwaka moja. Anasema hivi: “Mwanzoni, nilipaswa kujikaza sana ili kujua ndugu na dada. Lakini sasa wako kama familia yangu, na niko mwenye furaha.” Allen anaelewa kuwa kuhama kwake hakukufanya apoteze rafiki yeyote. Lakini, alipata marafiki wapya, wenye pengine wataendelea kuwa marafiki wake katika maisha yake yote.

^ fu. 2 Majina fulani yamebadilishwa.