Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Roho Inatoa Ushahidi Pamoja na Roho Yetu

Roho Inatoa Ushahidi Pamoja na Roho Yetu

‘Roho yenyewe inatoa ushahidi pamoja na roho yetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu.’WAROMA 8:16.

NYIMBO: 109, 108

1-3. Ni matukio gani yenye ilifanya siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 ikuwe ya pekee, na namna gani matukio hayo ilitimiza mambo yenye Maandiko ilikuwa imetabiri? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

NI SIKU YA YENGA asubuhi huko Yerusalemu. Siku hiyo ni ya pekee na yenye kufurahisha. Watu wanafanya sikukuu ya Pentekoste, yenye ilikuwa sikukuu takatifu yenye ilifanywa mwanzoni mwa mavuno ya ngano. Kama kawaida, asubuhi hiyo kuhani mukubwa anatoa zabihu kwenye hekalu. Kisha, saa tatu (9h00) hivi, anatoa mikate mbili yenye kuwa na chachu, yenye ilifanywa na ngano ya kwanza ao matunda ya kwanza ya mavuno. Kuhani mukubwa anatikisa mikate hiyo huku na huku ili kuitoa kwa Yehova. Hiyo ni Pentekoste ya mwaka wa 33.—Walawi 23:15-20.

2 Kila mwaka, kuhani mukubwa alikuwa anafanya toleo hilo la kutikiswa. Toleo hilo lilihusu kabisa jambo fulani la maana sana lenye lilitokea kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33. Jambo hilo liliwafikia wanafunzi 120 wa Yesu wenye walikuwa wanasali pamoja katika chumba kimoja cha juu huko Yerusalemu. (Matendo 1:13-15) Kulikuwa kumepita miaka 800 tangu nabii Yoeli atabiri tukio hilo. (Yoeli 2:28-32; Matendo 2:16-21) Ni jambo gani la maana sana lenye lilitokea?

3 Soma Matendo 2:2-4. Kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33, Mungu aliwapatia Wakristo hao roho yake takatifu, kwa hiyo, wakakuwa watiwa-mafuta. (Matendo 1:8) Kisha, watu wengi wakaanza kuwakaribia, na wanafunzi hao wakaanza kusema mambo ya ajabu yenye walitoka tu kuona na kusikia. Mutume Petro alieleza jambo lenye lilikuwa tu limetokea na sababu gani lilikuwa la maana sana. Kwa hiyo, aliambia watu hao hivi: ‘Mutubu, na muache kila mumoja wenu abatizwe katika jina la Yesu Kristo kwa musamaha wa zambi zenu, na ninyi mutapokea zawadi ya bure ya roho takatifu.’ Siku hiyo, watu 3000 hivi walibatizwa, nao pia wakapokea roho takatifu.—Matendo 2:37, 38, 41.

4. (a) Sababu gani tunapaswa kupendezwa na mambo yenye ilitokea kwenye Pentekoste? (b) Ni jambo lingine gani la maana lenye pengine lilifanywa siku hiyohiyo miaka mingi mbele ya hapo? (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.)

4 Kuhani mukubwa alifananisha nani, na toleo lenye alikuwa anafanya siku ya Pentekoste lilifananisha nini? Kuhani mukubwa alifananisha Yesu. Mikate ilifananisha wanafunzi watiwa-mafuta wa Yesu. Wanafunzi hao wamechaguliwa kati ya wanadamu wenye zambi na wanaitwa “matunda ya kwanza.” (Yakobo 1:18) Mungu amewakubali wanadamu hao kuwa watoto wake na amewachagua ili wakuwe wafalme pamoja na Yesu katika Ufalme wake. (1 Petro 2:9) Yehova atatumia Ufalme wake ili kuletea baraka wanadamu wote wenye kumutii. Kwa hiyo, iwe tutaishi mbinguni pamoja na Yesu ao katika paradiso duniani, Pentekoste ya mwaka wa 33 ni ya maana sana kwetu. [1] —Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.

NI NINI INATOKEA WAKATI MUTU ANATIWA MAFUTA?

5. Namna gani tunajua kwamba wale wote wenye wametiwa mafuta hawatiwe mafuta kwa njia moja?

5 Wanafunzi wenye walikuwa katika chumba cha juu hawangesahau hata kidogo siku hiyo. Kila mumoja wao alikuwa na kitu fulani chenye kuwaka kama moto juu ya kichwa chake. Yehova aliwapatia uwezo wa kusema katika luga zingine. Walikuwa hakika kwamba walikuwa wametiwa mafuta kupitia roho takatifu. (Matendo 2:6-12) Lakini, Wakristo wote hawaone jambo hilo lenye kushangaza wakati wanatiwa mafuta. Kwa mufano, Biblia haiseme kwamba kitu fulani chenye kuwaka kama moto kilionekana juu ya vichwa vya watu wengine wengi wenye walitiwa mafuta katika Yerusalemu siku hiyo. Lakini, walitiwa mafuta wakati walibatizwa. (Matendo 2:38) Pia, Wakristo wote hawatiwe mafuta wakati wanabatizwa. Wasamaria walitiwa mafuta muda fulani kisha kubatizwa. (Matendo 8:14-17) Na jambo la pekee lilifanyika: Kornelio na watu wa nyumba yake walitiwa mafuta mbele ya kubatizwa.—Matendo 10:44-48.

6. Wakristo wote watiwa-mafuta wanapokea nini, na hilo linakuwa na matokeo gani juu yao?

6 Ni wazi kwamba Wakristo wanatambua kwa njia mbalimbali kwamba wametiwa mafuta. Pengine, wamoja wametambua palepale kwamba Yehova aliwatia mafuta. Wengine walitambua jambo hilo kisha muda fulani. Lakini mutume Paulo alieleza jambo lenye linamufikia kila mutiwa-mafuta. Alisema hivi: ‘Baada ya ninyi kuamini, mulitiwa muhuri kwa roho takatifu iliyoahidiwa, ambayo ni rehani [uhakikisho] ya kimbele ya uriti wetu.’ (Waefeso 1:13, 14) Kwa hiyo, Yehova anatumia roho yake takatifu ili kuhakikishia kabisa Wakristo hao kwamba amewachagua ili waende mbinguni. Kwa njia hiyo, roho takatifu “ni rehani ya kimbele,” ao jambo lenye kuwahakikishia kwamba wakati unaokuja wataishi milele mbinguni, hawataishi tena katika dunia.—Soma 2 Wakorintho 1:21, 22; 5:5.

Kila Mukristo mutiwa-mafuta hapaswe kuruhusu jambo fulani limuzuie kumutumikia Yehova

7. Kila Mukristo mutiwa-mafuta anapaswa kufanya nini ili apate zawadi yake ya kuenda mbinguni?

7 Wakati Mukristo anatiwa mafuta, je, hilo linamaanisha mara moja kwamba atapokea zawadi yake? Hapana. Anakuwa hakika kwamba amealikwa kuenda mbinguni. Lakini atapata zawadi yake ikiwa tu anabakia muaminifu kwa Yehova. Mutume Petro alieleza jambo hilo kwa kusema hivi: ‘Kwa sababu hiyo, akina ndugu, mufanye hata zaidi yote munayoweza ili kufanya mwito na kuchaguliwa kwenu kukuwe hakika kwa ajili yenu wenyewe; kwa maana mukiendelea kufanya mambo hayo, hamutashindwa hata kidogo. Kwa kweli, hivyo ndivyo mutakavyowezeshwa kwa wingi kuingia katika Ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.’ (2 Petro 1:10, 11) Kwa hiyo, kila Mukristo mutiwa-mafuta hapaswe kuruhusu jambo fulani limuzuie kumutumikia Yehova. Hata kama amealikwa, ao kuitwa, ili kuenda mbinguni, anaweza kukosa zawadi hiyo ikiwa haendelee kuwa mwaminifu.—Waebrania 3:1; Ufunuo 2:10.

NAMNA GANI MUTU ANAJUA KWAMBA AMETIWA MAFUTA?

8, 9. (a) Sababu gani watu wengi wanashindwa kuelewa muzuri jambo lenye kufanyika wakati mutu fulani anatiwa mafuta? (b) Mutu anajua namna gani kwamba amepata mwaliko wa kuenda mbinguni?

8 Leo, watumishi wengi wa Mungu wanaweza kushindwa kuelewa muzuri jambo lenye kufanyika wakati Mungu anatia mutu fulani mafuta. Hiyo ni kweli kwa sababu hawako watiwa-mafuta. Mungu aliumba wanadamu ili waishi milele duniani, hakuwaumba ili waishi mbinguni. (Mwanzo 1:28; Zaburi 37:29) Lakini Yehova amechagua wanadamu fulani ili wakuwe wafalme na makuhani huko mbinguni. Wakati anawatia mafuta, tumaini na mawazo yao vinabadilika kabisa. Kwa hiyo, wanangojea kuishi mbinguni.—Soma Waefeso 1:18.

9 Lakini, namna gani mutu anajua kwamba amepata mwaliko wa kuenda mbinguni? Ona jambo lenye mutume Paulo aliwaambia Wakristo watiwa-mafuta wa Roma, wenye ‘waliitwa wakuwe watakatifu.’ Aliwaandikia hivi: “Hamukupokea roho ya utumwa inayosababisha uoga tena, bali [lakini] mulipokea roho ya kufanywa kuwa wana, roho ambayo kupitia hiyo tunapaaza sauti: ‘Abba, Baba!’ Roho yenyewe inatoa ushahidi pamoja na roho yetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu.” (Waroma 1:7; 8:15, 16) Kupitia roho yake takatifu, Mungu anamuhakikishia mutu kwamba amemualika kutawala pamoja na Yesu huko mbinguni.—1 Wathesalonike 2:12.

10. Andiko la 1 Yohana 2:27 linamaanisha nini wakati linasema kwamba Mukristo mutiwa-mafuta hana lazima mutu fulani amufundishe?

10 Wale wenye Mungu amealika ili waende mbinguni hawana lazima mutu fulani awaambie kwamba wametiwa mafuta. Yehova anawahakikishia jambo hilo. Mutume Yohana aliambia Wakristo watiwa-mafuta hivi: ‘Mumepata kutiwa mafuta kutoka kwa yule mutakatifu; ninyi nyote muna ujuzi.’ Alisema pia hivi: ‘Kwa habari yenu, kule kutiwa mafuta ambako mulipokea kutoka kwake kunakaa ndani yenu, nanyi hamuhitaji yeyote akuwe akiwafundisha; lakini, kama vile kutiwa mafuta kutoka kwake kunavyowafundisha ninyi juu ya mambo yote, na ni kweli wala si uongo. Na kama vile kumewafundisha ninyi, mukae katika muungano na yeye.’ (1 Yohana 2:20, 27) Watiwa-mafuta wako na lazima ya kufundishwa na Yehova kama vile Wakristo wengine wote. Lakini hawana lazima mutu fulani awahakikishie kwamba wametiwa mafuta. Yehova ametumia nguvu yake kubwa zaidi, ni kusema, roho yake takatifu ili kuwahakikishia kabisa kwamba wametiwa mafuta!

‘WANAZALIWA TENA’

11, 12. Mukristo mwenye ametiwa mafuta anaweza kujiuliza nini, lakini iko hakika na jambo gani?

11 Wakati Wakristo wanatiwa mafuta kwa roho takatifu, wanabadilika kabisa. Ndiyo sababu Yesu alisema kwamba ‘wanazaliwa tena’ ao “wanazaliwa kutoka juu.” (Yohana 3:3, 5) Kisha alieleza hivi: ‘Usistaajabu [usishangae] kwa sababu nimekuambia: Ninyi lazima muzaliwe tena. Upepo unavuma mahali ambapo unataka, na wewe unasikia muvumo wake, lakini haujue mahali ambapo huo unatoka wala mahali unapoenda. Ndivyo alivyo kila mutu ambaye amezaliwa kwa roho.’ (Yohana 3:7, 8) Ni wazi kwamba, ni vigumu kabisa kufasiria mutu mwenye hajatiwa mafuta namna mutu anajisikia wakati anatiwa mafuta. [2]—Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.

Mutu mwenye ametiwa mafuta iko hakika kwamba Yehova amemuchagua

12 Mutu mwenye ametiwa mafuta anaweza kujiuliza hivi: ‘Sababu gani Yehova amenichagua mimi kuliko kuchagua mutu mwengine?’ Anaweza hata kujiuliza ikiwa iko na uwezo wa kutimiza daraka hilo. Lakini iko hakika kwamba Yehova amemuchagua. Kwa kweli, anafurahi sana na ni mwenye shukrani kwa sababu ya zawadi hiyo. Watiwa-mafuta wanajisikia namna mutume Petro alijisikia wakati aliandika hivi: ‘Abarikiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, kwa maana kulingana na rehema yake kubwa alituzaa sisi upya kwenye tumaini lililo hai kupitia ufufuo wa Yesu Kristo kutoka kwa wafu, kwenye uriti usioharibika na usiotiwa unajisi [uchafu] na usiofifia. Huo umewekwa akiba mbinguni kwa ajili yenu.’ (1 Petro 1:3, 4) Wakati watiwa-mafuta wanasoma maneno hayo, wako hakika kabisa kwamba Baba yao anasema nao moja kwa moja.

13. Wakati mutu anatiwa mafuta kwa roho takatifu, namna gani mawazo yake inabadilika, na ni nini inaleta mabadiliko hayo?

13 Mbele Yehova awaalike Wakristo hao waende mbinguni, walikuwa na tumaini la kuishi milele duniani. Walikuwa wanangojea wakati Yehova atafanya dunia ikuwe paradiso na kutosha mambo yote mabaya. Pengine walikuwa wanawaza namna watapokea mutu fulani wa familia ao rafiki yao wakati wa ufufuo. Na walikuwa wanangojea wakati watajenga nyumba na kuishi ndani ao kupanda miti na kula matunda yake. (Isaya 65:21-23) Sababu gani mawazo yao imebadilika? Wanabadilika kwa sababu walivunjika moyo ao kuteseka sana? Wameamua mara moja kwamba watachoka kuishi milele katika dunia na kwamba hawatakuwa na furaha? Ao wanapenda tu kuishi maisha ya mbinguni? Hapana. Lakini, Mungu ndiye anachukua uamuzi huo. Wakati anawaalika, anatumia roho yake takatifu ili kubadilisha mawazo na tumaini lao.

14. Watiwa-mafuta wanaona namna gani maisha yao hapa duniani?

14 Sasa, ni kusema kwamba watiwa-mafuta wanapenda wakufe? Mutume Paulo alieleza namna watiwa-mafuta wanajisikia. Alilinganisha mwili wa mwanadamu na “hema,” kisha alisema hivi: “Kwa kweli, sisi tulio katika hema hili tunaugua [tunateseka], tukilemewa; kwa sababu tunataka, si kulivua, bali kuvaa lile lingine, ili uhai [uzima] ukimeze kile kinachoweza kufa.” (2 Wakorintho 5:4) Wakristo hao hawapendi wakufe. Wanapenda kuishi na wanataka kutumia kila siku maisha yao ili kumutumikia Yehova pamoja na familia na marafiki wao. Lakini, katika mambo yote yenye wanafanya, wanakumbuka yote yenye Yehova amewaahidi kwa ajili ya wakati unaokuja.—1 Wakorintho 15:53; 2 Petro 1:4; 1 Yohana 3:2, 3; Ufunuo 20:6.

YEHOVA AMEKUALIKA?

15. Ni nini haiwezi kuonyesha kwamba Mukristo ametiwa mafuta kwa roho takatifu?

15 Pengine unajiuliza ikiwa Yehova amekualika uende mbinguni. Ikiwa unaona hivyo, ufikirie maulizo haya ya maana: Unaona kuwa uko na bidii sana katika kazi ya kuhubiri? Unafurahia kabisa kujifunza Biblia na kujua “mambo mazito ya Mungu”? (1 Wakorintho 2:10) Unaona kuwa Yehova amekusaidia kupata matokeo mazuri zaidi katika kazi ya kuhubiri? Unafurahia zaidi kufanya mapenzi ya Yehova kuliko mambo mengine yote? Unapenda kabisa wengine na unaona kwamba uko na daraka kubwa la kuwasaidia wamutumikie Yehova? Umejionea namna Yehova amekusaidia katika sehemu mbalimbali ya maisha yako? Ikiwa unajibu ndiyo kwa maulizo hayo yote, hilo linamaanisha kwamba umepata mwaliko wa kuenda mbinguni? Hapana. Sababu gani? Kwa sababu watumishi wote wa Mungu wanaona hivyo, iwe ni watiwa-mafuta ao hapana. Yehova anaweza kutumia roho yake takatifu ili kupatia watumishi wake wote uwezo uleule, hata kama wako na tumaini la kuishi mbinguni ao duniani. Kwa kweli, ikiwa unajiuliza kama utaenda mbinguni, hilo linamaanisha kwamba haujapata mwaliko wa kuenda mbinguni. Wale wenye Yehova amechagua hawajiulize hivyo! Wanajua!

16. Ni nini inaonyesha kwamba watu wote wenye walipata roho takatifu ya Mungu hawakualikwa kuenda mbinguni?

16 Biblia inazungumuzia mifano mingi ya watumishi waaminifu wenye walipata roho takatifu ya Yehova lakini hawakuenda mbinguni. Yohana Mubatizaji iko kati ya watu hao. Yesu alisema kwamba hakukuwa mwanaume mukubwa zaidi kuliko Yohana, lakini aliongezea pia kwamba Yohana hatatawala pamoja naye huko mbinguni. (Mathayo 11:10, 11) Mufalme Daudi pia aliongozwa na roho takatifu. (1 Samweli 16:13) Roho takatifu ilimusaidia aelewe mambo mazito juu ya Yehova na ilimuongoza pia aandike sehemu fulani za Biblia. (Marko 12:36) Hata hivyo, mutume Petro alisema kwamba Daudi “hakupanda mbinguni.” (Matendo 2:34) Yehova alitumia roho yake takatifu ili kupatia watu hao uwezo wa kufanya mambo yenye kushangaza, lakini hakutumia roho hiyo ili kuwapatia mwaliko wa kuenda mbinguni. Je, hilo linamaanisha kwamba hawakuwa waaminifu kabisa kwake ao hawakustahili kuwa watawala huko mbinguni? Hapana. Hilo linamaanisha tu kwamba Yehova atawafufua ili waishi katika Paradiso duniani.—Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15.

17, 18. (a) Leo, watumishi wengi wa Yehova wako na tumaini gani? (b) Tutajibu maulizo gani katika habari yenye kufuata?

17 Leo, watumishi wengi wa Mungu hawana tumaini la kuenda mbinguni. Kama Abrahamu, Daudi, Yohana Mubatizaji, na wanaume na wanawake wengine wengi wa zamani, watumishi hao wanangojea kuishi katika dunia wakati serikali ya Mungu itatawala. (Waebrania 11:10) Ni wanadamu 144000 tu ndio watatawala pamoja na Yesu mbinguni. Lakini Biblia inazungumuzia ‘mabaki,’ ni kusema, watiwa-mafuta wenye wangali wanaishi duniani katika siku hizi za mwisho. (Ufunuo 12:17) Kwa hiyo, wengi kati ya wale 144000 wamekwisha kufa na wako tayari mbinguni.

18 Lakini, ikiwa mutu anasema kwamba ni mutiwa-mafuta, wale wenye kuwa na tumaini la kuishi katika dunia wanapaswa kujisikia namna gani? Ikiwa mutu fulani katika kutaniko lenu anaanza kula mukate na kunywa divai kwenye Ukumbusho, utamutendea namna gani? Unapaswa kuhangaika kwa sababu unaona hesabu ya wale wenye wanasema kwamba ni watiwa-mafuta inaendelea kuongezeka? Tutajibu maulizo hayo katika habari yenye kufuata.

^ [1] (fungu la 4) Inawezekana Musa alipewa Sheria kwenye Mulima Sinai siku ileile katika mwezi wenye Sikukuu ya Pentekoste ilikuwa inafanywa. (Kutoka 19:1) Kwa hiyo, pengine Musa alipatanisha taifa la Israeli na Mungu kupitia agano la Sheria siku ileile ya mwaka yenye Yesu alipatanisha Wakristo watiwa-mafuta na Mungu kupitia agano jipya.

^ [2] (fungu la 11) Ili kupata mafasirio mengi zaidi juu ya maana ya kuzaliwa tena, soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 4, 2009, ukurasa wa 3-11.