Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Nimebarikiwa kwa Kutumika Pamoja na Wanaume Wenye Kukomaa Kiroho

Nimebarikiwa kwa Kutumika Pamoja na Wanaume Wenye Kukomaa Kiroho

KATIKATI ya miaka ya 1930, baba yangu James Sinclair na mama yangu Jessie, walihamia katika Bronx, eneo lenye kuwa katika Muji wa New York. Willie Sneddon mumoja kati ya watu wenye walifikia kujuana nao, naye pia alitoka Écosse. Wakati walikutana kwa mara ya kwanza, kisha tu dakika kidogo, wote watatu walianza kuzungumuza juu ya familia zao. Hilo lilitokea miaka fulani mbele nizaliwe.

Mama alimuambia Willie kama muda mufupi mbele ya Vita Kubwa kuanza, baba yake na kaka yake walikufa katika maji wakati mashua yao ya kuvua samaki iligonga bombe katika Bahari ya Kaskazini. Willie alimujibia hivi: “Baba yako iko katika helo!” Willie alikuwa Shahidi wa Yehova, na ni katika njia hiyo yenye kukasirisha ndiyo mama yangu alifikia kusikia kweli ya Biblia kwa mara ya kwanza.

Willie Sneddon pamoja na Liz

Mambo yenye Willie alisema yalimukasirisha mama yangu kwa sababu alikuwa anajua kuwa baba yake alikuwa mutu muzuri. Lakini Willie aliongezea hivi: “Utajisikia muzuri ikiwa ninakuambia kuwa Yesu alienda katika helo?” Mama alikumbuka mafundisho ya kanisa, yenye tangu zamani yalifundisha kuwa Yesu alishuka katika helo na alifufuliwa siku ya tatu. Kwa hiyo, alijiuliza hivi: ‘Ikiwa helo ni mahali kwenye kuwa moto kwenye watu wabaya wanateseka, sababu gani Yesu alienda huko?’ Hilo lilifanya mama yangu aanze kupendezwa na kweli. Akaanza kuenda kwenye mikutano katika Kutaniko la Bronx na akabatizwa katika mwaka wa 1940.

Niko pamoja na mama yangu, na kisha pamoja na baba yangu

Wakati huo, wazazi Wakristo hawakutiwa sana moyo wajifunze Biblia pamoja na watoto wao. Wakati nilikuwa mutoto, baba yangu alikuwa ananichunga wakati mama yangu alikuwa anaenda kwenye mikutano na katika kazi ya kuhubiri kila mwisho wa juma. Kisha miaka kidogo, mimi na baba yangu tulianza kuenda kwenye mikutano pamoja na mama yangu. Alikuwa na bidii sana katika kazi ya kuhubiri habari njema na aliongoza mafunzo mbalimbali ya Biblia na watu wenye kupendezwa. Wakati fulani alijifunza hata na wanafunzi fulani wa Biblia katika vikundi kwa sababu wanafunzi wake walikuwa wanaishi katika eneo moja. Nilimusindikiza katika kazi ya kuhubiri wakati wa mapumuziko ya masomo. Katika njia hiyo, nilijifunza mambo mengi juu ya Biblia na namna ya kufundisha watu mambo yenye inasema.

Ninahuzunika kusema kwamba wakati nilikuwa mutoto, sikupendezwa sana na kweli. Niliona kweli kuwa jambo la kawaida. Hata hivyo, wakati nilikuwa na miaka 12, nikakuwa muhubiri wa Ufalme na tangu wakati huo nilifanya kazi ya kuhubiri kwa ukawaida. Wakati nilikuwa na miaka 16, nilitoa maisha yangu kwa Yehova na kubatizwa tarehe 24 Mwezi wa 7, 1954, kwenye mukusanyiko mumoja katika Toronto, Kanada.

KUTUMIKA KWENYE BETELI

Ndugu fulani katika kutaniko letu walikuwa Wanabeteli na wengine walikuwa wamekwisha kutumikia kwenye Beteli. Walinichochea sana. Uwezo wao kufundisha katika mahubiri na wakati wanatoa hotuba ulinishangaza sana. Hata kama walimu wangu walipenda nisome masomo ya juu, nilikuwa na muradi wa kuenda kwenye Beteli. Kwa hiyo, nilijaza ombi la kuingia kwenye Beteli kwenye mukusanyiko huo katika Toronto. Nilifanya hivyo tena katika mwaka wa 1955 kwenye mukusanyiko mwingine katika Yankee Stadium, Muji wa New York. Muda mufupi kisha hapo, wakati nilikuwa na miaka 17, nilipata mualiko wa kutumikia kwenye Beteli ya Brooklyn tarehe 19 Mwezi 9, 1955. Katika siku yangu ya pili kwenye Beteli, nilianza kutumika mahali pa kuunganisha vitabu katika 117 Adams Street. Bila kukawia nilianza kutumika na mashine ya kuunganisha vitabu, yenye iliunganisha kurasa 32 za vitabu ili ziende kwenye mashine ya kushona.

Nilianza kutumikia kwenye Beteli ya Brooklyn wakati nilikuwa na miaka 17

Kisha kutumika mwezi moja hivi mahali pa kuunganisha vitabu, nilitumwa kutumika katika Idara ya Magazeti kwa sababu nilikuwa ninajua kuandika kwa kutumia mashine. Wakati huo, ndugu na dada walikuwa wanaandika adresi za watu wapya wenye walijiandikisha ili kupokea Munara wa Mulinzi na Amuka! kwa kutumia chombo kidogo cha chuma chenye kuwa na herufi mbalimbali. Kisha miezi kidogo, nilianza kutumika katika Idara ya Usafirishaji. Klaus Jensen, mwangalizi wa idara hiyo, aliniuliza ikiwa ningependa kusindikiza ndugu mwenye alikuwa anatembeza motokari kubwa ili kuenda kupakiza katika mashua vichapo vya kuenda katika dunia yote. Kulikuwa pia na mifuko ya magazeti yenye ilipaswa kupelekwa kwenye biro ya poste ili itumwe katika makutaniko ya Amerika yote. Ndugu Jensen alisema kuwa ingekuwa muzuri nifanye kazi yenye ingeniomba kutumia nguvu ya mwili. Nilikuwa ninapima kilo 57 hivi na nilikuwa mwenye kugonda sana. Safari za kuenda mahali mashua zilizoea kusimama na kuenda kwenye poste zilinitia nguvu kimwili. Ndugu Jensen alijua kabisa kuwa hilo lilikuwa muzuri kwangu!

Idara ya Magazeti ilishugulikia pia ombi za magazeti za kutaniko. Kwa hiyo, nilijua luga zenye kutumiwa ili kuchapisha magazeti yetu katika Brooklyn na kutumwa katika sehemu zingine za ulimwengu. Nilikuwa sijasikia luga nyingi kati ya luga hizo lakini nilifurahi sana kujua kuwa makumi ya maelfu ya magazeti yalikuwa yanatumwa katika maeneo ya mbali sana. Hata kama sikujua hilo wakati huo, ningepata pendeleo la kutembelea maeneo mengi kati ya hayo katika miaka yenye ilikuwa mbele.

Pamoja na Robert Wallen, Charles Molohan, na Don Adams

Katika mwaka wa 1961, nilipewa mugawo wa kutumika katika Biro ya Kuweka Feza yenye ilikuwa inasimamiwa na Grant Suiter. Kisha kutumika miaka fulani katika biro hiyo, niliitwa katika biro ya Nathan Knorr, mwenye alikuwa anasimamia kazi yetu katika dunia yote wakati huo. Aliniambia kuwa ndugu mumoja mwenye alikuwa anatumika katika biro yake angeenda kusoma Masomo ya Huduma ya Ufalme kwa mwezi moja, na kisha angetumikia katika Idara ya Utumishi. Nilipewa mugawo wa kutumika nafasi yake na kutumika pamoja na Don Adams. Bila kuwazia, Don alikuwa ndugu mwenye alikubali ombi langu la kutumika kwenye Beteli kwenye mukusanyiko wa mwaka wa 1955. Ndugu wawili wenye walikuwa tayari wanatumika katika biro hiyo ni Robert Wallen na Charles Molohan. Sisi wote ine tulitumika pamoja kwa zaidi ya miaka 50. Nimepata furaha ya kutumika pamoja na wanaume hao waaminifu wenye kukomaa kiroho!​—Zab. 133:1.

Ziara yangu ya kwanza ya eneo la dunia katika Venezuela, katika mwaka wa 1970

Kuanzia mwaka wa 1970, nilipewa mugawo wa kusafiri kwa majuma fulani kila mwaka ao kila miaka mbili ili kutembelea biro mbalimbali za tawi za Shirika Watch Tower, ili kufanya ziara ya mwangalizi wa eneo la dunia, kama vile iliitwa zamani. Hilo lilitia ndani kutembelea ndugu na dada wa familia za Beteli na wamisionere katika dunia yote, kuwatia moyo kiroho, na kuchunguza dosye za tawi. Nilifurahi sana kukutana na wanafunzi fulani wa kwanza-kwanza wa Masomo ya Gileadi na walikuwa wangali wanatumikia kwa uaminifu katika inchi zingine! Nimepata pendeleo na furaha ya kutembelea zaidi ya inchi 90 katika kazi hiyo.

Nimefurahi sana kutembelea ndugu katika zaidi ya Inchi 90!

NILIPATA BIBI MWAMINIFU

Ndugu na dada wote wa familia ya Beteli ya Brooklyn walitumwa katika makutaniko yenye kuwa katika eneo la Muji wa New York. Mimi nilitumwa katika kutaniko la Bronx. Kutaniko la kwanza katika eneo hilo lilikuwa limekuwa na ongezeko na kuzaa kutaniko lingine. Kutaniko mama liliitwa Kutaniko la Upper Bronx, nilikuwa katika kutaniko hilo.

Katikati ya miaka ya 1960 familia moja ya Mashahidi kutoka Latvia wenye walikuwa wamekubali kweli katika Bronx ya kusini walihamia katika eneo la kutaniko hilo. Livija, mutoto mukubwa mwanamuke wa familia hiyo, akakuwa painia wa kawaida kisha tu kumaliza masomo ya segondere. Kisha miezi kidogo, akahamia katika Massachusetts ili kutumikia katika eneo lenye lilikuwa na lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme. Nilianza kumuandikia ili kumujulisha habari za kutaniko, naye alikuwa ananiandikia juu ya matokeo ya muzuri yenye alipata katika kazi ya kuhubiri katika eneo la Boston.

Niko pamoja na Livija

Kisha kupita miaka kidogo, Livija aliwekwa kuwa painia wa pekee. Alipenda kufanya mengi zaidi katika kazi ya Yehova, kwa hiyo, alijaza ombi la kutumika kwenye Beteli, na alialikwa mwaka wa 1971. Hilo lilionekana kuwa jibu kutoka kwa Yehova! Tarehe 27 Mwezi wa 10, 1973, tulioana na tulipata pendeleo la kutolewa hotuba ya ndoa na Ndugu Knorr. Methali 18:22 inasema hivi: ‘Je, mutu amepata muke [bibi] mwema? Amepata kitu chema, na mutu anapata nia njema kutoka kwa Yehova.’ Kwa hiyo, mimi na Livija tumepata pendeleo la kutumikia kwenye Beteli kwa zaidi ya miaka 40. Na tunaendelea kutegemeza kutaniko lenye kuwa katika eneo hilo la Bronx.

KUTUMIKA BEGA KWA BEGA PAMOJA NA NDUGU ZA KRISTO

Kutumika pamoja na Ndugu Knorr kuliniletea furaha kabisa. Alikuwa anatumika kwa bidii kwa ajili ya kweli na alikuwa mwenye shukrani sana kwa wamisionere wenye kutumika katika dunia yote. Wengi kati yao walikuwa Mashahidi wa kwanza katika inchi mbalimbali kwenye walitumwa. Nilihuzunika sana kuona Ndugu Knorr anasumbuliwa na ugonjwa wa kansere katika mwaka 1976. Wakati fulani, wakati hakukuwa tena anatoka kwenye kitanda, aliniomba nimusomee habari fulani zenye zilikuwa zinatayarishwa ili kuchapishwa. Aliniomba nimuitie Frederick Franz ili akuje pia na kusikiliza usomaji huo. Nilifikia kujua kwamba, kwa sababu Ndugu Franz hakukuwa anaona tena muzuri, Ndugu Knorr alikuwa ametumia wakati mwingi ili kumusomea habari kama hizo.

Katika ziara ya eneo la dunia pamoja na Daniel Sydlik na Marina katika mwaka wa 1977

Ndugu Knorr alikufa katika mwaka wa 1977, lakini wale wenye walimujua na kumupenda, walifarijiwa kwa sababu alikuwa amefikia mwisho wa maisha yake hapa duniani kwa uaminifu. (Ufu. 2:10) Kisha hapo, Ndugu Franz alianza kusimamia kazi yetu.

Wakati huo, nilikuwa mwandishi wa Ndugu Milton Henschel, mwenye alitumika pamoja na Ndugu Knorr kwa miaka mingi. Ndugu Henschel aliniambia kuwa mugawo wangu wa kwanza kwenye Beteli ulikuwa sasa kumusaidia Ndugu Franz katika njia yoyote yenye alihitaji kusaidiwa. Nilimusomea kwa ukawaida habari mbele zichapishwe. Ndugu Franz alikuwa na uwezo mukubwa wa kuweka mambo katika akili, na kukazia kabisa akili mambo yenye yalikuwa yanasomwa. Nilifurahi kumusaidia mupaka mwisho wa maisha yake hapa duniani katika Mwezi wa 12, 1992!

124 Columbia Heights, kwenye nilitumikia kwa miaka mingi

Miaka 61 yenye nimefanya kwenye Beteli imepita mbio. Wazazi wangu wote wawili walikufa waaminifu kwa Yehova, na ninangojea kwa hamu kuwakaribisha katika ulimwengu mupya. (Yoh. 5:28, 29) Hakuna kitu chenye ulimwengu huu unatoa chenye kinaweza kulinganishwa na pendeleo la ajabu la kutumika pamoja na wanaume na wanawake waaminifu kwa ajili ya watu wa Mungu katika dunia yote. Mimi na Livija tunaweza kusema kwa uhakika kuwa katika miaka yetu ya utumishi wa wakati wote, ‘shangwe ya Yehova [imekuwa] ngome yetu.’​—Neh. 8:10.

Kazi ya kuhubiri kweli za Ufalme inaendelea na haitegemee mutu yeyote katika tengenezo la Yehova. Nimepata furaha na pendeleo la kutumika kwa miaka mingi pamoja ndugu na dada washikamanifu na wenye kujitoa. Wengi kati ya watiwa-mafuta wenye nilitumika pamoja nao, hawako tena hapa dunia. Lakini niko mwenye shukrani kwa sababu nimetumika katika kazi ya Yehova pamoja na watu hao waaminifu na wenye kukomaa kiroho.