Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Komalisha Sifa ya Kujizuia

Komalisha Sifa ya Kujizuia

‘Tunda la roho ni . . . kujizuia.’​GAL. 5:22, 23.

NYIMBO: 83, 52

1, 2. (a) Kukosa kujizuia kunaweza kuleta matokeo gani? (b) Sababu gani ni jambo la maana tuzungumuzie leo sifa ya kujizuia?

KUJIZUIA ni sifa yenye kutoka kwa Mungu. (Gal. 5:22, 23) Yehova anaonyesha sifa ya kujizuia kwa ukamilifu. Hata hivyo, kwa sababu wanadamu hawakamilike, ni vigumu kwao kuendelea kuonyesha sifa ya kujizuia. Kwa kweli, magumu mengi yenye watu wanapata katika ulimwengu leo yanatokea kwa sababu watu wanakosa kujizuia. Kukosa sifa hiyo kunaweza kuleta matokeo ya kuchelewesha mambo na kushindwa kutumika muzuri kwenye masomo ao kwenye kazi. Kunaweza pia kuongoza kwenye matukano, ulevi, jeuri, kuvunja ndoa, kukamata madeni yenye haiko ya lazima, kuwa watumwa wa mambo fulani, kufungwa katika gereza, maumivu ya moyoni, kuwa na magonjwa yenye kupitishwa kwa njia ya ngono, kupata mimba yenye mutu hapendi, na mambo mengine.​—Zab. 34:11-14.

2 Kwa kweli, watu wenye kukosa kujizuia wanajiletea magumu wao wenyewe na wengine pia. Na watu wanaendelea kupoteza sifa ya kujizuia. Katika miaka ya 1940, uchunguzi ulifanywa juu ya kukosa kujizuia, lakini uchunguzi wa hivi karibuni umeonyesha kuwa watu wamepoteza hata zaidi sifa ya kujizuia. Jambo hilo halishangaze wale wenye kujifunza Neno la Mungu kwa sababu Biblia ilitabiri kuwa, kati ya alama zenye kuonyesha kuwa tunaishi katika “siku za mwisho” ni kwamba watu wangekuwa “wasiojizuia.”​—2 Tim. 3:1-3.

3. Sababu gani Wakristo wanapaswa kukomalisha sifa ya kujizuia?

3 Sababu gani tunapaswa kukomalisha sifa ya kujizuia? Fikiria sababu mbili za maana. Kwanza, imeonekana kuwa watu wenye kuwa na uwezo wa kuzuia tamaa zao, kwa kawaida hawapatwe na matatizo mengi makubwa-makubwa. Ni wenye kutulia zaidi moyoni, wanafanya urafiki wenye kujenga, na hawana hasira na mara nyingi hawahangaike ao kushuka moyo kama vile watu wenye kutenda haraka-haraka bila kufikiri. Pili, kuwa na uwezo wa kupinga jaribu na wa kuzuia tamaa za mubaya ni mambo ya maana sana ili Mungu atukubali. Kwa mufano, Adamu na Eva walishindwa kuonyesha sifa hizo, kwa hiyo, Mungu hakuwakubali tena. (Mwa. 3:6) Na pia fikiria matokeo ya mubaya yenye watu wengine wamepata tangu wakati huo kwa sababu ya kukosa kuonyesha sifa hiyo ya maana.

4. Ni nini inapaswa kumutia moyo mutu mwenye anajikaza sana ili kuonyesha sifa ya kujizuia?

4 Mwanadamu mwenye hakamilike hawezi kuonyesha kwa ukamilifu sifa ya kujizuia. Yehova anaelewa kuwa ni vigumu kwa watumishi wake kuonyesha sifa hiyo, na anapenda kuwasaidia ili waweze kuzuia tamaa zao za zambi. (1 Fal. 8:46-50) Kama Rafiki mwenye upendo, anatia moyo watu wenye kuwa na mioyo ya muzuri wenye wanapenda kumutumikia lakini wanashindwa kuonyesha sifa ya kujizuia katika hali fulani za maisha yao. Tuzungumuzie basi mufano mukamilifu wa Yehova. Kisha tutazungumuzia mifano ya muzuri na ya mubaya yenye kupatikana katika Biblia. Na tutazungumuzia pia mashauri yenye kufaa yenye yanaweza kutusaidia kukomalisha sifa ya kujizuia.

YEHOVA ANAONYESHA MUFANO

5, 6. Yehova anaonyesha mufano gani juu ya kuonyesha sifa ya kujizuia?

5 Yehova anaonyesha kwa ukamilifu sifa ya kujizuia, kwa sababu yeye ni mukamilifu katika mambo yote yenye anafanya. (Kum. 32:4) Lakini sisi, hatukamilike. Hata hivyo, ili tuelewe sifa hiyo ya kujizuia, tunapaswa kuchunguza mufano wa Yehova ili tuweze kumuiga muzuri zaidi. Yehova alionyesha sifa ya kujizuia katika hali gani fulani za maana?

6 Fikiria namna Yehova alionyesha sifa ya kujizuia wakati alishugulikia uasi mubaya sana wa Shetani. Mashitaka ya Shetani yalipaswa kujibiwa. Bila shaka, viumbe wa mbinguni washikamanifu kwa Mungu walihuzunika, walikasirika, na kuchukizwa kwa sababu ya uasi wenye Shetani alitokeza. Pengine wewe pia unajisikia hivyo wakati unaona mateso yote yenye Shetani ametokeza. Lakini, Yehova hakutenda haraka-haraka. Alifikiri na kutenda kwa njia yenye kufaa kabisa. Amekuwa si mwepesi wa hasira na amekuwa mwenye haki katika namna yake ya kutenda juu ya uasi wa Shetani. (Kut. 34:6; Ayu. 2:2-6) Sababu gani? Yehova ameacha wakati upite kwa sababu hapendi mutu yeyote aharibiwe lakini ‘anataka wote wafikie toba.’​—2 Pet. 3:9.

7. Mufano wa Yehova unaweza kutufundisha nini?

7 Namna Yehova anaonyesha sifa ya kujizuia inatufundisha kuwa tunapaswa kuchunguza maneno yetu na kufikiria kwa uangalifu matendo yetu; tunapaswa kuepuka kufanya mambo haraka-haraka. Wakati unapaswa kukamata uamuzi fulani wa maana, uchukue wakati wa kufikiri ili utende kwa hekima. Usali ili kupata hekima ya kusema ao kufanya mambo yenye kuwa sawa. (Zab. 141:3) Wakati tuko na hasira, ni mwepesi sana kutenda bila kufikiri. Wengi kati yetu wamefikia kuhuzunika kwa sababu walisema na kufanya mambo fulani haraka-haraka bila kufikiri!​—Met. 14:29; 15:28; 19:2.

MIFANO YA MUBAYA NA YA MUZURI​—KATI YA WATU WA MUNGU

8. (a) Ni wapi unaweza kupata mifano ya watu wenye walionyesha sifa ya kujizuia? (b) Ni nini ilimusaidia Yosefu asikubali wakati bibi ya Potifa alijaribu kumutongoza? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

8 Ni mifano gani yenye kupatikana katika Biblia yenye kukazia faida ya kuzuia matendo yetu? Kwa kweli, unaweza kukumbuka watu mbalimbali wenye kuzungumuziwa katika Biblia wenye walionyesha sifa ya kujizuia wakati walijaribiwa. Mutu mumoja ni Yosefu, mwana wa Yakobo. Alionyesha sifa ya kujizuia wakati alikuwa anatumikia katika nyumba ya Potifa, mukubwa wa walinzi wa Farao. Bibi ya Potifa alikuwa anamutamani Yosefu, mwenye alikuwa “mwenye umbo zuri na mwenye sura ya kupendeza,” na alijaribu kumuchochea alale naye. Bibi ya Potifa alimutongoza Yosefu kila mara. Lakini ni nini ilimusaidia asikubali? Kwa kweli, alichukua wakati wa kufikiria sana matokeo yenye angepata ikiwa angeangukia katika jaribu hilo. Na wakati hali ilikuwa mubaya sana, Yosefu alikimbia. Alisema hivi: ‘Ninawezaje kufanya ubaya huu mukubwa na kwa kweli nimutendee Mungu zambi?’​—Mwa. 39:6, 9; soma Methali 1:10.

9. Namna gani unaweza kujitayarisha ili kushinda majaribu?

9 Mufano wa Yosefu unatufundisha nini? Jambo moja ni kwamba tunapaswa kukimbia jaribu lenye linaweza kutuchochea tuvunje sheria fulani ya Mungu. Watu fulani wenye wako sasa Mashahidi, zamani walikuwa na tabia ya kula kupita kiasi, kunywa pombe sana, kuvuta tumbako, kutumia dawa za kulewesha, kufanya uasherati, na mambo mengine. Hata kisha kubatizwa, wakati fulani wanaweza kujaribiwa kurudilia matendo yao ya zamani. Lakini, ikiwa unajaribiwa kuvunja sheria moja kati ya sheria za Yehova, utie nguvu hali yako ya kiroho kwa kuchukua wakati wa kufikiria sana matokeo ya mubaya ya kiroho yenye unaweza kupata ikiwa unashindwa kuzuia tamaa zako za zambi. Unaweza kufikiria mbele ya wakati hali zenye zinaweza kukuingiza katika jaribu na kuamua namna unaweza kuziepuka. (Zab. 26:4, 5; Met. 22:3) Ikiwa unapambana na jaribu kama hilo, umuombe Yehova akupatie hekima na sifa ya kujizuia ili upate ushindi.

10, 11. (a) Vijana wengi wanapambana na jaribu gani kwenye masomo? (b) Ni nini inaweza kusaidia vijana Wakristo wapinge mikazo ya kuwa na mwenendo mubaya?

10 Vijana wengi Wakristo wanapatwa na jaribu kama lile la Yosefu. Fikiria mufano wa Kimberly, kijana mwanamuke. Wengi kati ya wanafunzi wenzake walizoea kufanya ngono, na kisha mwisho wa juma, walikuwa wanajisifu juu ya ngono zenye walifanya. Kimberly hakukuwa na habari kama hizo za kueleza. Alisema kama wakati fulani kuwa tofauti na wengine kulimufanya ajisikie kuwa “pekee yake,” na wanafunzi wenzake walimuona kuwa ni pumbavu kwa sababu hakukuwa anafanya urafiki wa kimapenzi. Lakini, Kimberly alikuwa na hekima sana kwa sababu alijua kuwa kwa vijana wengi, jaribu la kufanya ngono ni lenye nguvu sana. (2 Tim. 2:22) Mara nyingi wanafunzi wenzake walimuuliza ikiwa alikuwa angali bikira. Hilo lilimutolea nafasi ya kueleza sababu gani hafanye ngono. Tunajivunia vijana Wakristo wenye kuazimia kupinga mukazo wa kufanya uasherati, na Yehova pia anajivunia vijana hao!

11 Biblia inazungumuzia mifano yenye kuonya ya watu wenye walikosa kujizuia juu ya mambo ya uasherati. Inaonyesha pia matokeo ya mubaya yenye mutu anaweza kupata ikiwa hazuie tabia kama hiyo. Mutu yeyote mwenye kupambana na hali kama ya Kimberly anapaswa kufikiria mufano wa kijana mwanaume mwenye alitenda bila kufikiri mwenye kuzungumuziwa katika Methali sura ya 7. Fikiria pia, mufano wa Amnoni na matokeo ya mubaya sana ya matendo yake. (2 Sam. 13:1, 2, 10-15, 28-32) Wazazi wanapaswa kusaidia watoto wao wakomalishe sifa ya kujizuia na hekima juu ya mambo ya urafiki wa kimapenzi kwa kuzungumuzia katika ibada ya familia mifano yenye tumetaja.

12. (a) Namna gani Yosefu alionyesha sifa ya kujizuia wakati alikutana na ndugu zake? (b) Ni katika hali gani tunaweza kuonyesha sifa ya kujizuia?

12 Yosefu alituachia mufano mwengine wa muzuri wa kuonyesha sifa ya kujizuia. Ili kujua mambo yenye yalikuwa katika mioyo ya ndugu zake, Yosefu hakujitambulisha kwao wakati walifika Misri ili kuuza chakula. Na wakati alijisikia mubaya sana katika moyo wake, alienda nafasi ya siri ili wasione namna anatokwa machozi. (Mwa. 43:30, 31; 45:1) Ikiwa Mukristo mwenzako ao mupendwa wako anatenda bila kufikiri kwa njia fulani, kujizuia namna Yosefu alifanya kunaweza kukusaidia kuepuka kutenda haraka-haraka. (Met. 16:32; 17:27) Ikiwa uko na watu wa jamaa wenye wametengwa na kutaniko, unaweza kuwa na lazima ya kuzuia namna unajisikia katika moyo wako na kuepuka kuzungumuza nao bila sababu zenye kufaa. Tunapaswa kujikaza ili kujizuia katika hali kama hizo, lakini ni mwepesi ikiwa tunatambua kuwa matendo yetu yanapatana na mufano wa Mungu na kupatana na mashauri yake.

13. Mufano wa Mufalme Daudi unaweza kutufundisha nini?

13 Biblia inazungumuzia mufano muzuri wa Mufalme Daudi. Alikuwa na uwezo mukubwa, hata hivyo, alijizuia kuutumia kwa hasira wakati alichokozwa na Sauli na Shimei. (1 Sam. 26:9-11; 2 Sam. 16:5-10) Lakini hilo halimaanishe kuwa sikuzote Daudi alionyesha sifa ya kujizuia; zambi yenye alifanya pamoja na Bath-sheba na namna alitenda kwanza juu ya pupa ya Nabali inaonyesha jambo hilo. (1 Sam. 25:10-13; 2 Sam. 11:2-4) Hata hivyo, mufano wa Daudi unaweza kutufundisha mambo ya maana. Kwanza, waangalizi wenye kuwa kati ya watu wa Mungu wanapaswa kuwa waangalifu hata zaidi ili kuonyesha sifa ya kujizuia ili waepuke kutumia mubaya mamlaka yao. Pili, hakuna mutu mwenye anapaswa kujitumainia kupita kiasi, na kufikiri kuwa hawawezi kujaribiwa.​—1 Kor. 10:12.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

14. Ndugu mumoja alijionea jambo gani, na sababu gani kutenda kama yeye katika hali kama hizo ni jambo la maana?

14 Unaweza kufanya nini ili ukomalishe sifa ya kujizuia? Fikiria hali hii yenye ilitokea kabisa. Motokari fulani iligonga sehemu ya nyuma ya motokari ya Luigi. Hata kama alikuwa na makosa, mwanaume mwenye alikuwa anatembeza motokari hiyo alianza kumutukana Luigi na kujaribu kupigana. Luigi alisali, aliomba Yehova amusaidie kujizuia, na alijikaza kumutuliza mwanaume huyo, lakini akakataa. Wakati alikuwa angali anatomboka, Luigi aliandika namba za motokari ya mwanaume huyo ili kuzipeleka kwenye kompanyi ya asiranse. Kisha juma moja, Luigi alimurudilia mwanamuke mumoja, na alitambua kuwa bwana ya mwanamuke huyo ni ule mwanamume mwenye alikuwa amegonga motokari yake! Mwanaume huyo alisikia haya na kuomba musamaha juu ya namna alimuchambua. Alisema kuwa atazungumuza na kompanyi ya asiranse ya Luigi ili kumaliza mambo haraka. Mwanaume huyo alishiriki katika mazungumuzo ya Biblia na alipendezwa na mambo yenye walikuwa wanazungumuzia. Kwa hiyo, Luigi aliona namna ilikuwa muzuri sana kubakia mwenye kutulia wakati wa aksidenti hiyo na namna ingekuwa mubaya sana ikiwa angekasirika haraka.​—Soma 2 Wakorintho 6:3, 4.

Kutulia ao kukasirika haraka kunaweza kuwa na matokeo juu ya kazi yetu ya kuhubiri (Picha hizi zinapatana na fungu la 14)

15, 16. Namna gani kujifunza Biblia kunaweza kukusaidia wewe na familia yako kukomalisha sifa ya kujizuia?

15 Kujifunza Biblia kwa bidii na kwa uangalifu kunaweza kusaidia Wakristo wakomalishe sifa ya kujizuia. Kumbuka kuwa Mungu alimuambia Yoshua hivi: ‘Kitabu hiki cha sheria kisiondoke katika kinywa chako, nawe ukisome kwa sauti ya chini muchana na usiku, upate kuangalia kufanya kulingana na yote ambayo yameandikwa ndani yake; kwa maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha utatenda kwa hekima.’ (Yos. 1:8) Namna gani kujifunza Biblia kunaweza kukusaidia kukomalisha sifa ya kujizuia?

16 Kama vile tumeona, Maandiko iko na mifano yenye kuonyesha wazi faida ya kuonyesha sifa ya kujizuia na matokeo ya matendo yetu. Yehova aliandikisha habari hizo kwa kusudi fulani. (Rom. 15:4) Ni jambo la hekima kusoma, kutafakari, na kujifunza mifano hiyo! Ujikaze kuelewa namna mifano hiyo inakuhusu wewe na familia yako. Muombe Yehova akusaidie kutumikisha Neno lake. Ikiwa unatambua kuwa hauonyeshe sifa ya kujizuia katika njia fulani, ukubali jambo hilo. Kisha usali juu ya jambo hilo, na ujikaze kuona namna unaweza kufanya mabadiliko. (Yak. 1:5) Kwa kweli, kutafuta habari katika vichapo vyetu kutakusaidia kupata habari za maana sana zenye zitakusaidia zaidi.

17. Ni katika njia gani wazazi wanaweza kusaidia watoto wao wakomalishe sifa ya kujizuia?

17 Namna gani unaweza kusaidia watoto wako wakomalishe sifa ya kujizuia? Wazazi, mujue kama watoto hawazaliwe na sifa hiyo. Na kama sifa zingine zote zenye watoto wao wanapaswa kujifunza, wazazi wanapaswa kuonyesha mufano. (Efe. 6:4) Kwa hiyo, ikiwa unaona kuwa watoto wako wanashindwa kuzuia tamaa zao, ujiulize ikiwa unawaonyesha mufano muzuri. Ikiwa unahubiri, unakusanyika, na kuongoza ibada ya familia kwa ukawaida, hilo linaweza kuwa na matokeo ya muzuri juu ya watoto wako. Usiogope kukatalia watoto wako mambo fulani ikiwa ni lazima kufanya hivyo! Yehova aliwekea Adamu na Eva mipaka; mipaka hiyo ingewasaidia kuheshimia mamlaka yake. Vilevile, nizamu yenye wazazi wanapatia watoto wao na mufano wenye wanawaonyesha vinawafundisha sifa ya kujizuia. Kupenda mamlaka ya Mungu na kuheshimia kanuni zake ni kati ya mambo ya maana sana yenye unaweza kukazia katika moyo wa watoto wako.​—Soma Methali 1:5, 7, 8.

18. Sababu gani unaweza kuwa hakika kama kuwa na marafiki wazuri kunaleta baraka?

18 Kwa kweli, iwe uko muzazi ao hapana, ni jambo la lazima uchague marafiki wako kwa hekima. Tafuta marafiki wenye watakutia moyo kufuatilia miradi ya maana na kuepuka magumu. (Met. 13:20) Wakristo wenye kuwa na hali ya muzuri kiroho watakuchochea uige namna wanaonyesha sifa ya kujizuia katika maisha yao. Na kwa kweli, mwenendo wako wa muzuri utachochea marafiki wako. Ni jambo la maana kuonyesha sifa ya kujizuia ili kuendelea kukubaliwa na Mungu katika maisha yetu ya kila siku na kuwa na uhusiano muzuri pamoja na wapendwa wetu.