Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 16

Endelea Kuonyesha Shukrani juu ya Bei ya Ukombozi

Endelea Kuonyesha Shukrani juu ya Bei ya Ukombozi

‘Mwana wa binadamu alikuja . . . kutoa uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.’​—MK. 10:45.

WIMBO 18 Tuko na Shukrani juu ya Bei ya Ukombozi

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Bei ya ukombozi njo nini, na juu ya nini tuko nayo lazima?

WAKATI Adamu, mwanaume mukamilifu alifanya zambi, alipoteza nafasi ya kuishi milele. Haiko tu yeye peke, lakini pia watoto wenye angezaa. Adamu hakukuwa na sababu ya kufanya zambi, alifanya vile kwa kupenda. Lakini tuseme nini juu ya watoto wake? Watoto wake hawakufanya jambo lolote la mubaya, na hawakumukaza Adamu afanye zambi. Alistahili kifo juu ya mambo yenye alifanya. (Ro. 5:12, 14) Lakini, kuko jambo lenye Yehova angefanya ili kusaidia watoto wa Adamu waishi milele? Ndiyo! Kisha tu Adamu kufanya zambi, Yehova alifunua hatua kwa hatua namna angeweza kuokoa mamilioni ya wazao wa Adamu kutokana na laana ya zambi na kifo. (Mwa. 3:15) Kwa wakati wake, Yehova angetuma Mwana wake kutoka mbinguni ili “atoe uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.”​—Mk. 10:45; Yoh. 6:51.

2 Bei ya ukombozi njo nini? Kulingana na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, bei ya ukombozi ni bei yenye Yesu alitoa ili kulipia jambo lenye Adamu alikuwa amepoteza. (1 Ko. 15:22) Juu ya nini tuko na lazima ya bei ya ukombozi? Ni juu, kulingana na kanuni za Yehova za haki, Sheria iliomba kutoa uzima kwa uzima. (Kut. 21:23, 24) Adamu alipoteza uzima wake mukamilifu. Ili kutimiza haki ya Mungu, Yesu alitoa uzima wake mukamilifu. (Ro. 5:17) Kwa hiyo, Yesu akakuwa “Baba wa Milele” kwa wale wote wenye kuonyesha imani katika bei ya ukombozi.​—Isa. 9:6; Ro. 3:23, 24.

3. Kulingana na Yohana 14:31 na 15:13, juu ya nini Yesu alikuwa tayari kutoa uzima wake mukamilifu?

3 Yesu alikuwa tayari kutoa uzima wake juu alimupenda sana Baba yake, na juu alitupenda sana. (Soma Yohana 14:31; 15:13.) Ile njo ilimuchochea aendelee kubakia muaminifu maisha yake yote na atimize mapenzi ya Baba yake. Juu ya mambo yenye Yesu alifanya, kusudi la Yehova kwa ajili ya wanadamu na dunia litatimia. Mu hii habari tutaona ni juu ya nini Yehova aliacha Yesu ateseke sana mbele akufe. Tutaona pia kwa kifupi mufano wa muandikaji mumoja wa Biblia mwenye alionyesha shukrani sana juu ya bei ya ukombozi. Na ku mwisho, tutaona namna tunaweza kuonyesha shukrani yetu juu ya bei ya ukombozi, na namna tunaweza kuendelea kuonyesha shukrani zaidi juu ya zabihu yenye Yehova na Yesu walitutolea.

JUU YA NINI YESU ALIPASWA KUTESEKA?

Fikiria mateso yote yenye Yesu alivumilia juu ya kututolea bei ya ukombozi! (Ona fungu la 4)

4. Fasiria namna Yesu alikufa.

4 Fikiria mambo yenye ilitokea siku ya mwisho mbele Yesu akufe. Yesu angeweza kuita malaika wengi wamulinde, lakini hakufanya vile. Aliacha maaskari Waroma wamukamate na kumupiga bila huruma. (Mt. 26:52-54; Yoh. 18:3; 19:1) Walimupiga kwa kutumia fimbo yenye ilimuumiza sana. Kisha, walimubebesha muti wenye ulikuwa kilo sana na kuutia ku mugongo wake wenye ulikuwa unavuya damu. Yesu alijaribu kubeba ile muti juu ya kuipeleka fasi kwenye alipaswa kuuawa, lakini kisha wakati kidogo, maaskari Waroma waliamuru mutu fulani aibebe. (Mt. 27:32) Wakati Yesu alifika ile fasi, wale maaskari walimupigilia misumari ku mikono na ku miguu ku ile muti. Uzito wa mwili wa Yesu wenye kupigiliwa ku misumari ulifanya maumivu iongezeke tena sana. Marafiki wake walihuzunika sana, na mama yake alilia sana, lakini viongozi Wayahudi walimuchekelea Yesu. (Lu. 23:32-38; Yoh. 19:25) Vile wakati ilikuwa inapita njo vile maumivu ya Yesu ilikuwa inaongezeka. Namna alitundikwa ku muti ilifanya aanze kupumua kwa shida, na hata moyo na mapafu yake haikutumika tena muzuri. Lakini mbele akate roho, alitoa sala kwa Yehova. Kisha pale, aliinamisha kichwa yake na akakufa. (Mk. 15:37; Lu. 23:46; Yoh. 10:17, 18; 19:30) Kusema kweli, kifo ya Yesu ilikuwa ya polepole, yenye maumivu sana na ya haya sana!

5. Ni nini ilimuhuzunisha sana Yesu?

5 Namna Yesu aliuawa, haiko ile njo ilimuhuzunisha sana. Lakini sababu yenye ilifanya watu wamuue njo ilimuhuzunisha sana. Alishitakiwa kwa uongo kama amemutukana Mungu, ni kusema, hakuheshimia Mungu, wala jina la Mungu. (Mt. 26:64-66) Ile njo ilifanya Yesu ahuzunike sana na alitumaini kama Baba yake hangeruhusu akufe mu ile njia yenye ilikuwa ya haya sana. (Mt. 26:38, 39, 42) Juu ya nini Yehova aliacha Mwana wake mupendwa ateseke na kufa? Tuzungumuzie basi sababu tatu.

6. Juu ya nini Yesu alipaswa kutundikwa ku muti wa mateso?

6 Kwanza, Yesu alipaswa kutundikwa ku muti ili kuweka huru Wayahudi kutoka katika laana. (Gal. 3:10, 13) Walipata ile laana juu waliahidi kama watatii Sheria ya Mungu, lakini hawakufanya vile. Kwa hiyo, walistahili kufa juu walikuwa watoto wa Adamu, lakini pia juu walikuwa na ile laana. (Ro. 5:12) Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli ilisema kama mutu mwenye alifanya zambi yenye inastahili kifo, alipaswa kuuawa. Na mu hali fulani, maiti ya mutu mwenye aliuawa, ilitundikwa ku muti. * (Kum. 21:22, 23; 27:26) Juu Yesu alitundikwa ku muti, Wayahudi wangeweza kuwa huru kutoka katika ile laana, na zabihu yake ingewasaidia hata kama walimukataa.

7. Ni sababu gani ya pili yenye ilifanya Mungu aache Mwana wake ateseke?

7 Ona sasa sababu ya pili yenye ilifanya Mungu aache Mwana wake ateseke. Alikuwa anamutayarisha Yesu kwa ajili ya daraka lenye angepata kisha, ni kusema, kuwa Kuhani Mukubwa. Yesu alijionea namna ni nguvu kutii Mungu wakati mutu iko mu majaribu ya nguvu sana. Wakati alikuwa mu ile hali, alisali “kwa vilio vyenye nguvu na machozi.” Kusema kweli, juu Yesu alipita mu hali za nguvu, anaweza kuelewa mambo yenye tuko nayo lazima na ‘anaweza kutusaidia’ wakati ‘tunajaribiwa.’ Tunamushukuru sana Yehova juu ametuwekea Kuhani Mukubwa mwenye ‘anaweza kusikilia uzaifu wetu huruma’!​—Ebr. 2:17, 18; 4:14-16; 5:7-10.

8. Ni sababu gani ya tatu yenye ilifanya Mungu aruhusu Yesu ateseke sana?

8 Sababu ya tatu yenye ilifanya Yehova aache Yesu ateseke sana ilikuwa ni juu ya kujibia hii ulizo ya maana: Inawezekana wanadamu wabakie waaminifu kwa Yehova wakati wanajaribiwa sana? Shetani anasema hapana! Anasema kama wanadamu wanamutumikia tu Mungu juu wanapenda Mungu awapatie jambo fulani. Iko hakika kama hawamupende Yehova sawa vile Adamu. (Yob. 1:9-11; 2:4, 5) Juu alikuwa hakika kama Mwana wake angebakia muaminifu, Yehova aliruhusu Yesu ateseke mupaka kufikia kiasi mwanadamu anaweza kuvumilia. Yesu aliendelea kubakia muaminifu-mushikamanifu na kuonyesha kama Shetani ni muongo.

MUANDIKAJI MUMOJA WA BIBLIA MWENYE ALIONYESHA SHUKRANI ZAIDI JUU YA BEI YA UKOMBOZI

9. Ni mufano gani muzuri wenye Yohana alituachia?

9 Fundisho kuhusu bei ya ukombozi imetia nguvu imani ya Wakristo wengi. Imewasaidia waendelee kuhubiri ijapokuwa upinzani na imewasaidia wavumilie magumu mbalimbali yenye wamepata mu maisha. Fikiria mufano wa mutume Yohana. Kwa zaidi ya miaka 60 hivi aliendelea kufundisha kweli juu ya Kristo na juu ya bei ya ukombozi. Hata kama alikuwa na miaka karibu 100, serikali ya Roma ilimuona kuwa mutu hatari sana na njo maana walimufunga mu kisiwa cha Patmo. Alifanya kosa gani? ‘Alisema juu ya Mungu na kutoa ushahidi juu ya Yesu.’ (Ufu. 1:9) Yohana alituachia mufano muzuri sana wa imani na uvumilivu!

10. Namna gani vitabu vyenye Yohana aliandika vinaonyesha kama alikuwa mwenye shukrani juu ya bei ya ukombozi?

10 Mu vitabu vya Biblia vyenye aliandika, Yohana alionyesha namna gani alimupenda sana Yesu, na namna alikuwa mwenye shukrani juu ya zabihu ya Yesu. Na zaidi ya mara 100 alizungumuzia bei ya ukombozi, ao faida zenye ile bei inaleta. Kwa mufano, aliandika hivi: “Kama mutu yeyote anafanya zambi, tuko na musaidizi kwa Baba, Yesu Kristo, mwenye haki.” (1 Yo. 2:1, 2) Tena, vitabu vyenye Yohana aliandika, vinakazia ulazima wa “kutoa ushahidi juu ya Yesu.” (Ufu. 19:10) Kusema kweli, Yohana alionyesha shukrani zaidi juu ya bei ya ukombozi. Namna gani na siye tunaweza kufanya vile?

NAMNA GANI UNAWEZA KUONYESHA SHUKRANI YAKO JUU YA BEI YA UKOMBOZI?

Kama tunaona kabisa bei ya ukombozi kuwa ya maana tutapinga jaribu la kufanya zambi (Ona fungu la 11) *

11. Ni nini inaweza kutusaidia tupinge jaribu la kufanya zambi?

11 Upinge jaribu la kufanya zambi. Kama kabisa tunaonyesha shukrani juu ya bei ya ukombozi, hatutafikiri hivi: ‘Wakati najikuta mbele ya jaribu, haiko lazima nijikaze sana juu nisifanye zambi, naweza tu kufanya zambi na kisha nitaomba musamaha.’ Kuliko kufanya vile, wakati tunajaribiwa kufanya jambo la mubaya, tutasema: ‘Hapana! Kuona mambo yote yenye Yehova na Yesu walishanifanyia, namna gani naweza kufanya hii jambo?’ Tena, tunaweza kumulilia Yehova juu atupatie nguvu kwa kusema hivi: ‘Unisaidie nisiingie katika jaribu.’​—Mt. 6:13.

12. Namna gani tunaweza kutumikisha shauri lenye kuwa mu 1 Yohana 3:16-18?

12 Upende ndugu na dada zako. Wakati tunapenda ndugu na dada zetu, tunaonyesha pia shukrani juu ya bei ya ukombozi. Juu ya nini tunasema vile? Juu Yesu alitoa uzima wake kwa ajili yetu na pia kwa ajili ya ndugu na dada zetu. Yesu alikuwa tayari kuwakufia, ile inaonyesha kama anawapenda sana. (Soma 1 Yohana 3:16-18.) Tunaonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu mu namna yenye tuko tunawatendea. (Efe. 4:29, 31–5:2) Kwa mufano, tunawasaidia wakati wanagonjwa ao wakati wanavumilia majaribu makali sawa vile misiba ya asili. Lakini, tunaweza kufanya nini wakati Mukristo mwenzetu anafanya ao anasema jambo fulani lenye linatukwaza?

13. Juu ya nini tunapaswa kusamehe wengine?

13 Wakati fulani, unaonaka ni nguvu kusamehe Mukristo mwenzako? (Law. 19:18) Kama ni vile, fuata hii shauri: “Muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa kupenda hata kama mutu yeyote iko na sababu ya kulalamika juu ya mwingine. Kama vile Yehova aliwasamehe ninyi kwa kupenda, ninyi pia munapaswa kufanya vilevile.” (Kol. 3:13) Kila mara wakati tunasamehe ndugu ao dada yetu, tunaonyesha Baba yetu wa mbinguni kama tuko kabisa wenye shukrani juu ya bei ya ukombozi. Namna gani tunaweza kuendelea kuonyesha shukrani zaidi juu ya hii zawadi yenye Mungu ametupatia?

NAMNA GANI UNAWEZA KUENDELEA KUONYESHA SHUKRANI YAKO JUU YA BEI YA UKOMBOZI?

14. Ni mu njia gani moja tunaweza kuendelea kuonyesha shukrani zaidi juu ya bei ya ukombozi?

14 Umushukuru Yehova juu ya bei ya ukombozi. Joanna, dada wa miaka 83, mwenye anaishi India, anasema hivi: “Naona kama ni muzuri kutaja bei ya ukombozi kila siku mu sala zangu na kumushukuru Yehova juu ya ile.” Kila siku wakati unasali, umuambie Yehova mambo yote ya mubaya yenye umefanya na umuombe akusamehe. Lakini, kama ulifanya zambi nzito, tafuta musaada kwa wazee. Watakusikiliza na watakupatia mashauri ya muzuri kutoka mu Neno la Mungu. Watasali na weye na kumuomba Yehova akusamehe kwa musingi wa zabihu ya Yesu ‘ili uponyeshwe kiroho.’​—Yak. 5:14-16.

15. Juu ya nini inaweza kuwa muzuri ukamate wakati wa kujifunza na kufikiri sana juu ya bei ya ukombozi?

15 Ufikiri sana juu ya bei ya ukombozi. Rajamani, dada wa miaka 73, anasema hivi: “Kila mara wakati nasoma juu ya mateso yenye Yesu alipata, nasikiaka machozi inaniyala mu macho.” Na weye unaweza kujisikia vile wakati unafikiri juu ya mateso yenye Mwana wa Mungu alipata. Lakini, kadiri unaendelea kufikiri sana juu ya zabihu yenye Yesu alitoa, ni vile utamupenda zaidi yeye na Baba yake. Kitu yenye inaweza kukusaidia ufikiri sana juu ya bei ya ukombozi, ni kupanga wakati wa kujifunza ili kuijua muzuri, hauone vile?

Kupitia mulo wenye kuwa mwepesi, Yesu anaonyesha wanafunzi wake namna ya kukumbuka zabihu yake (Ona fungu la 16)

16. Kufundisha wengine juu ya bei ya ukombozi kunatusaidia namna gani? (Ona picha ku jalada.)

16 Ufundishe wengine juu ya bei ya ukombozi. Kila mara tunaambia wengine juu ya bei ya ukombozi, ile itafanya tukuwe wenye shukrani zaidi. Tuko na vichapo na video za muzuri sana zenye zinaweza kutusaidia tufasirie wengine wajue juu ya nini Yesu alitukufia. Kwa mufano, tunaweza kutumia somo ya 4 ya broshua Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu! Ile somo iko na kichwa “Yesu Kristo Ni Nani?” Ao tunaweza kutumia sura ya 5 ya kitabu Biblia Inatufundisha Nini? Ile sura iko na kichwa “Bei ya Ukombozi: Zawadi Kubwa Zaidi Kutoka kwa Mungu.” Na kila mwaka tunaendelea kuonyesha shukrani yetu juu ya bei ya ukombozi kwa kuhuzuria Ukumbusho wa kifo ya Yesu, na kwa kualika wengine kwa bidii ili wakuje kuhuzuria na siye. Yehova ametupatia pendeleo kubwa sana la kufundisha wengine juu ya Mwana wake!

17. Juu ya nini bei ya ukombozi njo zawadi kubwa yenye Mungu amepatia wanadamu?

17 Bila shaka tuko na sababu ya muzuri ya kuendelea kuonyesha shukrani yetu zaidi juu ya bei ya ukombozi. Bei ya ukombozi inatusaidia tukuwe na urafiki wa karibu sana pamoja na Yehova, hata kama hatukamilike. Tena, kupitia ile bei ya ukombozi, kazi za Ibilisi zitavunjwa kabisa. (1 Yo. 3:8) Ile bei ya ukombozi itasaidia pia kusudi lenye Yehova alikuwa nalo ku mwanzo kuhusu dunia litimie. Dunia yote itakuwa paradiso. Mu ile dunia, kila mutu atamupenda na kumutumikia Yehova. Kwa hiyo basi, kila siku tuendelee kutafuta nafasi ya kuonyesha shukrani yetu juu ya zawadi kubwa yenye Mungu amepatia wanadamu, ni kusema, bei ya ukombozi!

WIMBO 20 Ulimutoa Mwana Wako Mupendwa

^ fu. 5 Juu ya nini Yesu alipata mateso ya nguvu sana na kuuawa? Hii habari itajibia ile ulizo. Tena itatusaidia tuendelee kuonyesha shukrani zaidi juu ya bei ya ukombozi.

^ fu. 6 Waroma walikuwa na desturi ya kupigilia misumari watenda-mabaya ao kuwafunga ku muti wakati wangali wazima, Yehova pia aliacha Mwana wake akufe mu ile njia.

^ fu. 55 MAFASIRIO YA PICHA: Kila ndugu anapinga jaribu fulani: Wa kwanza jaribu la kuangalia picha za mubaya, wa pili jaribu la kuvuta tumbako, na wa tatu jaribu la kuitika rushwa ao kata-midomo.