Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Je, watu walitumia mafunjo ili kutengeneza mashua?

Mimea ya mafunjo

WATU wengi wanajua kama zamani, ili kuandika, Wamisri walikuwa wanatumia zaidi sana karatasi zenye zilifanywa na mafunjo (papyrus). Wagiriki na Waroma pia waliandika ku mafunjo. * Lakini haiko watu wengi njo wanajua kama mafunjo ilitumiwa pia ili kutengeneza mashua (bateaux).

Aina mbili ya mashua yenye kufanywa na mafunjo yenye ilipatikana mu kaburi moja kule Misri

Zaidi ya miaka 2 500 hivi mbele, nabii Isaya aliandika kama “watu wenye kuishi katika eneo la mito ya Etiopia” walituma ‘wajumbe kupitia bahari, wenye walivuka maji katika vyombo vya mafunjo.’ Kisha, nabii Yeremia alitabiri kama wakati muji wa Babiloni ungeshambuliwa na Wamedi na Waajemi, wangeteketeza “mashua za mafunjo” za Wababiloni, ili wasikimbie.​—Isa. 18:1, 2; Yer. 51:32.

Biblia iliongozwa na roho ya Mungu, njo maana wanafunzi wa Biblia hawashangae wakati wanasikia kama watu wenye kufanya kazi ya kuvumbua vitu walifkia kuvumbua kama, mafunjo ilitumiwa zamani ili kutengeneza mashua. (2 Ti. 3:16) Ni vitu gani walivumbua? Walivumbua kama mu Misri, watu walitumia mafunjo ili kutengeneza mashua.

MASHUA YENYE KUFANYWA NA MAFUNJO ILITENGENEZWA NAMNA GANI?

Ku makaburi ya Wamisri kulikuwa michoro yenye kuonyesha namna watu walitumia mafunjo ili kutengeneza mashua. Wanaume walikata shina za mafunjo, walizifunga pamoja mu mafungo-mafungo, kisha walifinya pamoja ile mafungo-mafungo. Shina za mafunjo ziko na umbo ya pembe tatu (triangle). Wakati zile shina zinafinywa muzuri, zinatokeza fungo moja lenye liko nguvu sana. Kulingana na kitabu kimoja, mashua yenye ilifanywa na mafunjo ingeweza kufikia urefu wa metre 17 hivi, na ile ingefanya kukuwe makasia 10 ao 12 ku kila upande wa mashua. (A Companion to Ancient Egypt)

Ukuta moja kule Misri wenye kuonyesha namna mashua yenye kufanywa na mafunjo ilitengenezwa

JUU YA NINI WATENGENEZAJI WA MASHUA WALITUMIA MAFUNJO?

Mu Misri, mimea mingi ya mafunjo ilikomalia mu bonde la muto Nile. Zaidi ya ile, ilikuwa mwepesi kutengeneza mashua yenye kufanywa na mafunjo. Hata wakati watu walianza kutumia mbao ili kutengeneza mashua ya mukubwa-mukubwa, inawezekana wavuvi na wawindaji waliendelea kutumia vyelezo (radeaux) na mashua ya kidogo yenye kufanywa na mafunjo.

Kwa wakati murefu, watu waliendelea kutumia mashua yenye kufanywa na mafunjo. Plutarque, muandikaji mumoja Mugiriki, mwenye aliishi wakati wa mitume, alisema kama ile wakati watu waliendelea kutumia mashua yenye kufanywa na mafunjo.

^ fu. 3 Mimea ya mafunjo inakomalaka fasi ya tingitingi na fasi kwenye maji haishukake mbiombio. Mumea moja unaweza kuwa na urefu wa metre 5 hivi na shina yake inaweza kuwa na ukubwa wa santimetre 15 hivi.