Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 14

Shambulizi Kutoka Kaskazini!

Shambulizi Kutoka Kaskazini!

“Taifa limeingia katika inchi yangu.”​—YOE. 1:6.

WIMBO 95 Nuru Inazidi Kuongezeka

KIFUPI CHA HABARI *

1. Ndugu Russell na wenzake walikuwa wanatumia njia gani ili kujifunza, na juu ya nini njia hiyo ilikuwa ya muzuri?

MIAKA zaidi ya mia moja yenye imepita, Ndugu Russell na wenzake, ni kusema, kikundi kidogo cha wanafunzi wengine wa Neno la Mungu, walianza kukutana pamoja. Walipenda kuona ikiwa wangeweza kujifunza kabisa mambo yenye Biblia inafundisha juu ya Yehova Mungu, Yesu Kristo, hali ya wafu, na bei ya ukombozi. Walikuwa wanatumia njia ya mwepesi ya kujifunza. Mutu mumoja alikuwa anauliza ulizo fulani, na kisha watu wa kikundi chote walikuwa wanachunguza kila andiko lenye kuhusu ulizo hilo. Kisha, walikuwa wanaandika mambo yenye walipata. Kwa baraka za Yehova, wanaume hao waaminifu walivumbua kweli za musingi za Biblia zenye tunafurahia mupaka leo.

2. Wakati fulani, ni mambo gani inaweza kufanya tukose kuelewa muzuri unabii fulani wa Biblia?

2 Lakini, wanafunzi wa Biblia walitambua bila kukawia kama ni nguvu zaidi kuelewa unabii wa Biblia kuliko kuelewa mafundisho ya musingi ya Biblia. Sababu gani? Sababu moja ni kwamba mara mingi unabii fulani wa Biblia unaeleweka muzuri zaidi wakati uko unatimia ao kisha kutimia. Lakini kuko sababu ingine. Ili kuelewa muzuri unabii fulani, kwa kawaida tunapaswa kuchunguza sehemu zote za unabii huo. Kama tunakaza akili juu ya sehemu moja ya unabii fulani na kuacha sehemu zingine zote, tunaweza kuelewa mubaya unabii huo. Inaonekana kama ilikuwa vile juu ya unabii wa kitabu cha Yoeli. Tuzungumuzie tena unabii huo na tuone juu ya nini tunapaswa kubadilisha namna tulikuwa tunaelewa unabii huo.

3-4. Mupaka sasa, namna gani tumetumia unabii wenye kuwa katika Yoeli 2:7-9?

3 Soma Yoeli 2:7-9. Yoeli alitabiri kama pigo la nzige lingeharibu inchi ya Israeli. Nzige hao wenye kuwa na meno na mataya (mifupa ya kinywa yenye kubeba meno) kama ya simba wangekula mimea yote katika inchi ya Israeli! (Yoe. 1:4, 6) Kwa miaka mingi, tumetumia unabii huo kwa njia ya mufano ili kuzungumuzia namna watu wa Yehova, wenye kulinganishwa na vikundi vya nzige wenye hawawezi kuzuiwa, wanafanya kazi yao ya kuhubiri. Tulikuwa tunaelewa kama kazi hiyo imekuwa na matokeo ya mubaya juu ya “inchi,” ao watu wenye kuongozwa na viongozi wa dini. *

4 Inaonekana kama ile inaweza kuwa mafasirio ya muzuri kama tunasoma tu Yoeli 2:7-9. Lakini wakati tunachunguza unabii wote, tunaona kama tunapaswa kubadilisha namna yetu ya kuelewa. Tuzungumuzie sababu ine zenye kuonyesha vile.

SABABU INE ZENYE ZINAFANYA TUBADILISHE NAMNA TULIELEWA UNABII HUO

5-6. Tunajiuliza ulizo gani wakati tunasoma (a) Yoeli 2:20? (b) Yoeli 2:25?

5 Sababu ya kwanza inategemea ahadi yenye Yehova anatoa juu ya pigo la nzige: “Nitafukuza mukaaji wa kaskazini [nzige] mbali na ninyi.” (Yoe. 2:20) Ikiwa nzige wanafananisha Mashahidi wa Yehova wenye kutii amri ya Yesu ya kuhubiri na kufanya wanafunzi, juu ya nini Yehova anasema kama atawafukuza mbali? (Eze. 33:7-9; Mt. 28:19, 20) Ni wazi kama Yehova hafukuze mbali watumishi wake waaminifu, lakini anafukuza mbali kitu fulani ao mutu fulani mwenye kutendea watu wake kwa ukali.

6 Sababu ya pili inategemea mambo yenye kuandikwa katika Yoeli 2:25. Katika andiko hilo, Yehova anasema hivi: Nitawalipa kwa ajili ya miaka yenye nzige mwenye kupatikana kwa wingi, nzige mwenye hana mabawa, na nzige mwenye kula sana, na nzige mwenye kumeza kila kitu amekula, jeshi langu kubwa lenye nilituma kati yenu.” Ona kama Yehova anatoa ahadi ya ‘kulipia’ uharibifu wenye nzige hao wamefanya. Kama nzige wanafananisha wahubiri wa Ufalme, hilo lingemaanisha kama ujumbe wenye wanahubiri unaleta uharibifu. Lakini ujumbe huo wenye kuokoa uzima unaweza kuchochea watu fulani waovu watubu. (Eze. 33:8, 19) Ile inaweza kuwa baraka kubwa kwao!

7. Kwenye Yoeli 2:28, 29, neno “kisha” linatusaidia kuelewa nini?

7 Soma Yoeli 2:28, 29. Fikiria sababu ya tatu: namna matukio katika unabii huo inafuatana. Je, uliona kama Yehova anasema hivi: “Kisha nitamwanga roho yangu”; ni kusema, kisha nzige kumaliza kufanya kazi yao? Ikiwa nzige ni wahubiri wa Ufalme wa Mungu, juu ya nini Yehova alisema kama atamwanga roho yake juu yao kisha kumaliza kazi yao ya kutoa ushahidi? Kwa kweli, bila musaada wa roho takatifu ya Mungu yenye nguvu sana, hawangeweza kabisa kuendelea kuhubiri miaka mingi hata kama wanapingwa na hata kama kazi yao inakatazwa.

Ndugu Rutherford na watumishi wengine watiwa-mafuta wametangaza kwa bidii hukumu za Mungu juu ya ulimwengu huu muovu (Ona fungu la 8)

8. Nzige wenye kuzungumuziwa katika Ufunuo 9:1-11 wanafananisha nani? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

8 Soma Ufunuo 9:1-11. Sasa tuzungumuzie sababu ya ine. Zamani, tulifananisha pigo la nzige lenye Yoeli anazungumuzia na kazi yetu ya kuhubiri kwa sababu ya unabii wenye kufanana na unabii huo wenye kupatikana katika kitabu cha Ufunuo. Unabii huo unazungumuzia vikundi vya nzige wenye kuwa na nyuso za wanadamu na wenye kuwa na “kitu chenye kuonekana kama mataji ya zahabu” kwenye vichwa vyao. (Ufu. 9:7) Wanatesa “watu [maadui wa Mungu] wenye hawana muhuri wa Mungu kwenye mapaji ya nyuso zao” kwa miezi tano, muda wenye kwa kawaida nzige wanaishi. (Ufu. 9:4, 5) Inaonekana kuwa unabii huo unazungumuzia watumishi wa Yehova wenye kutiwa mafuta. Wanatangaza kwa uhodari ujumbe wa hukumu wa Mungu juu ya mupangilio huu muovu wa mambo na, kwa hiyo, wanafanya watu wenye kuunga mukono mupangalio huu wajisikie mubaya sana.

9. Kuko tofauti gani kubwa kati ya nzige wenye Yoeli aliona na wale wenye Yohana aliona?

9 Kwa kweli, kuko mambo yenye kufanana kati ya unabii wenye kuwa katika Ufunuo na ule wenye kuwa katika kitabu cha Yoeli. Lakini, kuko tofauti kubwa. Fikiria jambo hili: Katika unabii wa Yoeli, nzige wanakula mimea yote. (Yoe. 1:4, 6, 7) Katika maono ya Yohana, nzige wanaambiwa “wasiharibishe majani ya dunia.” (Ufu. 9:4) Nzige wenye Yoeli aliona walitoka kaskazini. (Yoe. 2:20) Nzige wenye Yohana aliona walitoka katika abiso. (Ufu. 9:2, 3) Nzige wenye Yoeli aliona walifukuzwa mbali. Katika kitabu cha Ufunuo, nzige hawafukuzwe mbali lakini wanaruhusiwa kumaliza kazi yao. Hakuna jambo lenye kuonyesha kama Yehova hapendezwe na nzige hao.​—Ona kisanduku “ Unabii Juu ya Nzige: Unafanana Lakini Uko Tofauti.”

10. Ni mufano gani wa Maandiko wenye kuonyesha kama nzige wenye Yoeli aliona na wale wenye Yohana aliona wanaweza kufananisha mambo tofauti?

10 Tofauti kubwa zenye kuwa kati ya unabii huo mbili zinatusaidia kuelewa kama kila unabii uko na maana yake. Je, tunapenda kusema kama nzige wenye Yoeli anazungumuzia wako tofauti na nzige wenye kuzungumuziwa katika kitabu cha Ufunuo? Ndiyo. Katika Biblia, wakati fulani usemi moja wa mufano unaweza kumaanisha mambo mbalimbali kulingana na habari. Kwa mufano, kwenye Ufunuo 5:5, Yesu anaitwa “Simba wa kabila la Yuda,” lakini katika 1 Petro 5:8, Ibilisi anazungumuziwa kuwa “simba mwenye kunguruma.” Kwa sababu namna tunaelewa sasa inaleta maulizo fulani, tunapaswa kutafuta mafasirio ingine juu ya unabii wa Yoeli. Inaweza kuwa mafasirio gani?

MAANA YA UNABII WA YOELI

11. Namna gani Yoeli 1:6 na 2:1, 8, 11 inatusaidia kuelewa nzige ni nani?

11 Wakati tunachunguza mistari ingine katika unabii wa Yoeli, tunaelewa kama nabii alikuwa anatabiri shambulizi la kijeshi. (Yoe. 1:6; 2:1, 8, 11) Yehova alisema kama angetumia “jeshi [lake] kubwa” (maaskari wa Babiloni) ili kupatia malipizi Waisraeli wenye kuasi. (Yoe. 2:25) Njo maana jeshi lenye lilishambulia linaitwa “mukaaji wa kaskazini” kwa sababu Wababiloni wangetokea kaskazini ili kushambulia Israeli. (Yoe. 2:20) Jeshi hilo linafananishwa na kikundi cha nzige wenye kupangwa muzuri. Juu yao, Yoeli anasema hivi: “Kila [askari] anaendelea mbele katika njia yake. . . . Wanaingia haraka katika muji, wanakimbia kwenye ukuta. Wanapanda juu ya nyumba, na wanaingia kupitia madirisha kama mwizi.” (Yoe. 2:8, 9) Unaweza kuona picha ya hali hiyo katika akili yako? Maaskari wako kila mahali. Hakuna nafasi ya kujificha. Hakuna mwenye anaweza kuponyoka upanga wa Wababiloni!

12. Namna gani unabii wa Yoeli juu ya nzige ulitimia?

12 Kama vile nzige, Wababiloni (ao, Wakaldayo) walishambulia muji wa Yerusalemu katika mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Biblia inasema hivi: “Mufalme wa Wakaldayo . . . , mwenye aliua wanaume wao vijana kwa upanga . . . hakusikilia huruma kijana mwanaume wala bikira, muzee wala muzaifu. Mungu alitia kila kitu katika mukono wake. Akateketeza nyumba ya Mungu wa kweli, akabomoa ukuta wa Yerusalemu, akateketeza kwa moto minara yake yote yenye ngome, na kuharibu kila kitu chenye samani.” (2 Ny. 36:17, 19) Wakati Wababiloni walimaliza kushambulia inchi, watu wangesema tu hivi: “Ni inchi yenye imeachwa yenye haina mwanadamu na munyama, na imetiwa katika mukono wa Wakaldayo.”​—Yer. 32:43.

13. Fasiria maana ya andiko la Yeremia 16:16, 18.

13 Miaka 200 hivi kisha Yoeli kutoa unabii, Yehova alimutumia Yeremia ili atabiri jambo lingine juu ya shambulizi hilo. Alionyesha kama wale washambulizi wangetafuta kwa uangalifu Waisraeli wenye walikuwa wanafanya mambo ya mubaya na wangewakamata wote. Yeremia alisema hivi: “‘Angalia, ninaita wavuvi wengi wa samaki,’ ni vile Yehova anasema, ‘na watawavua. Kisha, nitaita wawindaji wengi, na watawawinda kwenye kila mulima na kila kilima na kutoka katika mipasuko ya miamba. . . . Nitalipa kiasi kamili chenye kustahili kosa lao na zambi yao.’” Hata bahari ao pori haingeweza kuficha Waisraeli wenye hawatubu ili wasipate malipizi kutoka kwa Yehova.​—Yer. 16:16, 18.

HABARI NJEMA

14. Ni wakati gani andiko la Yoeli 2:28, 29 lilitimia?

14 Kwa njia yenye kupendeza, Yoeli anazungumuzia sasa habari njema. Inchi itazaa tena matunda. (Yoe. 2:23-26) Kisha, wakati wenye kuja, chakula cha kiroho kitapatikana kwa wingi. Yehova anasema hivi: “Nitamwanga roho yangu juu ya kila namna ya mwili, na watoto wenu wanaume na watoto wenu wanamuke watatoa unabii . . . Na hata juu ya watumwa wangu wanaume na watumwa wangu wanamuke nitamwanga roho yangu.” (Yoe. 2:28, 29) Mungu hakumwanga roho yake kisha tu Waisraeli kutoka katika Babiloni na kurudia katika inchi yao. Lakini, jambo hilo lilifanyika miaka mingi kisha pale, kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33. Ni nini inaonyesha vile?

15. Kulingana na Matendo 2:16, 17, ni marekebisho gani yenye Petro alifanya juu ya andiko la Yoeli 2:28, na hilo linaonyesha nini?

15 Kwa kuongozwa na roho ya Mungu, mutume Petro alitumia Yoeli 2:28, 29 kuhusu tukio lenye lilifanyika siku hiyo ya Pentekoste. Karibu saa tatu asubui hiyo, roho takatifu ilimwangwa kwa njia ya muujiza na ilichochea wale wenye waliipata waanze kusema “juu ya mambo makubwa ya Mungu.” (Mdo. 2:11) Kwa kuongozwa na roho ya Mungu, Petro alitumia maneno yenye kuwa tofauti kidogo wakati alitaja unabii wa Yoeli. Je, uliona marekebisho yenye alifanya? (Soma Matendo 2:16, 17.) Petro hakutumia maneno “kisha” yenye inatumiwa katika unabii wa Yoeli lakini alisema hivi: “Na katika siku za mwisho.” Katika andiko hili, maneno “siku za mwisho” ni mwisho wa mupangilio wa mambo wa Wayahudi (wakati wenye Yerusalemu na hekalu lake vilikuwa karibu kuharibiwa). Wakati huo, roho ya Mungu ingemwangwa “juu ya kila namna ya mwili.” Hilo linaonyesha kama kulipita wakati murefu mbele unabii wa Yoeli utimie.

16. Roho ya Mungu ilikuwa na matokeo gani juu ya kazi ya kuhubiri wakati wa mitume, na iko na matokeo gani juu ya kazi ya kuhubiri leo?

16 Kisha Mungu kumwanga roho yake juu ya Wakristo wa wakati wa mitume, walianza kufanya kazi ya kuhubiri yenye kisha wakati fulani ingefika katika dunia yote. Kufikia wakati mutume Paulo aliandikia Wakolosai barua, karibu na mwaka wa 61, alisema kama habari njema ilikuwa inahubiriwa “katika uumbaji wote chini ya mbingu.” (Kol. 1:23) Katika wakati wa Paulo, maneno “uumbaji wote” ilimaanisha maeneo ya ulimwengu kwenye Paulo na wengine wangeweza kusafiri. Kwa musaada wa roho takatifu ya Yehova, kazi ya kuhubiri imeenea sana katika siku zetu, mupaka “kwenye miisho ya dunia”!​—Mdo. 13:47; ona kisanduku “ Nitamwanga Roho Yangu.”

NI NINI IMEBADILIKA?

17. Ni mabadiliko gani yenye imefanywa juu ya namna tulikuwa tunaelewa unabii wa Yoeli juu ya nzige?

17 Ni nini imebadilika? Sasa tunaelewa muzuri zaidi unabii wenye kuwa katika Yoeli 2:7-9. Kwa kifupi, ile mistari haizungumuzie kazi yetu ya kuhubiri kwa bidii, lakini inazungumuzia shambulizi la jeshi la Babiloni juu ya Yerusalemu katika mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu.

18. Ni nini yenye haikubadilika juu ya watu wa Yehova?

18 Ni nini yenye haikubadilika? Watu wa Yehova wanaendelea kuhubiri habari njema kila mahali, kwa kutumia kila njia yenye wanaweza. (Mt. 24:14) Hakuna serikali inaweza kutuzuia kutimiza kazi yetu ya kuhubiri. Na kwa baraka za Yehova, tunahubiri habari njema ya Ufalme kwa bidii sana na bila woga kuliko wakati mwingine wowote! Tunaendelea kumutegemea Yehova kwa unyenyekevu ili atusaidie tuelewe unabii wa Biblia, na tuko hakika kama kwa wakati wenye kufaa, atatuongoza “katika kweli yote”!​—Yoh. 16:13.

WIMBO 97 Uhai Unategemea Neno la Mungu

^ fu. 5 Kwa miaka mingi, tulikuwa tunaamini kama unabii wenye kupatikana katika sura ya 1 na ya 2 ya kitabu cha Yoeli unazungumuzia kazi ya kuhubiri katika siku zetu. Lakini, kuko sababu ine zenye zinafanya ikuwe lazima tubadilishe namna tulikuwa tunaelewa ile sehemu ya unabii wa Yoeli. Ni sababu gani?

^ fu. 3 Kwa mufano, ona habari “Hekima ya Yehova Inaonekana Katika Uumbaji” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 4, 2009, fu. 14-16.