Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Nina Tumaini kwa Mungu”

“Nina Tumaini kwa Mungu”

‘Adamu wa mwisho akakuwa roho inayotoa uhai [uzima].’ ​—1 KOR. 15:45.

NYIMBO: 151147

1-3. (a) Ni fundisho gani lenye kuwa kati ya mambo ya musingi yenye tunaamini? (b) Sababu gani fundisho la ufufuo ni la maana sana? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

IKIWA mutu fulani anakuuliza, ‘Ni mafundisho gani yenye kuwa musingi wa imani yako?’ Utamujibia namna gani? Kwa kweli, utasema kuwa Yehova ni Muumbaji na ni yeye ndiye alitupatia uzima. Inawezekana kabisa kuwa utataja imani yako katika Yesu Kristo, mwenye alikufa ili kuwa zabihu ya ukombozi. Na kwa furaha, unaweza kuongezea kuwa karibuni dunia itakuwa paradiso, nafasi kwenye watu wa Mungu wataishi milele. Lakini, unaweza kutaja ufufuo kuwa moja kati ya mambo yenye unaamini na yenye unapenda zaidi?

2 Tuko na sababu za muzuri za kusema kuwa ufufuo uko kati ya mafundisho yetu ya musingi, hata kama tuko na tumaini la kuokoka ziki kubwa na kuishi milele katika dunia. Mutume Paulo alionyesha sababu gani ufufuo ni wa maana kwa ajili ya imani yetu. Alisema hivi: “Ikiwa, kwa kweli, hakuna ufufuo wa wafu, basi Kristo hakufufuliwa.” Ikiwa Kristo hakufufuliwa, hangekuwa Mufalme wetu mwenye kutawala, na fundisho letu juu ya utawala wa Kristo halingekuwa na maana. (Soma 1 Wakorintho 15:12-19.) Lakini, tunajua kama Yesu alifufuliwa. Kwa sababu tuko na uhakika huo, tuko tofauti na Masadukayo wenye walikataa kabisa kuwa watu wenye kufa wanaweza kufufuliwa. Hata kama watu wanatuchekelea, tunashikamana na imani yetu katika ufufuo.​—Mk. 12:18; Mdo. 4:2, 3; 17:32; 23:6-8.

3 Wakati Paulo aliandika juu ya ‘fundisho la musingi juu ya Kristo,’ alitaja “fundisho juu ya . . . kufufuliwa kwa wafu.” (Ebr. 6:1, 2) Pia, alisema kuwa anaamini kabisa ufufuo. (Mdo. 24:10, 15, 24, 25) Lakini, hata kama ufufuo uko kati ya mafundisho ya musingi, moja kati ya ‘mambo ya musingi ya maneno matakatifu ya Mungu,’ tungali na lazima ya kujifunza kwa uangalifu fundisho hilo. (Ebr. 5:12) Sababu gani?

4. Tunaweza kujiuliza maulizo gani juu ya ufufuo?

4 Wakati watu wanaanza kujifunza Biblia, wengi wanasoma juu ya ufufuo wenye ulifanywa zamani, kama vile ufufuo wa Lazaro. Na wanajifunza kuwa Abrahamu, Ayubu, na Danieli walikuwa hakika kuwa wakati wenye kuja, watu wenye kufa watafufuliwa. Lakini, unaweza kujibia namna gani ikiwa mutu anakuomba ushuhuda wenye kuonyesha kama ahadi ya ufufuo ni ya kweli hata kama kumepita miaka mingi tangu itolewe? Biblia inaonyesha kabisa ni wakati gani ufufuo utafanywa? Majibu ya maulizo hayo yatatia nguvu imani yetu; kwa hiyo, tuone basi mambo yenye Maandiko yanasema.

UFUFUO UNAFANYIKA KISHA MIAKA MINGI

5. Tutazungumuzia nini kwanza?

5 Ni mwepesi kuelewa kwamba mutu mwenye amekufa hivi karibuni anaweza kufufuliwa. (Yoh. 11:11; Mdo. 20:9, 10) Lakini, tuseme nini juu ya ahadi ya kwamba ufufuo utafanyika kisha kupita miaka mingi, ao hata mamia ya miaka wakati wenye kuja? Unaweza kutumainia ahadi hiyo ya muda murefu, iwe ilitolewa juu ya mutu mwenye amekufa hivi karibuni ao mwenye alikufa zamani sana? Kwa kweli, ufufuo ulifanyika hata kama kulikuwa kumepita miaka mingi sana tangu wakati ulitabiriwa, na unaamini ufufuo huo. Namna gani? Na namna gani unahusu tumaini lako juu ya ufufuo wa wakati wenye kuja?

6. Namna gani Zaburi ya 118 ilitimia juu ya Yesu?

6 Kuhusu ufufuo wenye ulitabiriwa zamani sana, tuzungumuzie Zaburi ya 118, yenye watu fulani wanasema kuwa iliandikwa na Daudi. Zaburi hiyo iko na maneno haya ya kuomba musaada: ‘Yehova, utuokoe, tafazali! . . . Abarikiwe Yeye anayekuja katika jina la Yehova.’ Pengine unakumbuka kuwa watu walisema maneno hayo yenye kuzungumuzia Masiya wakati Yesu aliingia Yerusalemu tarehe 9 mwezi wa Nisani, muda mufupi mbele ya kifo chake. (Zab. 118:25, 26; Mt. 21:7-9) Lakini namna gani Zaburi ya 118 ilizungumuzia ufufuo wenye ungetokea kisha miaka mingi wakati wenye kuja? Ona jambo lingine lenye Zaburi hiyo yenye kuwa na unabii ilisema: ‘Jiwe ambalo wajenzi walilikataa limekuwa jiwe kubwa la pembeni.’​—Zab. 118:22.

‘Wajenzi walimukataa’ Masiya (Picha hizi zinapatana na fungu la 7)

7. Namna gani Wayahudi walimukataa Yesu?

7 “Wajenzi,” ni kusema, viongozi Wayahudi, walimukataa Masiya. Zaidi ya kumukataa Yesu, ao kukataa kukubali kuwa yeye ni Kristo walifanya jambo lingine. Wayahudi wengi walimukataa mupaka wakafikia kuomba kabisa auawe. (Lu. 23:18-23) Kwa kweli, waliunga mukono kifo cha Yesu.

Yesu mwenye alifufuliwa iko mbinguni kwenye kiti chake cha ufalme (Picha hii inapatana na fungu la 8, 9)

8. Namna gani Yesu angefikia kuwa ‘jiwe kubwa la pembeni’?

8 Kwa sababu Yesu alikataliwa na kuuawa, namna gani angekuwa ‘jiwe kubwa la pembeni’? Hilo lingetokea tu ikiwa anafufuliwa na kuishi tena. Yesu mwenyewe alionyesha jambo hilo. Alitoa mufano wa walimaji wenye walitesa wale wenye mwenye shamba alituma, kama tu vile Waisraeli walitesa manabii wenye Mungu alituma kwao. Mwishowe, katika mufano huo, mwenye shamba alituma mwana wake mupendwa mwenye alikuwa muriti. Walikubali mwana wake? Hapana kabisa. Walimaji walifikia hata kumuua. Yesu alimalizia mufano huo kwa kusema maneno ya kiunabii yenye kuwa katika Zaburi 118:22. (Lu. 20:9-17) Mutume Petro alizungumuzia pia jambo hilo wakati alikuwa anazungumuza na “watawala . . . na wanaume wazee na waandishi katika Yerusalemu.” Alizungumuzia ‘Yesu Kristo Munazareti, ambaye walimutundika mutini lakini ambaye Mungu alimufufua kutoka kwa wafu.’ Kisha, Petro akasema hivi waziwazi: “Hilo ndilo ‘jiwe ambalo ninyi wajenzi mulilitendea kana kwamba si la maana ambalo limekuwa jiwe kubwa la pembeni.’”​—Mdo. 3:15; 4:5-11; 1 Pet. 2:5-7.

9. Ni tukio gani la pekee lenye lilitabiriwa katika Zaburi 118:22?

9 Kwa kweli, mamia ya miaka mbele ya hapo, maneno ya kiunabii yenye kutajwa katika Zaburi 118:22 yalionyesha kama ufufuo ungetokea. Watu wangekataa Masiya na kumuua, lakini angefufuliwa na kuwa jiwe kubwa la pembeni. Jina la Mwana huyo mwenye alifufuliwa ndilo tu “walilopewa wanadamu ambalo kupitia hilo lazima sisi tupate kuokolewa.”​—Mdo. 4:12; Efe. 1:20.

10. (a) Zaburi 16:10 ilitabiri nini? (b) Sababu gani tunaweza kuwa hakika kuwa Zaburi 16:10 haikutimia juu ya Daudi?

10 Tuzungumuzie andiko lingine lenye lilionyesha kama kutakuwa ufufuo wakati wenye kuja. Liliandikwa zaidi ya miaka elfu moja mbele ya ufufuo huo kufanyika, hilo linapaswa kutusaidia tukuwe hakika kabisa kuwa ufufuo unaweza kufanyika hata kama kumepita muda murefu tangu ulitabiriwa ao kuahidiwa. Katika Zaburi ya 16, yenye iliandikwa na Daudi, tunasoma hivi: ‘Hautaiacha nafsi yangu katika Kaburi. Hautamuruhusu mushikamanifu wako aone shimo.’ (Zab. 16:10) Daudi hakukuwa anasema kama hatakufaka ao hataingiaka katika kaburi kama wanadamu wengine. Neno la Mungu linaonyesha wazi kama Daudi alizeeka. Kisha kufa, ‘alilala pamoja na mababu zake, akazikwa katika Jiji la Daudi.’ (1 Fal. 2:1, 10) Kwa hiyo, Zaburi 16:10 inamaanisha nini?

11. Ni wakati gani Petro alizungumuzia Zaburi 16:10?

11 Mafasirio juu ya andiko hilo yalitolewa. Zaidi ya miaka elfu moja kisha zaburi hiyo kuandikwa na majuma fulani kisha Yesu kufa na kufufuliwa, Petro alizungumuzia Zaburi 16:10 pamoja na maelfu ya Wayahudi na watu wa mataifa wenye walikuwa wamekubali dini ya Wayahudi. (Soma Matendo 2:29-32.) Alisema kwamba, kwa kweli Daudi alikuwa amekufa na kuzikwa. Wale wenye walikuwa wanamusikiliza Petro walijua jambo hilo. Na Biblia haiseme kuwa mutu yeyote kati yao alipinga maneno ya Petro kuwa Daudi “aliona kimbele na kusema kuhusu ufufuo” wa Masiya mwenye angekuja.

12. Zaburi 16:10 ilitimia namna gani, na hilo linahakikisha nini juu ya ahadi ya ufufuo?

12 Petro alikazia maelezo yake kwa kutaja maneno ya Daudi yenye kuwa katika Zaburi 110:1. (Soma Matendo 2:33-36.) Mafasirio ya Petro yenye kupatana na Maandiko yalisadikisha kikundi kikubwa cha watu kuwa Yesu ni “Bwana na pia Kristo.” Zaidi ya hilo, watu walikubali kuwa Zaburi 16:10 ilitimia wakati Yesu alifufuliwa. Kisha, mutume Paulo alitumia mafasirio hayo yenye kusadikisha wakati alikuwa anazungumuza na Wayahudi katika muji wa Antiokia katika Pisidia. Mafasirio yake yaliwagusa sana moyo na walipenda kusikia mengi zaidi. (Soma Matendo 13:32-37, 42.) Sisi pia tunapaswa kuguswa moyo kujua kwamba unabii wa Biblia juu ya ufufuo wa wakati wenye kuja ulitimia kabisa, hata kama kulikuwa kumepita miaka mingi sana tangu muujiza huo utabiriwe.

UFUFUO UTAFANYWA WAKATI GANI?

13. Tunaweza kujiuliza maulizo gani juu ya ufufuo?

13 Tunapaswa kutiwa moyo kujua kwamba ufufuo unaweza kufanyika miaka mingi kisha kuahidiwa. Lakini, mutu anaweza kujiuliza hivi: ‘Hilo linamaanisha kuwa ninapaswa kungojea muda murefu ili nione mupendwa wangu? Ufufuo wenye ninangojea utafanyika wakati gani?’ Kwa kweli, Yesu aliambia mitume wake kwamba kulikuwa mambo yenye hawakujua na yenye hawangejua. Kuko mambo juu ya ‘nyakati ao majira ambayo Baba ameweka katika mamlaka yake mwenyewe.’ (Mdo. 1:6, 7; Yoh. 16:12) Lakini, hilo halimaanishe kuwa hatujue habari yoyote juu ya wakati wenye ufufuo utafanywa.

14. Namna gani ufufuo wa Yesu ulikuwa tofauti na ufufuo wenye ulifanywa mbele yake?

14 Ili kukusaidia kuelewa, kumbuka ufufuo wenye Biblia ilitabiri. Kwa kweli, ufufuo wa maana zaidi ni ule wa Yesu. Ikiwa Yesu hangefufuliwa hakuna mutu mwenye angekuwa na tumaini la kuona tena wapendwa wake wenye wamekufa. Wale wenye walifufuliwa mbele ya Yesu, kama vile wale wenye Eliya na Elisha walifufua, hawakuishi milele. Walikufa tena na miili yao ikaharibika katika kaburi. Lakini, Yesu “amekwisha kufufuliwa kutoka kwa wafu; kifo si bwana juu yake tena.” Huko mbinguni, ‘anaishi milele na milele,’ bila kuona uharibifu hata siku moja.​—Rom. 6:9; Ufu. 1:5, 18; Kol. 1:18; 1 Pet. 3:18.

15. Sababu gani Yesu anaitwa “matunda ya kwanza”?

15 Yesu ndiye alikuwa wa kwanza kufufuliwa ili kuenda mbinguni, bila shaka, ufufuo wake ndio wa maana zaidi. (Mdo. 26:23) Lakini haiko yeye tu ndiye mwenye aliahidiwa ufufuo wa kuenda mbinguni na kuwa kiumbe wa roho. Yesu alihakikishia mitume wake waaminifu kuwa wangetawala pamoja naye mbinguni. (Lu. 22:28-30) Ili wapate zawadi hiyo walipaswa kwanza kufa. Kisha, kama Yesu, wangefufuliwa na mwili wa roho. Paulo aliandika kama “Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo.” Paulo alionyesha pia kwamba kungekuwa wengine wenye wangefufuliwa ili waishi mbinguni, aliongezea hivi: ‘Kila mumoja katika daraja [ao, mupangilio] lake mwenyewe: Kristo aliye matunda ya kwanza, baadaye wale walio wa Kristo wakati wa kuwapo kwake.’​1 Kor. 15:20, 23.

16. Ni nini inatusaidia kujua ni wakati gani wale wa kuenda mbinguni wangeanza kufufuliwa?

16 Hilo linatusaidia kujua ni wakati gani watu wa kuenda mbinguni wangeanza kufufuliwa. Wangeanza kufufuliwa “wakati wa kuwapo kwake.” Kwa muda murefu, Mashahidi wa Yehova wametumia Maandiko ili kuonyesha kwamba kuanzia mwaka wa 1914 tunaishi katika kipindi cha “kuwapo” kwa Yesu chenye aliahidi. Kipindi hicho kingali kinaendelea, na sasa mwisho wa ulimwengu huu muovu uko karibu sana.

17, 18. Ni nini itawapata watiwa-mafuta fulani wakati wa kuwapo kwa Kristo?

17 Biblia inaeleza mambo mengine juu ya ufufuo wa wale wenye watafufuliwa ili kuenda mbinguni. Inasema hivi: ‘Hatutaki mukose kujua kuhusu wale walalao usingizi katika kifo . . . Kwa maana ikiwa imani yetu ni kwamba Yesu alikufa na kufufuliwa tena, vivyo hivyo pia, wale ambao wamelala usingizi katika kifo . . . Sisi tulio hai ambao tutabaki mupaka kuwapo kwa Bwana hatutawatangulia kwa vyovyote wale ambao wamelala usingizi katika kifo; kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni akiwa na mwito wenye amri, . . . na wale walio wafu katika muungano na Kristo watafufuliwa kwanza. Baadaye sisi tulio hai tuliobaki tutanyakuliwa, pamoja nao, katika mawingu ili kukutana na Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana sikuzote.’​—1 Tes. 4:13-17.

18 Ufufuo wa kwanza ungefanyika wakati fulani kisha kipindi cha “kuwapo” kwa Kristo kuanza. Watiwa-mafuta wenye watakuwa wangali wazima wakati wa ziki kubwa ‘watanyakuliwa . . . katika mawingu.’ (Mt. 24:31) Wale wenye ‘watanyakuliwa’ ‘hawatalala usingizi katika kifo,’ ni kusema, hawatabakia kwa muda murefu katika kifo. ‘Wote watabadilishwa kwa muda mufupi, kufumba na kufumbua jicho, wakati wa tarumbeta ya mwisho.’​—1 Kor. 15:51, 52.

19. Ufufuo “ulio bora” ni nini?

19 Leo, Wakristo wengi waaminifu hawako watiwa-mafuta na hawana mualiko wa kuenda kutawala pamoja na Yesu mbinguni. Lakini, wanangojea mwisho wa ulimwengu huu muovu wakati wa “siku ya Yehova.” Hakuna mutu mwenye anaweza kujua kabisa-kabisa ni wakati gani mwisho utakuja, lakini ushuhuda unaonyesha kama mwisho uko karibu. (1 Tes. 5:1-3) Kisha hapo, aina ingine ya ufufuo itafanywa, watu watafufuliwa ili waishi katika dunia paradiso. Wale wenye watafufuliwa watakuwa na tumaini la kufikia kuwa wakamilifu na kuishi milele. Kwa kweli, huo utakuwa “ufufuo ulio bora [ao, muzuri zaidi]” kuliko ule wenye ulifanywa zamani wakati “wanawake waliwapokea wafu wao kwa ufufuo” kisha wakafikia tena kufa wakati fulani.​—Ebr. 11:35.

20. Sababu gani tunaweza kuwa hakika kuwa ufufuo wa wakati wenye kuja utafanywa kwa njia yenye kupangwa muzuri?

20 Kuhusu ufufuo wa watu wa kuenda mbinguni, Biblia inasema kama kila mumoja wao atafufuliwa katika “daraja lake mwenyewe.” (1 Kor. 15:23) Tunaweza kuwa hakika kuwa ufufuo wa watu wenye wataishi katika dunia utafanywa pia kwa njia yenye kupangwa muzuri. Hilo ni tumaini lenye kupendeza sana. Je, wale wenye walikufa hivi karibuni watafufuliwa mwanzoni mwa Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu na kukaribishwa na wapendwa wao wenye wanawajua? Wanaume waaminifu wa zamani wenye kuwa na uwezo wa kuongoza mambo watafufuliwa mbele ili wasaidie kupanga watu wa Mungu katika dunia mupya? Tuseme nini juu ya watu wenye hawakumutumikia Yehova hata kidogo? Watafufuliwa wakati gani na wapi? Tunaweza kujiuliza maulizo mengi. Lakini, kusema kweli, haiko jambo la lazima tufikirie sana maulizo hayo sasa. Ni muzuri zaidi tungojee na kuona namna mambo yatakuwa. Tunaweza kuwa hakika kwamba tutafurahi kujionea namna Yehova atashugulikia mambo hayo.

21. Uko na tumaini gani juu ya ufufuo?

21 Mbele wakati huo ufike, tunapaswa kutia nguvu imani yetu katika Yehova, mwenye alituhakikishia kupitia Yesu kuwa watu wenye kuwa katika kumbukumbu la Mungu watafufuliwa. (Yoh. 5:28, 29; 11:23) Ili kuhakikisha kuwa Yehova iko na uwezo wa kufufua watu wenye kufa, wakati fulani Yesu alisema kama Abrahamu, Isaka, na Yakobo “kwake, hao wote wako hai [ao, wanaishi].” (Lu. 20:37, 38) Lakini kwa sasa, tuko na sababu za muzuri za kuwa na tumaini kama Paulo mwenye alisema hivi: “Nina tumaini kwa Mungu . . . kwamba kutakuwa na ufufuo.”​—Mdo. 24:15.