Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Neno la Mungu Wetu Litadumu” Milele

“Neno la Mungu Wetu Litadumu” Milele

‘Majani mabichi yamekauka, ua limenyauka [limekauka]; lakini kwa habari ya neno la Mungu wetu, litadumu mupaka wakati usio na kipimo [milele].’​ISA. 40:8.

NYIMBO: 116, 115

1, 2. (a) Maisha yangekuwa namna gani bila Biblia? (b) Ni nini inatusaidia kufaidika na Neno la Mungu?

UNAWEZA kuwazia maisha yako yangekuwa namna gani bila Biblia? Haungepata muongozo wenye kutegemeka wa kukuongoza katika maisha ya kila siku. Haungepata majibu yenye kusadikisha juu ya maulizo yako juu ya Mungu, maisha, na juu ya wakati wenye kuja. Na haungejua namna Yehova alitendea wanadamu zamani.

2 Jambo la kufurahisha ni kwamba hatuko katika hali hiyo yenye kuhuzunisha. Yehova ametupatia Neno lake, Biblia. Na ametuhakikishia kuwa ujumbe wake utadumu ao utaendelea milele. Mutume Petro alitaja maneno ya andiko la Isaya 40:8. Kama vile tunajua, andiko hilo halizungumuzie moja kwa moja Biblia; lakini, maneno hayo yenye yaliongozwa na roho ya Mungu yanaweza pia kuzungumuzia ujumbe wote wa Biblia. (Soma 1 Petro 1:24, 25.) Kwa kweli, Biblia inaweza kutuletea faida kabisa ikiwa inapatikana katika luga yenye tunaelewa muzuri. Tangu zamani wale wenye kupenda Neno la Mungu wametambua jambo hilo. Hata kama haikukuwa vyepesi sikuzote, kwa miaka mingi watu wenye kumuogopa Mungu wamejikaza kutafsiri na kugawanyia watu Maandiko. Tamaa yao ilipatana na mapenzi ya Mungu, anapenda “watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli.”​—1 Tim. 2:3, 4.

3. Tutazungumuzia nini katika habari hii? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

3 Katika habari hii, tutazungumuzia mifano fulani yenye kuonyesha namna Neno la Mungu limedumu hata kama kulikuwa (1) mabadiliko katika luga, (2) mabadiliko katika mambo ya politike yenye yalikuwa na matokeo juu ya luga ya watu wa kawaida, na (3) upinzani wa kutafsiriwa kwa Biblia. Kuzungumuzia mambo hayo kutatuletea faida gani? Kutatusaidia tupendezwe zaidi na Neno la Mungu. Pia, kutatia nguvu upendo wetu kwa ule mwenye aliandikisha Biblia, mwenye alitupatia Biblia kwa faida yetu.​—Mika 4:2; Rom. 15:4.

MABADILIKO KATIKA LUGA

4. (a) Namna gani mabadiliko yanakuwa katika luga kadiri wakati unapita? (b) Ni nini inaonyesha kuwa Mungu habague watu wa luga yoyote, na hilo linakufanya ujisikie namna gani?

4 Kadiri wakati unapita, kunakuwa mabadiliko katika luga. Maana ya maneno na misemo fulani inaweza kufikia kubadilika kabisa. Pengine unafikiria mifano fulani yenye kuonyesha namna mabadiliko yamekuwa katika luga yenye unazungumuza. Ni hivyo pia kuhusu Kiebrania na Kigiriki, luga zenye zilitumiwa ili kuandika sehemu kubwa ya Biblia. Kiebrania na Kigiriki cha sasa ni tofauti na Kiebrania na Kigiriki cha wakati wa zamani. Kwa hiyo, karibu watu wote wenye wanapenda kuelewa Neno la Mungu wanapaswa kusoma tafsiri ya Neno hilo, hata wale wenye wanajua Kiebrania na Kigiriki cha leo. Watu fulani wameona kuwa wanapaswa kujifunza Kiebrania na Kigiriki cha zamani ili waweze kusoma Biblia katika luga zenye zilitumiwa ili kuiandika. Lakini, pengine kufanya hivyo hakutawaletea faida kama vile wanawazia. * Jambo la kufurahisha ni kwamba, leo Biblia nzima ao sehemu fulani za Biblia zimetafsiriwa katika luga karibu 3 000. Ni wazi kwamba Yehova anapenda watu wa ‘kila taifa na kabila na luga’ waweze kufaidika na Neno lake. (Soma Ufunuo 14:6.) Kwa kweli, hilo linakuchochea umukaribie zaidi Mungu wetu mwenye upendo na mwenye hana ubaguzi. Sivyo?​—Mdo. 10:34.

5. Ni nini ilifanya tafsiri ya King James Version kuwa ya maana?

5 Kwa sababu kunakuwa mabadiliko katika luga kadiri wakati unapita, hilo linahusu pia luga ambamo Biblia imetafsiriwa. Tafsiri ya Biblia yenye ilikuwa mwepesi kuelewa wakati ilitolewa kwa mara ya kwanza, inaweza kufikia kukosa kueleweka muzuri. Fikiria kwa mufano tafsiri fulani ya Biblia ya Kiingereza. Tafsiri ya King James Version ilitolewa kwa mara ya kwanza katika mwaka wa 1611. Ilifikia kuwa kati ya Biblia za Kiingereza zenye zilitumiwa sana, na ilifikia kuwa na matokeo makubwa juu ya luga ya Kiingereza. * Lakini, tafsiri ya King James Version haikutumia sana jina la Mungu. Ilitumia jina “Yehova” katika hesabu kidogo ya maandiko, na ilitumia neno “BWANA” kwa herufi kubwa katika maandiko mengine katika Maandiko ya Kiebrania nafasi kwenye jina la Mungu lilipatikana katika maandishi ya zamani. Biblia zingine za tafsiri hiyo zenye zilifikia kuchapishwa zilitumia pia neno “BWANA” katika herufi kubwa katika maandiko fulani katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kwa hiyo, tafsiri ya King James Version ilijua kabisa nafasi kwenye jina la Mungu lilipaswa kupatikana katika sehemu ya Biblia yenye inazoea kuitwa Agano Jipya.

6. Sababu gani tuko wenye shukrani juu ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya?

6 Hata hivyo, kadiri miaka ilipita, maneno mengi yenye kupatikana katika tafsiri ya King James Version hayakutumiwa tena. Ni hivyo pia kuhusu tafsiri zingine za Biblia za kwanza-kwanza za luga zingine. Kwa kweli, sisi ni wenye shukrani sana kwa sababu tuko na Biblia Takatifu​—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya yenye kutumia maneno ya sasa. Tafsiri hiyo inapatikana ikiwa nzima ao kwa sehemu katika luga zaidi ya 150, kwa hiyo, watu wengi zaidi wanaweza kuipata leo. Maneno yake yenye kuwa wazi yanasaidia ujumbe wa Neno la Mungu uguse moyo wetu. (Zab. 119:97) Jambo la maana zaidi, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inarudisha jina la Mungu nafasi kwenye linastahili kupatikana katika Maandiko.

LUGA YA WATU WA KAWAIDA

7, 8. (a) Sababu gani Wayahudi wengi hawakuweza kuelewa Maandiko ya Kiebrania katika miaka kati ya 201 na 300? (b) Septante ya Kigiriki ni nini?

7 Wakati fulani, mabadiliko katika mambo ya politike yamekuwa na matokeo juu ya luga ya watu wa kawaida katika kipindi fulani. Mungu amefanya nini ili mabadiliko hayo yasizuie watu kuelewa Neno lake? Mufano mumoja wa zamani utatusaidia kujibia ulizo hilo. Vitabu 39 vya kwanza vya Biblia viliandikwa na Waisraeli ao Wayahudi. Walikuwa taifa lenye ‘lilikabiziwa [lilipewa] maneno matakatifu ya Mungu’ kwa mara ya kwanza. (Rom. 3:1, 2) Hata hivyo, kufikia miaka kati ya 201 na 300 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Wayahudi wengi hawakuelewa tena Kiebrania. Sababu gani? Kwa sababu Alexandre Mukubwa alipata ushindi juu ya maeneo mengi na kupanua utawala wa Ugiriki. (Dan. 8:5-7, 20, 21) Kadiri utawala wake uliendelea kupanuka, Kigiriki kilifikia kuwa luga ya watu wengi zaidi wa utawala huo, kutia ndani Wayahudi wenye walitawanywa katika eneo hilo kubwa. Kadiri Wayahudi wengi waliendelea kuzungumuza Kigiriki, ilikuwa vigumu zaidi kwa wengi kati yao kuelewa Maandiko ya Kiebrania. Sasa, iliomba kufanya nini?

8 Katika mwaka wa 250 hivi mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, vitabu tano vya kwanza vya Biblia vilitafsiriwa katika Kigiriki. Maandiko mengine ya Kiebrania yalimalizwa kutafsiriwa katika Kigiriki katika miaka kati ya 101 na 200 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Vitabu hivyo vyote vya Biblia vilitiwa pamoja na vilifikia kuitwa Septante ya Kigiriki. Tafsiri ya Septante ndiyo tafsiri ya kwanza yenye kujulikana ya Maandiko yote ya Kiebrania.

9. (a) Namna gani Septante na tafsiri zingine za zamani zilisaidia watu kusoma Neno la Mungu? (b) Ni sehemu gani ya Maandiko ya Kiebrania yenye unapenda sana?

9 Tafsiri ya Septante ilisaidia sana Wayahudi wenye kuzungumuza Kigiriki na wengine kuelewa Maandiko ya Kiebrania. Fikiria namna walipaswa kufurahi sana kusikia ao kusoma Neno la Mungu katika luga yenye ilikuwa sasa luga yao ya kizalikio! Kisha, sehemu za Biblia zilitafsiriwa katika luga zingine za watu wa kawaida kama vile Kisiria, Kigoti, na Kilatini. Wakati watu walisoma Maandiko Matakatifu katika luga yenye wangeweza kuelewa, bila shaka wengi walifikia kuwa na sehemu fulani yenye walifurahia zaidi, kama sisi leo. (Soma Zaburi 119:162-165.) Kwa kweli, Neno la Mungu limeendelea kudumu hata kama kumekuwa mabadiliko katika luga ya watu wa kawaida.

KUPINGA KAZI YA KUTAFSIRI BIBLIA

10. Wakati wa John Wycliffe, sababu gani watu wengi hawakuweza kusoma Biblia?

10 Wakati fulani, viongozi wenye mamlaka wamejaribu kuzuia watu wa kawaida kusoma Biblia. Lakini, watu wenye kumuogopa Mungu waliendelea kutafsiri Biblia hata kama walipingwa. Kwa mufano, fikiria mwanateolojia mwenye aliitwa John Wycliffe mwenye aliishi katika Uingereza kumepita miaka 600 hivi. Aliamini kabisa kuwa kila mutu alipaswa kusoma Neno la Mungu. Lakini wakati wake, ilikuwa vigumu kwa watu wa kawaida katika Uingereza kupata Biblia. Sababu gani? Sababu moja ni kwamba watu wengi hawakukuwa na uwezo wa kuuza Biblia, kwa sababu kopi za Biblia zilifanywa kwa mukono na zilikuwa na bei kali. Zaidi ya hilo, watu wengi hawakujua kusoma. Kwa kweli, wangeweza kusikia maandiko yanasomwa wakati walienda kwenye kanisa. Lakini, inawezekana kuwa hawakuelewa mambo yenye walikuwa wanasikia. Sababu gani? Biblia yenye Kanisa ilizoea kutumia sana (tafsiri ya Vulgate) iliandikwa katika Kilatini. Lakini, katika kipindi cha mwaka kati ya 500 na 1500 watu wa kawaida hawakuzungumuza tena Kilatini! Namna gani watu hao wangepata hazina ya maana sana yenye kupatikana katika Biblia?​—Met. 2:1-5.

John Wycliffe na wengine walitamani kila mutu akuwe na Neno la Mungu. Uko na tamaa kama hiyo?

(Picha hii inapatana na fungu la 11)

11. Biblia ya Wycliffe ilileta matokeo gani?

11 Katika mwaka wa 1382, tafsiri ya Kiingereza yenye ilifikia kuitwa Biblia ya Wycliffe ilitolewa. Bila kukawia, ilienea kati ya wafuasi wa Wycliffe. Kwa sababu walitamani sana kusaidia watu wa kawaida waelewe Neno la Mungu, wahubiri wenye kusafiri, wenye walijulikana kwa jina la Waloladi, walisafiri kwa miguu kijiji mupaka kijiji katika Uingereza yote. Mara nyingi, Waloladi walisomea watu wenye walikutana nao sehemu za Biblia ya Wycliffe, na waliwaachia kopi zenye kuandikwa kwa mukono. Bidii yao ilikuwa na matokeo ya muzuri kabisa, ilisaidia watu wapendezwe tena na Neno la Mungu.

12. Viongozi wa dini walitendea namna gani Wycliffe na wafuasi wake?

12 Viongozi wa dini walitenda namna gani? Walichukia Wycliffe, Biblia yake, na wafuasi wake. Viongozi wa dini waliwatesa Waloladi na walitafuta na kuharibu kopi nyingi za Biblia ya Wycliffe zenye walipata. Hata kisha kifo chake, Wycliffe alitangazwa kuwa muasi-imani. Kwa kweli, haikuwezekana kupatia malipizi mutu mwenye alikuwa amekufa. Lakini, viongozi wa dini walichimbua mifupa ya Wycliffe na kuiunguza, na majivu ya mifupa hiyo yalitupwa katika muto Swift. Hata hivyo, Kanisa halikuweza kumaliza hamu yenye watu walikuwa nayo ya kusoma na kuelewa Neno la Mungu. Katika miaka yenye ilifuata, watu katika Ulaya na katika sehemu zingine za dunia walianza kutafsiri Biblia na kuigawanya kwa watu wa kawaida.

“YEYE ANAYEKUFUNDISHAILI UJIFAIDI MWENYEWE”

13. Tuko hakika juu ya jambo gani, na namna gani hilo linatia nguvu imani yetu?

13 Leo, Wakristo hawapaswe kufikiri kuwa kazi ya kutafsiri Biblia ya Septante, Biblia ya Wycliffe, tafsiri ya King James Version, ao tafsiri ingine yoyote iliongozwa na roho ya Mungu. Hata hivyo, wakati tunachunguza historia ya tafsiri hizo na tafsiri zingine zenye zimechapishwa, hilo linaunga mukono kweli hii: Kama vile Yehova aliahidi, Neno lake limedumu. Je, hilo halitie imani yako nguvu kuwa ahadi zingine zote zenye Yehova ametoa zitatimia pia?​—Yos. 23:14.

14. Namna gani Neno la Mungu linatusaidia tumupende zaidi?

14 Zaidi ya kutia nguvu imani yetu, kuzungumuzia namna Biblia imedumu kwa miaka mingi kunatia nguvu upendo wetu kwa Yehova. * Kwa kweli, ni sababu gani kubwa yenye ilimufanya atupatie Neno lake? Na sababu gani alituhakikishia kuwa litadumu? Kwa sababu anatupenda, na anapenda kutufundisha ili tupate faida sisi wenyewe. (Soma Isaya 48:17, 18.) Kwa hiyo, upendo wa Yehova unapaswa kutuchochea kumupenda pia na kutii amri zake.​—1 Yoh. 4:19; 5:3.

15. Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

15 Inafaa kabisa kusema kama kwa sababu tunapenda Neno la Mungu, tutapenda kufaidika kabisa na Neno hilo. Namna gani tunaweza kufaidika kabisa na usomaji wetu wa Biblia? Ni nini inaweza kutusaidia kukazia Biblia katika kazi yetu ya kuhubiri? Namna gani wale wenye kufundisha kwenye jukwaa wanaweza kufanya Maandiko yakuwe musingi wa mafundisho yao? Tutapata majibu ya maulizo hayo katika habari yenye kufuata.

^ fu. 4 Ona habari “Je, Unahitaji Kujifunza Kiebrania na Kigiriki?” katika gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 11, 2009.

^ fu. 5 Maneno mengi ya Kiingereza ya usemi wa mufano yanatoka katika King James Version.

^ fu. 14 Ona kisanduku “ Ujionee Wewe Mwenyewe!