Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uendelee Kumutumikia Yehova kwa Furaha

Uendelee Kumutumikia Yehova kwa Furaha

UFIKIRIE siku yenye furaha zaidi katika maisha yako. Je, ni siku yenye ulioa ao kuolewa, ao ni siku yenye mutoto wako wa kwanza alizaliwa? Ao ni siku yenye ulibatizwa? Inawezekana siku hiyo ndiyo ilikuwa ya maana sana na yenye furaha zaidi katika maisha yako. Pia, siku hiyo ndugu na dada zako walifurahi sana kuona namna ulionyesha kwamba unamupenda Mungu kwa moyo wako wote, kwa nafsi yako yote, kwa akili yako yote, na kwa nguvu zako zote!—Marko 12:30.

Inawezekana, tangu wakati ulibatizwa umepata furaha nyingi katika kazi ya Yehova. Lakini, furaha yenye wahubiri fulani walikuwa nayo wakati walibatizwa imepunguka. Sababu gani? Sababu gani tunapaswa kuendelea kumutumikia Yehova kwa furaha?

SABABU GANI WAHUBIRI FULANI WAMEPOTEZA FURAHA YAO

Ujumbe wa Ufalme unatuletea furaha nyingi. Sababu gani? Kwa sababu Yehova ameahidi kwamba hivi karibuni Ufalme wake utaharibu ulimwengu huu muovu na kuleta dunia mupya. Sefania 1:14 inasema hivi: ‘Siku kubwa ya Yehova iko karibu. Iko karibu, nayo inaharakisha sana!’ Lakini, ikiwa tunaona kwamba tumengojea sana siku hiyo kuliko namna tuliwazia, tunaweza kupoteza furaha yenye tulikuwa nayo mbele. Hilo linaweza kufanya tupunguze bidii yetu katika kazi ya Mungu.—Methali 13:12.

Kupitisha wakati pamoja na ndugu na dada zetu kunatuchochea tuendelee kumutumikia Yehova kwa furaha. Pengine mwenendo muzuri wa Mashahidi wa Yehova ndio ulituchochea tukubali ibada ya kweli na kutusaidia tuanze kumutumikia Mungu kwa furaha. (1 Petro 2:12) Lakini, tunaweza kufanya nini ikiwa ndugu ao dada fulani anakaripiwa kwa sababu hakutii amri za Mungu? Hilo linaweza kufanya ndugu ao dada fulani katika kutaniko wavunjike moyo na kupoteza furaha yao.

Kupenda sana vitu vya kimwili kunaweza pia kutufanya tupoteze furaha yetu. Namna gani? Ulimwengu wa Shetani unatuchochea tuuze vitu fulani vyenye hatuna navyo lazima kabisa. Kwa hiyo, tunapaswa kukumbuka maneno haya ya Yesu: ‘Hakuna anayeweza kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana ama [ao] atamuchukia mumoja na kumupenda yule mwingine, ama atashikamana na mumoja na kumuzarau yule mwingine. Hamuezi kutumikia Mungu na Utajiri.’ (Mathayo 6:24) Hatuwezi kumutumikia Yehova kwa furaha na wakati uleule kujaribu kupata kila kitu chenye kuwa katika ulimwengu huu.

KUPATA FURAHA KATIKA KAZI YA YEHOVA

Wale wenye wanamupenda Yehova hawaone kwamba kumutumikia ni muzigo muzito. (1 Yohana 5:3) Kumbuka kwamba Yesu alisema hivi: ‘Mukuje kwangu, nyote munaotaabika [wenye kuteseka] na kulemewa na mizigo, nami nitawaburudisha [nitawachangamucha] ninyi. Muchukue nira yangu na mujifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mwenye tabia-pole na munyenyekevu moyoni, nanyi mutapata burudisho kwa ajili ya nafsi zenu. Kwa maana nira yangu ni laini na muzigo wangu ni mwepesi.’ (Mathayo 11:28-30) Kuwa Mukristo wa kweli kunachangamusha na kunatuletea furaha. Tuko na sababu nzuri za kumutumikia Yehova kwa furaha. Tuchunguze basi sababu tatu kati ya sababu hizo.—Habakuki 3:18.

Tunatumikia Mupaji-Uzima wetu, Mungu mwenye furaha. (Matendo 17:28; 1 Timotheo 1:11) Tunajua kwamba ni Muumbaji wetu ndiye alitupatia uzima. Tuendelee basi kumutumikia kwa furaha, hata kama tumebatizwa tangu miaka mingi.

Héctor anaendelea kuwa na furaha kwa sababu anakumbuka tumaini lake la Ufalme na anaendelea kuhubiri kwa bidii

Tuzungumuzie mufano wa ndugu Héctor, mwenye amekuwa mwangalizi wa muzunguko kwa miaka 40. Hata wakati wa uzee anaendelea kumutumikia Yehova kwa furaha. (Zaburi 92:12-14) Magonjwa ya bibi yake imemuzuia kufanya mengi zaidi katika kazi ya Mungu, lakini Héctor anaendelea kuwa na furaha. Anasema hivi: “Kuona namna afya ya bibi yangu inaendelea kuwa mubaya kunaniletea huzuni na imekuwa vigumu kumuhangaikia; lakini sikuacha hali hiyo inifanye nipoteze furaha yangu katika kazi ya Mungu. Kujua kwamba Yehova, mwenye aliumba mwanadamu kwa kusudi fulani, ndiye alinipatia uzima, kunafanya nimupende sana na kumutumikia kwa moyo wote. Ninajikaza kuhubiri kwa bidii, na ninajikaza kuchunga tumaini la Ufalme pa nafasi ya kwanza katika akili yangu ili nisipoteze furaha yangu.”

Yehova ametoa zabihu ya ukombozi, na hilo linatusaidia tukuwe na maisha yenye furaha. Kwa kweli, ‘Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu anayemuamini asiangamizwe [asiharibiwe] bali akuwe na uzima wa milele.’ (Yohana 3:16) Ndiyo, tunaweza kusamehewa zambi zetu na kupata uzima wa milele ikiwa tunaonyesha imani katika zawadi yenye upendo ya Mungu, ni kusema, zabihu ya ukombozi. Kwa kweli, hiyo ni sababu nzuri zaidi ya kuonyesha shukrani! Pia, kuonyesha shukrani juu ya zabihu ya ukombozi kutatuchochea tumutumikie Yehova kwa furaha.

Jesús alifanya maisha yake yakuwe mepesi na alimutumikia Yehova kwa furaha kwa miaka mingi

Ndugu Jesús, mwenye aliishi Meksiko, alisema hivi: “Nilikuwa mutumwa wa kazi, wakati fulani nilitumika saa nyingi sana hata kama sikulazimishwa kufanya hivyo. Nilifanya hivyo ili nipate feza nyingi. Kisha nilijifunza juu ya Yehova na namna amemutoa Mutoto wake mupendwa kwa ajili ya wanadamu. Nilikuwa na tamaa kubwa ya kumutumikia. Kwa hiyo, nilitoa maisha yangu kwa Yehova, na niliamua kuacha kazi yangu yenye nilikuwa nimefanya kwa miaka 28, ili nianze utumishi wa wakati wote.” Sasa, Jesús alianza kumutumikia Yehova kwa furaha.

Kuwa na mwenendo muzuri kunatuletea furaha katika maisha. Unakumbuka maisha yako yalikuwa namna gani mbele ufikie kumujua Yehova? Mutume Paulo alikumbusha Wakristo katika muji wa Roma kwamba ‘[wakati fulani] walikuwa watumwa wa zambi’ lakini wamekuwa “watumwa wa uadilifu [haki].” Walikuwa na tumaini la kuishi milele kwa sababu walifanya mabadiliko katika maisha yao. (Waroma 6:17-22) Sisi pia tunatii kanuni za Yehova; kwa hiyo, tunaepuka kupata huzuni yenye inapata watu wenye kuwa na mwenendo mubaya ao maisha yenye kujaa jeuri. Hilo linatuletea furaha kubwa sana!

“Miaka yenye furaha zaidi katika maisha yangu ni ile yenye nimefanya katika kazi ya Yehova.”—Jaime

Tuzungumuzie mufano wa Jaime; alikuwa mupiganaji wa ngumi, alikuwa anaamini mageuzi, na hakuwa anaamini kwamba Mungu iko. Jaime alianza kuhuzuria mikutano ya Kikristo, na upendo wenye aliona kati ya ndugu na dada uligusa moyo wake. Ili aache maisha yake ya zamani, Jaime alimuomba Yehova amusaidie akuwe na imani katika Yeye. Jaime anasema hivi: “Polepole, nilivumbua kwamba kuna Baba mwenye upendo na Mungu mwenye rehema. Kutii kanuni za haki za Yehova kumenilinda. Ikiwa sikufanya mabadiliko katika maisha yangu, ningekuwa tayari nimekufa, kama marafiki wangu wa zamani wenye walikuwa pia wapiganaji wa ngumi. Miaka yenye furaha zaidi katika maisha yangu ni ile yenye nimefanya katika kazi ya Yehova.”

USICHOKE!

Tunapaswa kujisikia namna gani wakati tunangojea mwisho wa ulimwengu huu muovu? Kumbuka kwamba, tunafanya mapenzi ya Mungu na tunangojea uzima wa milele. ‘Kwa hiyo na tusife moyo katika kufanya yaliyo mema, kwa maana katika majira yanayofaa tutavuna ikiwa hatuchoke kabisa.’ (Wagalatia 6:8, 9) Yehova atusaidie basi ili tuendelee kuvumilia, tujikaze sana ili kukomalisha sifa zenye tuko nazo lazima ili kuokoka ‘ziki kubwa [mateso makubwa],’ na kuendelea kumutumikia kwa furaha.—Ufunuo 7:9, 13, 14; Yakobo 1:2-4.

Tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atabariki uvumilivu wetu kwa sababu anajua kazi yenye tunafanya na upendo wenye tunamuonyesha na jina lake. Ikiwa tunaendelea kumutumikia kwa furaha, tutakuwa kama Daudi, mwandikaji wa zaburi, mwenye alisema hivi: ‘Nimemuweka Yehova mbele yangu daima [sikuzote]. Kwa sababu yuko upande wa mukono wangu wa kuume, sitatikiswa. Kwa hiyo, moyo wangu unashangilia, nao utukufu wangu una mwelekeo wa kuwa na shangwe. Pia, mwili wangu mwenyewe utakaa katika usalama [nitaishi katika usalama].’—Zaburi 16:8, 9.