Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Vijana​—‘Muendelee Kufanyia Kazi Wokovu Wenu Wenyewe’

Vijana​—‘Muendelee Kufanyia Kazi Wokovu Wenu Wenyewe’

‘Kwa jinsi ambavyo mumekuwa mukitii sikuzote, . . . muendelee kufanyia kazi wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.’​—FLP. 2:12.

NYIMBO: 133, 135

1. Sababu gani ubatizo ni hatua ya maana sana? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

KILA mwaka maelfu ya wanafunzi wa Biblia wanabatizwa. Wengi wao ni vijana wenye kuwa kati ya miaka 13 na 19 na wengine wenye wako chini ya miaka hiyo. Pengine wamekomalia katika kweli. Na wewe pia uko kati yao? Ikiwa ni ndiyo, unastahili pongezi. Mukristo anapaswa kubatizwa ili apate wokovu.​—Mt. 28:19, 20; 1 Pet. 3:21.

2. Sababu gani haupaswe kuogopa ao kuepuka kujitoa kwa Yehova?

2 Hata kama ubatizo unaleta baraka nyingi, ni daraka pia. Namna gani? Siku yenye ulibatizwa ulijibia ndiyo kwa ulizo hili: “Kwa musingi wa zabihu ya Yesu Kristo, umetubu zambi zako na kujitoa kwa Yehova katika sala ili kufanya mapenzi yake?” Ubatizo wako unaonyesha kama umejitoa kwa Yehova. Ni ahadi nzito yenye ulitoa kwa Yehova kuwa utamupenda na kutia mapenzi yake pa nafasi ya kwanza. Hiyo ni ahadi nzito. Unapaswa kujuta kwa sababu umetoa ahadi hiyo? Hapana, haupaswe kujuta hata kidogo. Hautajuta hata siku moja kwa sababu umeacha Yehova aongoze maisha yako. Kwa upande mwingine, mutu mwenye hamutumikie Yehova iko chini ya utawala wa Shetani. Shetani hahangaikie wokovu wako. Kwa kweli, anaweza kufurahi ikiwa unapoteza uzima wako wa milele kwa kujiunga naye ili kupinga haki ya Yehova ya kutawala.

3. Kujitoa kwa Yehova kunakuletea baraka gani?

3 Kuliko kumuunga Shetani mukono, fikiria baraka zenye uko nazo kwa sababu umejitoa kwa Yehova na kubatizwa. Kwa sababu sasa umetoa maisha yako kwa Yehova, unaweza kusema hivi kwa uhakika mukubwa kuliko wakati mwingine wowote: ‘Yehova yuko upande wangu; sitaogopa. Mutu wa udongo anaweza kunitenda nini?’ (Zab. 118:6) Hakuna pendeleo lenye kuwa kubwa zaidi kuliko kuwa upande wa Mungu na kukubaliwa naye.

NI DARAKA LA MUTU YEYE MWENYEWE

4, 5. (a) Sababu gani kujitoa kwa Yehova ni daraka la mutu yeye mwenyewe? (b) Ni magumu gani vijana na Wakristo wengine wanapambana nayo?

4 Kwa sababu wewe ni Mukristo mwenye kubatizwa hauwezi kuona urafiki wako pamoja na Yehova kama mali ao shamba la familia lenye unaweza kuriti. Lakini, sasa wokovu wako uko katika mikono yako mwenyewe hata kama ungali unaishi pamoja na wazazi wako. Sababu gani ni jambo la maana kukumbuka hilo? Kwa sababu hauwezi kujua kila mara ni magumu gani yenye utapambana nayo wakati wenye kuja. Ikiwa ulibatizwa wakati ulikuwa chini ya miaka 13, pengine namna unajisikia itabadilika ao utapambana na magumu mapya wakati utakuwa na zaidi ya miaka 13. Kijana mumoja mwanamuke anasema hivi juu ya jambo hilo: “Kwa kawaida mutoto hatachukia kuwa Shahidi kwa sababu tu hakukubali kwenye masomo kipande cha keki wakati wa kukumbuka siku ya kuzaliwa ya mutu fulani. Lakini kisha miaka fulani wakati mukazo wa kufanya ngono unakuwa wenye nguvu, anapaswa kuwa hakika kabisa kuwa kutii sheria za Yehova ni uamuzi wa muzuri zaidi sikuzote.”

5 Kwa kweli, haiko vijana tu ndio wanapambana na magumu ya mupya wakati wanabatizwa. Hata imani ya wale wenye walibatizwa wakiwa watu wazima, inajaribiwa katika njia zenye hawakuwazia. Majaribu hayo yanaweza kuhusu ndoa, matatizo ya afya, ao kazi. Kwa kweli, kila mutu, iwe iko na miaka ngapi, atapambana na hali zenye zitamuomba aonyeshe uaminifu kwa Yehova.​—Yak. 1:12-14.

6. (a) Ahadi ya kumutumikia Yehova hata kutokee nini, maana yake nini? (b) Andiko la Wafilipi 4:11-13 linaweza kukufundisha nini?

6 Ili ubakie muaminifu katika hali yoyote, usisahau hata kidogo kama ulimuahidi Yehova kuwa utamutumikia hata kutokee nini. Hilo linamaanisha kuwa umeambia Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi ya Ulimwengu Wote kuwa utaendelea kumutumikia hata kama rafiki zako ao wazazi wako wanaacha kufanya hivyo. (Zab. 27:10) Katika hali zote, Yehova anaweza kukusaidia kwa kukupatia nguvu ya kutimiza ahadi yako ya kumutumikia.​—Soma Wafilipi 4:11-13.

7. Kufanyia kazi wokovu wako mwenyewe kwa “kuogopa na kutetemeka,” maana yake nini?

7 Yehova anapenda ukuwe rafiki yake. Lakini inaomba kujikaza ili kuendelea kuwa rafiki yake na kufanyia kazi wokovu wako mwenyewe. Kwa kweli Wafilipi 2:12 inasema hivi: ‘Endelea kufanyia kazi wokovu wako mwenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.’ Maneno hayo yanaonyesha kuwa unapaswa kufikiria namna utatia nguvu urafiki wako pamoja na Yehova na kuendelea kuwa muaminifu hata kama unapatwa na magumu gani. Haupaswe kujitumainia kupita mipaka. Hata wamoja kati ya wale wenye wamemutumikia Yehova kwa muda murefu wameacha kuwa waaminifu. Kwa hiyo, unaweza kuchukua hatua gani ili kufanyia kazi wokovu wako mwenyewe?

KUJIFUNZA BIBLIA NI JAMBO LA MAANA

8. Funzo la pekee linatia ndani nini, na sababu gani ni la maana?

8 Ili kuwa na urafiki pamoja na Yehova inaomba kumusikiliza na kuzungumuza naye. Funzo la pekee la Biblia ndiyo njia kubwa ya kumusikiliza Yehova. Hilo linatia ndani kuongeza ujuzi wetu kwa kusoma na kutafakari juu ya Neno la Mungu na vichapo vyetu vyenye kutegemea Biblia. Wakati unafanya hivyo, kumbuka kuwa kujifunza Biblia haiko tu kuweka mambo mengi katika akili. Haipaswe kuwa kama vile unaweka habari nyingi katika akili ili uweze mashindano kwenye masomo. Funzo lenye kuleta faida liko kama matembezi yenye mutu anaweza kufanya ili kuona na kuvumbua mambo ya mupya juu ya utu ao sifa za Yehova. Hilo litakusaidia umukaribie Mungu, kisha naye atakukaribia.​—Yak. 4:8.

Unamusikiliza Yehova na kuzungumuza naye muzuri kabisa? (Picha hizi zinapatana na fungu la 8-11)

9. Ni vyombo gani vyenye vimekusaidia katika funzo lako la pekee?

9 Tengenezo la Yehova limetoa vyombo mbalimbali vya kukusaidia ukuwe na programu ya muzuri ya kujifunza. Kwa mufano, “Mazoezi ya Kujifunza Biblia” yenye kupatikana kwenye sehemu “Vijana” kwenye jw.org, inaweza kukusaidia kujifunza mambo mbalimbali juu ya matukio yenye kuzungumuziwa katika Biblia. Pia, unaweza kupata kwenye jw.org misaada ya kujifunza yenye kichwa, “Biblia Inafundisha Kabisa Nini?” yenye inaweza kukusaidia kutia nguvu imani yako katika mambo yenye unaamini. Misaada hiyo ya kujifunza inaweza kukusaidia kujua namna ya kuelezea wengine mambo yenye unaamini. Unaweza kupata mambo mengine ya kukusaidia kujifunza katika habari yenye kichwa “Vijana Huuliza . . . Ninaweza Kufanya Nini ili Nifurahie Kusoma Biblia?” katika Amuka! ya Mwezi wa 4, 2009. Kujifunza na kutafakari ni mambo ya maana sana ili kufanyia kazi wokovu wako mwenyewe.​—Soma Zaburi 119:105.

SALA NI YA MAANA SANA

10. Sababu gani kusali ni jambo la maana kwa Mukristo mwenye kubatizwa?

10 Wakati tunafanya funzo la pekee tunamusikiliza Yehova, na wakati tunasali tunazungumuza naye. Mukristo hapaswe kuona sala kuwa jambo la desturi tu lenye halina maana ao kama vile ‘hirizi ya bahati’ ya kumusaidia kupata matokeo ya muzuri katika kazi fulani. Lakini, sala ni njia ya kuzungumuza na Muumbaji wetu moja kwa moja. Yehova anapenda kusikiliza sala zako. (Soma Wafilipi 4:6.) Wakati unapambana na mahangaiko yoyote, ufuate shauri hili la Biblia lenye hekima: ‘Mutupie Yehova muzigo wako.’ (Zab. 55:22) Unaamini kabisa jambo hilo? Kuko mamilioni ya ndugu na dada wenye wanaweza kukuhakikishia kuwa jambo hilo limewasaidia. Linaweza kukusaidia wewe pia!

11. Sababu gani unapaswa kumushukuru Yehova sikuzote?

11 Zaidi ya kumuomba tu Yehova akusaidie, sala inakutolea nafasi ya kufanya jambo lingine. Biblia inasema hivi: ‘Mujionyeshe kuwa wenye shukrani.’ (Kol. 3:15) Wakati fulani tunaweza kulemewa ao kuhangaishwa sana na magumu yetu mupaka tunasahau baraka nyingi zenye tuko nazo. Ni muzuri kufikiria kila siku mambo tatu ao zaidi yenye umefurahia, kisha, umushukuru Yehova katika sala juu ya baraka hizo. Abigail mwenye kuwa na miaka 18 mwenye alibatizwa wakati alikuwa na miaka 12, alisema hivi: “Ninafikiri kuwa Yehova anastahili zaidi shukrani yetu kuliko mutu mwingine yeyote katika ulimwengu. Tunapaswa kumushukuru kila wakati kwa ajili ya zawadi zenye ametupatia. Wakati fulani nilisikia shauri hili la muzuri sana: Ikiwa tunaamuka kesho na mambo yenye tulimushukuru Yehova kwa ajili ya leo, tutasema mambo mengine gani?” *

MAMBO YENYE UMEJIONEA NI YA MAANA

12, 13. Sababu gani ni jambo la maana wewe mwenyewe ufikirie namna umeonja wema wa Yehova?

12 Daudi, mufalme wa zamani mwenye Yehova alikomboa kutoka katika majaribu mengi makali, aliimba hivi: ‘Muonje muone ya kuwa Yehova ni mwema; mwenye furaha ni mwanaume ambaye anamukimbilia.’ (Zab. 34:8) Andiko hilo linaonyesha kuwa mambo yenye mutu amekwisha kujionea ni ya maana sana. Wakati unasoma Biblia na vichapo vyetu na wakati unahuzuria mikutano ya Kikristo, unasikia mambo yenye kutia moyo juu ya namna Mungu amesaidia wengine wabakie waaminifu. Lakini wakati unaendelea kukomaa kiroho, unapaswa kuona mukono wa Yehova katika maisha yako mwenyewe. Namna gani wewe mwenyewe umeonja na kuona kuwa Yehova ni mwema?

13 Kuko njia moja yenye Wakristo wote wameonja na kuona kuwa Yehova ni mwema. Mungu amewaalika wamukaribie yeye na Mwana wake. Yesu alisema hivi: ‘Hakuna mutu anayeweza kuja kwangu isipokuwa Baba, aliyenituma, amuvute.’ (Yoh. 6:44) Unaona kuwa maneno hayo yanakuhusu? Kijana anaweza kufikiri hivi, ‘Yehova alivuta wazazi wangu, na mimi niliwafuata tu.’ Lakini wakati ulijitoa kwa Yehova katika sala na kubatizwa, ulionyesha kama umeanzisha urafiki wa pekee pamoja naye. Sasa anakujua kabisa. Biblia inatuhakikishia hivi: ‘Ikiwa yeyote anamupenda Mungu, huyo anajulikana naye.’ (1 Kor. 8:3) Ujikaze kupendezwa, na kufurahia nafasi yako katika tengenezo la Yehova.

14, 15. Namna gani kazi ya kuhubiri inaweza kukusaidia kutia nguvu imani yako?

14 Njia ingine yenye unaweza kuonja wema wa Yehova ni kwa kuona namna anakutegemeza wakati unaelezea wengine mambo yenye unaamini. Unaweza kufanya hivyo wakati uko katika kazi ya kuhubiri ao kwenye masomo. Vijana fulani wanaona kuwa ni vigumu kuhubiria wanafunzi wenzao kwenye masomo. Pengine unaweza kuelewa ni kwa sababu gani. Haujue watatenda namna gani. Inaweza kuwa vigumu zaidi kuzungumuza na kikundi cha wanafunzi kuliko kuzungumuza na mwanafunzi mumoja-mumoja. Ni nini inaweza kukusaidia?

15 Kwanza, fikiria sababu gani unasadiki mambo yenye unaamini. Misaada ya kusaidia kujifunza yenye kuwa kwenye jw.org inapatikana katika luga yako? Ikiwa hauko hakika, ukamate wakati wa kuitafuta. Sehemu hiyo imetayarishwa ili kukusaidia kufikiria mambo yenye unaamini, sababu gani unayaamini, na namna gani unaweza kuelezea wengine mambo yenye unaamini. Wakati uko na imani yenye nguvu na umejitayarisha muzuri, utakuwa tayari kutoa ushahidi kwa ajili ya jina la Yehova.​—Yer. 20:8, 9.

16. Ni nini inaweza kukusaidia usisite kuzungumuza na wengine juu ya mambo yenye unaamini?

16 Lakini, hata kama umejitayarisha unaweza kusita kuzungumuza na wengine juu ya mambo yenye unaamini. Dada mumoja mwenye kuwa na miaka 18 mwenye alibatizwa wakati alikuwa na miaka 13, anasema hivi: “Ninajua mambo yenye ninaamini, lakini wakati fulani ni vigumu kwangu kusema mawazo yangu.” Anafanya nini ili kumaliza tatizo hilo? Anasema hivi: “Ninajikaza kuzungumuza kwa njia ya kawaida. Wanafunzi wenzangu wanajisikia huru kuzungumuza juu ya mambo yenye wanafanya. Mimi pia ninapaswa kujisikia huru kufanya hivyo. Kwa hiyo, ninasema tu jambo moja kama vile, ‘Siku moja nilikuwa ninafundisha watu Biblia, na . . .’ Kisha ninaendelea kuzungumuzia habari yangu. Hata kama jambo lenye ninazungumuzia halihusu moja kwa moja Biblia, mara nyingi wengine wanataka kujua mambo yenye ninafanya wakati ninafundisha watu Biblia. Wakati fulani wanauliza maulizo juu ya jambo hilo. Kadiri ninaendelea kutumikisha njia hiyo, inakuwa mwepesi zaidi. Na kisha, kila mara ninajisikia kuwa na furaha!”

17. Ni mambo gani mengine yanaweza kukusaidia kuzungumuza na wengine?

17 Wakati unaheshimia wengine na kuonyesha kuwa unawapenda, inawezekana kabisa kuwa watakuwa tayari kukusikiliza. Olivia mwenye kuwa na miaka 17 na mwenye alibatizwa wakati alikuwa hajaeneza miaka 13, anasema hivi: “Niliogopa sikuzote kuwa ikiwa ninataja Biblia katika mazungumuzo, watu wataniona kuwa mutu mwenye kutetea mawazo ya dini fulani.” Kisha alianza kuwa na mawazo yenye kuwa tofauti. Kuliko kufikiria sana woga wake, Olivia alifikiri hivi: “Vijana wengi hawajue jambo lolote juu ya Mashahidi wa Yehova. Sisi tu ndio Mashahidi wenye wanaweza kuzungumuza nao. Kwa hiyo, namna tunatenda inaweza kuwa na matokeo juu ya namna wataitikia. Watatuona namna gani ikiwa tunasikia haya ao ni vigumu kwetu kuzungumuza juu ya imani yetu, ao ikiwa tunaogopa wakati tunazungumuza? Wanaweza kuona kuwa hatujivunie imani yetu. Wanaweza hata kutujibia mubaya kwa sababu tunaogopa. Hata hivyo, ikiwa tunazungumuza kwa uhuru na kwa uhakika juu ya mambo yenye tunaamini, na kuyazungumuzia kwa ukawaida, inawezekana kabisa kuwa watatuheshimia.”

ENDELEA KUFANYIA KAZI WOKOVU WAKO MWENYEWE

18. Unapaswa kufanya mambo gani ili kufanyia kazi wokovu wako mwenyewe?

18 Kama vile tumeona, kuendelea kufanyia kazi wokovu wako mwenyewe ni daraka nzito. Mambo fulani ya kufanya ni kusoma Neno la Mungu na kutafakari juu ya mambo yenye unasoma, kusali kwa Yehova, na kufikiria namna Yehova amekubariki. Kufanya mambo hayo kutakusaidia ukuwe hakika zaidi kuwa uko na pendeleo la kuwa na urafiki pamoja na Yehova. Na hilo litakuchochea kuzungumuza na wengine juu ya mambo yenye unaamini.​—Soma Zaburi 73:28.

19. Sababu gani ni jambo la maana kufanyia kazi wokovu wako?

19 Yesu alisema hivi: ‘Mutu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe na kuuchukua muti wake wa mateso na kunifuata sikuzote.’ (Mt. 16:24) Ni wazi kwamba kuwa mwanafunzi, kunatia ndani kujitoa kwa Yehova katika sala na kubatizwa; kila Mukristo anapaswa kufanya mambo hayo. Yanakufungulia mulango wa kupata baraka nyingi sasa na uzima wa milele katika ulimwengu mupya wa Mungu. Kwa hiyo, unapaswa kujikaza sana ili kufanyia kazi wokovu wako mwenyewe!

^ fu. 11 Ili kupata mashauri zaidi, ona habari “Vijana Huuliza​—Sababu Gani Ninapaswa Kusali?” na karatasi yake ya mazoezi kwenye jw.org.