Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 14

“Mufuate Hatua Zake kwa Ukaribu”

“Mufuate Hatua Zake kwa Ukaribu”

“Kristo aliteseka kwa ajili yenu, akiwaachia ninyi mufano ili mufuate hatua zake kwa ukaribu.”​—1 PE. 2:21.

WIMBO 13 Kristo Ni Mufano Muzuri

KIFUPI CHA HABARI *

Yesu alituachia alama za miguu zenye tunapaswa kufuata kwa ukaribu (Ona fungu la 1-2)

1-2. Inawezekana kwetu kufuata hatua za Yesu? Leta mufano.

WAZA uko mu kikundi ya watu wenye kutembea mu jangwa lenye kuwa hatari na lenye kujaa muchanga. Mbele yenu kuko kiongozi mwenye uzoefu. Wakati iko anatembea, alama za miguu yake ziko zinaonekana mu muchanga. Kisha wakati fulani, hauone tena kiongozi wenu! Lakini, hauogope. Weye na wale wenye kuwa mu kikundi munajikaza kabisa kufuata alama za miguu za kiongozi wenu!

2 Mu njia fulani, siye Wakristo wa kweli tuko pia tunatembea mu jangwa lenye hatari, ni kusema, ulimwengu huu muovu. Lakini, tuko wenye shukrani sana juu Yehova alitupatia Kiongozi muzuri zaidi, ni kusema, Mwana wake Yesu Kristo, mwenye alituachia hatua zenye tunaweza kufuata kwa ukaribu. (1 Pe. 2:21) Kulingana na kitabu moja yenye kutoa maelezo juu ya Biblia, hapa Petro iko analinganisha Yesu na kiongozi. Kama vile kiongozi mwenye kuacha alama za miguu yake, ni vile pia Yesu aliacha alama ao hatua zenye tunaweza kufuata. Tujibie basi hii maulizo tatu: Kufuata hatua za Yesu njo nini? Juu ya nini tunapaswa kuzifuata? Na namna gani tunaweza kufanya vile?

KUFUATA HATUA ZA YESU NJO NINI?

3. Kufuata hatua za mutu njo nini?

3 Kufuata hatua za mutu njo nini? Wakati fulani mu Biblia, maneno “kutembea” na “miguu” inaweza kumaanisha mambo yenye mutu fulani anafanya mu maisha yake. (Mwa. 6:9; Mez. 4:26) Mambo yenye mutu anafanya mu maisha iko sawa vile alama ao hatua zenye anaacha nyuma yake wakati iko anatembea. Njo maana kufuata hatua za mutu ni kufuata mufano wake ao kumuiga.

4. Kufuata hatua za Yesu njo nini?

4 Sasa, kufuata hatua za Yesu njo nini? Kwa kifupi ni kufuata mufano wake. Mu andiko letu la musingi, mutume Petro iko anazungumuzia mufano muzuri wenye Yesu alituachia juu alivumilia magumu. Lakini, kuko mambo ingine ya muzuri yenye Yesu alifanya yenye tunaweza kuiga. (1 Pe. 2:18-25) Kwa kweli, maisha yote ya Yesu, ni kusema, mambo yote yenye alifanya na kusema, ni mufano muzuri wenye tunaweza kufuata.

5. Je, wanadamu wenye hawakamilike, wanaweza kweli kufuata mufano mukamilifu wa Yesu? Fasiria.

5 Lakini, je, wanadamu wenye hawakamilike wanaweza kweli kufuata mufano wa Yesu? Ndiyo kabisa. Kumbuka kama mutume Petro alitutia moyo ‘tufuate hatua [za Yesu] kwa ukaribu,’ hapana kwa ukamilifu. Kama tunafuata hatua za Yesu kwa ukaribu, kwa kufanya yetu yote, hata kama hatukamilike, tutaonyesha kama tunatii maneno hii yenye mutume Yohana alisema: ‘Muendelee kutembea kama vile Yesu alitembea.’​—1 Yo. 2:6.

JUU YA NINI TUNAPASWA KUFUATA HATUA ZA YESU?

6-7. Juu ya nini tunaweza kusema kama kufuata hatua za Yesu kunaweza kutufanya tumukaribie Yehova zaidi?

6 Kufuata hatua za Yesu kutafanya tumukaribie Yehova zaidi. Juu ya nini tunasema vile? Kwanza, ni juu Yesu alituwekea mufano muzuri sana wenye kutusaidia kuelewa namna tunaweza kuishi maisha yenye kumufurahisha Mungu. (Yoh. 8:29) Njo maana wakati tunafuata hatua za Yesu, tutamufurahisha Yehova. Na tukuwe hakika kama Baba yetu wa mbinguni atakaribia wale wote wenye wanajikaza kuwa marafiki wake.​—Yak. 4:8.

7 Pili, ni juu Yesu alimuiga Baba yake kwa ukamilifu. Na njo maana Yesu alisema: “Kila mutu mwenye ameniona mimi amemuona Baba pia.” (Yoh. 14:9) Tunaweza kuiga sifa za Yesu na namna alitendea wengine. Kwa mufano, alisikilia huruma mutu mumoja mwenye alikuwa na ukoma, alijitia pa nafasi ya mwanamuke mumoja mwenye alikuwa na ugonjwa wa mubaya sana, na alitendea kwa huruma wale wenye walipoteza wapendwa wao. Wakati tunamuiga Yesu, tunamuiga Yehova pia. (Mk. 1:40, 41; 5:25-34; Yoh. 11:33-35) Na kadiri tunaiga sifa za Yehova, ni vile tutamukaribia zaidi.

8. Kufuata hatua za Yesu kutatusaidia tuendelee ‘kushinda’ ulimwengu. Namna gani?

8 Kufuata hatua za Yesu kunatusaidia tusikengeushwe na ulimwengu huu muovu. Usiku wa mwisho wa maisha yake hapa ku dunia, Yesu alifikia kusema hivi: “Nimeshinda ulimwengu.” (Yoh. 16:33) Alipenda kusema kama alikataa kabisa kufuata mawazo, miradi, na matendo ya watu wa ulimwengu huu. Yesu hakusahau hata siku moja kusudi lenye lilifanya akuje ku dunia, ni kusema, kumutetea Yehova. Halafu siye? Mu hii ulimwengu kuko mambo mingi yenye inaweza kufanya tusiendelee kumutumikia Yehova kwa moyo wetu wote. Lakini kama tunaendelea kufanya mapenzi ya Yehova, sawa vile Yesu, na siye pia ‘tutashinda’ ulimwengu.​—1 Yo. 5:5.

9. Tunaweza kufanya nini juu tuendelee kutembea mu barabara yenye inaongoza kwenye uzima wa milele?

9 Tukifuata hatua za Yesu, tunaweza kuishi milele. Wakati kijana moja tajiri alimuuliza Yesu ili kujua ni mambo gani alipaswa kufanya juu apate uzima wa milele, Yesu alimuambia hivi: “Ukuje ukuwe mufuasi wangu.” (Mt. 19:16-21) Na kwa Wayahudi fulani wenye hawakuamini kama Yesu alikuwa Kristo, yeye aliwaambia: “Kondoo wangu . . . wananifuata. Mimi ninawapatia uzima wa milele.” (Yoh. 10:24-29) Na wakati alikuwa anazungumuza na Nikodemo, mushiriki mumoja wa Sanhedrini mwenye alianza kupendezwa na mafundisho yake, Yesu alimuambia kama wale wenye ‘wanamuamini’ njo ‘watapata uzima wa milele.’ (Yoh. 3:16) Tunaonyesha kama tunamuamini Yesu wakati tunatumikisha mafundisho yake, na tunaiga mufano wake. Tukifanya vile, tutaendelea kutembea mu barabara yenye inaongoza kwenye uzima wa milele.​—Mt. 7:14.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUFUATA HATUA ZA YESU KWA UKARIBU?

10. Tunapaswa kufanya nini ili ‘tufikie kumujua’ Yesu muzuri zaidi? (Yohana 17:3)

10 Tunapaswa kufikia kumujua Yesu muzuri mbele ya kufuata hatua zake kwa ukaribu. (Soma Yohana 17:3.) ‘Kufikia kumujua’ Yesu haiko kazi ya siku moja tu, lakini ni ya kuendelea. Tunapaswa kuendelea kujifunza ili kumujua muzuri zaidi, ni kusema, kujua sifa zake, mawazo yake, na kanuni zenye zinamuongoza. Hata kama tulishafanya masiku ngapi mu tengenezo, tunapaswa kuendelea kujikaza ili kufikia kujua muzuri zaidi Yehova na Mwana wake.

11. Vitabu ine vya Injili viko na mambo gani?

11 Kwa upendo, Yehova ametupatia vitabu ine vya Injili ili kutusaidia tumujue muzuri Mwana wake. Ndani ya vile vitabu muko habari juu ya maisha ya Yesu na juu ya utumishi wake. Tena, vile vitabu vinatuonyesha mambo yenye Yesu alisema, mambo alifanya, na namna alikuwa anajisikia. Vile vitabu ine vinatusaidia ‘tufikirie sana’ mufano wa Yesu. (Ebr. 12:3) Kusema kweli, vile vitabu vinaonyesha hatua zenye Yesu alituachia. Njo maana tutafikia kumujua Yesu muzuri zaidi kama tunajifunza vile vitabu. Ile njo itafanya tufuate hatua zake kwa ukaribu.

12. Tunapaswa kufanya nini juu Vitabu vya Injili vituletee faida?

12 Juu vitabu ine vya Injili vituletee faida, hatupaswe tu kuvisoma, tunapaswa pia kufanya mambo ingine. Tunapaswa kukamata wakati wa kujifunza kwa uangalifu sana na kufikiri sana juu ya vile vitabu. (Linganisha na Yoshua 1:8, maelezo ya chini.) Tuzungumuzie basi mambo mbili yenye inaweza kutusaidia tufikiri sana juu ya vile vitabu ine vya Injili na namna tunaweza kutumikisha mambo yenye tunasoma mu vile vitabu.

13. Namna gani unaweza kufanya habari ya Injili yenye uko unasoma ikuwe ya kweli kwako?

13 Kwanza, fanya habari ya Injili yenye unasoma ikuwe ya kweli kwako. Wakati uko unasoma habari fulani ya Injili, fanya sawa vile uko pale, uko unaona, na uko unasikiliza mambo yenye iko inatokea. Ili uweze kufanya vile, utafute habari mu vichapo vyenye vinatolewa na tengenezo la Yehova juu ya kupata maelezo zaidi. Mu habari yenye uko unajifunza chunguza mambo yenye ilitokea mbele na kisha pale. Tafuta maelezo zaidi juu ya watu na mahali mbalimbali yenye inazungumuziwa mu ile habari. Linganisha namna habari moja yenye uko unajifunza mu kitabu fulani ya Injili inazungumuziwa pia mu kitabu ingine ya Injili. Wakati fulani, muandikaji mumoja wa kitabu ya Injili anazungumuzia jambo la maana sana lenye muandikaji wa kitabu ingine ya Injili hakuzungumuzia.

14-15. Namna gani tunaweza kutumikisha mambo yenye tunajifunza mu Vitabu vya Injili?

14 Pili, tumikisha mu maisha yako habari yenye uko unasoma mu kitabu ya Injili. (Yoh. 13:17) Kisha kujifunza kwa uangalifu habari fulani ya Injili, ujiulize hivi: ‘Kuko jambo fulani mu hii habari lenye ninaweza kutumikisha mu maisha yangu? Namna gani naweza kutumikisha hii habari juu ya kusaidia mutu fulani?’ Fikiria mutu fulani, na kisha, kwa wakati wenye kufaa, umuambie mambo yenye ulijifunza. Lakini ufanye vile kwa upendo na busara.

15 Tuzungumuzie basi mufano moja wenye utatusaidia kuona namna ya kutumikisha ile mambo mbili. Tutazungumuzia habari ya mujane maskini mwenye Yesu alionaka mu hekalu.

MUJANE MASKINI KATIKA HEKALU

16. Namna gani unaweza kufasiria mambo yenye kuzungumuziwa mu Marko 12:41?

16 Fanya habari ikuwe ya kweli kwako. (Soma Marko 12:41.) Fikiria mambo yenye ilitokea. Ni tarehe 11, Mwezi wa Nisani, Mwaka wa 33 K.K.Y, masiku kidogo mbele Yesu akufe. Ile siku, Yesu alipitisha wakati mingi na iko anafundisha mu hekalu. Lakini, viongozi wa dini walikuwa wanamupinga. Mbele ya pale, wamoja kati yao walitilia mashaka mambo yenye alikuwa anafanya. Wengine walimuuliza maulizo yenye waliwaza kama hataweza kuwajibia. (Mk. 11:27-33; 12:13-34) Sasa Yesu anaenda fasi ingine katika hekalu. Pengine iko mu fasi yenye inaitwa Kiwanja ya Wanamuke na anaona masanduku ya hazina yenye kuwa pembeni-pembeni ya ukuta wa hekalu. Anakaa na kisha anaanza kuangalia watu wakati wako wanatia michango yao katika masanduku ya hazina. Anaona matajiri wengi wenye wako wanatumbukiza feza mingi za vichele mu ile masanduku. Pengine iko karibu sana na ile masanduku na iko anasikia makelele ya vile vichele wakati viko vinatumbukizwa ndani.

17. Mujane maskini mwenye kutajwa mu Marko 12:42 alifanya nini?

17 Soma Marko 12:42. Kisha wakati fulani, Yesu anaona mwanamuke mumoja. Ni “mujane maskini.” (Lu. 21:2) Ule mwanamuke iko na maisha ya nguvu sana; na pengine hana hata feza za kutosha juu ya kuuza vitu vya lazima ili kuishi. Lakini, bila kupenda kujionyesha, alienda kutumbukiza feza mbili za kichele, zenye pengine, hazikuleta makelele sana wakati zilitumbukizwa mu sanduku ya hazina. Yesu alijua feza zenye alitumbukiza mu sanduku, alitumbukiza leptoni mbili, na ile njo ilikuwa feza zenye samani kidogo sana mu ile wakati. Ilikuwa feza kidogo sana na haingeweza hata kuuza ndege shomoro moja. Ile wakati, ndege shomoro ilikuwa kati ya ndege zenye watu waliuza kwa bei ya chini sana kwa ajili ya chakula.

18. Kulingana na Marko 12:43, 44, Yesu alisema nini kuhusu muchango wa ule mujane?

18 Soma Marko 12:43, 44. Ule mujane anamushangaza sana Yesu. Njo maana anaita wanafunzi wake na anawaambia wamuangalie ule mujane, kisha anasema: “Mujane huyu maskini ametoa zaidi ya wote.” Kisha anaongezea hivi: “Wote [zaidi sana matajiri] walitumbukiza ndani kutokana na wingi wa feza zao, lakini yeye, hata kama ni maskini, alitumbukiza ndani kila kitu chenye alikuwa nacho, yote yenye alikuwa nayo ili kuishi.” Wakati ule mujane muaminifu alitoa feza yote yenye alikuwa nayo ile siku, ile ilionyesha kama alitumainia kuwa Yehova atamuhangaikia.​—Zb. 26:3.

Wakati unaona wengine wanamupatia Yehova mambo ya muzuri zaidi, kama Yesu, ukuwe tayari kuwapongeza (Ona fungu la 19-20) *

19. Habari kuhusu mujane maskini mwenye Yesu alizungumuzia inatufundisha nini?

19 Tumikisha mambo yenye unajifunza. Ujiulize hivi: ‘Habari ya mujane maskini mwenye Yesu alizungumuzia inaweza kunifundisha nini?’ Fikiria ule mujane. Bila shaka alipenda kumutolea Yehova zaidi ya ile yenye alitoa. Lakini, alimutolea Yehova jambo la muzuri zaidi lenye alikuwa nalo kulingana na uwezo wake wote. Na Yesu alijua kama Baba yake aliona ule muchango kuwa wa maana sana. Hapa, jambo la maana lenye tunajifunza ni hili: Yehova anafurahi wakati tunamutolea jambo la muzuri zaidi lenye tuko nalo, ni kusema, utumishi wenye tunamutolea kwa moyo wetu wote na kwa nafsi yetu yote. (Mt. 22:37; Kol. 3:23) Yehova anafurahi wakati anaona tunafanya yote yenye tunaweza! Ile inatia ndani wakati na nguvu yenye tunatumia ili kumuabudu, kama vile, kuhubiri na kukusanyika.

20. Namna gani unaweza kutumikisha mambo yenye umejifunza mu habari yenye inazungumuzia ule mujane maskini? Leta mufano.

20 Namna gani unaweza kutumikisha mambo yenye umejifunza mu habari yenye kuzungumuzia ule mujane maskini? Fikiria watu fulani wenye unaona kama wanaweza kutiwa moyo, ikiwa unawakumbusha kama, Yehova anafurahia sana mambo ya muzuri yenye wako wanamufanyia. Kwa mufano, unajua dada fulani mwenye kuzeeka, mwenye hana nguvu mingi tena na iko na matatizo ya afya, na mwenye anajiona kuwa iko na kosa ao pengine anajiona kuwa wa bure juu hahubiri tena sana sawa vile zamani? Ao pengine ndugu mwenye iko na ugonjwa wa mubaya sana wenye unafanya masiku mingi, na mwenye amevunjika moyo sababu hawezi kukusanyika ku kila mukutano? Tumia maneno ya “muzuri ili kujenga” ndugu na dada wenye kuwa mu hali ya vile. (Efe. 4:29) Uwaelezee mambo ya muzuri na yenye kutia moyo yenye tumejifunza mu habari kuhusu ule mujane maskini. Maneno yako yenye kutia moyo itawakumbusha kama Yehova anafurahi wakati tunamutolea mambo ya muzuri zaidi yenye tuko nayo. (Mez. 15:23; 1 Te. 5:11) Wakati unapongeza wengine kwa sababu wanamutolea Yehova mambo ya muzuri zaidi yenye wako nayo, hata kama inaweza kuonekana kuwa ya kidogo, kwa kweli unaonyesha kama uko unafuata hatua za Yesu kwa ukaribu.

21. Unaazimia kufanya nini?

21 Tuko wenye shukrani sana sababu Vitabu vya Injili vinatupatia maelezo ya mingi sana juu ya maisha ya Yesu, na ile inatusaidia tujue namna ya kumuiga, ni kusema, namna ya kufuata hatua zake kwa ukaribu! Inaweza kuwa muzuri mu funzo lako la kipekee ao mu Ibada yenu ya Familia mujiwekee muradi wa kujifunza vile Vitabu vya Injili, hauone vile? Tusisahau kama, juu funzo letu lifikie kutuletea faida, tunapaswa kujikaza kufanya ile habari yenye tuko tunasoma ikuwe ya kweli; na pia tutumikishe mambo yenye tuko tunajifunza. Tunapaswa kuiga mambo yenye Yesu alifanya, lakini pia kutumikisha mambo yenye alisema. Mu habari yenye kufuata, tutaona mambo yenye tunaweza kujifunza mu maneno yenye Yesu alisema mbele akufe.

WIMBO 15 Tumusifu Muzaliwa wa Kwanza wa Yehova!

^ fu. 5 Juu tuko Wakristo wa kweli, tunapaswa “kufuata hatua [za Yesu] kwa ukaribu.” Yesu alituachia “hatua” gani zenye tunapaswa kufuata? Hii habari itajibia ile ulizo. Itazungumuzia pia juu ya nini tunapaswa kufuata hatua zake kwa ukaribu, na namna gani tunaweza kufanya vile.

^ fu. 60 MAELEZO YA PICHA: Kisha kufikiri sana juu ya mambo yenye Yesu alisema kuhusu ule mujane maskini, dada fulani anapongeza dada mumoja mwenye kuzeeka juu anamutumikia Yehova kwa nafsi yake yote.