Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Wakristo wenye kuoana wanaweza kuona ufundi wa kuweka chombo fulani katika tumbo la uzazi kuwa njia yenye kupatana na Maandiko ya kuzuia kupata mimba?

Kuhusu jambo hilo, bwana na bibi Wakristo wanapaswa kufikiria muzuri mambo mbalimbali na kanuni za Biblia. Kisha wanapaswa kufanya uamuzi wenye utawasaidia waendelee kuwa na zamiri safi mbele ya Mungu.

Zamani, wakati kulikuwa tu wanadamu wawili katika dunia (na kisha Garika wakati kulikuwa watu munane), Yehova alitoa amri hii: ‘Muzae, mukuwe wengi.’ (Mwa. 1:28; 9:1) Biblia haiseme kuwa amri hiyo inahusu Wakristo. Lakini, bibi na bwana Wakristo wanapswa kuamua wao wenyewe ikiwa watatumia njia fulani ya kupanga uzazi ao kuamua ni wakati gani watazaa watoto. Wanapaswa kufikiria mambo gani?

Wakristo wanapaswa kuchunguza kila njia ya kuzuia kupata mimba kwa kutumia kanuni za Biblia. Kwa hiyo, Wakristo wanakataa kabisa kuona kutosha mimba kuwa ni njia ya kupanga uzazi. Kutosha mimba hakupatane kabisa na mambo yenye Biblia inasema juu ya kuheshimia uzima. Wakristo hawapaswe kuua uzima wenye kisha wakati fulani unaweza kuzaliwa na kuwa mwanadamu. (Kut. 20:13; 21:22, 23; Zab. 139:16; Yer. 1:5) Tuseme nini juu kuweka chombo fulani katika tumbo la uzazi ili kuzuia kupata mimba (dispositif intra-utérin ao DIU)?

Jambo hilo lilizungumuziwa katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 5, 1979 (ukurasa wa 30-31). Vyombo vyenye vilitumiwa sana wakati huo vilikuwa vyombo fulani vya plastiki vyenye viliwekwa ndani ya tumbo la uzazi ili kuzuia kupata mimba. Habari hiyo ilionyesha kama haijulikane kabisa-kabisa namna vyombo hivyo vinafanya kazi. Watu wengi wenye kuwa na elimu walisema kuwa vyombo hivyo vilitokeza hali fulani katika tumbo la uzazi na kuzuia shahawa ao mbegu ya mwanaume kuunganishwa na mayai ya mwanamuke ili kutokeza mimba. Ikiwa jambo hilo halifanyike, mimba haiwezi kutokea.

Lakini, ushuhuda fulani ulionyesha kuwa wakati fulani mimba inatokea. Mimba hiyo inaweza kukomalia ndani ya njia ya kuenda kwenye tumbo la uzazi (mimba ya inje ya tumbo la uzazi) ao inaweza kuenda kwenye tumbo la uzazi. Ikiwa inaingia katika tumbo la uzazi, chombo hicho cha kuzuia kupata mimba kinaweza kuzuia mimba kuingia katika sehemu ya ndani ya tumbo la uzazi na kuzuia mimba kukomaa kwa njia ya kawaida. Kuua uzima wenye umeanza kukomaa ni kama kutosha mimba. Habari hiyo ilimalizia hivi: “Mukristo mwenye moyo muzuri mwenye anajiuliza ikiwa inafaa kutumia chombo cha kuweka katika tumbo la uzazi ili kuzuia mimba anapaswa kufikiria kwa uzito habari kama hizo kulingana na mambo yenye Biblia inasema juu ya kuheshimia utakatifu wa uzima.”​—Zab. 36:9.

Kumekuwa maendeleo makubwa katika mambo ya sayansi ao ya matunzo tangu wakati habari hiyo ilichapishwa katika mwaka wa 1979?

Aina mbili ya vyombo vya kuzuia mimba vyenye kuwekwa katika tumbo uzazi vimeanza kutumiwa sana. Aina moja ya vyombo hivyo yenye kuwa na shaba ilianza kutumiwa sana katika Amerika katika mwaka wa 1988. Aina ingine ya vyombo hivyo yenye kuwa na homoni ilianza kutumiwa katika mwaka wa 2001. Ni mafasirio gani yametolewa juu ya namna aina hizo mbili zinatumika?

Shaba: Kama vile tumesema, inaonekana kuwa chombo chenye kuwekwa katika tumbo la uzazi kinafanya ikuwe vigumu kwa shahawa kuweza kupita katika tumbo la uzazi na kufikia yai. Zaidi ya hilo, vyombo vyenye kuwekwa katika tumbo la uzazi vyenye kuwa na shaba, shaba hiyo inaonekana kuwa kama sumu kwa shahawa, inatenda kama kitu chenye kuua shahawa. * Pia inasemekana kuwa vyombo vya kuzuia kupata mimba vyenye kuwa na shaba vinabadilisha sehemu ya ndani ya tumbo la uzazi.

Homoni: Kuko vyombo mbalimbali vya kuzuia kupata mimba vyenye kuwa na homoni kama ile yenye kupatikana katika dawa za kukunywa ili kuzuia mutu kupata mimba. Vyombo hivyo vinaingiza homoni hiyo katika tumbo la uzazi. Inaonekana kuwa vyombo hivyo vinazuia mwanamuke kutokeza mayai. Kwa kweli, ikiwa hakuna yai lenye kutokezwa, mimba haiwezi kutokea. Zaidi ya ufundi huo, inasemekana kuwa homoni yenye kuwa katika vyombo hivyo inapunguza ukubwa wa sehemu ya ndani ya tumbo la uzazi. * Pia inagandisha umajimaji wenye kuwa kwenye mulango wa tumbo la uzazi, na kufanya shahawa ya mwanaume isiende kutoka katika uke mupaka katika tumbo la uzazi. Mambo hayo ni kati ya matokeo yenye kuletwa na vyombo hivyo vyenye kuwekwa ndani ya tumbo la uzazi ili kuzuia kupata mimba.

Kama vile tumeona, inaonekana kuwa aina hizo mbili za vyombo vya kuzuia kupata mimba vinabadilisha sehemu ya ndani ya tumbo la uzazi. Lakini, tuseme nini ikiwa mwanamuke anatoa mayai na mimba inatokea? Inaweza kuingia katika tumbo la uzazi lakini inashindwa kubakia humo kwa sababu haiko tena nafasi ya muzuri. Hilo linaweza kuua mimba yenye ingali kwenye mwanzo. Lakini wanasayansi wanaamini kuwa jambo hilo linatokea mara chache, kama vile linaweza kutokea wakati fulani kwa wale wenye kutumia dawa za kukunywa ili kuzuia kupata mimba.

Kwa hiyo, hakuna mutu mwenye anaweza kusema kwa uhakika kuwa vyombo vyenye kuwekwa katika tumbo la uzazi vyenye kuwa na shaba ao homoni haviwezi hata kidogo kuzuia mutu kupata mimba. Lakini, wanasayansi wanatoa ushuhuda kuwa kwa sababu ya ufundi mbalimbali wenye tumezungumuzia, mimba inatokea mara chache wakati mutu anatumia vyombo kama hivyo.

Bibi na bwana Wakristo wenye wanapenda kutumia chombo cha kuweka katika tumbo la uzazi ili kuzuia kupata mimba, wanapaswa kuzungumuza na munganga mwenye ufundi juu ya vyombo vyenye vinaweza kupatikana katika eneo lao na faida na hatari yenye vinaweza kuleta kwa mwanamuke. Bibi na bwana hawapaswe kuruhusu mutu mwengine, hata munganga, awaamulie jambo lenye wanapaswa kufanya. (Rom. 14:12; Gal. 6:4, 5) Wanapaswa kuchukua uamuzi wao wenyewe. Wanapaswa kuchukua uamuzi wenye kuonyesha kwamba wanapenda kumupendeza Mungu na kwamba wanapenda kuendelea kuwa na zamiri safi mbele yake.​—Linganisha na 1 Timotheo 1:18, 19; 2 Timotheo 1:3.

^ fu. 3 Habari fulani kutoka Huduma ya Afya ya Kitaifa ya Uingereza inaripoti hivi: “Vyombo vya kuweka katika tumbo la uzazi vyenye kuwa na shaba nyingi zaidi vinaleta matokeo ya muzuri zaidi ao asilimia 99 (99%). Hilo linamaanisha kuwa kati ya wanawake 100 wenye kutumia chombo chenye kuwekwa ndani ya tumbo la uzazi, inawezekana karibu mwanamuke mumoja ndiye atapata mimba kwa mwaka mumoja. Vyombo vya kuzuia kupata mimba vyenye kuwa na shaba kidogo havilete matokeo ya muzuri.”

^ fu. 4 Kwa sababu zinapunguza ukubwa wa sehemu ya ndani ya tumbo la uzazi, homoni zenye kuwa katika vyombo hivyo zinapendekezwa kwa wanawake wenye kuolewa ao wenye hawajaolewa ili kumaliza tatizo la kutokwa na damu nyingi sana wakati wa kipindi cha mwezi.