Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 18

Kuko Sababu Inaweza Kufanya Ukatale Kumufuata Yesu?

Kuko Sababu Inaweza Kufanya Ukatale Kumufuata Yesu?

“Mwenye furaha ni mutu mwenye hapate ndani yangu sababu yoyote ya kukwazika.”​—MT. 11:6.

WIMBO 54 “Hii Ndiyo Njia”

KIFUPI CHA HABARI *

1. Pengine nini njo ilikushangaza wakati ulianza kuambia wengine mambo ulijifunza mu Biblia?

UNAKUMBUKA siku yenye ulijua kama umepata kweli? Ilikuwa mwepesi kwako kuelewa mambo yote yenye ulikuwa unajifunza mu Biblia! Uliwaza kama kila mutu atakubali mafundisho yenye umetoka kuamini. Ulikuwa hakika kama ujumbe wenye kuwa mu Bibllia ungewasaidia wakuwe na maisha ya muzuri zaidi sasa, na wakuwe na tumaini ya muzuri zaidi ya wakati wenye kuja. (Zb. 119:105) Kwa hiyo, ulianza kuambia marafiki wako na watu wa familia yako kweli zenye ulikuwa umejifunza. Lakini, nini njo ilitokea? Jambo la kushangaza, watu wengi walikatala mambo yenye uliwaambia.

2-3. Watu wengi wa wakati wa Yesu walitenda namna gani kumuhusu?

2 Hatupaswe kushangaa wakati watu wanakatala ujumbe wenye tunawatolea. Wakati wa Yesu watu wengi walimukatala, hata kama alifanya miujiza yenye ilionyesha kama Mungu alikuwa anamusaidia. Kwa mufano, Yesu alimufufua Lazaro, ile ilikuwa muujiza wenye wapinzani wake hawangeweza kukatala. Hata vile, viongozi Wayahudi hawakuamini kuwa Yesu ni Masiya. Walitaka hata kuwaua wote, ni kusema, Yesu na Lazaro!​—Yoh. 11:47, 48, 53; 12:9-11.

3 Yesu alijua kama watu wengi watakatala kuamini kama yeye ni Masiya. (Yoh. 5:39-44) Yesu aliambia wanafunzi wa Yohana mubatizaji hivi: “Mwenye furaha ni mutu mwenye hapate ndani yangu sababu yoyote ya kukwazika.” (Mt. 11:2, 3, 6) Juu ya nini watu wengi walimukatala Yesu?

4. Ni mambo gani tutaona mu hii habari?

4 Mu hii habari na habari yenye kufuata tutaona sababu zenye zilifanya watu wengi wa wakati wa Yesu wasimuamini. Tutaona pia juu ya nini leo watu wengi wanakatala ujumbe wetu. Na jambo la maana zaidi, tutaona juu ya nini tunapaswa kuwa na imani yenye nguvu kumuhusu Yesu ili jambo lolote lisituzuie kumufuata.

(1) FASI KWENYE YESU ALIKOMALIA

Sababu yenye kufuata ilifanya watu wamukatale Yesu: fasi kwenye alikomalia. Namna gani zile sababu zinaweza kufanya watu fulani watukatale pia leo? (Ona fungu la 5) *

5. Pengine ni juu ya nini watu fulani waliwaza kama Yesu haiko njo Masiya mwenye walikuwa wanangojea?

5 Kujua fasi kwenye Yesu alikomalia kulifanya watu wengi wamukatale. Walijua kama Yesu alikuwa mwalimu mwenye kufundisha muzuri sana na alifanya miujiza. Lakini, walimuona tu kama mwana wa semarala mumoja maskini. Na alikomalia Nazareti, muji wenye ulionekana kuwa hauna wa maana sana. Hata Natanaeli, mwenye alifikia kuwa mwanafunzi wa Yesu, ku mwanzo alisema hivi: “Je, kuko kitu kizuri chenye kinaweza kutoka Nazareti?” (Yoh. 1:46) Pengine Natanaeli hakufurahia muji kwenye Yesu aliishi. Ao pengine alikuwa anakumbuka unabii wenye kuwa mu Mika 5:2, wenye ulitabiri kama Masiya angezaliwa Betlehemu, hapana Nazareti.

6. Nini njo ingesaidia watu wa wakati wa Yesu wajue kama yeye njo Masiya?

6 Maandiko ilisema nini? Nabii Isaya alitabiri kama maadui wa Yesu hawangekazia uangalifu “habari za kizazi [cha Masiya].” (Isa. 53:8) Habari mingi za vile zilikuwa zilishatabiriwa. Ikiwa wale watu wangekuwa na wakati wa kuchunguza habari za kweli, wangejua kama Yesu alizaliwa Betlehemu na kama alitoka mu kizazi cha Mufalme Daudi. (Lu. 2:4-7) Kwa hiyo, unabii wa Mika 5:2 ulitabiri kama Masiya angezaliwa Betlehemu, na ni kule Yesu alizaliwa. Sasa, wale watu walikuwa na tatizo gani? Walimuhukumu Yesu haraka-haraka na hawakukuwa na habari zote. Ile njo ilifanya wamukatale.

7. Juu ya nini leo watu wengi wanakatala watumishi wa Yehova?

7 Ile tatizo iko pia leo? Ndiyo. Juu watumishi wengi wa Yehova hawako matajiri na hawajulikane sana, watu wengi wanawaona kuwa watu wenye “hawana elimu na watu wa kawaida.” (Mdo. 4:13) Watu fulani wanawaza kama watumishi wa Yehova hawapaswe kufundisha Biblia juu hawayasomaka masomo ya dini yenye kujulikana sana. Wengine wanasema kama Mashahidi wa Yehova ni “dini ya watu wa Amerika.” Lakini kusema kweli, Mashahidi wa Yehova wengi hawaishi mu inchi ya Amerika. Na wengine wanasikiaka kama Mashahidi hawamuamini Yesu. Kwa miaka mingi wameita Mashahidi wa Yehova “watu wa Shetani,” “wenye kuwa na musimamo mukali,” na watu wengi wanasema kama dini yetu ni “kanisa la wazungu.” Juu wale watu wenye wanasikiliza zile habari hawajue kweli kuhusu watumishi wa Yehova, ile inafanya wawakatale.

8. Kulingana na Matendo 17:11, watu wanapaswa kufanya nini kama wanapenda kujua watumishi wa Mungu leo?

8 Ni nini inaweza kukusaidia usipoteze imani? Ni lazima kutafuta kujua habari za kweli. Ile njo jambo Luka, muandikaji wa Biblia, alijikaza kufanya. Alijikaza kutafuta kwa “uangalifu mambo yote tangu mwanzo.” Alipenda wasomaji wake ‘wajue muzuri kabisa uhakika wa mambo’ yenye walisikia kuhusu Yesu. (Lu. 1:1-4) Wayahudi wenye waliishi mu Beroya ya zamani walikuwa tu sawa Luka. Wakati walisikia habari njema kuhusu Yesu kwa mara ya kwanza, waliilinganisha na Maandiko ya Kiebrania ili kuwa hakika kama mambo yenye walifundishwa ilikuwa ya kweli. (Soma Matendo 17:11.) Leo pia, watu wanapaswa kufanya vile. Wanapaswa kulinganisha mambo yenye watumishi wa Yehova wanafundisha ili kuona kama inapatana na Maandiko. Wanapaswa pia kujifunza mambo yenye watumishi wa Yehova wa wakati wetu wamefanya. Kama wanatafuta kujua habari za kweli, hawataacha ubaguzi ao mambo ya kusikia-sikia iwadanganye.

(2) YESU ALIKATALA KUFANYA MIUJIZA ILI KUJIONYESHA

Sababu yenye kufuata ilifanya watu wamukatale Yesu: alikatala kufanya miujiza ili kujionyesha. Namna gani ile sababu zinaweza kufanya watu fulani watukatale pia leo? (Ona fungu la 9-10) *

9. Watu walitenda namna gani wakati Yesu alikatala kuwaonyesha alama kutoka mbinguni?

9 Mu wakati wa Yesu, watu fulani hawakutosheka na mafundisho yake. Walipenda nini? Walipenda Yesu awahakikishie kabisa kama yeye ni Masiya kwa kuwaonyesha “alama kutoka mbinguni.” (Mt. 16:1) Pengine walipenda Yesu afanye vile juu ya kukosa kuelewa muzuri Danieli 7:13, 14. Tena, wakati wa Yehova wa kutimiza ule unabii ulikuwa hauyafika. Mambo yenye Yesu alikuwa anafundisha ilitosha ili kuwahakikishia kama alikuwa Masiya. Lakini wakati Yesu alikatala kuwaonyesha alama yenye walikuwa wanatafuta walikatala kumufuata.​—Mt. 16:4.

10. Namna gani Yesu alitimiza unabii wenye Isaya aliandika kuhusu Masiya?

10 Maandiko ilisema nini? Nabii Isaya aliandika hivi kuhusu Masiya: “Hatalalamika wala kupandisha sauti yake, na hatafanya sauti yake isikike katika barabara.” (Isa. 42:1, 2) Yesu alitimiza utumishi wake bila kufanya wengine wamukazie uangalifu. Hakujenga mahekalu ya munene-munene, hakuvala nguo za pekee za kidini wala hakupenda watu wamuite kwa majina ya cheo ya kidini. Wakati wa majaribu, alikatala kumufurahisha Mufalme Herode kwa kumufanyia muujiza hata kama maisha yake, ni kusema, Yesu, ilikuwa mu hatari. (Lu. 23:8-11) Ijapokuwa alifanya miujiza fulani, kazi ya maana sana kwake ilikuwa kuhubiri habari njema. Njo maana aliambia wanafunzi wake hivi: “Hiyo ndiyo sababu nimekuja.”​—Mk. 1:38.

11. Leo watu wako na mawazo gani ya mubaya?

11 Ile tatizo iko pia leo? Ndiyo. Leo, watu wengi wanashangazwa na majengo ya munene-munene ya dini yenye kupambwa mu njia ya ajabu na majina ya cheo yenye kuonyesha kama viongozi wa dini ni watu wa maana sana. Na wengine wanashangazwa na sikukuu zenye zinafanywa na watu wengi na wanasahau kama zile sikukuu haziko za Kikristo. Lakini watu wenye wanaendaka ku zile dini, hawajue mambo mingi kuhusu Mungu na makusudi yake. Wale wenye wanakusanyika ku mikutano yetu ya Kikristo, wanajifunza mambo mingi juu ya Yehova na wanajifunza mambo ya kufanya ili kumupendeza. Hata kama Majumba yetu ya Ufalme haiko ya ajabu-ajabu, inasafishwa muzuri na inapambwa kwa kiasi. Wale wenye wanaongoza hawavalake nguo za pekee ao kuitwa ku majina yenye kuonyesha kama ni watu wa maana sana. Mambo yenye tunaamini na kufundisha inatoka mu Biblia. Hata vile, watu wengi leo wanakatala ujumbe wetu juu wanawaza kama namna yetu ya kumuabudu Mungu haishangaze tu sana na kama mambo tunafundisha haiko njo yenye wanapendaka kusikia.

12. Kulingana na Waebrania 11:1, 6, nini njo inaweza kutia nguvu imani yetu?

12 Ni nini inaweza kukusaidia usipoteze imani? Mutume Paulo aliambia hivi Wakristo wenye kuishi Roma: “Imani inafuata jambo lenye lilisikiwa. Na jambo lenye lilisikiwa ni kupitia neno juu ya Kristo.” (Ro. 10:17) Kwa hiyo, kujifunza Maandiko njo kutafanya imani yetu ikuwe nguvu, hapana kushiriki mu karamu zenye Biblia inaonyesha kama ni za mubaya hata kama zinaweza kuonekana kuwa zenye kufurahisha ao zenye kupendeza. Tunapaswa kuwa na imani yenye nguvu na yenye inategemea ujuzi wenye hauna makosa, juu “bila imani haiwezekane kumupendeza Mungu.” (Soma Waebrania 11:1, 6.) Kwa hiyo, hatuna lazima ya alama yenye kushangaza kutoka mbinguni yenye kuonyesha kama tumepata kweli. Kujifunza kwa uangalifu mafundisho ya Biblia yenye kutia nguvu imani yetu njo inaweza kutusaidia tujihakikishie kama tumepata kweli na ile inatusaidia kuondoa mashaka yoyote yenye tunaweza kuwa nayo.

(3) YESU HAKUFUATA DESTURI MINGI ZA WAYAHUDI

Sababu yenye kufuata ilifanya watu wamukatale Yesu: hakufuata desturi mingi za Wayahudi. Namna gani ile sababu inaweza kufanya watu fulani watukatale pia leo? (Ona fungu la (Ona fungu la 13)) *

13. Juu ya nini watu wengi walimukatala Yesu?

13 Mu wakati wa Yesu, wanafunzi wa Yohana Mubatizaji walishangaa wakati waliona kama wanafunzi wa Yesu hawakukuwa wanafunga. Yesu alifasiria kama hawakukuwa na sababu ya kufunga juu alikuwa angali muzima. (Mt. 9:14-17) Hata vile, Wafarisayo na watu wengine wenye walikuwa wanamupinga walimuhukumu Yesu juu hakukuwa anafuata desturi zao. Walikasirika sana wakati aliponyesha wagonjwa siku ya Sabato. (Mk. 3:1-6; Yoh. 9:16) Ngambo moja walikuwa wanasema kama wanaheshimiaka Sabato na ngambo ingine walikuwa wanafanya biashara mu hekalu. Walikasirika sana wakati Yesu aliwaambia waziwazi kama mambo yenye walikuwa wanafanya ilikuwa ya mubaya. (Mt. 21:12, 13, 15) Na wale wenye Yesu alihubiria mu sinagogi kule Nazareti, walikasirika sana wakati alitumia mifano fulani ya taifa la Israeli juu ya kuwasaidia waelewe kama walikuwa wachoyo na kama hawakukuwa na imani. (Lu. 4:16, 25-30) Watu wengi walimukatala juu waliona kama hakuwafanyia mambo yenye walipenda afanye.​—Mt. 11:16-19.

14. Juu ya nini Yesu alionyesha waziwazi kama ni mubaya kufuata desturi za wanadamu zenye zilipingana na Maandiko?

14 Maandiko ilisema nini? Yehova alisema hivi kupitia nabii Isaya: “Watu hawa wananikaribia kwa vinywa vyao, na wananiheshimia kwa midomo yao, lakini moyo wao uko mbali sana na mimi, na wananiogopa kwa kutegemea amri za wanadamu zenye wamefundishwa.” (Isa. 29:13) Yesu alikuwa na sheria ya kuonyesha kama ni mubaya kufuata desturi za wanadamu zenye zilipingana na Maandiko. Wale wenye waliwaza kama desturi na sheria za wanadamu njo za maana zaidi kuliko Maandiko, walikatala Yehova na Masiya mwenye alituma.

15. Juu ya nini watu wengi leo hawapendake Mashahidi wa Yehova?

15 Ile tatizo iko pia leo? Ndiyo. Watu wengi wanahuzunika sana wakati wanaona Mashahidi wa Yehova hawafanye nao pamoja karamu zenye hazipatane na Maandiko, sawa vile sikukuu za kuzaliwa na Noeli. Wengine wanakasirika sana juu Mashahidi wa Yehova hawawaunge mukono ili kufanya sikukuu za kitaifa ao juu hawafuate desturi za mazishi zenye zinapingana na Neno la Mungu. Wale wenye wanakwazika mu ile njia wanaweza kuwaza kabisa kama wako wanamuabudu Mungu mu njia yenye anapenda. Lakini kusema kweli, hawawezi kumufurahisha kama wanafuata desturi za hii dunia zenye zinapingana kabisa na mafundisho ya kweli yenye kuwa mu Biblia.​—Mk. 7:7-9.

16. Kulingana na Zaburi 119:97, 113, 163-165, tunapaswa kufanya nini na tunapaswa kukatala nini?

16 Ni nini inaweza kukusaidia usipoteze imani? Tunapaswa kupenda sana sheria za Yehova na kanuni zake. (Soma Zaburi 119:97, 113, 163-165.) Kama kweli tunamupenda Yehova, tutakatala desturi yoyote yenye inamuchukiza. Hatutaruhusu kitu fulani kifanye tuache kumupenda Yehova.

(4) YESU HAKULETA MABADILIKO MU MAMBO YA POLITIKE

Sababu yenye kufuata ilifanya watu wamukatale Yesu: hakuleta mabadiliko mu mambo ya politike. Namna gani ile sababu inaweza kufanya watu fulani watukatale pia leo? (Ona fungu la 17) *

17. Watu wengi mu wakati wa Yesu walitazamia kama Masiya angefanya nini?

17 Wakati Yesu alikuwa hapa ku dunia watu fulani walipenda kukuwe mabadiliko mu mambo ya politike. Walitazamia kama Masiya angewakomboa kutoka mu utawala wa Waroma wenye walikuwa wanawatesa. Lakini wakati walipima kumufanya Yesu kuwa mufalme alikatala. (Yoh. 6:14, 15) Makuhani na watu wengine waliogopa juu waliwaza kama Yesu angeleta mabadiliko mu mambo ya politike. Kama angefanya vile, Waroma wangekasirika sana na kukamata mamlaka yote yenye walikuwa wamepatia makuhani. Juu walihangaikia sana mambo ya politike Wayahudi wengi walimukatala Yesu.

18. Ni maunabii gani ya Biblia yenye ilizungumuzia Masiya yenye watu wengi hawakukazia uangalifu?

18 Maandiko ilisema nini? Kuko maunabii fulani yenye ilitabiri kama Masiya angefikia kuwa mupiganaji-vita mwenye ushindi. Lakini ingine ilionyesha kama alipaswa kwanza kufa kwa ajili ya zambi zetu. (Isa. 53:9, 12) Sasa juu ya nini watu wengi mu wakati wa Yesu hawakukuwa na mawazo yenye kufaa juu ya Masiya? Ni juu hawakukazia uangalifu unabii wowote wenye haukutabiri mwisho wa magumu yenye walikuwa nayo ile wakati.​—Yoh. 6:26, 27.

19. Ni mawazo gani yenye haifae yenye imefanya watu wengi wakatale ujumbe wetu?

19 Ile tatizo iko pia leo? Ndiyo. Leo watu wengi wanatukatala juu hatujiingize mu mambo ya politike. Wanawaza kama na siye tunapaswa kuchagua mutu fulani wakati wa vote. Lakini, tunajua kama kulingana na mawazo ya Yehova, kama tunachagua mwanadamu fulani akuwe kiongozi wetu, ni kusema, tunamukatala Yeye. (1 Sa. 8:4-7) Tena, wengine wanaweza kuwaza kama tunapaswa kujengea watu masomo na hopitali ili kuwasaidia sawa vile watu wengine wanafanyaka. Wanakatala kusikiliza ujumbe wetu juu hatuwasaidie kumaliza magumu ya hii dunia lakini tunakazia akili kazi yetu ya kuhubiri.

20. Kulingana na Matayo 7:21-23, nini njo inapaswa kuwa kusudi letu kubwa?

20 Ni nini inaweza kutusaidia tusipoteze imani yetu? (Soma Matayo 7:21-23.) Kusudi letu kubwa linapaswa kuwa kufanya kazi yenye Yesu alituamuru kufanya. (Mt. 28:19, 20) Tusiache hata kidogo mambo ya politike ao kujaribu kumaliza magumu ya watu itukengeushe. Tunapenda watu na tunahangaikia sana magumu yenye wako nayo, lakini tunajua kama njia ya muzuri ya kuwasaidia ni kuwafundisha kuhusu Ufalme wa Mungu na kuwasaidia wakuwe na urafiki wa karibu pamoja na Yehova.

21. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

21 Mu hii habari tumeona sababu ine zenye zilifanya watu wamukatale Yesu wakati wake, na zenye pengine zinaweza kufanya watu fulani leo wakatale wafuasi wake. Lakini ni zile sababu ine tu? Hapana. Mu habari ya kufuata tutachunguza sababu ine zingine. Tuazimie basi kumufuata Yesu na kuendelea kutia nguvu imani yetu!

WIMBO 56 Acha Kweli Ikuongoze

^ fu. 5 Hata kama Yesu njo alikuwa mwalimu mukubwa mwenye aliishi hapa ku dunia, watu wengi wa wakati wake walimukatala. Juu ya nini? Mu hii habari tutazungumuzia sababu ine zenye zilifanya watu wamukatale Yesu. Tutaona pia juu ya nini watu wengi leo wanakatala kusikiliza wafuasi wa kweli wa Yesu juu ya mambo yenye wanasema na kufanya. Na jambo la maana zaidi, tutajifunza juu ya nini tunapaswa kuwa na imani yenye nguvu juu tusiache kumufuata Yesu.

^ fu. 60 MAFASIRIO YA PICHA: Filipo anamutia moyo Natanaeli aende aonane na Yesu.

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu anahubiri habari njema.

^ fu. 64 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu anaponyesha mwanaume mwenye kuwa na mukono wenye kupooza na wale wenye wanamupinga wako wanamuangalia.

^ fu. 66 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu anaenda yeye peke ku mulima.