Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unakumbuka?

Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu habari za hivi karibuni katika Munara wa Mulinzi? Ikiwa ni hivyo, jaribu kujibu maulizo haya:

Ili kusaidia watoto wao kiroho, sababu gani wazazi wenye kuhamia katika inchi ingine wanapaswa kufikiria sana matatizo ya luga?

Inawezekana kuwa watoto watajifunza luga ya mahali kwenye wanaishi kwenye masomo na katika eneo lao. Inaweza kuwa muzuri mutoto ajue zaidi ya luga moja. Wazazi wanapaswa kufikiria ni wapi vijana wataelewa muzuri zaidi kweli na kufanya maendeleo ya kiroho, ni katika kutaniko lenye kutumia luga ya eneo ao katika kutaniko lenye kutumia luga ya watu wenye walihamia katika inchi ingine. Wazazi Wakristo wanapaswa kutia mahitaji ya kiroho ya watoto wao pa nafasi ya kwanza.​—w17.05, uku. 9-11.

Wakati Yesu aliuliza Petro hivi: “Unanipenda kuliko hawa?” Neno “hawa” linazungumuzia nini? (Yohana 21:15)

Inaonekana kuwa Yesu alikuwa anazungumuzia samaki wenye walikuwa wamewekwa karibu nao na kazi ya kuvua samaki. Kisha Yesu kufa Petro alirudilia kazi yake ya zamani, ni kusema, kazi ya kuvua samaki. Wakristo wanapaswa kufikiria kwa uzito ikiwa kazi ya kimwili inachukua nafasi gani katika mioyo yao.​—w17.05, uku. 22-23.

Sababu gani Abrahamu alimuambia bibi yake aseme kuwa alikuwa dada yake? (Mwa. 12:10-13)

Kwa kweli, Sara alikuwa dada ya Abrahamu mwenye alizaliwa na mwanamuke mwengine. Ikiwa Sara angesema kuwa alikuwa bibi yake, pengine Abrahamu angeuawa na hangetokeza tena uzao wenye Mungu alikuwa amemuahidi.​—wp17.3, uku. 14-15.

Ni ufundi gani wenye Elias Hutter alianzisha ili kusaidia wale wenye kupenda kujifunza Kiebrania?

Alipenda kusaidia wanafunzi wajue tofauti kati ya musingi wa maneno ya Kiebrania yenye kutumiwa katika Biblia na viambishi (préfixes et suffixes) vyovyote vyenye kutumiwa. Aliandika sehemu ya musingi ya maneno kwa kutumia herufi nzito lakini alitumia herufi zenye haziko nzito kwa ajili ya viambishi. Les Saintes Écritures. Traduction du monde nouveau (avec notes et références) inatumia njia kama hiyo katika maelezo ya chini.​—wp17.4, uku. 11-12.

Mukristo anapaswa kufikiria mambo gani juu ya kuwa na silaha ya kutumia risasi ili kujilinda kutokana wanadamu wengine?

Ona mambo fulani: Mungu anaona uzima kuwa takatifu. Yesu hakuomba wanafunzi wake wakuwe na mipanga ili kujilinda. (Luka 22:36, 38) Tunapaswa kugeuza mipanga yetu kuwa majembe. Uzima ni wa maana sana kuliko vitu vya kimwili. Tunaheshimia zamiri za wengine, na tunapenda kuonyesha mufano muzuri. (2 Kor. 4:2)​—w17.07, uku. 31-32.

Sababu gani habari ya Mathayo na ya Luka juu ya maisha ya Yesu ya wakati alikuwa mutoto zinatofautiana?

Mathayo anazungumuzia sana Yosefu, kama vile namna alitenda wakati alisikia kuwa Maria iko na mimba na ujumbe kutoka kwa Mungu wa kumuomba akimbilie Misri na kisha arudie. Luka yeye anazungumuzia sana Maria; kwa mufano, namna alimutembelea Elizabethi na namna alitenda wakati kijana Yesu alibakia kwenye hekalu.​—w17.08, uku. 32.

Biblia imeendelea kudumu hata kama kulikuwa matatizo gani?

Maana ya maneno na misemo yenye kutumiwa katika Biblia imebadilika kadiri wakati inapita. Mabadiliko katika mambo ya politike yamekuwa na matokeo juu ya luga ya watu wa kawaida. Kazi ya kutafsiri Biblia katika luga za watu wa kawaida imepingwa.​—w17.09, uku. 19-21.

Tuko na malaika mulinzi?

Hapana. Yesu alikuwa anazungumuzia malaika wa wanafunzi wake wenye kuangalia uso wa Mungu. (Mt. 18:10) Yesu alikuwa akisema tu kwamba malaika wanapendezwa sana na wanafunzi wake, lakini hakumaanisha kuwa malaika wanalinda kwa njia ya muujiza kila mumoja wao.​—wp17.5, uku. 5.

Ni aina gani ya upendo yenye kuwa ya hali ya juu zaidi?

Wakati inategemea kanuni zenye kufaa, a.gaʹpe ni aina ya upendo yenye kuwa ya hali juu zaidi. Inaweza kutia ndani, kuhangaikia wengine na kuwachangamukia. Lakini unaonyesha kanuni za hali ya juu, kama vile matendo mazuri yenye tunafanyia wengine bila uchoyo.​—w17.10, uku. 7.