Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Juu ya nini Yesu alitaja maneno ya Daudi yenye kuwa mu Zaburi 22:1 mbele tu akufe?

Kati ya maneno ya mwisho yenye Yesu alisema mbele akufe, kuko maneno yenye kupatikana mu Matayo 27:46 yenye inasema hivi: “Mungu wangu, Mungu wangu, sababu gani umeniacha?” Kwa kusema vile, Yesu alitimiza maneno ya muandikaji wa zaburi Daudi yenye kupatikana mu Zaburi 22:1. (Mk. 15:34) Kusema kama Yesu alitaja hii maneno juu alivunjika moyo, ao juu kwa wakati fulani alikuwa alishapoteza imani yake kwa Mungu ni uongo kabisa. Yesu alijua muzuri kabisa juu ya nini alipaswa kufa, na alikuwa tayari kufanya vile. (Mt. 16:21; 20:28) Alijua pia kama wakati wa kifo yake, Yehova angeondoa ‘ukuta wowote wa ulinzi’ wenye kumuzunguka. (Yob. 1:10) Njo maana, Yehova aliacha kumulinda Yesu ili aonyeshe kama angeweza kuendelea kubakia muaminifu hata kifo yake ikuwe ya namna gani.​—Mk. 14:35, 36.

Sasa juu ya nini Yesu alitaja maneno ya mu ile zaburi? Kusema kweli, hatujue kabisa. Lakini tuone sababu zenye pengine zilifanya Yesu ataje ile maneno. *

Kwa kutaja ile maneno, pengine Yesu alipenda kukazia kama Yehova hangemupigania wakati wa kifo yake. Yesu alipaswa kulipa bei ya ukombozi bila musaada wa Yehova. Alipaswa kufa ili “aonje kifo kwa ajili ya kila mutu.”​—Ebr. 2:9.

Kwa kutaja maneno fulani ya ile zaburi, pengine Yesu alipenda watu wafikirie maneno yote ya mu ile zaburi. Ile wakati Wayahudi walizoea kutia mu akili zaburi mingi. Wakati walisikia mustari moja wa zaburi fulani, mara moja wangefikiria mistari yote ya ile zaburi. Kama ni vile njo Yesu alipenda kufanya, ni kusema, angesaidia wafuasi wake Wayahudi wakumbuke unabii mbalimbali wenye kupatikana mu ile zaburi. Na ile zaburi ilizungumuzia mambo yenye ingetokea wakati wa kifo ya Yesu. (Zb. 22:7, 8, 15, 16, 18, 24) Tena, mistari ya mwisho ya ile zaburi inamutukuza Yehova na inamuonyesha kuwa Mufalme juu ya dunia yote.​—Zb. 22:27-31.

Kwa kutaja ile maneno ya Daudi, pengine Yesu alikuwa anaonyesha kama hakukuwa na kosa. Mbele Yesu auawe, tribinali ya Sanhedrini ilifanya mukutano wenye haukubaliwe na sheria. Na Yesu alikuhukumiwa kuwa alimutukana Mungu. (Mt. 26:65, 66) Washiriki wa Sanhedrini walikutana haraka-haraka usiku ili kumusambisha. Kufanya vile ilipingana na sheria. (Mt. 26:59; Mk. 14:56-59) Wakati Yesu aliuliza hivi: “Mungu wangu, Mungu wangu, sababu gani umeniacha?” Pengine alipenda kukazia kama hakufanya jambo la mubaya lenye lingefanya auawe.

Pengine Yesu alipenda kukumbusha watu kama, wakati Daudi muandikaji wa hii zaburi aliteseka, ile haimaanishe kama Yehova hakumukubali tena. Ulizo yenye Daudi aliuliza haionyeshe kama hakukuwa na imani katika Mungu, juu kisha kuuliza ile ulizo Daudi alisema alitumaini kama Yehova ataokoa watu wake. Na Yehova aliendelea kumubariki. (Zb. 22:23, 24, 27) Vilevile, hata kama Yesu, “Mwana wa Daudi,” aliteseka ku muti wa mateso, ile haionyeshe kama Yehova hakumukubali tena.​—Mt. 21:9.

Pengine Yesu alipenda kuonyesha huzuni yake juu Yehova aliondoa ulinzi Wake ili aonyeshe kabisa uaminifu-mushikamanifu kwa Baba yake. Ku mwanzo, haikukuwa kusudi la Yehova Mwana wake ateseke na akufe. Ilikuwa lazima kufanya vile kisha tu Adamu na Eva kuasi. Yesu hakufanya jambo lolote la mubaya, lakini alipaswa kuteseka na kufa ili kujibia mashitaka ya Shetani na kutoa bei ya ukombozi ili kulipia wanadamu mambo yenye walipoteza. (Mk. 8:31; 1 Pe. 2:21-24) Na ile ingewezekana tu ikiwa, kwa mara ya kwanza mu maisha ya Yesu, Yehova angeacha kumulinda kwa wakati fulani.

Pengine Yesu alipenda kusaidia wafuasi wake wakazie akili sababu yenye ilifanya Yehova amuache auawe ku muti wa mateso. * Yesu alijua kama kufa ku muti wa mateso sawa mutenda-mabaya kungefanya watu wengi wajikwae. (1 Ko. 1:23) Ikiwa wafuasi wa Yesu wangekazia akili sababu ya kweli yenye ilifanya Yesu akufe, wangeelewa maana ya kifo yake. (Gal. 3:13, 14) Ile ingewasaidia wamuone Yesu kuwa Mukombozi wao, hapana mutenda-mabaya.

Hata ikuwe ni sababu gani njo ilifanya Yesu ataje ile maneno, alijua kama juu alikufa ku muti wa mateso alifanya mapenzi ya Yehova. Na wakati kidogo tu kisha Yesu kutaja maneno ya ile zaburi, alisema hivi: “Imetimizwa!” (Yoh. 19:30; Lu. 22:37) Kusema kweli, juu Yehova aliacha kumusaidia Yesu kwa wakati kidogo, ile ilimusaidia atimize kwa ukamili mambo yote yenye alitumwa kufanya hapa ku dunia. Ile ilimusaidia pia atimize mambo yote yenye iliandikwa kumuhusu “katika Sheria ya Musa na katika Manabii, na Zaburi.”​—Lu. 24:44.

^ fu. 2 Ona pia fungu la 9 na la 10 la habari “Maneno ya Mwisho ya Yesu Inaweza Kutufundisha Nini?” yenye iko mu hii gazeti.

^ fu. 4 Wakati fulani mu utumishi wake, Yesu alisema mambo fulani ao kuuliza maulizo yenye haikuonyesha namna alijisikia. Alifanya vile juu alipenda wafuasi wake waeleze mawazo yao.​—Mk. 7:24-27; Yoh. 6:1-5; ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 10, 2010, uku. 4-5.