Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 19

Hakuna Kitu Inaweza Kufanya Mwenye Haki Ajikwae

Hakuna Kitu Inaweza Kufanya Mwenye Haki Ajikwae

“Wale wenye kupenda sheria yako wako na amani nyingi; hakuna kitu chochote chenye kinaweza kuwafanya wajikwae.”​—ZB. 119:165.

WIMBO 122 Tukuwe na Nguvu na Tusitikisike!

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Muandikaji mumoja alisema nini, na tutazungumuzia nini mu hii habari?

LEO mamilioni ya watu wanasema kama wanaamini Yesu lakini hawafuate mambo yenye alifundisha. (2 Ti. 4:3, 4) Muandikaji mumoja alisema hivi: “Kama leo kungekuwa mutu mwenye kuwa sawa Yesu je, tungemukubali ao tungemukatala sawa vile watu walimukatala Yesu wakati wake? . . . Kwa ujumla jibu ni ndiyo, tungemukatala.”

2 Wakati Yesu alikuwa hapa ku dunia, watu wengi walisikia wakati alikuwa anafundisha na waliona wakati alifanya miujiza, lakini walikatala kumuamini. Juu ya nini? Mu habari yenye ilitangulia tulizungumuzia sababu ine zenye zilifanya watu wamukatale Yesu juu ya mambo yenye alisema na kufanya. Tuzungumuzie basi sababu ine zingine. Tutaona pia juu ya nini leo watu wanakatala wafuasi wa Yesu na mambo yenye inaweza kutusaidia tusiache kumutumikia Yehova.

(1) YESU HAKUKUWA NA UBAGUZI

Sababu yenye kufuata ilifanya watu fulani wamukatale Yesu: marafiki wenye alichagua. Namna gani ile sababu inaweza kufanya watu fulani watukatale pia leo? (Ona fungu la 3) *

3. Yesu alifanya mambo gani yenye ilifanya watu wamukatale?

3 Wakati Yesu alikuwa hapa ku dunia, alipitisha wakati pamoja na watu wa namna zote. Alikula pamoja na matajiri na watu wenye walikuwa na mamlaka, lakini pia alipitisha wakati mingi pamoja na maskini na watu wenye kuwa na lazima ya musaada. Tena, alisikilia huruma watu wenye wengi waliona kuwa “watenda-zambi.” Watu fulani wenye majivuno walimukatala Yesu juu ya ile mambo yenye alifanya. Waliuliza wanafunzi wake hivi: “Sababu gani munakula na kunywa pamoja na wakusanya-kodi na watenda-zambi?” Kisha Yesu akawajibu: “Watu wenye afya hawana lazima ya munganga, lakini wagonjwa ndio wako na lazima yake. Sikukuja kuita watu wenye haki, lakini nilikuja kuita watenda-zambi ili watubu.”​—Lu. 5:29-32.

4. Kulingana na mambo yenye nabii Isaya aliandika, Wayahudi wangepaswa kutazamia nini kumuhusu Masiya?

4 Maandiko ilisema nini? Mbele Masiya akuje hapa ku dunia, nabii Isaya alionyesha kama hangekubaliwa na ulimwengu. Unabii ulisema hivi: “Alizarauliwa na kuepukwa na wanadamu . . . Ilikuwa kama vile uso wake ulifichwa tusiuone. Alizarauliwa, na hatukumuona kuwa mutu wa maana.” (Isa. 53:3) Unabii ulionyesha kama Masiya angeepukwa na “wanadamu.” Njo maana Wayahudi wa wakati wa Yesu wangetazamia kama watu watamukatala Yesu.

5. Leo watu wengi wanaona namna gani wafuasi wa Yesu?

5 Ile tatizo iko pia leo? Ndiyo. Wakubwa wengi wa dini wanafurahiaka wakati wanaona watu wa maana sana, matajiri na wenye ulimwengu unaona kuwa wenye hekima wanajiunga na kanisa yao. Wale wakubwa wa dini wanaacha wale watu wakuwe mu kanisa yao hata kama wanafanya mambo yenye inapingana na kanuni za Mungu. Lakini viongozi wa dini wanazarau watumishi wa Yehova wenye kuwa na bidii na mwenendo safi, juu hawako watu wenye kujulikana sana. Kama vile Paulo alisema, Mungu alichagua wale wenye “kuzarauliwa.” (1 Ko. 1:26-29) Lakini, Yehova anaona watumishi wake wote waaminifu kuwa wa maana sana.

6. Namna gani tunaweza kuiga mawazo ya Yesu yenye kuwa mu Matayo 11:25, 26?

6 Ni nini inaweza kukusaidia usipoteze imani? (Soma Matayo 11:25, 26.) Tusiache mawazo ya ulimwengu itufanye tukuwe na mawazo yenye haifae juu ya watu wa Mungu. Tukubali kama Yehova anatumikishaka tu watu wanyenyekevu ili kufanya mapenzi yake. (Zb. 138:6) Wazia mambo yote yenye Yehova amefanya kwa kutumikisha watu wenye ulimwengu unaona kuwa hawana hekima ao watu wenye hawana elimu.

(2) YESU ALIFUNUA MAFUNDISHO YA UONGO

7. Juu ya nini Yesu aliita Wafarisayo wanafiki, na walitenda namna gani?

7 Bila kuogopa, Yesu alionyesha waziwazi kama viongozi wa dini walikuwa na kosa juu hawakufundisha watu namna ya kumuabudu Yehova mu njia yenye kufaa. Kwa mufano, alionyesha kama Wafarisayo walikuwa wanafiki juu walihangaikia sana namna walikuwa wananawa mikono kuliko kuhangaikia wazazi wao. (Mt. 15:1-11) Pengine maneno ya Yesu ilishangaza sana wanafunzi wake. Njo maana walimuuliza: “Unajua kama Wafarisayo walikwazika wakati walisikia maneno yenye ulisema?” Yesu aliwajibu: “Kila mumea wenye Baba yangu wa mbinguni hakupanda utangolewa. Muwaache. Wao ni viongozi vipofu. Basi, kama kipofu anamuongoza kipofu, wote wawili wataanguka ndani ya shimo.” (Mt. 15:12-14) Hata kama viongozi wa dini walimukasirikia Yesu juu ya mambo yenye alisema, Yesu hakuacha kusema kweli.

8. Namna gani Yesu alionyesha kama Mungu hakubali mafundisho ya dini zote?

8 Yesu alionyesha pia kama viongozi fulani wa dini walifundisha mambo ya uongo. Hakusema kama Mungu anakubali mafundisho ya dini zote, alisema kama watu wengi wangepita kupitia barabara kubwa yenye kuongoza kwenye uharibifu lakini ni watu kidogo tu njo wangepita kupitia barabara yenye kuongoza kwenye uzima. (Mt. 7:13, 14) Alionyesha waziwazi kama watu fulani wangesema kama wanamutumikia Mungu, lakini kusema kweli hawafanye vile. Alionya hivi: “Mufanye angalisho na manabii wa uongo wenye wanakuja kwenu katika ngozi ya kondoo, lakini ndani wao ni imbwa wa pori wakali. Mutawatambua kwa matunda yao.”​—Mt. 7:15-20.

Sababu yenye kufuata ilifanya watu fulani wamukatale Yesu: kuonyesha waziwazi kama mafundisho na desturi fulani zilikuwa za uongo. Namna gani ile sababu inaweza kufanya watu fulani watukatale pia leo? (Ona fungu la 9) *

9. Ni mafundiso gani fulani ya dini yenye Yesu alionyesha kama ni ya uongo?

9 Maandiko ilisema nini? Unabii wa Biblia ulionyesha kama Masiya angekuwa na bidii sana kwa ajili ya nyumba ya Yehova. (Zb. 69:9; Yoh. 2:14-17) Ile bidii ilimuchochea Yesu kuonyesha waziwazi mafundisho na desturi za uongo za dini. Kwa mufano, Wafarisayo waliamini kama nafsi haikufake lakini Yesu alifundisha kama wafu wako wanalala. (Yoh. 11:11) Wasadukayo hawakuamini kama kuko ufufuo lakini Yesu alimufufua rafiki yake Lazaro. (Yoh. 11:43, 44; Mdo. 23:8) Wafarisayo walifundisha kama Mungu ao nguvu fulani yenye haionekanake njo inaongozaka mambo yote yenye inatufikiaka mu maisha na mambo yenye tutafanyaka. Lakini Yesu alifundisha kama wanadamu wanaweza kuchagua kumutumikia Mungu ao hapana.​—Mt. 11:28.

10. Juu ya nini mafundisho yetu inafanya watu wengi watukatale?

10 Ile tatizo iko pia leo? Ndiyo. Watu wengi wanatukatala juu tunatumia Biblia ili kuwaonyesha kama mafundisho fulani ya dini ni ya uongo. Viongozi wa dini wanafundisha wafuasi wao kama Mungu anachomaka watu wabaya mu moto ya mateso. Wanatumia ile fundisho ili kuogopesha watu na kuwafanya wabakie mu dini yao. Tukiwa watumishi wa Yehova, tunamuabudu Mungu wa upendo, tunasaidia watu waelewe kama ile fundisho ni ya uongo. Wale viongozi wanafundisha pia kama nafsi haikufake. Kama ile fundisho ingekuwa ya kweli hakuna mwenye angepaswa kufufuliwa. Njo maana tunaonyesha waziwazi kama ile fundisho haiko mu Biblia. Tena, dini za mingi zinafundisha kama mambo yote yenye tunafanyaka ilishakapangiwa na Mungu tangu zamani, lakini siye tunafundisha kama mwanadamu iko na uhuru wa kuchagua na akipenda anaweza kuchagua kumutumikia Mungu ao hapana. Wakati viongozi wa dini wanasikiaka ile mafundisho yenye tunafundisha wanajisikiaka namna gani? Mara mingi wanasirikaka!

11. Kulingana na maneno ya Yesu yenye kuwa mu Yohana 8:45-47, Mungu anapenda watu wake wafanye nini?

11 Ni nini inaweza kukusaidia usipoteze imani? Kama tunapenda kweli tunapaswa kuamini na kutii maneno ya Mungu. (Soma Yohana 8:45-47.) Tofauti na Shetani Ibilisi, siye tunashikamana na kweli. Kila mara tunaepukaka kufanya mambo yenye inapingana na imani yetu. (Yoh. 8:44) Mungu anapenda watu wake ‘wachukie sana mambo maovu’ na ‘washikamane na mambo mema,’ kama vile Yesu alifanya.​—Ro. 12:9; Ebr. 1:9.

(3) YESU ALITESWA

Sababu yenye kufuata ilifanya watu fulani wamukatale Yesu: kifo yake ku muti wa mateso. Namna gani ile sababu inaweza kufanya watu fulani watukatale pia leo? (Ona fungu la 12) *

12. Namna Yesu alikufa ilifanya Wayahudi wengi wamukatale. Juu ya nini?

12 Ni sababu gani ingine yenye ilifanya Wayahudi wamukatale Yesu? Paulo alisema hivi: “Tunahubiri Kristo mwenye aliuawa kwenye muti, kwa Wayahudi hiyo ni sababu ya kujikwaa.” (1 Ko. 1:23) Namna Yesu alikufa ilifanya Wayahudi wengi wamukatale. Juu ya nini? Kwao, vile Yesu alikufa ku muti wa mateso ilionyesha kama hakukuwa Masiya lakini alikuwa muovu na mutenda-zambi.​—Kum. 21:22, 23.

13. Wayahudi wenye walimukatala Yesu walishindwa kukubali nini?

13 Wayahudi wenye walimukatala Yesu walishindwa kukubali kama Yesu hakukuwa na kosa, kama alishitakiwa mambo ya uongo na kama alitendewa mubaya. Tribinali kubwa ya Wayahudi yenye ilikuwa inamusambisha Yesu haikumusambisha muzuri. Waamuzi wa ile tribinali walikutana haraka na wakamuhukumu Yesu tofauti na vile sheria ilisema. (Lu. 22:54; Yoh. 18:24) Kuliko kuchunguza muzuri mashitaka na ushuhuda mbalimbali wenye watu walileta juu ya Yesu, wale waamuzi walijitafutia wao wenyewe “ushuhuda wa uongo juu ya Yesu ili wamuue.” Wakati hawakupata ushuhuda wowote, kuhani mukubwa alijaribu kumuuliza Yesu maulizo fulani ili apate sababu fulani yenye ingefanya ahukumiwe. Huruma sana! Ile ilikuwa tofauti kabisa na sheria. (Mt. 26:59; Mk. 14:55-64) Kisha Yesu kufufuliwa, wale waamuzi wenye hawako wenye haki, walilipa maaskari wa Roma wenye walikuwa wanachunga kaburi la Yesu “hesabu kubwa ya vipande vya feza,” ili kueneza habari ya uongo yenye ingefasiria ni juu ya nini kaburi la Yesu lilikuwa wazi.​—Mt. 28:11-15.

14. Ni mambo gani Maandiko ilitabiri kuhusu kifo ya Masiya?

14 Maandiko ilisema nini? Hata kama Wayahudi wengi wa wakati wa Yesu hawakuwazia kama Masiya angepaswa kufa, ona mambo yenye Maandiko ilitabiri kumuhusu: “Alimwanga uzima wake hata mupaka kifo na alihesabiwa kati ya wakosaji; alibeba zambi ya watu wengi, na alitetea wakosaji.” (Isa. 53:12) Kwa hiyo, juu Yesu alishitakiwa mambo ya uongo na kuuawa haiko ile njo ingefanya Wayahudi wamukatale.

15. Ni mashitaka gani juu ya Mashahidi wa Yehova yenye imefanya watu fulani wawakatale?

15 Ile tatizo iko pia leo? Ndiyo. Yesu alishitakiwa mambo ya uongo na akahukumiwa kama alikuwa na kosa; leo pia watu wanatendea vile Mashahidi wa Yehova. Fikiria mifano fulani. Kati ya 1930 na 1950, Mashahidi wa Yehova wa Amerika walisamba sana ku tribinali ili kutetea uhuru wao wa kumuabudu Mungu. Bila haya, waamuzi fulani walituhukumu kwa njia yenye haiko ya haki. Katika Québec, mu Kanada, kanisa na serikali zilitumika pamoja ili kupinga kazi yetu. Wahubiri wengi walifungwa juu tu walihubiria majirani wao habari njema kuhusu Ufalme wa Mungu. Mu Alemanye, utawala wa Nazi uliua ndugu vijana wengi wenye walikuwa waaminifu kwa Yehova. Mu miaka kidogo yenye imepita ndugu wengi wenye kuwa mu Urusi walihukumiwa kama walikuwa na kosa na walifungwa juu walizungumuza na watu juu ya Biblia. Serikali ilisema kama ile ni “kazi ya watu wenye musimamo mukali.” Hata Biblia​—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya ya luga ya Kirusi ilikatazwa na kuonwa kuwa “kitabu hatari” juu inatumia jina Yehova.

16. Kulingana na 1 Yohana 4:1, juu ya nini hatupaswe kusikiliza habari za uongo zenye watu wanasema juu ya Mashahidi wa Yehova?

16 Ni nini inaweza kukusaidia usipoteze imani? Tunapaswa kutafuta kujua habari za kweli. Katika Mahubiri yake ya kwenye Mulima, Yesu aliwaonya wasikilizaji wake kama watu fulani ‘wangewasingizia kila namna ya uovu.’ (Mt. 5:11) Ile uongo yote inatoka kwa Shetani. Anachochea wale wenye wanatupinga waeneze habari za uongo zenye kuumiza juu ya wale wenye wanapenda kweli. (Ufu. 12:9, 10) Hatupaswe kusikiliza uongo wenye kusemwa na wale wenye wanatupinga. Hatupaswe hata kidogo kuacha ile uongo ituogopeshe kumutumikia Yehova ao kuregeza imani yetu.​—Soma 1 Yohana 4:1.

(4) YESU ALISALITIWA NA KUACHWA

Sababu yenye kufuata ilifanya watu fulani wamukatale Yesu: kusalitiwa na Yuda. Namna gani ile sababu inaweza kufanya watu fulani watukatale pia leo? (Ona fungu la 17-18) *

17. Namna gani mambo yenye ilitokea mbele ya kifo ya Yesu ilifanya watu fulani wamukatale?

17 Mbele akufe, Yesu alisalitiwa na mumoja kati ya mitume wake 12. Mutume wake mwingine alimukana mara tatu, na mitume wake wote walimuacha mangaribi mbele ya kifo yake. (Mt. 26:14-16, 47, 56, 75) Ile haikumushangaza. Alikuwa alishatabiri kama ile mambo ingetokea. (Yoh. 6:64; 13:21, 26, 38; 16:32) Wakati ile mambo ilitokea, watu fulani wangeamua kama hawatakuwa wanafunzi wake. Pengine wangesema hivi: ‘Kama njo vile mitume wa Yesu walitenda, sasa miye njo nikuwe mwanafunzi wake? Hapana!’

18. Ni maunabii gani ilitimia mbele Yesu akufe?

18 Maandiko ilisema nini? Miaka mingi mbele Yesu akuje ku dunia, Yehova alifunua mu Neno lake kama Masiya atasalitiwa kwa vipande 30 vya feza. (Zek. 11:12, 13) Mwenye angemusaliti Yesu angekuwa mumoja kati ya marafiki wake wa karibu. (Zb. 41:9) Nabii Zekaria aliandika pia hivi: “Piga muchungaji, na kundi litawanyike.” (Zek. 13:7) Kuliko kukwazika juu ya mambo yenye ilitokea, watu wenye moyo muzuri walipaswa kutiwa moyo wakati waliona maunabii kuhusu Yesu inatimia.

19. Watu wenye moyo muzuri wanajua nini?

19 Ile tatizo iko pia leo? Ndiyo. Leo Mashahidi fulani wameacha kumutumikia Yehova, wamekuwa waasi-imani, na wamechochea wengine wawafuate. Wameeneza habari za mubaya, wamepotosha watu, na kusema mambo ya uongo juu ya Mashahidi wa Yehova. Kwa mufano, wanafanya vile kupitia radio, televizyo, na Enternete. Lakini watu wenye moyo muzuri hawadanganywe, wanajua kama Biblia ilitabiri kuwa ile mambo itatokea.​—Mt. 24:24; 2 Pe. 2:18-22.

20. Nini njo inaweza kutusaidia tusidanganywe na wale wenye wameacha kweli? (2 Timoteo 4:4, 5)

20 Ni nini inaweza kukusaidia usipoteze imani? Tunapaswa kuendelea kutia nguvu imani yetu kwa kujifunza kwa ukawaida, kwa kusali bila kuacha na kwa kuendelea kutimiza kwa bidii kazi yenye Yehova ametupatia. (Soma 2 Timoteo 4:4, 5.) Kama tuko na imani hatutaogopa wakati tunasikia habari za mubaya kuhusu Mashahidi wa Yehova. (Isa. 28:16) Kupenda Yehova, Neno lake, na ndugu zetu kutatusaidia tusidanganywe na wale wenye wameacha kweli.

21. Hata kama watu wengi leo wanakatala ujumbe wetu tunaweza kuwa hakika na jambo gani?

21 Wakati wa mitume, watu wengi walimukatala Yesu. Lakini kulikuwa watu wengine wengi wenye walimukubali. Kwa mufano, kulikuwa mushiriki mumoja wa Sanedrini na hata “makuhani wengi sana.” (Mdo. 6:7; Mt. 27:57-60; Mk. 15:43) Leo pia kuko mamilioni ya watu wenye wameamua kumufuata Yesu. Juu ya nini? Juu, wanajua na wanapenda kweli yenye kupatikana mu Maandiko. Neno la Mungu linasema hivi: “Wale wenye kupenda sheria yako wako na amani nyingi; hakuna kitu chochote chenye kinaweza kuwafanya wajikwae.”​—Zb. 119:165.

WIMBO 124 Tukuwe Washikamanifu

^ fu. 5 Mu habari yenye ilitangulia tulijifunza sababu ine zenye zilifanya watu wamutakale Yesu na tuliona ni juu ya nini leo watu wanakatala wafuasi wake. Mu hii habari, tutazungumuzia sababu ine zingine na tutaona juu ya nini wale wenye kumupenda kabisa Yehova hawaache jambo lolote liwafanye waache kumutumikia.

^ fu. 60 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu iko anakula pamoja na Matayo na wakusanya-kodi.

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu anafukuza wafanyabiashara mu hekalu.

^ fu. 64 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu anaambiwa abebe muti wa mateso.

^ fu. 66 MAFASIRIO YA PICHA: Yuda anamusaliti Yesu kwa kumubusu.