Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 17

Yehova Anakupenda Sana!

Yehova Anakupenda Sana!

“Yehova anafurahia watu wake.”​—ZB. 149:4.

WIMBO 108 Mungu Iko na Upendo Mushikamanifu

KIFUPI CHA HABARI *

Baba yetu wa mbinguni “anafurahia” kila mumoja wetu (Ona fungu la 1)

1. Yehova anaona mambo gani kwa watu wake?

YEHOVA MUNGU “anafurahia watu wake.” (Zb. 149:4) Ile inatufurahisha sana! Yehova anaona sifa zetu za muzuri, anaona uwezo wetu mbalimbali na anatusaidia tukuwe marafiki wake. Kama tunabakia waaminifu kwake, ataendelea kuwa karibu na siye milele!​—Yoh. 6:44.

2. Juu ya nini watu fulani wanaona ni nguvu kuamini kama Yehova anawapenda?

2 Watu fulani wanaweza kusema hivi: ‘Najua kama Yehova anapenda watu wake wakiwa kikundi, lakini, namna gani naweza kuwa hakika kama Yehova ananipenda miye kipekee?’ Nini njo inaweza kufanya mutu ajiulize ile ulizo? Oksana, * mwenye aliteseka sana wakati alikuwa mutoto, anasema hivi: “Nilifurahi sana wakati nilibatizwa na kuanza kazi ya upainia. Lakini kisha miaka 15, nilianza kukumbuka mambo ya mubaya sana yenye ilinifikia wakati nilikuwa mutoto. Nilianza kufikiri kama Yehova hanikubali na kama sistahili kabisa kupendwa naye.” Dada Yua, painia mumoja mwenye pia alikuwa na magumu mingi wakati alikuwa mutoto, anasema hivi: “Nilitoa maisha yangu kwa Yehova juu nilipenda kumufurahisha. Lakini nilikuwa hakika kama, hawezi kunipenda hata siku moja.”

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Kama wale Wakristo waaminifu wenye tumetoka kutaja, weye pia unamupenda Yehova sana. Lakini, pengine unaweza kuwa na mashaka kama Yehova pia anakupenda. Juu ya nini unapaswa kuwa hakika kama Yehova anakuhangaikia kabisa? Na ni nini inaweza kukusaidia wakati unawaza kama Yehova hakupende? Tujibie basi ile maulizo.

NI HATARI KUWA NA MASHAKA KAMA YEHOVA ANAKUPENDA

4. Juu ya nini ni hatari kuwa na mashaka kama Yehova anatupenda?

4 Ikiwa tuko hakika kama Yehova anatupenda, tutamutumikia kwa uwezo wetu wote hata kama maisha yetu iko nguvu. Lakini ikiwa tuko na mashaka kama Mungu anatuhangaikia, ‘nguvu zetu zitakuwa kidogo.’ (Mez. 24:10) Na wakati tunavunjika moyo na tunaanza kuwaza kama Mungu hatupende, hatutaweza kusimama wakati Shetani anatushambulia.​—Efe. 6:16.

5. Ni nini ilifikia ndugu na dada fulani wenye walikuwa na mashaka kama Mungu anawapenda?

5 Leo, ndugu na dada fulani wameanza kufikiri kama Yehova hawapende na hawahangaikie, na ile imefanya imani yao ikuwe zaifu. Muzee mumoja mwenye kuitwa James anasema hivi: “Nilikuwa natumika ku Beteli na nilikuwa mu kutaniko la luga ya kigeni. Lakini, sikukuwa hakika kama Yehova alikuwa anafurahia utumishi wenye nilikuwa namutolea. Wakati fulani nilianza hata kujiuliza ikiwa Yehova alikuwa anasikiliza sala zangu.” Dada Eva, mwenye pia iko mu utumishi wa wakati wote anasema hivi: “Nilijifunza kuwa ni hatari kuwaza kama Yehova hatupende. Juu ile inaweza kuwa na matokeo ya mubaya juu ya utumishi wenye tuko tunamutolea. Inaweza kufanya tupoteze hamu ya kufanya mambo ya kiroho na tupoteze furaha ya kumutumikia.” Michael, mwenye ni muzee na pia painia wa kawaida, anasema hivi: “Kama hauamini kuwa Yehova anakuangaikia, utakuwa mbali naye.”

6. Tunapaswa kufanya nini ikiwa tunaanza kuwaza kama Mungu hatupende?

6 Maelezo ya wale Wakristo inatuonyesha matokeo ya mubaya yenye tunaweza kupata wakati tunawaza kama Yehova hatupende. Lakini tunaweza kufanya nini kama tunaanza kuwa na mawazo ya vile? Tunapaswa kuitosha mara moja mu akili yetu! Umuombe Yehova akusaidie ubadilishe ile “mawazo yenye kusumbua” na akupatie ‘amani Yake yenye italinda moyo wako na nguvu zako za akili.’ (Zb. 139:23; maelezo ya chini.; Flp. 4:6, 7) Na usisahau kama hauko weye peke, ndugu na dada wengine waaminifu wako wanapiganisha ile mawazo ya mubaya. Na hata watumishi fulani wa Yehova wa zamani walipiganisha mawazo ya vile. Tuone sasa mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia mufano wa mutume Paulo.

TUNAWEZA KUJIFUNZA NINI KUPITIA MAMBO YENYE PAULO ALIKUTANA NAYO?

7. Paulo alikuwa na magumu gani?

7 Wakati fulani, unajisikiaka sawa vile uko na madaraka mingi sana na kama ni nguvu sana kuitimiza yote? Kama ni vile, unaweza kumuelewa Paulo. Alihangaikia sana, hapana tu kutaniko moja, lakini, “makutaniko yote.” (2 Ko. 11:23-28) Uko na magonjwa yenye inakuhangaishaka sana, yenye inafanyaka upoteze furaha yako? Paulo alikuwa na “mwiba katika mwili” yenye ilimuhangaisha sana, pengine ilikuwa ni tatizo la afya na alipenda ile tatizo iishe. (2 Ko. 12:7-10) Wakati fulani, unavunjika moyo sababu ya uzaifu wako? Ile hali ilimufikia Paulo wakati fulani. Alijiita yeye mwenyewe kuwa “maskini” sababu kila mara alipaswa kupiganisha hali yake ili afikie kufanya mambo ya muzuri.​—Ro. 7:21-24.

8. Ni nini ilimusaidia Paulo avumilie magumu yake?

8 Paulo aliendelea kumutumikia Yehova hata kama alipata ile magumu yote. Ni nini ilimusaidia? Hata kama alijua uzaifu wake, alikuwa na imani ya nguvu sana katika bei ya ukombozi. Tena alijua muzuri hii ahadi ya Yesu: ‘Kila mutu mwenye anamuamini Yesu . . . atapata uzima wa milele.’ (Yoh. 3:16; Rom. 6:23) Bila shaka Paulo alikuwa kati ya watu wenye walionyesha imani katika bei ya ukombozi. Alikuwa hakika kama Yehova iko tayari kusamehe hata wale wenye walifanya zambi nzito kama wanatubu.​—Zb. 86:5.

9. Maneno ya Paulo yenye kuwa mu Wagalatia 2:20, inatufundisha nini?

9 Paulo alikuwa hakika kama Yehova anamupenda sana, juu Mungu alituma Yesu ili akufe kwa ajili yake. (Soma Wagalatia 2:20.) Tunaona uhakika wa Paulo mu maneno yenye alisema ku mwisho ya Wagalatia 2:20. Paulo alisema hivi: “Mwana wa Mungu . . . alinipenda na kujitoa mwenyewe kwa ajili yangu.” Paulo hakuwaza kama Mungu hangemupenda juu alikuwaka mutu mubaya, hakufikiri hivi: ‘Minajua juu ya nini Yehova anapenda ndugu na dada zangu, lakini pengine hawezi kunipenda miye.’ Paulo alikumbusha Waroma hivi: “Wakati tulikuwa tungali watenda-zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.” (Ro. 5:8) Upendo wa Mungu hauna mipaka!

10. Waroma 8:38, 39, inatufundisha nini?

10 Soma Waroma 8:38, 39. Paulo alikuwa hakika kama upendo wa Mungu uko na nguvu sana. Aliandika kama hakuna kitu ‘kitaweza kututenganisha na upendo wa Mungu.’ Paulo alijua kama Yehova alitendea kwa uvumilivu taifa la Israeli. Alijua pia namna Yehova alimuonyesha rehema. Mu maneno ingine Paulo alikuwa anasema, ‘Juu Yehova alituma Mwana wake akufe kwa ajili yangu, sipaswe kuwa na mashaka kama ananipenda.’​—Ro. 8:32.

Kwa Mungu, mambo yenye uko unafanya sasa na yenye utafanya njo anaona kuwa ya maana. Hapana makosa yenye ulifanya zamani (Ona fungu la 11) *

11. Hata kama Paulo alifanya zambi kama zile zenye zinatajwa mu 1 Timoteo 1:12-15, juu ya nini alikuwa hakika kuwa Mungu alimupenda?

11 Soma 1 Timoteo 1:12-15. Inawezekana Paulo alijisikia mubaya sana wakati alikumbuka mambo yenye alifanya zamani mbele akuwe Mukristo. Haitushangaze kuona vile alijiita mutenda-zambi wa “kwanza kabisa”! Mbele Paulo ajifunze kweli alikuwa anatesa Wakristo katika muji moja kisha ingine. Aliingiza wamoja mu gereza na akakubali wengine wauawe. (Mdo. 26:10, 11) Unawaza Paulo angejisikia namna gani wakati angeona kijana Mukristo mwenye wazazi wake waliuawa juu yeye njo alikubaliana na ile maamuzi? Paulo alihuzunika sana juu ya mambo yenye alifanya, lakini alijua kama hangeweza kubadilisha mambo ya zamani. Aliamini kama Yesu alikufa kwa ajili yake, njo maana aliandika hivi: “Kwa fazili zenye hazistahiliwe za Mungu mimi niko kile niko.” (1 Ko. 15:3, 10) Ile inatufundisha nini? Unapaswa kuwa hakika kama Yesu alikufa kwa ajili yako na ile inafanya ukuwe na urafiki wa karibu sana pamoja na Yehova. (Mdo. 3:19) Kwa Mungu, mambo yenye uko unafanya sasa na yenye utafanya njo anaona kuwa ya maana. Hapana makosa yenye ulifanya zamani, ikuwe ile wakati ulikuwa Shahidi wa Yehova ao hapana.​—Isa. 1:18.

12. Maneno yenye kuwa mu 1 Yohana 3:19, 20 inaweza kutusaidia namna gani wakati tunajiona kuwa wa bure ao wakati tunawaza kama Mungu hatupende?

12 Kuhusu kifo ya Yesu kwa ajili ya zambi zako, pengine unaweza kuwaza hivi, ‘Sistahili kabisa kupata hii zawadi ya maana sana.’ Juu ya nini unaweza kuwaza vile? Moyo wetu mudanganyifu unaweza kufanya tujisikie kama tuko wa bure na kama Mungu hatupende. (Soma 1 Yohana 3:19, 20.) Wakati tunaanza kuwaza vile ni lazima tukumbuke kama “Mungu ni mukubwa kuliko mioyo yetu.” Hata kama tunawaza kuwa Yehova hatupende ao hatatusamehe, tukuwe hakika kama Baba yetu wa mbinguni angali anatupenda na atatusamehe. Tunapaswa kujihakikishia kama Yehova anatupenda. Ili tuweze kufanya vile, tunapaswa kujifunza Neno la Mungu kwa ukawaida, kusali kwake bila kuacha, na kupitisha wakati pamoja na watu wake wenye wanamuabudu. Juu ya nini ni jambo la maana sana kufanya ile mambo yote?

TUNAWEZA KUPATA MUSAADA KUPITIA FUNZO LA BIBLIA, SALA, NA MARAFIKI WAZURI MU KUTANIKO

13. Kujifunza Neno la Mungu kunaweza kutusaidia namna gani? (Ona kisanduku “ Namna Neno la Mungu Iiliwasaidia.”)

13 Ujifunze Neno la Mungu kila siku. Ile itakusaidia uelewe muzuri zaidi sifa mingi za Yehova zenye kupendeza. Tena, utafikia kuelewa kabisa ni kwa kiasi gani Yehova anakupenda. Wakati unafikiri sana juu ya Neno la Mungu kila siku, ile inaweza kukusaidia ukuwe na mawazo yenye kufaa, na ‘itanyoosha mambo’ mu akili na mu moyo wako. (2 Ti. 3:16) Kevin, muzee mumoja mwenye alikuwa na mawazo yenye haifae juu yake mwenyewe, anasema hivi: “Kusoma na kufikiri sana juu ya Zaburi ya 103 imenisaidia kubadilisha mawazo yangu na kuelewa namna Yehova ananiona kabisa.” Eva, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Kila siku mbele nilale nafikiriaka sana mambo yenye Yehova anaona kuwa ya maana. Ile inafanya nikuwe na amani ya moyo na inajenga imani yangu.”

14. Sala inaweza kutusaidia namna gani?

14 Usali bila kuacha. (1 Te. 5:17) Kama unapenda kufanya urafiki na mutu fulani unapaswa kuzungumuza naye kwa ukawaida na kumuambia namna unajisikia. Ni vile pia kama tunapenda kufanya urafiki pamoja na Yehova. Wakati tunamuambia mu sala mawazo yetu, namna tunajisikia na mahangaiko yetu, tunaonyesha kama tunamutumainia na kama tunajua kuwa anatupenda. (Zb. 94:17-19; 1 Yo. 5:14, 15) Yua, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Wakati nasali, simuambie Yehova tu mambo yenye nilifanya ile siku, namuambia pia mambo yenye niko nawaza kabisa, na vile niko najisikia. Pole kwa pole, nilifikia kumuona Yehova kuwa sawa vile Baba mwenye anapenda kabisa watoto wake, hapana sawa vile boss wa kompani fulani.”​—Ona kisanduku “ Ulishakaisoma?

15. Namna gani Yehova anaonyesha kama anatuhangaikia?

15 Upitishe wakati pamoja na marafiki wazuri mu kutaniko. Wao ni zawadi kutoka kwa Yehova. (Yak. 1:17) Baba yetu wa mbinguni anaonyesha kama anatuhangaikia kwa kutupatia familia ya kiroho ya ndugu na dada wenye wanatuonyesha upendo “nyakati zote.” (Mez. 17:17) Mu barua yake kwa Wakolosai, Paulo alitaja Wakristo fulani wenye walimutegemeza na aliwaita “chanzo cha faraja nyingi.” (Kol. 4:10, 11) Hata Yesu Kristo alikuwa na lazima ya musaada na alionyesha shukrani wakati marafiki wake walimusaidia, ikuwe malaika ao wanadamu.​—Lu. 22:28, 43.

16. Namna gani marafiki wazuri mu kutaniko wanaweza kutusaidia tumukaribie Yehova?

16 Unaombaka musaada kwa marafiki wako mu kutaniko na kuukubali? Haiko uzaifu kuambia Mukristo mwenye kukomaa kiroho mambo yenye inakuhangaisha; kufanya vile kunaweza kukulinda. Fikiria mambo yenye James, mwenye tumeshataja anasema: “Kuwa na urafiki pamoja na Wakristo wenye kukomaa kiroho kumenisaidia sana. Wakati mawazo ya mubaya inanihangaisha, wale marafiki wananisikiliza kwa uvumilivu na wananiambia kama wananipenda. Wakati wanafanya vile, ile inanisaidia kuona kama Yehova ananipenda na ananihangaikia.” Ni jambo la maana sana kufanya urafiki pamoja na ndugu na dada zetu wa kiroho!

UBAKIE KATIKA UPENDO WA YEHOVA

17-18. Tunapaswa kusikiliza nani na juu ya nini?

17 Shetani anapenda tuache kufanya mambo ya muzuri. Anapenda tuamini kama Yehova hatupende, na kama hatustahili kuokolewa. Lakini vile tumetoka kuona, ile ni uongo kabisa.

18 Yehova anakupenda. Anakuona kuwa wa maana sana. Ukimutii, sawa Yesu, na weye ‘utabakia katika upendo wake’ milele. (Yoh. 15:10) Kwa hiyo, usisikilize Shetani ao moyo wako mudanganyifu wenye unakufanya ujisikie kuwa Yehova hakupende. Kuliko kufanya vile, umusikilize Yehova mwenye anaona mambo ya muzuri yenye kila mumoja wetu iko nayo. Ukuwe hakika kama Yehova “anafurahia watu wake,” na weye!

WIMBO 141 Uzima Ni Muujiza

^ fu. 5 Ndugu na dada fulani wanaona ni nguvu kuamini kama Yehova anawapenda. Mu hii habari tutaona ni juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova anapenda kila mumoja wetu. Tutazungumuzia pia mambo yenye tunaweza kufanya wakati tuko na mashaka kama Yehova anatupenda.

^ fu. 2 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 67 MAFASIRIO YA PICHA Mbele Paulo ajifunze kweli, alitesa Wakristo na alipeleka wengi kati yao mu gereza. Wakati Paulo alikubali mambo yenye Yesu alikuwa amemufanyia, alibadilika na akatia moyo ndugu zake Wakristo. Na inawezekana wamoja kati yao walikuwa na watu wa familia wenye Paulo alitesaka.