Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 18

‘Kimbia Mbio Mupaka Mwisho’

‘Kimbia Mbio Mupaka Mwisho’

“Nimekimbia mbio mupaka mwisho.”​—2 TI. 4:7.

WIMBO 129 Tutaendelea Kuvumilia

KIFUPI CHA HABARI *

1. Sisi wote tunapaswa kufanya nini?

UNAWEZA kupenda ukimbie katika mbio yenye unajua kama iko nguvu, zaidi sana kama uko mugonjwa ao unachoka? Inawezekana hapana. Lakini, mutume Paulo alisema kama Wakristo wote wa kweli wako katika mbio. (Ebr. 12:1) Na sisi wote, vijana ao wazee, wenye nguvu ao wenye kuchoka, tunapaswa kuvumilia mupaka mwisho ikiwa tunapenda kupata zawadi yenye Yehova atatupatia.​—Mt. 24:13.

2. Kulingana na 2 Timoteo 4:7, 8, juu ya nini Paulo aliweza kutoa shauri hilo?

2 Paulo aliweza kutoa shauri hili kwa sababu alikuwa amekimbia mbio muzuri mupaka mwisho. (Soma 2 Timoteo 4:7, 8.) Lakini, mbio yenye Paulo alizungumuzia ni nini kabisa?

MBIO NI NINI?

3. Mbio yenye mutume Paulo alizungumuzia ni nini?

3 Wakati fulani, mutume Paulo alitumia mambo fulani yenye kuhusu michezo yenye ilikuwa inafanyika katika Ugiriki ya zamani ili kufundisha mambo fulani ya maana. (1 Ko. 9:25-27; 2 Ti. 2:5) Mara mingi, alilinganisha maisha ya Mukristo na kukimbia katika mbio. (1 Ko. 9:24; Gal. 2:2; Flp. 2:16) Mutu anaanza ile “mbio” wakati anajitoa kwa Yehova na kubatizwa. (1 Pe. 3:21) Anavuka mustari wa mwisho wakati Yehova anamupatia uzima wa milele.​—Mt. 25:31-34, 46; 2 Ti. 4:8.

4. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

4 Kuko mambo gani yenye kufanana kati ya mbio ya miguu ya mwendo murefu na maisha ya Mukristo? Kuko mambo mingi yenye kufanana. Tuzungumuzie mambo tatu kati ya ile mambo. Jambo la kwanza, tunapaswa kufuata njia yenye kufaa; jambo la pili, tunapaswa kukaza akili juu ya mustari wa mwisho; na jambo la tatu, tunapaswa kuendelea kukimbia hata wakati tuko na magumu.

FUATA NJIA YENYE KUFAA

Sisi wote tunapaswa kufuata njia ya maisha ya Kikristo (Ona fungu la 5-7) *

5. Tunapaswa kufuata njia gani, na juu ya nini?

5 Ili wastahili kupata ushindi katika mbio ya kwelikweli, wakimbiaji wanapaswa kufuata njia yenye wale wenye walipanga ile mashindano walitayarisha. Vilevile, kama tunapenda kupata zawadi ya uzima wa milele, tunapaswa kufuata njia ya Kikristo, ao namna Mukristo anapaswa kuishi. (Mdo. 20:24; 1 Pe. 2:21) Lakini, Shetani na wale wenye kufuata mufano wake hawapendi tufuate njia ya Kikristo; wanapenda ‘tuendelee kukimbia pamoja nao.’ (1 Pe. 4:4) Wanachekelea namna yetu ya kuishi na wanasema kama namna yao ya kuishi njo ya muzuri zaidi, njo yenye inaongoza kwenye uhuru. Lakini wanasema uongo.​—2 Pe. 2:19.

6. Mufano wa Brian unakufundisha nini?

6 Mutu yeyote mwenye anakimbia pamoja na wale wenye kuchochewa na ulimwengu wa Shetani hakawie kutambua kama njia yenye wamechagua haiwaongoze kwenye uhuru, lakini inawaongoza kwenye utumwa. (Ro. 6:16) Fikiria mufano wa Brian. Wazazi wake walimutia moyo afuate njia ya maisha ya Kikristo. Lakini, wakati alikuwa na miaka kati ya 13 na 19, alishakia kama ile njia ingemufanya akuwe na furaha. Brian aliamua kukimbia pamoja na wale wenye kuishi kulingana na kanuni za Shetani. Anasema hivi: “Muda mufupi baadaye, nilitambua kwamba ule wenye niliwazia kuwa uhuru ungeniongoza katika mazoea yenye kuharibu. Na kisha hapo, nikaanza kutumia sana dawa za kulewesha, kunywa pombe sana, na kuishi maisha mabaya sana. Kwa muda wa miaka mingi iliyofuata, hatua kwa hatua nilianza kutumia dawa za kulewesha zenye nguvu zaidi na nikakuwa mutumwa wa nyingi kati ya dawa hizo. . . . Nilianza kuziuzisha ili kuendeleza maisha yangu mabaya.” Kisha, Brian aliamua kuishi kulingana na kanuni za Yehova. Alibadilisha maisha yake na akabatizwa katika mwaka wa 2001. Iko na furaha ya kweli sasa kwa sababu anafuata njia ya maisha ya Kikristo. *

7. Kulingana na Matayo 7:13, 14, ni barabara gani mbili zenye ziko mbele yetu?

7 Ni jambo la maana sana kuchagua njia ya muzuri yenye tunaweza kufuata! Shetani anapenda sisi wote tuache kukimbia katika barabara nyembamba yenye “kuongoza kwenye uzima” na tuingie katika barabara kubwa yenye watu mingi wanatumia. Ni watu mingi njo wanasafiri katika barabara hiyo na ni mwepesi kusafiri ndani yake. Lakini ni “yenye kuongoza kwenye uharibifu.” (Soma Matayo 7:13, 14.) Ili tubakie katika barabara ya uzima na tusikengeushwe, tunapaswa kumutegemea Yehova na kumusikiliza.

ENDELEA KUKAZA MACHO MBELE WAKATI UKO UNAKIMBIA

Tunapaswa kukaza macho mbele na kuepuka kukwaza wengine (Ona fungu la 8-12) *

8. Ikiwa mukimbiaji anajikwaa, anaweza kufanya nini?

8 Wakimbiaji katika mbio ya mwendo murefu wanakaza macho juu ya barabara yenye kuwa mbele yao ili wasijikwae. Lakini, inawezekana wajigonge juu ya mukimbiaji mwenzao bila kutazamia ao kuangukia katika shimo. Ikiwa wanaanguka chini, wanasimama na kuendelea kukimbia. Zaidi sana wanakaza akili yao juu ya mustari wa mwisho na zawadi yenye wanatazamia kupata, hapana juu ya mambo yenye iliwafanya wajikwae.

9. Ikiwa tunajikwaa, tunapaswa kufanya nini?

9 Katika mbio yetu, tunaweza kujikwaa mara mingi katika maneno na matendo yetu. Wakimbiaji wenzetu wanaweza kufanya makosa yenye inatuumiza. Ile haipaswe kutushangaza. Sisi wote hatukamilike, na sisi wote tunakimbia katika barabara ileile nyembamba yenye inaongoza kwenye uzima. Kwa hiyo, “tutagongana” wakati fulani. Paulo alijua kama wakati fulani tunaweza kuwa na “sababu ya kulalamika” juu ya wengine. (Kol. 3:13) Lakini kuliko kukaza akili juu ya mambo yenye ilifanya tujikwae, ni muzuri tukaze akili juu ya zawadi yenye iko mbele yetu. Ikiwa tunajikwaa, tusimame tena na tuendelee kukimbia. Ikiwa tunakasirikia wengine na kuwawekea kinyongo na kuacha kumutumikia Yehova, hatutavuka mustari wa mwisho na kupata zawadi yetu. Kwa kuongezea, tunaweza kuwa kizuizi kwa wengine wenye wako wanajikaza kukimbia katika barabara nyembamba yenye inaongoza kwenye uzima.

10. Namna gani tunaweza kuepuka kuwa “kikwazo” kwa wengine?

10 Njia ingine ya kuepuka kuwa “kikwazo” kwa ndugu na dada zetu ni kuwaacha wafanye mambo namna wanapenda wakati inawezekana kuliko kupenda sikuzote wafanye mambo namna sisi tunapenda. (Ro. 14:13, 19-21; 1 Ko. 8:9, 13) Tuko tofauti na wakimbiaji katika mbio ya kwelikweli katika njia hii ya maana: Wakimbiaji wanatafuta kushindana, na kila mukimbiaji anajikaza ili yeye tu njo apate zawadi. Wale wakimbiaji wanafikiria kwanza faida zao wenyewe. Njo maana wanajaribu kusukuma wakimbiaji wengine ili wao wakuwe mbele. Lakini sisi, hatuko katika mashindano kati yetu. (Gal. 5:26; 6:4) Muradi wetu ni kusaidia watu wengi kadiri inawezekana wavuke mustari wa mwisho pamoja na sisi ili tupate zawadi ya uzima. Kwa hiyo, tunajikaza kutumikisha shauri la Paulo lenye liliongozwa na roho ya Mungu la “kuangalia, hapana faida zetu [sisi] wenyewe tu, lakini pia faida za wengine.”​—Flp. 2:4.

11. Mukimbiaji anakaza akili juu ya jambo gani, na juu ya nini?

11 Zaidi ya kuangalia barabara yenye iko mbele yao, wakimbiaji katika mbio ya kwelikweli wanakaza akili yao juu ya mustari wa mwisho. Hata kama hawawezi kuona mustari wa mwisho na macho yao, wanaweza kujiwazia wako wanavuka mustari huo na kupata zawadi. Kuendelea kufikiria zawadi yenye watapata kunawasaidia waendelee kukimbia kwa bidii.

12. Kwa sababu Yehova anapenda watu wake, amewahakikishia nini?

12 Kwa sababu Yehova anapenda watu wake, amewahakikishia kama, katika mbio yenye wako wanakimbia, watapata zawadi, ni kusema, uzima wa milele mbinguni ao mu dunia paradiso. Biblia inafasiria zawadi hiyo, ili tuweze kuwazia namna maisha yetu itakuwa muzuri sana wakati wenye kuja. Wakati tunaendelea kuwaza sana juu ya wakati wenye kuja wenye Yehova ametuahidi, tutaazimia zaidi kuendelea kuvumilia.

UENDELEE KUKIMBIA HATA KAMA KUKO MATATIZO

Tunapenda kuendelea kukimbia katika mbio ya uzima hata kama tunapambana na matatizo (Ona fungu la 13-20) *

13. Tuko na nini yenye wakimbiaji wa kwelikweli hawana?

13 Wakimbiaji katika michezo ya Wagiriki walipaswa kupambana na matatizo kama vile muchoko na maumivu. Lakini kile walipaswa kutegemea ni nguvu yao na mazoezi yenye walipata. Kama vile wale wakimbiaji, sisi pia tunapata mazoezi juu ya namna tunaweza kukimbia katika mbio yetu. Lakini tuko na jambo fulani lenye wakimbiaji wa kwelikweli hawana. Tunaweza kupata nguvu kutoka kwa Yehova na nguvu yake haina mipaka. Ikiwa tunamutegemea Yehova, anatuahidi kama atatuzoeza na pia atatutia nguvu!​—1 Pe. 5:10.

14. Namna gani 2 Wakorinto 12:9, 10 inatusaidia kupambana na magumu?

14 Paulo alipaswa kupambana na magumu mingi. Watu walimutukana na kumutesa. Na zaidi ya ile, wakati fulani alijisikia kuwa muzaifu na alipaswa kupiganisha tatizo fulani lenye aliita “mwiba katika mwili.” (2 Ko. 12:7) Lakini kuliko kuona ile magumu yote kuwa sababu ya kuacha kumutumikia Yehova, aliiona kuwa nafasi ya kumutegemea Yehova. (Soma 2 Wakorinto 12:9, 10.) Kwa sababu Paulo alikuwa na ile mawazo, Yehova alimusaidia kuvumilia magumu yake yote.

15. Kama tunamuiga Paulo, tutajionea nini?

15 Sisi pia tunaweza kutukanwa na kuteswa kwa sababu ya imani yetu. Tunaweza pia kupambana na matatizo ya afya ao kuchoka sana. Lakini, kama tunamuiga Paulo, ile magumu inaweza kututolea nafasi ya kujionea namna Yehova anatutegemeza kwa upendo.

16. Hata kama hauna afya ya muzuri, unaweza kufanya nini?

16 Je, hauwezi kutoka mu kitanda ao unatembeaka na kinga ya vilema? Uko na magoti yenye kuregea ao hauonake tena muzuri? Kama ni vile, je, unaweza kukimbia pamoja na wale wenye kuwa vijana na wenye kuwa na afya ya muzuri? Unaweza kabisa! Watu wengi wenye kuzeeka na wazaifu wako wanakimbia katika barabara ya uzima. Hawawezi kufanya vile kwa nguvu yao wenyewe. Lakini, wanapata nguvu kutoka kwa Yehova kwa kufuata mikutano ya Kikristo ku telefone ao kuangalia video za mikutano zenye kupatikana ku jw streaming. Wanaendelea kufanya kazi ya kufanya wanafunzi kwa kutolea ushahidi wanganga, na watu wa jamaa zao.

17. Yehova anaona namna gani wale wenye wako na matatizo ya afya?

17 Kama hauna uwezo wa kufanya mambo yote yenye ungependa kufanya katika kazi ya Yehova, usivunjike moyo na kuwaza kama hauwezi kuendelea kuvumilia mupaka mwisho. Yehova anakupenda kwa sababu ya imani yako na uvumilivu wako. Uko na lazima ya musaada wake sasa kuliko wakati mwingine wowote, na Yehova hatakuacha. (Zb. 9:10) Lakini, atakukaribia hata zaidi. Dada mumoja mwenye anapambana na matatizo fulani ya afya, alisema hivi: “Wakati matatizo yangu ya afya inaongezeka, sipate nafasi mingi za kuzungumuza na wengine juu ya kweli. Lakini, ninajua kama mambo kidogo yenye ninafanya inafurahisha moyo wa Yehova, na hilo linanifurahisha.” Wakati unavunjika moyo, kumbuka kama hauko peke yako. Fikiria mufano wenye Paulo alituachia, na ukumbuke maneno yake yenye kutia moyo. Alisema hivi: “Ninapendezwa na uzaifu, . . . kwa maana wakati niko muzaifu, ndio wakati ninakuwa na nguvu.”​—2 Ko. 12:10.

18. Ni magumu gani ya nguvu zaidi yenye watumishi fulani wa Yehova wanapambana nayo?

18 Wamoja kati ya wale wenye kukimbia katika barabara ya uzima wako na magumu ingine. Wanapambana na matatizo ya kipekee yenye wengine hawawezi kuona ao kuelewa. Kwa mufano, wanapambana na hali ya kushuka moyo ao mahangaiko mingi. Juu ya nini hali ya watumishi hao wa Yehova wenye anapenda iko ya nguvu zaidi? Juu kama mutu iko na mukono wenye kuvunjika ao anatembeaka na kinga ya vilema, kila mutu anaweza kuona magumu yake na anaweza kuchochewa kumusaidia. Lakini, wale wenye kuwa na tatizo fulani la akili ao la kihisia pengine hawaonekane kwa inje kama wako wanateseka. Huzuni yao iko kama vile tu huzuni ya mutu mwenye kuwa na mukono ao muguu wenye kuvunjika. Lakini, kwa sababu watu hawawezi kuona kama wako wanateseka, wanaweza kukosa kuwahangaikia na kuwaonyesha upendo wenye wako nao lazima.

19. Mufano wa Mefibosheti unatufundisha nini?

19 Kama uko na matatizo ya afya na unajisikia kama wengine wanakuelewa mubaya, mufano wa Mefibosheti unaweza kukutia nguvu. (2 Sa. 4:4) Alikuwa anapambana na afya ya mubaya, na Mufalme Daudi alimuwazia mubaya. Haiko Mefibosheti njo mwenye alijileteaka ile magumu. Lakini, hakuruhusu ile magumu imufanye akuwe na kinyongo; alifurahia mambo ya muzuri yenye alikuwa nayo katika maisha yake. Alikuwa mwenye shukrani juu ya wema wenye Daudi alikuwa amemuonyesha zamani. (2 Sa. 9:6-10) Wakati Daudi alimuelewa mubaya, Mefibosheti alifikiria mambo yote yenye ilihusu ile hali. Hakuacha makosa ya Daudi imufanye akuwe na kinyongo. Na hakumulaumu Yehova juu ya mambo yenye Daudi alifanya. Mefibosheti alikaza akili yake juu ya mambo yenye angeweza kufanya ili kumutegemeza mufalme mwenye Yehova alikuwa ameweka. (2 Sa. 16:1-4; 19:24-30) Yehova aliandikisha mufano muzuri sana wa Mefibosheti katika Neno lake ili utufundishe mambo fulani.​—Ro. 15:4.

20. Mahangaiko inaweza kuletea ndugu na dada fulani matatizo gani, lakini wanaweza kuwa hakika na jambo gani?

20 Kwa sababu ya mahangaiko mingi, ndugu na dada fulani wanajisikia kuwa na wasiwasi na wenye haya katika hali za kawaida kwenye wako pamoja na watu wengine. Wanaweza kuona kama ni nguvu kuwa kati ya watu wengi, lakini wanaendelea kuhuzuria mikutano, na mikusanyiko. Wanaona kuwa ni nguvu kuongea na watu wenye hawajue, lakini wanazungumuza na watu katika kazi ya kuhubiri. Kama uko mu ile hali, ukuwe hakika kama hauko peke yako. Watu mingi wanajisikia vile pia. Ukumbuke kama Yehova anapendezwa na yote unamufanyia kwa nafsi yako yote. Kwa sababu haujaacha kumutumikia, hilo linaonyesha kama anaendelea kukubariki na kukupatia nguvu yenye uko nayo lazima. * (Flp. 4:6, 7; 1 Pe. 5:7) Kama uko unamutumikia Yehova hata kama unavumilia matatizo ya kimwili ao ya kihisia, ukuwe hakika kama unamufurahisha Yehova.

21. Kwa musaada wa Yehova, sisi wote tutaweza kufanya nini?

21 Jambo la kupendeza ni kwamba, kuko tofauti kati ya mbio ya kwelikweli na ile yenye Paulo alizungumuzia. Katika mbio ya miguu ya kwelikweli ya wakati wa zamani, ni mutu mumoja tu njo mwenye alikuwa anapata zawadi. Lakini, kila mutu mwenye anavumilia kwa uaminifu katika mbio ya Kikristo ya uzima atapata zawadi ya uzima wa milele. (Yoh. 3:16) Na katika mbio ya kwelikweli, wakimbiaji wote walipaswa kuwa na afya ya muzuri; kama haiko vile hawangeweza kupata ushindi katika mbio yao. Lakini, wengi kati yetu wako na matatizo ya afya, hata hivyo wanaendelea kuvumilia. (2 Ko. 4:16) Kwa musaada wa Yehova, sisi wote tutakimbia mbio mupaka mwisho!

WIMBO 144 Kaza Macho Kwenye Zawadi!

^ fu. 5 Leo, watumishi wengi wa Yehova wanapambana na matatizo yenye kuletwa na uzee; wengine wanapambana na ugonjwa wenye kuwafanya wakuwe wazaifu. Na wakati fulani, sisi wote tunajisikia kuwa wenye kuchoka. Kwa hiyo, wazo la kukimbia katika mbio linaweza kutuogopesha. Habari hii inazungumuzia namna sisi wote tunaweza kukimbia kwa uvumilivu na kupata ushindi katika mbio ya uzima yenye mutume Paulo alizungumuzia.

^ fu. 6 Ona habari “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” katika gazeti Munara wa Mulinzi la Mwezi wa 1, 2013.

^ fu. 20 Ili kupata mashauri zaidi yenye kufaa juu ya namna ya kupambana na mahangaiko na mifano ya watu wenye wako wanapambana muzuri nayo, ona programu ya Mwezi wa 5, 2019 ku jw.org. Fungua sehemu MAKTABA > JW TÉLÉDIFFUSION.

^ fu. 63 MAFASIRIO YA PICHA: Kuendelea kufanya mambo mingi katika kazi ya kuhubiri kunasaidia ndugu huyu mwenye kuzeeka aendelee kutembea katika njia ya Kikristo.

^ fu. 65 MAFASIRIO YA PICHA: Tunaweza kukwaza wengine kwa kuwakaza wakunywe pombe mingi ao wakati sisi wenyewe tunakunywa bila kiasi.

^ fu. 67 MAFASIRIO YA PICHA: Hata kama hawezi kutoka mu kitanda cha hospitali, ndugu mumoja anabakia katika mbio ya Kikristo kwa kuhubiria wanganga wake.