Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mwanaume mwenye kuwa na kidau cha wino anafananisha Yesu Kristo. Yeye ndiye anatia alama wale wenye wataokolewa

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Katika maono ya Ezekieli, mwanaume mwenye kuwa na kidau (chupa) cha wino na wanaume sita wenye kuwa na silaha za kuponda wanafananisha nani?

Wanafananisha majeshi ya mbinguni yenye yalitumikishwa ili kuharibu Yerusalemu na yenye yatatumikishwa ili kuharibu ulimwengu muovu wa Shetani kwenye vita ya Har-magedoni. Hayo ni mafasirio ya mupya. Sababu gani tulikuwa na lazima mafasirio hayo?

Mbele ya mwaka 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Yehova alimuonyesha Ezekieli mambo yenye yangefanyika katika muji wa Yerusalemu mbele uharibiwe. Katika maono hayo, Ezekieli aliona mambo mengi ya mubaya yenye yalikuwa yanafanyika katika muji huo. Kisha aliona wanaume sita, kila mumoja wao alikuwa na ‘silaha yake ya kuponda mukononi mwake.’ Kulikuwa pia mwanaume fulani pamoja nao mwenye alikuwa ‘anavaa kitani’ na alikuwa na “kidau cha wino.” (Ezekieli 8:6-12; 9:2, 3) Mwanaume huyo aliambiwa apite katikati ya muji ‘na kutia alama kwenye mapaji ya uso ya watu wanaougua na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayofanywa katikati yake.’ Kisha, wanaume sita wenye kuwa na silaha waliambiwa waue watu wote katika muji wenye hawakukuwa na alama hiyo. (Ezekieli 9:4-7) Maono hayo yanaweza kutufundisha nini, na mwanaume mwenye kuwa na kidau cha wino ni nani?

Ezekieli alipata maono hayo katika mwaka wa 612 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Unabii huo ulitimizwa kwanza miaka tano kisha hapo, wakati Yehova aliacha jeshi la Babiloni liharibu Yerusalemu. Kwa kufanya hivyo, Yehova alitumikisha Wababiloni ili kupatia malipizi watu wake wenye walikosa utii. (Yeremia 25:9, 15-18) Lakini ni nini ilifikia Wayahudi waaminifu wenye walichukia mambo yote ya mubaya yenye yalikuwa yanafanyika katika muji huo? Yehova alikamata mipango ili waokolewe.

Katika maono hayo, Ezekieli hakutia mutu yeyote alama ya kwelikweli na hakuchangia katika uharibifu wa muji. Lakini, malaika ndio waliongoza uharibifu wa Yerusalemu. Kwa hiyo, unabii huo unatusaidia kuelewa mambo yenye kufanyika mbinguni. Yehova aliambia malaika zake wafanye mipango ya kuharibu watu waovu na kuhakikisha kama watu wenye haki waliokolewa. *

Unabii huo utatimia pia wakati unaokuja. Zamani tulikuwa tunasema kama ule mutu mwenye kuwa na kidau cha wino anafananisha Wakristo watiwa-mafuta wenye wangali katika dunia. Pia, tulikuwa tunasema kama watu walikuwa wanatiwa alama ya wokovu wakati walikuwa wanasikiliza na kukubali habari njema yenye tunahubiri. Lakini, hivi karibuni ilionekana wazi kama ilikuwa lazima tubadilishe namna tunafasiria unabii huo. Tumejifunza katika andiko la Mathayo 25:31-33 kama Yesu ndiye anahukumu watu. Atafanya hivyo wakati unaokuja wakati wa ziki kubwa (taabu kubwa). Wakati huo, wale wenye watahukumiwa kuwa kondoo wataokolewa, na wale wenye watahukumiwa kuwa mbuzi wataharibiwa.

Kwa hiyo, maono ya Ezekieli yanatufundisha nini? Yanatufundisha mambo tano haya:

  1. Mbele ya uharibifu wa Yerusalemu, Ezekieli, Yeremia, na Isaya, walionya watu juu ya mambo yenye yangefanyika katika muji huo. Walikuwa kama vile walinzi. Leo, Yehova anatumikisha kikundi kidogo cha watiwa-mafuta ili kufundisha watu wake na kuonya wengine mbele ziki kubwa ianze. Kwa kweli, watu wote wa Mungu, ni kusema, watumishi wa nyumbani wa Kristo, wanafanya kazi hiyo ya kuonya.—Mathayo 24:45-47.

  2. Ezekieli hakutia alama wale wenye wangeokolewa. Vilevile watumishi wa Mungu hawafanye hivyo leo. Wanahubiria tu wengine habari njema na kuwaonya juu ya mambo yenye yatatokea wakati unaokuja. Kazi hiyo ya kuhubiri katika dunia yote inafanyika kwa musaada wa malaika.—Ufunuo 14:6.

  3. Wale wenye waliokolewa katika siku za Ezekieli, hakukuwa na alama ya kwelikweli juu ya uso wao. Leo, wale wenye wataokolewa hawatakuwa na alama ya kwelikweli. Watu wanapaswa kufanya nini ili waokoke ziki kubwa? Wakati wanasikia onyo hilo, wanapaswa kujifunza kumuiga Yesu, kujitoa kwa Mungu, na kuunga mukono ndugu za Kristo kwa kuhubiri habari njema. (Mathayo 25:35-40) Wakati wa ziki kubwa, watu hao watapata alama, ni kusema, watachaguliwa ili waokoke.

  4. Mwanaume mwenye kuwa na kidau cha wino anafananisha Yesu. Wakati wa ziki kubwa, Yesu atatia mukutano mukubwa wa watu alama wakati anawahukumu kuwa kondoo. Kisha wataishi milele hapa duniani.—Mathayo 25:34, 46. *

  5. Leo, wale wanaume sita wenye kuwa na silaha za kuponda wanafananisha majeshi ya mbinguni yenye kuongozwa na Yesu. Wataharibu hivi karibuni mataifa na kumaliza uovu wote.—Ezekieli 10:2, 6, 7; Ufunuo 19:11-21.

Mambo yenye tunajifunza katika maono haya yanatusaidia tukuwe hakika kama Yehova hataharibu watu wenye haki pamoja na watu wabaya. (2 Petro 2:9; 3:9) Pia, yanatukumbusha kama kazi ya kuhubiri ni ya maana sana wakati wetu. Kila mutu anapaswa kusikia onyo mbele mwisho ufike!—Mathayo 24:14.

^ fu. 6 Wale wenye waliokolewa, kama vile Baruku (mwandishi wa Yeremia), Muethiopia Ebed-meleki, na Warekabu, hawakukuwa na alama ya kwelikweli kwenye nyuso zao. (Yeremia 35:1-19; 39:15-18; 45:1-5) Alama hiyo ya mufano ilionyesha tu kama wangeokolewa.

^ fu. 12 Watiwa-mafuta waaminifu hawatakuwa na lazima ya kutiwa alama ili waokolewe. Lakini, watatiwa muhuri kwa mara ya mwisho iwe mbele ya kufa ao mbele ziki kubwa ianze.—Ufunuo 7:1, 3.