Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Endelea Kukomaa Kiroho!

Endelea Kukomaa Kiroho!

‘Muendelee kutembea kwa roho.’​—GAL. 5:16.

NYIMBO: 22, 75

1, 2. Ndugu mumoja alitambua nini juu ya hali yake ya kiroho, na alifanya nini juu ya jambo hilo?

ROBERT alibatizwa wakati alikuwa angali kijana, lakini hakukamata kabisa kweli kwa uzito. Anasema hivi: “Sikufanya hata kosa moja, lakini sikuchukua mambo kwa uzito. Nilionekana kuwa mutu wa kiroho, nilihuzuria mikutano yote, na kufanya upainia musaidizi kwa miezi fulani katika mwaka. Lakini, nilikuwa ninakosa kitu fulani.”

2 Robert hakuelewa alikuwa na shida gani mupaka wakati alioa. Yeye na bibi yake walikuwa wanatumia wakati fulani ili kuulizana maulizo juu ya habari za Biblia. Bibi yake, mwenye alikuwa nguvu kiroho, hakukuwa na matatizo ya kujibia maulizo hayo, lakini mara nyingi Robert alisikia haya kwa sababu hakujua mambo ya kusema. Anasema hivi: “Ilikuwa kama vile sikujua jambo lolote. Niliwaza hivi, ‘Ili nikuwe kichwa cha kiroho cha bibi yangu, ninapaswa kufanya jambo fulani.’” Na Robert alifanya hivyo. Anasema hivi: “Nilijifunza Biblia na nikajifunza zaidi na zaidi, na nikaanza kuelewa mambo muzuri zaidi. Nilipata ujuzi, na jambo la maana zaidi, nikakuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova.”

3. (a) Mufano wa Robert unaweza kutufundisha nini? (b) Tutazungumuzia mambo gani matatu ya maana?

3 Mufano wa Robert unaweza kutufundisha mambo ya maana. Tunaweza kuwa na ujuzi fulani wa Biblia na pengine tunahuzuria kwa ukawaida mikutano ya kutaniko, lakini mambo hayo tu hayatufanye kuwa watu wa kiroho. Ao pengine tayari tumefanya maendeleo, lakini wakati tunajichunguza zaidi, tunatambua kama tungali tunaweza kufanya maendeleo ya kiroho. (Flp. 3:16) Ili kutusaidia kuendelea kukomaa kiroho, tutajibia maulizo matatu katika habari hii: (1) Ni nini itatusaidia kuchunguza kabisa hali yetu ya kiroho? (2) Namna gani tunaweza kukomaa kiroho na kuendelea kuwa watu wa kiroho? (3) Namna gani kuwa nguvu kiroho kunatusaidia katika maisha yetu ya kila siku?

UJICHUNGUZE MWENYEWE

4. Shauri lenye kupatikana katika Waefeso 4:23, 24 linahusu nani?

4 Wakati tulijitoa kwa Mungu, tulifanya mabadiliko. Mabadiliko hayo yaligusa hali zote za maisha yetu. Na tuliendelea kufanya mabadiliko hata kisha kubatizwa. Biblia inatuambia kama tuendelee ‘kufanywa upya katika nguvu zinazoendesha akili [yetu].’ (Efe. 4:23, 24) Kwa sababu hatukamilike, sisi wote tunapaswa kuendelea kufanya mabadiliko. Hata wale wenye wamemutumikia Yehova kwa muda murefu wanapaswa kuendelea kukomaa kiroho.​— Flp. 3:12, 13.

5. Ni maulizo gani yanaweza kutusaidia tujichunguze?

5 Ili kukomalisha hali yetu ya kiroho na kuendelea kuwa mutu wa kiroho, tunapaswa kujichunguza kabisa. Iwe tuko vijana ao wazee, tunaweza kujiuliza maulizo haya: ‘Ninaona mabadiliko yenye kuonyesha kama ninafanya maendeleo ya kiroho? Ninajikaza kuiga sifa za Kristo? Mawazo yangu na namna ninajiendesha kwenye mikutano ya Kikristo, vinaonyesha kuwa nimekomaa kiroho? Mazungumuzo yangu yanaonyesha nini juu ya tamaa zangu? Namna yangu ya kujifunza, namna yangu ya kuvaa na kujipamba, ao namna ninatenda wakati ninapewa mashauri vinaonyesha nini juu yangu? Ninatenda namna gani wakati ninapambana na majaribu? Nimefanya maendeleo na kufikia kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho kabisa?’ (Efe. 4:13) Kufikiri juu ya majibu ya maulizo hayo kunaweza kutusaidia tuchunguze ikiwa tumefanya maendeleo ya kiroho kwa kadiri gani.

6. Ili kuchunguza hali yetu ya kiroho, tunapaswa kufanya jambo gani lingine?

6 Ili kuchunguza hali yetu ya kiroho, wakati fulani tunaweza kuwa na lazima ya musaada wa wengine. Mutume Paulo alionyesha kama mutu wa kimwili hawezi kuelewa kama mwenendo wake wa mubaya unamuchukiza Mungu. Lakini, mutu wa kiroho anaelewa mawazo ya Mungu na anajua kama Yehova hapendi watu wenye wanakazia mambo ya mwili katika maisha yao. (1 Kor. 2:14-16; 3:1-3) Kwa sababu wazee wako na akili ya Kristo, mara nyingi wanaona alama zenye kuonyesha kama mutu fulani ameanza kuwa na mawazo ya kimwili. Ikiwa wanatushauria juu ya jambo hilo, tutakubali mashauri yao na kuyatumikisha? Ikiwa tunafanya hivyo, tunaonyesha kama tunapenda kukomaa kiroho.​—Mhu. 7:5, 9.

UKOMALISHE HALI YAKO YA KIROHO

7. Sababu gani haitoshe tu kuwa na ujuzi wa Biblia ili kuwa mutu wa kiroho?

7 Kumbuka kama haitoshe tu kuwa na ujuzi wa Biblia ili kuwa mutu wa kiroho. Mufalme Sulemani alikuwa na ujuzi mwingi juu ya njia za Yehova. Maneno yake yalifikia kuandikwa katika Biblia. Lakini, mwishowe alishindwa kuendelea kuwa mutu wa kiroho na kubakia mwaminifu kwa Yehova. (1 Fal. 4:29, 30; 11:4-6) Kwa hiyo, zaidi ya kuwa na ujuzi wa Biblia, tunapaswa kufanya jambo gani lingine? Tunapaswa kuendelea kukomaa kiroho. (Kol. 2:6, 7) Lakini, namna gani tunaweza kufanya hivyo?

8, 9. (a) Ni nini itatusaidia tukuwe nguvu kiroho? (b) Tunapaswa kuwa na kusudi gani wakati tunajifunza na kutafakari? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

8 Paulo alishauria Wakristo wa kwanza-kwanza ‘wasonge mbele kuelekea ukomavu.’ (Ebr. 6:1) Ili kutumikisha shauri la Paulo, tunapaswa kuchukua hatua gani? Hatua moja ya maana ni kujifunza kitabu Mubaki “Katika Upendo wa Mungu.” Kumaliza kujifunza kitabu hicho kutakusaidia kujua namna ya kutumikisha kanuni za Biblia katika maisha yako. Ikiwa umemaliza kujifunza kitabu hicho, unaweza kujifunza vichapo vingine vyenye vinaweza kukusaidia kutia nguvu imani yako? (Kol. 1:23) Unasali na kutafakari juu ya namna unaweza kutumia katika maisha yako mambo yenye unajifunza?

9 Kumbuka kwamba wakati tunajifunza na kutafakari, kusudi letu linapaswa kuwa kutaka kwa moyo wote kumupendeza Yehova na kutii sheria zake. (Zab. 40:8; 119:97) Na wakati huohuo, tunajikaza kuepuka mambo yenye yanaweza kutuzuia kukomaa kiroho.​—Tito 2:11, 12.

10. Vijana wanaweza kufanya nini ili wakomae kiroho?

10 Ikiwa uko kijana, uko na miradi ya kiroho? Wakati anahuzuria mikusanyiko ya muzunguko, ndugu mumoja mwenye kutumika kwenye Beteli anazoea kuzungumuza na watu wenye watabatizwa, anafanya hivyo mbele programu ianze. Wengi kati yao ni vijana. Ndugu huyo anawauliza ikiwa wako na miradi gani ya kiroho. Wengi wanatoa majibu yenye yanaonyesha kama wanajua muzuri mambo yenye wanapenda kufanya ili kumutumikia Yehova, pengine kwa kufanya utumishi fulani wa wakati wote ao kwa kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme. Lakini, wakati fulani, vijana fulani wanaonekana kuwa hawana jibu. Hilo linaweza kuonyesha kwamba wanaona kama hawana lazima ya kuwa na miradi ya kiroho? Kijana, ujiulize hivi: ‘Ninaenda kwenye mikutano na katika mahubiri kwa sababu tu wazazi wangu wanapenda nifanye hivyo? Ninaendelea kumukaribia Mungu zaidi kwa kuendelea kuwa na urafiki wa sana pamoja naye?’ Kwa kweli, haiko vijana tu ndio wanapaswa kutii shauri la kujiwekea miradi ya kiroho. Kuwa na miradi kama hiyo, kutatusaidia sisi wote, watumishi wa Yehova, kutia nguvu hali yetu ya kiroho.​—Mhu. 12:1, 13.

11. (a) Ili kufanya maendeleo ya kiroho, tunapaswa kufanya nini? (b) Ni mufano gani wa Biblia wenye tunaweza kuiga?

11 Wakati tunatambua mambo mbalimbali yenye tunapaswa kufanyia maendeleo, tunapaswa kukamata hatua zenye kufaa za kutusaidia kufanya maendeleo. Kuwa mutu wa kiroho ni jambo la maana sana. Kwa kweli, uzima wetu unategemea jambo hilo. (Rom. 8:6-8) Hata hivyo, kuwa watu wa kiroho hakumaanishe kama tunakuwa watu wakamilifu. Roho ya Yehova inaweza kutusaidia kufanya maendeleo yenye kuhitajiwa. Lakini, tunapaswa kujikaza kabisa. Wakati alitoa maelezo juu ya andiko la Luka 13:24, Ndugu John Barr, mwenye alitumikia katika Baraza Lenye Kuongoza alisema hivi kumepita miaka fulani: “Wengi wanashindwa kwa sababu hawajikaze sana ili kuwa na nguvu.” Tunapaswa kuwa kama Yakobo, mwenye hakuchoka kupigana na malaika mupaka wakati alipata baraka. (Mwa. 32:26-28) Hata kama tunaweza kufurahia funzo la Biblia, hatupaswe kutazamia kuwa Biblia itakuwa kama kitabu fulani chenye kiliandikwa ili kufurahisha watu. Tunapaswa kujikaza kutafuta mali ya kiroho yenye itatusaidia.

12, 13. (a) Ni nini itatusaidia kutumikisha andiko la Waroma 15:5? (b) Namna gani mufano wa mutume Petro na shauri lake vinaweza kutusaidia? (c) Unaweza kufanya nini ili ukomae kiroho? (Ona kisanduku “ Mambo Yenye Unaweza Kufanya ili Kukomaa Kiroho.”)

12 Wakati tunaendelea kujikaza ili kukomaa kiroho, roho takatifu itatupatia nguvu ya kufanya mabadiliko katika akili yetu. Kwa musaada wa roho takatifu, tunaweza kuanza pole kwa pole kufikiri zaidi na zaidi kama Kristo. (Rom. 15:5) Zaidi ya hilo, itatusaidia kuachana kabisa na tamaa za mwili na kutusaidia kuwa na sifa zenye kumupendeza Mungu. (Gal. 5:16, 22, 23) Ikiwa akili yako inakuchochea kufuatia mambo ya kimwili ao tamaa za kimwili, usivunjike moyo. Uendelee kuomba Mungu roho takatifu, na atakusaidia kuongoza akili yako ili ikazie mambo yenye kufaa. (Lu. 11:13) Kumbuka mutume Petro. Wakati fulani katika maisha yake, hakutenda kama vile mutu wa kiroho anapaswa kutenda. (Mt. 16:22, 23; Lu. 22:34, 54-62; Gal. 2:11-14) Lakini hakuvunjika moyo. Pole kwa pole, Petro alijifunza kufikiri kama Kristo. Sisi pia tunaweza kufanya hivyo.

13 Kisha, Petro alionyesha mambo yenye tunaweza kufanyia maendeleo. (Soma 2 Petro 1:5-8.) Ikiwa tunajikaza sana ili kukomalisha sifa kama vile kujizuia, subira ao uvumilivu, na upendo wa kindugu, hilo litatusaidia kuendelea kukomaa kiroho na kuwa watu wa kiroho. Kila siku, tunaweza kujiuliza hivi, ‘Ninaweza kufanya nini leo ili kufanya maendeleo ya kiroho?’

KUTUMIKISHA KANUNI ZA BIBLIA KATIKA MAISHA YETU YA KILA SIKU

14. Kuwa mutu wa kiroho kutakuwa na matokeo gani juu ya maisha yetu ya kila siku?

14 Kufikiri kama Kristo kutachochea maneno yetu na mwenendo wetu kwenye kazi ao kwenye masomo, na maamuzi yenye tunakamata kila siku. Maamuzi hayo yataonyesha kama tunajikaza kuwa wanafunzi wa Kristo. Kwa sababu tuko watu wa kiroho hatupendi kitu chochote kiharibu urafiki wetu pamoja na Baba yetu wa mbinguni. Wakati tunapambana na majaribu, kuwa na mawazo ya Kristo kutatusaidia kuyapinga kabisa. Mbele ya kukamata maamuzi tutafikiri kwanza juu ya maulizo haya: ‘Ni kanuni gani za Biblia zenye zitanisaidia kuamua? Kristo angefanya nini katika hali hii? Ni uamuzi gani wenye utamupendeza Yehova?’ Ili kujizoeza namna ya kufikiri hivyo, tuzungumuzie mifano fulani. Katika kila mufano, tutaona kanuni ya Maandiko yenye inaweza kutusaidia kukamata uamuzi wenye hekima.

15, 16. Namna gani kuwa na mawazo kama ya Kristo kunaweza kutusaidia wakati tunakamata maamuzi juu ya (a) kuchagua mutu wa kuoana naye? (b) kuchagua marafiki?

15 Wakati tunachagua mutu wa kuoana naye. Kanuni ya Maandiko inapatikana kwenye 2 Wakorintho 6:14, 15. (Soma.) Maneno ya mutume Paulo yanaonyesha wazi kama mutu wa kiroho hawezi kupatana kabisa na mutu wa kimwili. Namna gani tunaweza kutumikisha kanuni hiyo wakati tunachagua mutu wa kuoana naye?

16 Marafiki. Kanuni ya Maandiko inapatikana kwenye 1 Wakorintho 15:33. (Soma.) Mutu mwenye kumuogopa Mungu hatafanya urafiki na watu wenye wanaweza kutia hali yake ya kiroho katika hatari. Ni maulizo gani yenye yanaweza kukusaidia kutumia kanuni hiyo katika maisha yako? Kwa mufano, namna gani inahusu adresi za Internete za kuzungumuza na watu wengi? Ao unapaswa kufanya nini ikiwa watu wenye haujue wanakuomba ucheze nao michezo kwenye Internete?

Maamuzi yangu yatanisaidia kukomaa kiroho? (Picha hizi zinapatana na fungu la 17)

17-19. Namna gani kuwa watu wa kiroho kutatusaidia (a)  kuepuka matendo yenye hayana maana? (b)  kujiwekea miradi katika maisha? (c)  kushugulikia matatizo ya kukosa kuelewana?

17 Mambo yenye kuzuia mutu kukomaa kiroho. Maneno yenye Paulo aliandikia Wakristo wenzake yanatoa onyo fulani. (Soma Waebrania 6:1.) Ni “matendo [gani] yaliyokufa” yenye tunapaswa kuepuka? Matendo yoyote yenye hayatusaidie kuwa nguvu kiroho. Kanuni hiyo inaweza kutusaidia kupata majibu na maulizo mengi yenye yanaweza kutokea katika maisha yetu, kama vile: ‘Jambo hili liko kati ya matendo ya mwili? Nijiingize katika mipango hii ya kutafuta feza? Sababu gani sipaswe kujiunga na vikundi vya watu wa ulimwengu wenye kupenda mabadiliko?’

Maamuzi yangu yatanisaidia kujiwekea miradi ya kiroho? (Picha hizi zinapatana na fungu la 18)

18 Miradi ya kiroho. Maneno yenye Yesu alisema katika Mahubiri yake ya Mulimani yanatupatia muongozo wenye kuwa wazi juu ya kujiwekea miradi ya kiroho. (Mt. 6:33) Mutu wa kiroho anafuatia miradi yenye kukazia mambo ya kiroho. Kukumbuka kanuni hiyo kunatusaidia kujibia maulizo kama vile: ‘Ninapaswa kufuatia masomo ya juu? Ninapaswa kukubali kazi fulani?’

Maamuzi yangu yatanisaidia kufanya amani? (Picha hizi zinapatana na fungu la 19)

19 Kukosa kuelewana. Namna gani shauri la Paulo kwa kutaniko la Roma linatusaidia kushugulikia matatizo ya kukosa kuelewana? (Rom. 12:18) Kwa sababu tuko wanafunzi wa Kristo, tunajikaza kuwa “wenye kufanya amani na watu wote.” Wakati matatizo ya kukosa kuelewana yanatokea, tunatenda namna gani? Tunaona kuwa ni vigumu kuachilia mambo, ao tunajulikana kuwa watu wenye ‘kufanya amani’?​—Yak. 3:18.

20. Sababu gani unapenda kukomaa kiroho?

20 Hiyo ni mifano kidogo tu yenye kuonyesha namna kufikiri juu ya kanuni za Mungu kunaweza kutusaidia kukamata maamuzi yenye mutu wa kiroho anapaswa kukamata. Kuwa watu wa kiroho kunaweza kutusaidia kufanya maisha yetu ya kila siku yakuwe yenye furaha na yenye kutosheka zaidi. Robert, mwenye tulizungumuzia kwenye mwanzo wa habari hii anasema hivi: “Kisha kuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova, nikakuwa bwana na baba muzuri zaidi. Nikakuwa mwenye kutosheka na mwenye furaha.” Tunaweza kupata baraka kama hizo ikiwa tunafanya maendeleo ya kiroho kuwa jambo la maana zaidi katika maisha yetu. Kama tuko watu wa kiroho, tutakuwa na maisha yenye furaha zaidi leo, na wakati wenye kuja, “uzima ulio wa kweli.”​—1 Tim. 6:19.