Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uige Imani na Utii wa Noa, Danieli, na Ayubu

Uige Imani na Utii wa Noa, Danieli, na Ayubu

“Noa, Danieli na Ayubu, wao wenyewe kwa sababu ya uadilifu wao wangeikomboa nafsi yao.”​—EZE. 14:14.

NYIMBO: 89, 119

1, 2. (a) Sababu gani mufano wa Noa, Danieli, na Ayubu unaweza kututia moyo? (b) Hali ilikuwa namna gani wakati Ezekieli aliandika maneno yenye kuwa katika Ezekieli 14:14?

UNAPAMBANA na magumu kama vile magonjwa, matatizo ya kupata feza, ao mateso? Wakati fulani unaona kuwa ni vigumu kwako kuendelea kuwa na furaha katika utumishi wa Yehova? Kama ni ndiyo, mufano wa Noa, Danieli, na Ayubu unaweza kukutia moyo. Hawakukuwa wakamilifu, na walipambana na magumu mengi yenye tunapata leo, na hata magumu fulani yenye yalitia uzima wao katika hatari. Lakini, waliendelea kuwa washikamanifu, na Mungu akaona kuwa walikuwa mufano muzuri wa imani na utii.​—Soma Ezekieli 14:12-14.

2 Ezekieli aliandika maneno ya andiko letu la musingi katika Babiloni, mwaka wa 612 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. * (Eze. 1:1; 8:1) Uharibifu wenye ulikuwa umetabiriwa juu ya muji wa Yerusalemu wenye kuasi, ulikuwa umekaribia, na ulitokea katika mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Ni hesabu kidogo tu ya watu ndio walionyesha sifa kama za Noa, Danieli, na Ayubu, na kwa hiyo walitiwa alama ili kuokolewa. (Eze. 9:1-5) Kati ya watu hao kulikuwa Yeremia, Baruku, Ebed-meleki, na Warekabu.

3. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

3 Leo pia, wale tu wenye Yehova anaona kuwa watu wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa kama Noa, Danieli, na Ayubu, ndio watatiwa alama ili kuokolewa wakati ataharibu ulimwengu huu muovu. (Ufu. 7:9, 14) Tuzungumuzie basi sababu gani Yehova alitumia wanaume hao kuwa mufano wa uadilifu ao wa wale wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa. Wakati tutazungumuzia kila mumoja wao, tutakazia (1) magumu yenye alipambana nayo na (2) namna tunaweza kuiga imani na utii wake.

NOA​—MUAMINIFU NA MWENYE KUTII KWA MIAKA 900

4, 5. Noa alipambana na magumu gani, na sababu gani uvumilivu wake ulikuwa wa pekee?

4 Magumu yenye Noa alipambana nayo. Kufikia wakati wa Enoko, baba ya tate (nkambo) ya Noa, watu walikuwa wamekuwa wabaya sana. Walikuwa hata wanasema “mambo yote ya kushtua” juu ya Yehova. (Yuda 14, 15) Jeuri iliendelea kuongezeka. Kwa kweli, katika siku za Noa, ‘dunia [ilikuwa] imejaa jeuri.’ Malaika wabaya walivaa miili ya wanadamu, wakachukua wanawake, na kuzaa watoto wenye jeuri wenye hawakukuwa wa kawaida. (Mwa. 6:2-4, 11, 12) Lakini, Noa alikuwa tofauti kabisa. ‘Noa alipata kibali machoni pa Yehova. . . . Alionekana kuwa mutu asiye na kosa kati ya watu wa siku zake. Noa alitembea pamoja na Mungu wa kweli.’​—Mwa. 6:8, 9.

5 Maneno hayo yanaonyesha nini juu ya Noa? Kwanza, fikiria muda wenye Noa alimutumikia Mungu kwa uaminifu katika ulimwengu muovu mbele ya Garika. Haiko kwa miaka 70 ao 80 tu, miaka yenye watu wengi wanaishi leo, lakini kwa miaka 600 hivi! (Mwa. 7:11) Tofauti na sisi leo, hakukuwa na kutaniko la waabudu wenzake, inaonekana kama, hata ndugu zake hawakumutegemeza kiroho. *

6. Ni katika njia gani mbalimbali Noa alionyesha ujasiri mukubwa?

6 Noa hakufikiri kuwa inatosha tu kuwa mutu muzuri. Alikuwa pia ‘muhubiri wa uadilifu’ mwenye ujasiri, alielezea wengine imani yake katika Yehova. (2 Pet. 2:5) Mutume Paulo aliandika hivi: “Kupitia imani hiyo aliuhukumu ulimwengu.” (Ebr. 11:7) Kwa hiyo, inawezekana kabisa kwamba watu walimucheka Noa na kumupinga, na hata pengine walitaka kumutendea mubaya. Hata hivyo, ‘hakutetemeshwa na wanadamu.’ (Met. 29:25) Lakini, alikuwa na ujasiri wenye Yehova anapatia watumishi wake waaminifu.

7. Wakati Noa alikuwa anajenga safina, alipambana na magumu gani?

7 Kisha Noa kutembea pamoja na Mungu kwa zaidi ya miaka 500, Yehova alimuambia ajenge safina ili kuokoa uzima wa wanadamu na wa wanyama. (Mwa. 5:32; 6:14) Pengine Noa aliona kama kazi hiyo ya kujenga ilikuwa ya nguvu sana! Kwa kweli, Noa alijua kama kazi hiyo ingefanya watu wamucheke na kumupinga zaidi. Lakini, aliendelea kuonyesha imani na kumutii Yehova. “Alifanya vivyo hivyo.”​—Mwa. 6:22.

8. Namna gani Noa alimutumainia Yehova kuwa atamutimizia mahitaji yake na ya watu wa familia yake?

8 Noa alikuwa na magumu mengine. Alipaswa kutimizia bibi yake na watoto wake mahitaji yao ya kimwili. Mbele ya Garika, watu walipaswa kutumika sana ili kukomalisha chakula, na Noa pia alipaswa kufanya hivyo. (Mwa. 5:28, 29) Lakini, katika maisha yake alitia Mungu pa nafasi ya kwanza, kuliko kuhangaikia mambo ya kimwili. Hata wakati alikuwa anafanya kazi ya kujenga safina, yenye pengine ilifanya miaka 40 ao 50, Noa aliendelea kuweka mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza. Na aliendelea kufanya hivyo kwa miaka ingine 350 kisha Garika. (Mwa. 9:28) Noa ni mufano muzuri kabisa wa imani na utii!

9, 10. (a) Namna gani tunaweza kuiga imani na utii wa Noa? (b) Namna gani Mungu anaona wale wote wenye kuunga mukono kanuni zake?

9 Namna gani tunaweza kuiga imani na utii wa Noa? Tunaweza kufanya hivyo kwa kuunga mukono mawazo ya Yehova juu ya mambo yenye kuwa sawa, kuepuka kuwa sehemu ya ulimwengu wa Shetani, na kwa kuendelea kutia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza. (Mt. 6:33; Yoh. 15:19) Kwa kweli, namna tunaishi inafanya ulimwengu utuchukie. Hata leo katika inchi fulani, watu wanaeneza habari za mubaya juu yetu kwa sababu tunajikaza sana kutii sheria za Mungu juu ya mambo kama vile ndoa na mwenendo muzuri kuhusu mambo ya ngono. (Soma Malaki 3:17, 18.) Lakini, kama Noa, tunamuogopa Yehova, hapana wanadamu. Tunajua kama ni yeye tu ndiye anaweza kutupatia uzima wa milele.​—Lu. 12:4, 5.

10 Halafu wewe? Utaendelea ‘kutembea pamoja na Mungu’ hata wakati watu wengine wanakucheka ao kukuchambua, ao wakati matatizo ya kupata feza yanajaribu imani yako katika uwezo wa Yehova wa kukutimizia mahitaji yako ya kimwili? Ikiwa unaiga imani na utii wa Noa, unaweza kuwa hakika kama Yehova atakuhangaikia.​—Flp. 4:6, 7.

DANIELI​—MUAMINIFU NA MWENYE KUTII KATIKA MUJI MUBAYA

11. Danieli na wenzake watatu walipambana na magumu gani katika Babiloni? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

11 Magumu yenye Danieli alipambana nayo. Danieli aliishi katika uhamisho huko Babiloni, muji wenye ulijaa ibada ya sanamu na mambo ya uchawi. Zaidi ya hilo, Wababiloni walizarau Wayahudi, walikuwa wanawacheka na kucheka Mungu wao, Yehova. (Zab. 137:1, 3) Jambo hilo lilipaswa kuhuzunisha Wayahudi waaminifu kama vile Danieli! Pia watu wengi walikuwa wanaangalia kwa uangalifu Danieli na wenzake watatu, ni kusema, Hanania, Mishaeli, na Azaria, kwa sababu walipaswa kuzoezwa ili wamutumikie mufalme. Waliombwa hata wakule chakula cha mufalme. Kwa kweli, chakula na kinywaji vilifikia kuwa jaribu kwa sababu Danieli hakupenda ‘kujitia unajisi [kujichafua] kwa vyakula vitamu vya mufalme.’​—Dan. 1:5-8, 14-17.

12. (a) Danieli alionyesha sifa gani za muzuri? (b) Yehova alimuona Danieli namna gani?

12 Inawezekana Danieli alikuwa na jaribu lingine. Alikuwa na uwezo mbalimbali na hilo lilifanya apewe mapendeleo fulani ya pekee. (Dan. 1:19, 20) Lakini, kuliko kuwa na kiburi na kufikiri kama mawazo yake yalikuwa sawa sikuzote, aliendelea kuwa munyenyekevu na mwenye kiasi, na alimupatia Yehova utukufu sikuzote. (Dan. 2:30) Kwa kweli, wakati Danieli alikuwa angali kijana, Mungu alionyesha kama anastahili kuwa mufano wa uadilifu kama Noa na Ayubu. Mungu alikuwa na sababu za kumutumainia Danieli? Ndiyo kabisa! Danieli aliendelea kuwa muaminifu na mwenye kutii mupaka mwisho wa maisha yake. Kwa kweli, inawezekana alikuwa anakaribia kueneza miaka 100 wakati malaika wa Mungu alimuambia hivi kwa furaha: ‘Ee Danieli, wewe mutu mwenye kutamanika sana.’​—Dan. 10:11.

13. Pengine ni kwa sababu gani Yehova alimusaidia Danieli apate cheo cha juu?

13 Kwa sababu Mungu alimukubali Danieli, alipewa cheo cha juu wakati wa utawala wa Wababiloni na utawala wa Wamedi na Waperse. (Dan. 1:21; 6:1, 2) Pengine Yehova alifanya Danieli apate cheo hicho ili aweze kusaidia watu wake, kama vile ilikuwa juu ya Yosefu katika Misri na Esta na Mordekai katika Perse. * (Dan. 2:48) Wazia namna Wayahudi wenye walikuwa katika uhamisho, kama vile Ezekieli, walitiwa moyo kuona namna Yehova alitumia Danieli ili kuwasaidia!

Yehova anaona watu wenye kushikamana naye kuwa watu wa maana sana (Picha hii inapatana na fungu la 14, 15)

14, 15. (a) Namna gani hali yetu iko sawa na ya Danieli? (b) Mufano wa wazazi wa Danieli unaweza kufundisha wazazi nini?

14 Namna gani tunaweza kuiga imani na utii wa Danieli? Tunaishi kama wageni katika ulimwengu wenye kujaa mwenendo mubaya na ibada ya uwongo. Watu wanachochewa na Babiloni Mukubwa, ni kusema, dini zote za uwongo, “makao ya roho waovu.” (Ufu. 18:2) Kwa hiyo, sisi pia tuko tofauti na watu wengine, na wanaweza kutucheka. (Mk. 13:13) Kama Danieli, tuendelee basi kumukaribia Yehova, Mungu wetu. Wakati tunamutumainia kwa kumutii na kwa unyenyekevu, atatuona sisi pia kuwa watu wa maana sana.​—Hag. 2:7.

15 Mufano wa wazazi wa Danieli unaweza kufundisha wazazi jambo fulani. Namna gani? Hata kama ubaya ulikuwa umejaa katika Yuda wakati Danieli alikuwa mutoto, Danieli alifikia kumupenda Mungu wakati alikuwa anakomaa. Kwa kweli, jambo hilo halikujitokeza lenyewe. Hilo linaonyesha kama wazazi wake walimufundisha kabisa. (Met. 22:6) Hata jina la Danieli, lenye kumaanisha “Mwamuzi Wangu Ni Mungu,” linaonyesha kama wazazi wake walikuwa wanamuogopa Mungu. (Dan. 1:6) Kwa hiyo, wazazi, musichoke kufundisha watoto wenu, lakini muendelee kufanya hivyo kwa uvumilivu. (Efe. 6:4) Pia, musali pamoja nao na kwa ajili yao. Wakati munajikaza kuingiza kweli ya Biblia katika mioyo yao, Yehova atawabariki sana.​—Zab. 37:5.

AYUBU​—MUAMINIFU NA MWENYE KUTII WAKATI WA UTAJIRI NA UMASKINI

16, 17. Ayubu alipambana na magumu gani katika maisha yake?

16 Magumu yenye Ayubu alipambana nayo. Ayubu alipatwa na mabadiliko makubwa katika maisha yake. Mbele apate majaribu, alikuwa ‘mukubwa kuliko watu wote wa Mashariki.’ (Ayu. 1:3) Alikuwa tajiri, alijulikana sana, na watu walimuheshimia sana. (Ayu. 29:7-16) Lakini, hata kama alikuwa na mambo hayo yote, Ayubu hakuanza kuwa na kiburi ao kuona kama hakukuwa na lazima ya Mungu. Kwa kweli, Yehova alimuita, ‘mutumishi wangu,’ na aliongezea hivi: ‘Mutu asiye na lawama na munyoofu [ao, muaminifu], mwenye kumuogopa Mungu na kujiepusha na ubaya.’​—Ayu. 1:8.

17 Kwa muda mufupi sana, maisha ya Ayubu yalibadilika kabisa. Alipoteza mali yake yote na akashuka moyo sana. Tunajua kwamba mambo hayo yalimupata kwa sababu, Shetani muchongezi, alimushitaki Ayubu mambo ya uwongo kwamba anamuabudu Mungu kwa sababu ya faida fulani. (Soma Ayubu 1:9, 10.) Yehova alichukua mashitaka hayo kwa uzito. Alimupatia Ayubu nafasi ya kuonyesha ushikamanifu wake, ili kuonyesha kama alikuwa anamuabudu Mungu kwa moyo muzuri, haiko kwa sababu ya faida fulani.

18. (a) Ni nini inakushangaza juu ya ushikamanifu wa Ayubu? (b) Namna Yehova alimutendea Ayubu inaonyesha nini juu yake?

18 Shetani alimushambulia Ayubu mubaya katika njia mbalimbali na kumufanya afikiri kama ni Mungu ndiye alikuwa anamuletea mateso hayo. (Ayu. 1:13-21) Kisha, marafiki watatu wa uwongo wa Ayubu walimushambulia kwa maneno ya mubaya. Walimuambia kama alikuwa na makosa na kama Mungu alikuwa anamupatia malipizi! (Ayu. 2:11; 22:1, 5-10) Lakini, Ayubu aliendelea kuwa mushikamanifu. Ni kweli kwamba wakati fulani alisema bila kufikiri, lakini Yehova alielewa maumivu yenye Ayubu alikuwa anasikia. (Ayu. 6:1-3) Mungu alielewa kwamba Ayubu alisema hivyo kwa sababu alikuwa ameshuka moyo sana. Lakini Ayubu aliendelea kuwa mushikamanifu hata kama Shetani alimutesa na kusema mambo ya uwongo juu yake. Wakati majaribu hayo yalimalizika, Yehova alizidisha mara mbili vitu vyote vyenye Ayubu alikuwa navyo mbele ya majaribu kuanza, na akamuwezesha kuishi tena miaka ingine 140. (Yak. 5:11) Wakati huo, aliendelea kumutumikia Yehova kwa ushikamanifu. Ni nini inatuhakikishia jambo hilo? Kulikuwa kumepita miaka mingi tangu Ayubu akufe wakati Ezekieli aliandika maneno ya andiko letu la musingi.

19, 20. (a) Namna gani tunaweza kuiga imani na utii wa Ayubu? (b) Namna gani tunaweza kuonyesha wengine huruma kama Yehova?

19 Namna gani tunaweza kuiga imani na utii wa Ayubu? Hata tukuwe katika hali gani, tutie Yehova pa nafasi ya kwanza sikuzote katika maisha yetu, kwa kumutumainia kabisa na kumutii kwa moyo wote. Kwa kweli, tuko hata na sababu nyingi zaidi za kufanya hivyo kuliko sababu zenye Ayubu alikuwa nazo! Fikiria jambo hili: Tunajua mambo mengi juu ya Shetani na njia zake. (2 Kor. 2:11) Kupitia Biblia, zaidi sana kupitia kitabu cha Ayubu, tunajua sababu gani Mungu anaruhusu mateso. Kupitia unabii wa Danieli, tunaelewa kwamba Ufalme wa Mungu ni serikali ya kweli yenye kuongozwa na Kristo Yesu. (Dan. 7:13, 14) Na tunajua kama, hivi karibuni Ufalme huo utamaliza kabisa mateso yote.

20 Mufano wa Ayubu unatufundisha pia kama tunapaswa kuonyesha huruma Wakristo wenzetu wenye pengine wanapatwa na magumu mbalimbali. Kama Ayubu, wakati fulani wamoja wanaweza hata kusema bila kufikiri. (Mhu. 7:7) Lakini kuliko kuwahukumu, tuwaelewe na kuwaonyesha huruma. Kwa kufanya hivyo, tunaiga Baba yetu, Yehova, mwenye upendo na huruma.​—Zab. 103:8.

YEHOVA “ATAWAFANYA NINYI KUWA WENYE NGUVU”

21. Namna gani maneno ya 1 Petro 5:10 yanaonyesha mambo yenye yalitokea katika maisha ya Noa, Danieli, na Ayubu?

21 Hata kama Noa, Danieli, na Ayubu waliishi katika wakati tofauti na walipatwa na magumu yenye kuwa tofauti sana, walivumilia magumu yenye walipambana nayo. Habari zao zinatukumbusha maneno ya mutume Petro mwenye aliandika hivi: ‘Mukiisha kuteseka kitambo [muda] kidogo, Mungu wa fazili zote zisizostahiliwa . . . yeye mwenyewe atamaliza mazoezi yenu, atawafanya ninyi kuwa imara, atawafanya ninyi kuwa wenye nguvu.’​—1 Pet. 5:10.

22. Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

22 Kupitia maneno ya Petro yenye kuongozwa na roho ya Mungu, Yehova anatuhakikishia kama atafanya watumishi wake wakuwe imara na wenye nguvu. Maneno hayo yanahusu pia watu wa Mungu leo. Sisi wote tunapenda Yehova atutie nguvu na tuendelee kuwa imara katika ibada yake. Kwa hiyo, tunapenda kuiga imani na utii wa Noa, Danieli, na Ayubu! Kama vile tutaona katika habari yenye kufuata, walibakia washikamanifu kwa Yehova kwa sababu walikuwa wanamujua muzuri. Kwa kweli, ‘walielewa kila jambo’ lenye alipenda wafanye. (Met. 28:5) Sisi pia tunaweza kufanya hivyo.

^ fu. 2 Ezekieli alipelekwa katika uhamisho mwaka wa 617 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Ezekieli 8:1–19:14 iliandikwa “katika mwaka wa sita” kisha Ezekieli kupelekwa katika uhamisho, ni kusema, mwaka wa 612 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu.

^ fu. 5 Lameki, baba ya Noa mwenye alikuwa anamuogopa Mungu, alikufa miaka tano hivi mbele ya Garika. Ikiwa mama ya Noa na ndugu zake walikuwa wazima wakati Garika ilianza, hawakuokoka.

^ fu. 13 Pengine mambo yalikuwa hivyo pia juu ya marafiki watatu wa Danieli, wenye walipewa pia vyeo vya mamlaka.​—Dan. 2:49.