Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 21

Yehova Atakutia Nguvu

Yehova Atakutia Nguvu

“Wakati niko muzaifu, ndio wakati ninakuwa na nguvu.”​—2 KO. 12:10.

WIMBO 73 Utusaidie Tusiogope

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Mashahidi wengi wanakutana na magumu gani?

MUTUME Paulo alimutia moyo Timoteo afanye yake yote ili kutimiza kwa ukamili utumishi wake. Ile kitia-moyo inahusu pia Wakristo wote. (2 Ti. 4:5) Njo maana tunakamata ile shauri ya Paulo kwa uzito. Lakini, wakati fulani haiko mwepesi kufanya vile juu wengi kati ya ndugu na dada zetu wako na woga wa kuhubiri. (2 Ti. 4:2) Kwa mufano, fikiria ndugu na dada zetu wenye wanaishi mu inchi zenye kazi yetu inatiliwa vizuizi ao inakatazwa. Wanahubiri hata kama wanajua pengine wanaweza kufungwa!

2 Watumishi wa Yehova wanakutana na magumu mingi yenye inaweza kuwavunja moyo. Kwa mufano, wengi wanapaswa kutumika sana ili kutimizia familia zao mahitaji ya musingi. Wangependa kuhubiri zaidi lakini wakati wanafika ku mwisho wa juma hawana nguvu mingi. Wengine wanaweza kufanya tu mambo kidogo mu kazi ya Yehova juu wako wagonjwa sana ao walishazeeka, ao tena juu hawawezi kutoka ku nyumba yao. Na wengine wanaendelea kujiona kuwa wa bure ku macho ya Yehova. Mary, * anasema hivi: “Najikazaka sana kuachana na mawazo ya mubaya; kufanya vile kunanichokeshaka sana. Kisha naanza kujilaumu juu sina tena wakati na nguvu ya kuhubiri.”

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Hata kama tuko na magumu gani, Yehova anaweza kutupatia nguvu yenye tuko nayo lazima ili tuendelee kumutumikia kulingana na uwezo wetu. Mbele tuzungumuzie namna Yehova anaweza kutusaidia, tuzungumuzie kwanza namna alitia Paulo na Timoteo nguvu ya kutimiza utumishi wao hata kama walikuwa na magumu.

YEHOVA ANATUPATIA NGUVU YA KUTIMIZA KAZI YETU YA KUHUBIRI

4. Paulo alipata magumu gani?

4 Paulo alipata magumu mingi. Alikuwa na lazima ya musaada wa Yehova zaidi sana wakati maadui wake walimupiga, wakati walimutia mu gereza na hata wakati walitaka kumuua. (2 Ko. 11:23-25) Paulo hakusikia haya kusema kama wakati fulani alipaswa kujikaza sana ili kupiganisha hali yake ya kuvunjika moyo. (Ro. 7:18, 19, 24) Tena, Paulo alipaswa kuvumilia matatizo ya afya yenye ilikuwa sawa vile “mwiba katika mwili,” na alipenda sana Mungu aiondoe.​—2 Ko. 12:7, 8.

Ni nini ilisaidia Paulo atimize muzuri utumishi wake? (Ona fungu la 5-6) *

5. Paulo alitimiza mambo gani hata kama alipata magumu?

5 Yehova alimutia nguvu Paulo ili aendelee na utumishi wake hata kama alikuwa na magumu mingi. Fikiria mambo yote yenye Paulo alitimiza. Kwa mufano, wakati alifungwa mu nyumba fulani kule Roma alitetea kwa bidii habari njema mbele ya viongozi Wayahudi na pengine mbele ya wakubwa wa serikali. (Mdo. 28:17; Flp. 4:21, 22) Tena, alihubiria walinzi wengi wa Mufalme na alitolea ushahidi watu wote wenye walimutembelea. (Mdo. 28:30, 31; Flp. 1:13) Mu ileile wakati, Paulo aliandika mabarua yenye kuongozwa na roho ya Mungu, yenye ilisaidia Wakristo wa kweli zamani na yenye iko inasaidia hata leo. Na zaidi ya ile, mufano wa Paulo ulitia nguvu kutaniko la Roma na ile ilifanya ndugu zake wakuwe na “uhodari mwingi wa kusema neno la Mungu bila woga.” (Flp. 1:14) Hata kama wakati fulani Paulo hakuweza kufanya mambo mingi vile angependa, alifanya yote yenye aliweza na ile ‘kwa kweli ilisaidia kuendeleza habari njema.’​—Flp. 1:12.

6. Kulingana 2 Wakorinto 12:9, 10, ni nini ilimusaidia Paulo atimize utumishi wake?

6 Paulo alijua kama mambo yote yenye alifanya mu utumishi wa Yehova haikukuwa kwa uwezo wake, lakini ilikuwa kwa nguvu ya Mungu. Alisema kama nguvu za Mungu “zinakamilishwa katika uzaifu.” (Soma 2 Wakorinto 12:9, 10.) Hata kama Paulo alipata mateso mingi sawa vile kufungwa, Yehova alitumia roho yake takatifu ili kumupatia nguvu ya kutimiza kwa ukamili utumishi wake.

Ni nini ilisaidia Timoteo atimize muzuri utumishi wake? (Ona fungu la 7) *

7. Ni magumu gani Timoteo alipaswa kupiganisha ili atimize muzuri utumishi wake?

7 Timoteo, mufanyakazi mwenzake na Paulo, alipaswa pia kutegemea nguvu za Mungu ili kutimiza muzuri utumishi wake. Timoteo alimusindikiza Paulo wakati alifanya safari za murefu za umisionere. Tena, Paulo alimutuma Timoteo aende mu safari zingine ili kutembelea makutaniko na kuitia moyo. (1 Ko. 4:17) Inawezekana Timoteo aliona kama hataweza kufanya vile. Pengine ile njo ilifanya Paulo amuambie: “Usiruhusu hata kidogo mutu yeyote azarau ujana wako.” (1 Ti. 4:12) Na mu ileile wakati, Timoteo alikuwa na mwiba wake katika mwili, ni kusema, “ugonjwa wa mara kwa mara.” (1 Ti. 5:23) Lakini Timoteo alijua kama roho takatifu ya Yehova ingemupatia nguvu yenye alikuwa nayo lazima ili ahubiri habari njema na atumikie ndugu zake.​—2 Ti. 1:7.

YEHOVA ANATUPATIA NGUVU YA KUBAKIA WAAMINIFU HATA KAMA TUKO NA MAGUMU

8. Namna gani Yehova anatia nguvu watumishi wake leo?

8 Leo, Yehova anapatia watumishi wake “nguvu zenye kupita zile za kawaida” ili waendelee kumutumikia kwa uaminifu. (2 Ko. 4:7) Tuzungumuzie basi njia ine zenye Yehova anatumia leo ili kututia nguvu na kutusaidia tuendelee kubakia waaminifu kwake: sala, Biblia, ndugu na dada, na kazi yetu ya kuhubiri.

Yehova anatutia nguvu kupitia sala (Ona fungu la 9)

9. Sala inaweza kutusaidia namna gani?

9 Sala. Mu Waefeso 6:18, Paulo anatutia moyo tusali kwa Mungu “kila wakati.” Mungu atajibia sala zetu kwa kututia nguvu. Jonnie, mwenye kuishi Bolivie, alijionea namna Yehova alimusaidia wakati alipata magumu mingi. Bibi yake na wazazi wake wote wawili waligonjwa sana mu wakati moja. Ilikuwa nguvu kwa Jonnie kuhangaikia wote watatu. Mama yake alikufa, na iliomba wakati murefu ili bibi yake na baba yake wapone. Saa anakumbuka mambo yenye ilimupata, Jonnie anasema hivi: “Wakati nilikuwa na mahangaiko sana, jambo lenye lilinisaidia ni kusali kwa Yehova na kumufasiria namna nilikuwa najisikia.” Yehova alimupatia Jonnie nguvu yenye alikuwa nayo lazima ili kuvumilia. Ronald, muzee mumoja mwenye kuishi Bolivie, alifikia kujua kama mama yake iko na kansere. Kisha mwezi moja mama yake akakufa. Ni nini ilimusaidia Ronald mu ile kipindi ya nguvu? Anasema hivi: “Kusali kwa Yehova na kumuambia vile nilikuwa najisikia kumenisaidia sana. Najua kama Yehova ananielewa muzuri zaidi kuliko mutu yeyote, na ananielewa muzuri zaidi hata kuliko miye peke.” Wakati fulani tunaweza kujisikia sawa vile hatutaweza kuvumilia magumu yetu na pengine tunaweza kushindwa kujua mambo ya kusema mu sala yetu. Lakini Yehova anatuomba tusali kwake hata kama tunaweza kuona kama ni nguvu kumufasiria namna tunajisikia.​—Ro. 8:26, 27.

Yehova anatutia nguvu kupitia Biblia (Ona fungu la 10)

10. Kulingana na Waebrania 4:12, juu ya nini ni jambo la maana sana kusoma na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma mu Biblia?

10 Biblia. Paulo alisoma Maandiko ili imutie nguvu na imufariji, siye pia tunapaswa kufanya vile. (Ro. 15:4) Vile tuko nasoma na kufikiri sana juu ya Neno la Mungu, Yehova anaweza kutupatia roho yake takatifu ili tuelewe muzuri zaidi namna tunaweza kutumikisha mashauri ya Biblia mu hali yetu. (Soma Waebrania 4:12.) Ronald, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Niko mwenye furaha sana kuona vile ninajikaza kusoma kila usiku sehemu fulani ya Biblia. Ninafikiriaka sana sifa za Yehova na namna anahangaikiaka watumishi wake kwa upendo. Kufanya vile kunanisaidiaka nipate tena nguvu.”

11. Namna gani Biblia ilitia nguvu dada mumoja mwenye alikuwa na huzuni sana?

11 Wakati tunafikiri sana juu ya Neno la Mungu ile inatusaidia tukuwe na mawazo ya muzuri juu ya magumu yetu. Fikiria namna Biblia ilimusaidia mujane mumoja mwenye alikuwa na huzuni sana. Muzee mumoja alimutia moyo asome kitabu ya Yobu, na mule atapata mambo mingi yenye itamusaidia. Wakati ule mujane alianza kufanya vile, kwanza, alianza tu kumulaumu Yobu juu ya mawazo yake ya mubaya. Alikuwa anafikiri hivi: “Yobu! Hapana kuwaza tu juu ya magumu yako!” Kisha akatambua kama na yeye alikuwa anawaza tu sawa Yobu. Ile ilimusaidia abadilishe mawazo yake na ilimutia nguvu ili aendelee kuvumilia huzuni yenye alikuwa nayo kisha kupoteza bwana yake.

Yehova anatutia nguvu kupitia ndugu na dada (Ona fungu la 12)

12. Namna gani Yehova anatutia nguvu kupitia ndugu na dada zetu?

12 Ndugu na dada. Yehova anatumia pia ndugu na dada wenzetu ili kututia nguvu. Mu barua yenye aliandikia Wakristo wa Roma, Paulo alionyesha kama alipenda sana yeye na ndugu na dada zake ‘watiane moyo.’ (Ro. 1:11, 12) Mary, mwenye tulishataja, anapendaka sana kuwa pamoja na ndugu na dada zake. Anasema hivi: “Yehova alitumia ndugu na dada zangu wenye hawakujua hata magumu yangu. Walinitia moyo ao waliniandikia ujumbe fulani, na ile njo nilikuwa nayo lazima. Nilipata nafasi ya kuongea na dada wenye walikuwa na magumu sawa yangu, na kujua mambo yenye walifanya ili kupambana na ile magumu ilinisaidia sana. Na kila mara wazee wanafanya nijisikie kuwa wa maana mu kutaniko.”

13. Namna gani tunaweza kutiana nguvu ku mikutano yetu?

13 Mikutano ni moja kati ya fasi za muzuri sana kwenye tunaweza kutiana moyo. Wakati tunaenda ku mikutano ni muzuri kuambia wengine kama tunawapenda na kuwashukuru juu ya mambo yenye wamefanya. Kwa mufano, siku moja mbele mukutano uanze, Peter muzee mumoja, aliambiaka hivi dada mumoja mwenye bwana yake haiko Shahidi: “Kukuona tu hapa kunatutiaka moyo sana. Kila mara unakuyaka na watoto wako wa sita na wako tayari kutoa maelezo.” Wakati tu ule dada alisikia ile maneno, machozi ilimuyala mu macho na alisema hivi: “Hauwezi kujua ni kwa kiasi gani nilikuwa na lazima ya kusikia maneno ya vile leo.”

Yehova anatutia nguvu kupitia mahubiri (Ona fungu la 14)

14. Namna gani kazi ya kuhubiri inatusaidiaka?

14 Mahubiri. Wakati tunahubiria wengine tunajisikia muzuri, ikuwe waitike ao wakatale. (Mez. 11:25) Dada Stacy alijionea yeye mwenyewe namna gani mahubiri inatiaka nguvu. Alihuzunika sana wakati mutu moja mu familia yao alitengwa na kutaniko. Alikuwa anajiuliza hivi: ‘Kuko kitu ingine nilipaswa kufanya juu nimusaidie?’ Ile hali ilikuwa inamuhangaisha sana. Ni nini ilimusaidia apambane na ile jaribu? Mahubiri! Kuhubiri kulimusaidia akaze akili yake juu ya watu wenye walikuwa na lazima ya musaada. Anasema hivi: “Mu ile wakati, Yehova alinisaidia nipate mwanafunzi wa Biblia mwenye alifanya maendeleo ya haraka. Ile ilinitia moyo sana. Kama kuko kitu ilinisaidia sana nitulie ni mahubiri.”

15. Mambo yenye Mary alisema inakufundisha nini?

15 Juu ya hali fulani, ndugu na dada fulani wanajisikia kama hawana na uwezo wa kufanya mingi mu kazi ya kuhubiri. Kama na weye unajisikia vile, kumbuka kama Yehova anafurahia yenye uko unafanya kulingana na uwezo wako. Tufikirie tena mufano wa Mary. Wakati alihamia fasi kwenye watu wanazungumuza luga ingine, alijiona kuwa wa bure kabisa. Anasema hivi: “Kwa wakati fulani kile nilikuwa naweza tu kufanya ni kuleta ka jibu ka fupi, kusoma andiko moja ya Biblia, ao kuangusha trakte.” Wakati alijilinganisha na wale wenye walikuwa wanasema muzuri sana ile luga, alijiona kuwa wa bure sana. Lakini, alifikia kubadilisha namna yake ya kuwaza. Alifikia kuanza kuelewa kama Yehova angemutumia hata kama hakukuwa anajua kusema muzuri ile luga. Anasema tena hivi: “Kweli zenye kuwa mu Biblia ziko mwepesi sana, na ni zile kweli njo zinabadilishaka maisha ya watu.”

16. Ni nini inaweza kutia nguvu ndugu na dada wenye hawana uwezo wa kutoka kwao?

16 Yehova anaona na anafurahia sana tamaa yenye tuko nayo ya kuhubiri habari njema hata kama hatuna uwezo wa kutoka ku nyumba. Anaweza kutupatia nafasi mbalimbali ili kuhubiria wale wenye wako wanatuchunga ao hata wanganga. Lakini kama tunalinganisha mambo yenye tulikuwa na uwezo wa kufanya zamani na yenye tuko tunafanya sasa, tutavunjika moyo bure. Hata vile, tukitambua kama Yehova iko anatusaidia sasa, ile itatupatia nguvu ya kuvumilia magumu kwa furaha.

17. Kulingana na Muhubiri 11:6, juu ya nini tunapaswa kuendelea kuhubiri hata kama hatuone matokeo ya muzuri palepale?

17 Hatujue ni mbegu gani ya kweli yenye tunapanda yenye itatia mizizi na kuanza kukomala. (Soma Muhubiri 11:6.) Kwa mufano, Barbara, dada mwenye iko na miaka 80 hivi, anazoeaka kuhubiri kupitia telefone na barua. Mu barua moja, alitiaka Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 3, 2014, wenye ulikuwa na habari yenye kichwa “Mambo Yenye Mungu Amekufanyia.” Bila kujua, alitumia ile barua bibi na bwana wenye hawakukuwa tena Mashahidi wa Yehova. Waliisoma ile gazeti mara mingi. Bwana alijisikia sawa vile Yehova alikuwa anaongea naye. Walianza tena kuhuzuria mikutano na ku mwisho wakarudishwa, kisha zaidi ya miaka 27. Dada Barbara alitiwa moyo sana kuona matokeo ya muzuri yenye alipata juu tu ya barua moja yenye alitumaka!

Yehova anatutia nguvu kupitia (1) sala, (2) Biblia, (3) ndugu na dada, na (4) mahubiri (Ona fungu la 9-10, 12, 14)

18. Tunaweza kufanya nini ili Yehova atutie nguvu?

18 Yehova anatutia nguvu kupitia njia mbalimbali. Wakati tunatumia zile njia, kama vile sala, Biblia, ndugu na dada, na mahubiri, tunaonyesha kama tunamutegemea ili atusaidie. Kwa hiyo, tuendelee kila siku kumutegemea Baba yetu wa mbinguni, mwenye “anapenda kuonyesha nguvu zake kwa ajili ya wale wenye moyo wao ni kamili kumuelekea yeye.”​—2 Ny. 16:9.

WIMBO 61 Tuende Mbele

^ fu. 5 Leo, tuko tunaishi mu kipindi ya nguvu sana, lakini Yehova anatusaidia kuvumilia. Mu hii habari, tutajifunza namna Yehova alisaidia mutume Paulo na Timoteo waendelee kumutumikia hata kama walikuwa na magumu. Tutazungumuzia pia njia ine zenye Yehova anatumia leo ili kutusaidia tuvumilie.

^ fu. 2 Jina limebadilishwa.

^ fu. 53 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati iko mu kifungo kule Roma, Paulo anaandikia barua makutaniko fulani na iko pia anahubiria wale wenye wanakuja kumutembelea.

^ fu. 55 MAFASIRIO YA PICHA: Timoteo anatia moyo ndugu wa makutaniko yenye anatembelea.