Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uache ‘Zawadi ya Bure Isiyoelezeka’ ya Mungu Ikuchochee

Uache ‘Zawadi ya Bure Isiyoelezeka’ ya Mungu Ikuchochee

“Mungu apewe shukrani kwa ajili ya zawadi yake ya bure isiyoelezeka.” 2 WAKORINTHO 9:15.

NYIMBO: 121, 63

1, 2. (a) ‘Zawadi ya bure isiyoelezeka’ ya Mungu inamaanisha nini? (b) Tutajibu maulizo gani katika habari hii?

YEHOVA alitupatia zawadi kubwa sana yenye kuonyesha upendo, wakati alimutuma katika dunia, Yesu, Mwana wake mupendwa! (Yohana 3:16; 1 Yohana 4:9, 10) Mutume Paulo aliita zawadi hiyo ‘zawadi ya bure isiyoelezeka.’ (2 Wakorintho 9:15) Sababu gani mutume Paulo alitumia maneno hayo?

2 Mutume Paulo alijua kwamba zabihu ya Yesu inahakikisha kwamba ahadi zote nzuri za Mungu zitatimia. (Soma 2 Wakorintho 1:20.) Maneno hayo inamaanisha kwamba ‘zawadi ya bure isiyoelezeka’ ya Mungu inamaanisha zabihu ya Yesu ya ukombozi na wema wote na upendo mushikamanifu wenye Yehova anatuonyesha. Ni vigumu kueleza zawadi hiyo ya maana kwa njia yenye kueleweka muzuri kabisa. Zawadi hiyo ya pekee inatuchochea tujisikie namna gani? Na namna gani zawadi hiyo inatuchochea wakati tunajitayarisha kwa ajili ya Ukumbusho wa kifo cha Kristo wenye utafanywa Siku ya Tatu, tarehe 23 Mwezi wa 3, 2016?

ZAWADI YA PEKEE YA MUNGU

3, 4. (a) Unajisikia namna gani wakati mutu fulani anakupatia zawadi? (b) Namna gani zawadi fulani ya pekee inaweza kubadilisha maisha yako?

3 Tunafurahi wakati mutu fulani anatupatia zawadi. Lakini zawadi fulani ni za maana ao ni za pekee na zinaweza kubadilisha maisha yetu. Kwa mufano, wazia kwamba ulifanya kosa fulani. Kisha unapewa hukumu ya kifo. Lakini palepale, mutu fulani mwenye haujue anajitoa ili yeye apewe malipizi hayo. Mutu huyo iko tayari kufa kwa ajili yako! Zawadi hiyo ya pekee itakuchochea ujisikie namna gani?

4 Zawadi hiyo ya pekee na yenye upendo itakuchochea ufanye mabadiliko katika maisha yako. Pengine, hilo litakuchochea pia ukuwe mwenye ukarimu na mwenye upendo zaidi na kusamehe kila mutu mwenye anakukosea. Katika maisha yako yote, utakuwa tayari kuonyesha shukrani kwa mutu mwenye alijitoa pa nafasi yako.

5. Namna gani zabihu ya ukombozi yenye Mungu alitutolea ni ya lazima zaidi kuliko zawadi ingine yoyote?

5 Zawadi ya zabihu ya ukombozi yenye Mungu alitutolea ni ya lazima zaidi kuliko ile yenye tumezungumuzia katika mufano. (1 Petro 3:18) Fikiria jambo hili: sisi wote tuliriti zambi kutoka kwa Adamu, na malipizi ya zambi ni kifo. (Waroma 5:12) Upendo ulimuchochea Yehova amutume Yesu katika dunia ili akufe kwa ajili ya wanadamu wote, ni kusema, “aonje kifo kwa ajili ya kila mwanadamu.” (Waebrania 2:9) Lakini zabihu ya Yesu ya ukombozi itatimiza mambo mengi zaidi! Itaondoa kifo milele. (Isaya 25:7, 8; 1 Wakorintho 15:22, 26) Wale wote wenye kuonyesha imani katika Yesu wataishi kwa amani na watakuwa na furaha ya milele, iwe watakuwa wafalme pamoja na Kristo huko mbinguni, ao wataishi katika utawala wa Ufalme wa Mungu hapa duniani. (Waroma 6:23; Ufunuo 5:9, 10) Zawadi yenye Yehova alitutolea itatuletea baraka gani zingine?

6. (a) Unangojea baraka gani zenye zawadi ya Yehova itakuletea? (b) Taja mambo tatu yenye zawadi ya Mungu itatuchochea kufanya.

6 Baraka zingine zenye zawadi ya Mungu itatuletea ni hizi: dunia itakuwa paradiso, wagonjwa watapona, na wafu watafufuliwa. (Isaya 33:24; 35:5, 6; Yohana 5:28, 29) Tunamupenda Yehova na Mwana wake mupendwa kwa sababu walitutolea ‘zawadi hiyo ya bure isiyoelezeka.’ Zawadi hiyo itatuchochea kufanya nini? Itatuchochea (1) kumuiga Yesu kwa uaminifu, (2) kupenda ndugu na dada zetu, na (3) kusamehe wengine kwa moyo wote.

‘UPENDO ALIO NAO KRISTO UNATULAZIMISHA’

7, 8. Tunapaswa kuona namna gani upendo wa Kristo, na upendo huo unapaswa kutuchochea tufanye nini?

7 Kwanza, tunapaswa kuchochewa kutumia maisha yetu ili kumuletea Yesu heshima. Mutume Paulo alisema hivi: ‘Upendo alio nao Kristo unatulazimisha.’ (Soma 2 Wakorintho 5:14, 15.) Mutume Paulo alijua kwamba ikiwa tunakubali upendo mukubwa wa Yesu, tutalazimishwa, ao kuchochewa kumupenda Yesu na kumuheshimia. Kwa kweli, wakati tunaelewa muzuri kabisa mambo yenye Yehova ametufanyia, upendo wake utatuchochea tuishi maisha yenye kuonyesha kwamba tunamuheshimia Yesu. Namna gani tunafanya hivyo?

8 Kumupenda Yehova kutatuchochea tuige mufano wa Yesu, ni kusema, kufuata hatua zake kwa uaminifu. (1 Petro 2:21; 1 Yohana 2:6) Wakati tunatii Mungu na Kristo, tunaonyesha kwamba tunawapenda. Yesu alisema hivi: ‘Yule aliye na amri zangu na kuzishika [kuzitii], huyo ndiye ambaye ananipenda. Naye anayenipenda atapendwa na Baba yangu, na mimi nitamupenda na kujionyesha wazi kwake.’—Yohana 14:21; 1 Yohana 5:3.

9. Tunapambana na hali gani?

9 Katika kipindi hiki cha Ukumbusho, itakuwa muzuri ikiwa tunafikiri sana juu ya namna tunatumia maisha yetu. Kwa hiyo ujiulize hivi: ‘Ni mambo gani yenye ninafanya ili kuonyesha kwamba ninamuiga Yesu? Ni mambo gani yenye ninapaswa kufanyia maendeleo?’ Ni muzuri kujiuliza maulizo hayo kwa sababu watu wa ulimwengu huu wanapenda tuige namna yao ya kuishi. (Waroma 12:2) Ikiwa hatuko waangalifu, tunaweza kuchochewa kuanza kuiga walimu, wachezaji, na watu wenye kujulikana sana wa ulimwengu huu. (Wakolosai 2:8; 1 Yohana 2:15-17) Namna gani tunaweza kuepuka mutego huo?

10. Tunaweza kujiuliza maulizo gani katika kipindi hiki cha Ukumbusho, na majibu ya maulizo hayo inaweza kutuchochea kufanya nini? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

10 Katika kipindi cha Ukumbusho, ni muzuri tuchukue wakati wa kuchunguza mavazi yetu, filme, miziki, na mambo yenye kupatikana katika ordinatere, telefone, ao katika tablette yetu. Ujiulize hivi: ‘Ikiwa Yesu angekuwa hapa na kuona namna yangu ya kuvaa, angechukizwa?’ (Soma 1 Timotheo 2:9, 10.) ‘Mavazi yangu ingeonyesha kwamba niko mufuasi wa Kristo? Yesu angefurahia kuangalia filme zenye ninapenda? Angefurahia kusikiliza miziki yenye ninapenda? Ikiwa Yesu anachukua tablette ao telefone yangu, atafurahia mambo yenye anaona? Nitashindwa kumuelezea Yesu sababu gani ninafurahia michezo ya video yenye ninapenda?’ Kumupenda Yehova kutatuchochea tuachane kabisa na kila kitu chenye hakifae kwa Mukristo, hata kama tulitumia feza nyingi ili kukipata. (Matendo 19:19, 20) Wakati tulitoa maisha yetu kwa Yehova, tulimuahidi kwamba tutatumia maisha yetu ili kumuletea Kristo heshima. Kwa hiyo, tunapaswa kuachana kabisa na kila kitu chenye kinaweza kufanya ikuwe vigumu kwetu kumuiga Yesu.—Mathayo 5:29, 30; Wafilipi 4:8.

11. (a) Namna gani upendo wetu kwa Yehova na Yesu unatuchochea katika kazi ya kuhubiri? (b) Namna gani upendo unaweza kutuchochea tusaidie wengine katika kutaniko?

11 Kumupenda Yesu kutatuchochea tuhubiri na kufundisha kwa bidii. (Mathayo 28:19, 20; Luka 4:43) Unaweza kufanya mabadiliko katika maisha yako ili ukuwe painia musaidizi wa kuhubiri saa 30 ao 50 katika kipindi cha Ukumbusho? Ndugu moja mujane mwenye kuwa na miaka 84 aliona kwamba hawezi kuwa painia kwa sababu ya uzee na matatizo ya afya. Lakini mapainia wa eneo lake walipenda kumusaidia. Walichagua eneo lenye kufaa kwenye angeweza kuhubiri na walikuwa wanamubeba katika eneo hilo. Kwa hiyo, ndugu huyo alifikia muradi wake wa kuhubiri saa 30. Unaweza kusaidia ndugu ao dada fulani katika kutaniko lenu ili akuwe painia musaidizi katika Mwezi wa 3 ao wa 4? Ni kweli kwamba sisi wote hatuwezi kuwa mapainia. Lakini tunaweza kutumia wakati na nguvu zetu ili kufanya mengi zaidi katika kazi ya Yehova. Ikiwa tunafanya hivyo, tutaonyesha kwamba tunachochewa na upendo wa Kristo kama mutume Paulo. Upendo wa Mungu utatuchochea tufanye jambo gani lingine?

TUMELAZIMISHWA KUPENDANA

12. Upendo wa Mungu unatuchochea tufanye nini?

12 Pili, upendo wa Mungu unapaswa kutuchochea tupende ndugu na dada zetu. Mutume Yohana aliandika hivi: “Wapendwa, ikiwa Mungu alitupenda hivi, basi sisi wenyewe tuko chini ya wajibu wa [tunalazimishwa] kupendana.” (1 Yohana 4:7-11) Kwa hiyo, ikiwa tunakubali upendo wa Mungu, tunapaswa kupenda ndugu na dada zetu. (1 Yohana 3:16) Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunawapenda?

13. Yesu alituachia mufano gani juu ya kupenda wengine?

13 Yesu alitufundisha namna ya kupenda wengine. Wakati alikuwa katika dunia, alisaidia watu, zaidi sana wale wenye walikuwa wanyenyekevu. Aliponyesha wagonjwa, vilema, vipofu, viziwi, na mabubu. (Mathayo 11:4, 5) Tofauti na viongozi wa dini, Yesu alifurahia kufundisha watu wenye walipenda kumujua Mungu. (Yohana 7:49) Alipenda watu hao wanyenyekevu na alitumika sana ili kuwasaidia.—Mathayo 20:28.

Unaweza kusaidia ndugu ao dada fulani mwenye kuzeeka ahubiri?(Picha hii inapatana na fungu la 14)

14. Unaweza kufanya nini ili kuonyesha kwamba unapenda ndugu na dada zako?

14 Kipindi cha Ukumbusho ni wakati wenye kufaa ili ufikirie namna unaweza pia kusaidia ndugu na dada wa kutaniko lenu, zaidi sana wale wenye kuzeeka. Unaweza kutembelea ndugu na dada hao wapendwa? Unaweza kuwapelekea chakula, kuwasaidia kufanya kazi fulani za nyumbani, kuwasaidia wafike kwenye mikutano, ao kuhubiri pamoja nao? (Soma Luka 14:12-14.) Uache basi upendo wa Mungu ukuchochee kuonyesha kwamba unapenda ndugu na dada zako!

TUSAMEHE NDUGU NA DADA ZETU

15. Tunapaswa kuelewa jambo gani?

15 Tatu, upendo wa Yehova unatuchochea tusamehe ndugu na dada zetu. Adamu alituachia sisi wote zambi na kifo; ndiyo sababu hakuna hata mutu moja mwenye anaweza kusema kwamba “hana lazima ya zabihu ya ukombozi.” Hata mutumishi mwaminifu sana wa Mungu iko na lazima ya zabihu ya ukombozi. Kila mumoja wetu amesamehewa deni kubwa sana! Sababu gani tunapaswa kuelewa jambo hilo? Jibu linapatikana katika mufano moja kati ya mifano yenye Yesu alitoa.

16, 17. (a) Tunajifunza nini katika mufano wa Yesu wa mufalme na watumwa wake? (b) Kisha kufikiri sana juu ya mufano huo, umeazimia kufanya nini?

16 Yesu alitoa mufano wa mufalme mwenye alisamehe mutumwa wake deni kubwa sana, ni kusema, dinari milioni 60. Lakini kisha hapo, mutumwa huyo alikataa kusamehe mutumwa mwenzake deni kidogo sana, ni kusema, dinari 100 tu. Huruma yenye mufalme alimuonyesha mutumwa huyo ilipaswa kumuchochea asamehe mutumwa mwenzake. Wakati mufalme alisikia kwamba mutumwa huyo alikataa kusamehe mutumwa mwenzake deni kidogo sana, alikasirika sana. Mufalme huyo alisema hivi: ‘Mutumwa muovu, nilifuta lile deni lote kwa ajili yako, uliponisihi [wakati ulinililia]. Haikukupasa wewe, nawe, kuwa na rehema juu ya mutumwa mwenzako, kama mimi pia nilivyokuwa na rehema juu yako?’ (Mathayo 18:23-35) Kama mufalme huyo, Yehova ametusamehe deni kubwa sana. Upendo wa Yehova na rehema yake vinapaswa kutuchochea tufanye nini?

17 Wakati tunajitayarisha kwa ajili ya Ukumbusho, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Ndugu ao dada fulani amenikwaza? Ninaona kuwa ni vigumu kumusamehe?’ Ikiwa ni hivyo, huu ndio wakati wenye kufaa ili kumuiga Yehova, mwenye kuwa “tayari kusamehe.” (Nehemia 9:17; Zaburi 86:5) Ikiwa tunaonyesha shukrani juu ya rehema kubwa ya Yehova, tutaonyesha wengine rehema na kuwasamehe kwa moyo wote. Ikiwa hatupende ndugu na dada zetu na kuwasamehe, tusifikiri kwamba Yehova pia atatupenda na kutusamehe. (Mathayo 6:14, 15) Wakati tunasamehe wengine, hilo halimaanishe kwamba hatukuumizwa, lakini hilo litatusaidia kuwa na wakati unaokuja wenye furaha.

18. Namna gani upendo wa Mungu ulisaidia dada moja avumilie uzaifu wa dada mwengine?

18 Inaweza kuwa vigumu kuvumilia uzaifu wa ndugu na dada zetu. (Soma Waefeso 4:32; Wakolosai 3:13, 14.) Jambo hilo lilimufikia dada Lily. [1] (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.) Alisaidia dada moja mujane mwenye kuitwa Carol. Kwa mufano, alimubeba dada Carol katika motokari yake nafasi yote kwenye alikuwa na lazima ya kuenda, alimusaidia kuuza vitu vyenye alikuwa navyo lazima, na alimufanyia mambo mengine mengi. Hata kama Lily alimufanyia mambo yote hayo, dada Carol alikuwa ananungunika kila mara, na hilo lilifanya Lily aone wakati fulani kuwa ni vigumu kumusaidia. Lakini dada Lily alikaza akili yake juu ya sifa za muzuri za dada Carol, na aliendelea kumusaidia kwa miaka fulani mupaka wakati dada Carol aligonjwa sana na kufa. Hata kama haikuwa mwepesi kwa dada Lily kumusaidia dada huyo, anasema hivi: “Ninangojea kwa hamu kumuona dada Carol wakati wa ufufuo. Nitafurahi kumuona wakati atakuwa mukamilifu.” Ni wazi kwamba, upendo wa Mungu unaweza kutuchochea tuvumilie uzaifu wa ndugu na dada zetu na kungojea wakati wanadamu wote watakuwa wakamilifu milele.

19. ‘Zawadi ya bure isiyoelezeka’ ya Mungu, itakuchochea kufanya nini?

19 Kwa kweli, Yehova ametupatia ‘zawadi ya bure isiyoelezeka.’ Tuendelee basi kuonyesha shukrani juu ya zawadi hiyo! Kipindi cha Ukumbusho ni wakati muzuri zaidi wa kufikiri sana juu ya mambo yote yenye Yehova na Yesu wametufanyia. Upendo wao utuchochee basi kumuiga Yesu kwa uaminifu, kupenda ndugu na dada zetu, na kuwasamehe kwa moyo wote.

^ [1] (fungu la 18) Katika habari hii majina fulani imebadilishwa.