Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 15

Uko na Mawazo Gani Juu ya Watu wa Eneo Lako?

Uko na Mawazo Gani Juu ya Watu wa Eneo Lako?

“Muinue macho yenu na muone mashamba, ni meupe kwa ajili ya kuvunwa.”​—YOH. 4:35.

WIMBO 64 Kuyashiriki Mavuno kwa Furaha

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Yesu alikuwa anazungumuzia nini wakati alisema maneno yenye kuwa katika Yohana 4:35, 36?

YESU amekuwa akisafiri katika mashamba, pengine ilikuwa mashamba ya shayiri ya rangi ya majani mabichi. (Yoh. 4:3-6) Ile mashamba ingekuwa tayari kuvunwa kisha miezi ine hivi. Yesu alisema jambo fulani lenye pengine lilionekana kuwa la kushangaza. Alisema hivi: “Muinue macho yenu na muone mashamba, ni meupe kwa ajili ya kuvunwa.” (Soma Yohana 4:35, 36.) Alipenda kusema nini?

2 Inaonekana Yesu alikuwa anazungumuzia mavuno ya mufano, ni kusema, watu. Fikiria jambo lenye lilikuwa limetokea tu mbele ya pale. Hata kama kwa kawaida Wayahudi walikuwa wanaepuka Wasamaria, Yesu alikuwa amehubiria mwanamuke Musamaria na ule mwanamuke alikuwa amesikiliza! Kwa kweli, wakati Yesu alikuwa anazungumuzia mashamba yenye ilikuwa “meupe kwa ajili ya kuvunwa,” kikundi cha Wasamaria wenye ule mwanamuke alizungumuza nao juu ya Yesu walikuwa wanakuja ili Yesu awafundishe mambo mingi. (Yoh. 4:9, 39-42) Kitabu kimoja chenye kutoa maelezo juu ya Biblia kinasema hivi: “Kwa sababu watu walikuja haraka ili kukutana na Yesu na kumusikiliza . . . hilo lilionyesha kama walikuwa kama nafaka yenye kuwa tayari kuvunwa.”

Tunapaswa kufanya nini kama tunaona kuwa mashamba ni “meupe kwa ajili ya kuvunwa”? (Ona fungu la 3)

3. Kama unaona watu kama vile Yesu aliwaona, utafanya nini ili upate matokeo ya muzuri katika kazi ya kuhubiri?

3 Uko na mawazo gani juu ya watu wenye unahubiria? Unawaona kama vile nafaka yenye kuwa tayari kwa ajili ya kuvunwa? Kama ni vile, utafanya mambo tatu. Jambo la kwanza, utahubiri kwa uharaka zaidi. Kipindi cha mavuno kiko kifupi; hakuna wakati wa kupoteza. Jambo la pili, utakuwa na furaha wakati unaendelea kuona namna watu wanakubali habari njema. Biblia inasema hivi: ‘Watu wanashangilia wakati wa mavuno.’ (Isa. 9:3) Na jambo la tatu, utaona kila mutu kama anaweza kuwa mwanafunzi wa Yesu, kwa hiyo, utapatanisha namna yako ya kuanzisha mazungumuzo na mambo yenye watu wanapendezwa nayo.

4. Katika habari hii, tutajifunza nini kupitia mufano wa mutume Paulo?

4 Pengine wanafunzi fulani wa Yesu waliwaza kama Wasamaria hawawezi kuwa wanafunzi wa Yesu, lakini Yesu yeye hakukuwa na ile mawazo. Hata hivyo, aliwaona kama wanaweza kuwa wanafunzi wake. Sisi pia tunapaswa kuona watu wa eneo letu kama wanaweza kuwa wanafunzi wa Kristo. Mutume Paulo alituachia mufano muzuri sana wenye tunaweza kuiga. Mufano wake unaweza kutufundisha mambo gani? Katika habari hii, tutazungumuzia namna (1) alijua habari fulani juu ya mambo yenye watu wenye alihubiria waliamini, (2) alitambua mambo yenye walipendezwa nayo, na (3) aliwaona kama wanaweza kuwa wanafunzi wa Yesu.

WANAAMINI NINI?

5. Juu ya nini Paulo angeweza kuelewa wasikilizaji wake katika sinagogi?

5 Mara mingi, Paulo alihubiri katika masinagogi ya Wayahudi. Kwa mufano, katika sinagogi moja mu muji wa Tesalonike, ‘kwa muda wa sabato tatu (3) alifikiri na [Wayahudi] kwa kutumia Maandiko.’ (Mdo. 17:1, 2) Paulo alikuwa anajisikia huru wakati alikuwa katika sinagogi kwa sababu alikuwa Muyahudi. (Mdo. 26:4, 5) Angeweza kuelewa hali ya Wayahudi, kwa hiyo aliweza kuwahubiria bila woga.​—Flp. 3:4, 5.

6. Namna gani watu wa soko la Atene walikuwa tofauti na watu wenye Paulo alihubiria katika sinagogi?

6 Kisha wapinzani wa Paulo kumufukuza katika Tesalonike na kisha katika Beroya, alifika katika muji wa Atene. Tena, ‘aliaanza kufikiri katika sinagogi pamoja na Wayahudi na watu wengine wenye walikuwa wanamuabudu Mungu.’ (Mdo. 17:17) Lakini, wakati alikuwa anahubiri katika soko, Paulo alikuwa anahubiria wasikilizaji wenye walikuwa tofauti na Wayahudi. Kati ya wasikilizaji hao, kulikuwa wanafilozofia na watu wengine wa mataifa wenye waliona ujumbe wa Paulo kuwa ‘fundisho la mupya.’ Walimuambia hivi: “Unaleta mambo mageni katika masikio yetu.”​—Mdo. 17:18-20.

7. Kulingana na Matendo 17:22, 23, namna gani Paulo alibadilisha namna yake ya kuhubiri?

7 Soma Matendo 17:22, 23. Paulo hakutangazia ujumbe wake Watu wa Mataifa katika Atene kwa kutumia namna ileile yenye alitumia wakati alizungumuza na Wayahudi katika sinagogi. Inawezekana kabisa kama Paulo alijiuliza hivi: ‘Watu hawa wa Atene wanaamini nini?’ Aliangalia kwa uangalifu mambo yenye ilikuwa inamuzunguka na alitambua desturi za watu za dini. Kisha, wakati Paulo aliwaambia kweli kutoka katika Maandiko, alianza na mambo yenye tayari walikuwa wanaamini. Mutu mumoja mwenye kutoa maelezo juu ya Biblia anasema hivi: “Kwa sababu alikuwa Mukristo Muyahudi, alielewa kama Wagiriki wapagani hawakukuwa wanaabudu Mungu wa ‘kweli’ wa Wayahudi na Wakristo, lakini alijikaza kuwaonyesha kama Mungu mwenye aliwatangazia haiko kwa kweli Mungu mugeni kwa watu wa Atene.” Kwa hiyo, Paulo alikuwa tayari kupatanisha namna yake ya kuhubiri kulingana na wasikilizaji wake. Aliambia watu wa Atene kama ujumbe wake unatoka kwa “Mungu Mwenye Hajulikane,” mwenye walikuwa wanajikaza kuabudu. Hata kama Watu wa Mataifa hawakukuwa wanajua Maandiko, Paulo hakuwaza kama hawawezi kuwa Wakristo. Lakini, aliwaona kama vile nafaka yenye kuwa tayari kuvunwa, na alibadilisha namna yake ya kuhubiri habari njema.

Uige mufano wa mutume Paulo kwa kuwa mutazamaji muzuri, kwa kupatanisha namna yako ya kuhubiri na hali ya wasikilizaji, na kuona watu kama wanaweza kuwa wanafunzi wa Yesu (Ona fungu la 8, 12, 18) *

8. (a) Ni nini inaweza kukusaidia kujua mambo yenye watu wa eneo lako wanaamini? (b) Kama mutu fulani anakuambia kama iko na dini yake, unaweza kumuambia nini?

8 Kama Paulo, ukuwe mutazamaji muzuri. Tafuta mambo yenye kuonyesha mambo yenye watu wa eneo lako wanaamini. Ni mambo gani yenye musikilizaji anatumia ili kupamba gari ao nyumba yake? Je, jina lake, namna anavaa, namna anajipamba, ao hata maneno yake inaonyesha kama ni mutu wa dini fulani? Pengine amekuambia moja kwa moja kama iko na dini yake. Kama mutu fulani anasema vile, painia mumoja wa pekee mwenye kuitwa Flutura, anasemaka hivi: “Siko hapa juu ya kukukaza uamini mambo yenye ninaamini, lakini nimekuja ili tuzungumuzie habari hii . . .”

9. Ni mambo gani yenye pengine munaweza kukubaliana na mutu wa dini fulani?

9 Ni habari gani unaweza kuzungumuzia na mutu mwenye anapenda mambo ya dini? Ujikaze kupata mambo yenye ninyi wawili munakubaliana. Pengine anaabudu Mungu mumoja tu, pengine anaamini kama Yesu ni Mukombozi wa wanadamu, ao pengine anaamini kama tunaishi wakati mubaya sana wenye utafikia mwisho hivi karibuni. Utumie mambo yenye ninyi wawili munaamini ili kuzungumuzia naye ujumbe wa Biblia kwa njia yenye itamupendeza.

10. Tunapaswa kujikaza kufanya nini, na juu ya nini?

10 Ukumbuke kama watu wengi wanaweza kuwa hawaamini mambo yote yenye dini zao zinafundisha. Kwa hiyo, hata kisha kutambua dini ya mutu, ujikaze kujua mambo yenye yeye anaamini. David, painia mumoja wa pekee wa Australia, anasema hivi: “Leo watu wengi wanachanga filozofia na mambo ya dini.” Dada Donalta wa Albania, anasema hivi: “Watu fulani wenye tunakutana nao wanasema kama wako katika dini fulani, lakini kisha wanasema kama hawamuamini kabisa Mungu.” Na ndugu mumoja misionere katika Argentina alitambua kama watu fulani wanasema kama wanaamini Utatu, lakini wanaweza kuwa hawaamini kabisa kama Baba, Mwana, na roho takatifu ni Mungu mumoja. Anasema hivi: “Kujua vile kunafanya ikuwe mwepesi zaidi kupata mambo yenye sisi wawili tunakubaliana.” Kwa hiyo, ujikaze kujua mambo yenye watu wanaamini kabisa. Ukifanya vile, unaweza kuwa “mambo yote kwa watu wa namna zote” kama Paulo.​—1 Ko. 9:19-23.

WANAPENDEZWA NA MAMBO GANI?

11. Kulingana na Matendo 14:14-17, namna gani Paulo alitangazia watu wa Listra ujumbe wake kwa njia yenye kupendeza?

11 Soma Matendo 14:14-17. Paulo alitambua mambo yenye ilipendeza wasikilizaji wake, na kisha alipatanisha namna yake ya kuhubiri na ile mambo. Kwa mufano, watu wenye alizungumuza nao katika Listra walikuwa wanajua mambo kidogo ao hawakujua kitu juu ya Maandiko. Kwa hiyo, Paulo alifikiri nao juu ya mambo yenye wangeweza kuelewa. Alizungumuzia namna Mungu anapatia watu mavuno mingi na uwezo wa kufurahia maisha. Alitumia maneno na mifano yenye wasikilizaji wake wangeweza kuelewa kwa vyepesi.

12. Namna gani unaweza kutambua mambo yenye mutu anapendezwa nayo na kupatanisha namna yako ya kuhubiri na ile mambo?

12 Tumia utambuzi ili kujua mambo yenye kupendeza watu wa eneo lenu na upatanishe namna yako ya kuhubiri na ile mambo. Namna gani unaweza kutambua mambo yenye mutu anapendezwa nayo wakati unamukaribia ao wakati unakaribia nyumba yake? Tena, ukuwe mutazamaji muzuri. Pengine iko anatengeneza bustani yake, iko anasoma kitabu, iko anatengeneza gari, ao iko anafanya kazi ingine. Kama inafaa, unaweza kutumia mambo yenye mutu iko anafanya ili kuanzisha mazungumuzo naye. (Yoh. 4:7) Hata nguo yenye mutu anavaa inaweza kukuambia jambo fulani juu yake, pengine inaonyesha inchi yake, kazi yake, ao timu fulani ya wachezaji yenye anapendaka. Gustavo anasema hivi: “Nilianzisha mazungumuzo na kijana mumoja wa miaka 19 mwenye alikuwa anavaa nguo yenye ilikuwa na picha ya muimbaji mumoja mwenye kujulikana sana. Nilimuuliza kijana huyo juu ya ile nguo, na aliniambia juu ya nini anapenda ule muimbaji. Kupitia ile mazungumuzo nilianza kujifunza naye Biblia, na sasa iko ndugu yetu.”

13. Wakati unaambia mutu kama unapenda kujifunza naye Biblia, namna gani unaweza kufanya vile kwa njia yenye itamufanya afurahie funzo?

13 Wakati unaambia mutu fulani kama ungependa kujifunza naye Biblia, ufanye vile kwa namna yenye itafanya afurahie funzo; umuonyeshe namna gani funzo litamusaidia. (Yoh. 4:13-15) Kwa mufano, mwanamuke mumoja mwenye alikuwa anapendezwa aliomba dada mumoja aingie mu nyumba yake. Wakati dada yetu aliona kwenye ukuta cheti chenye kuonyesha kama mwanamuke huyo alikuwa profesa mwenye alijifunza masomo ya kufundisha watu, alisema kama sisi pia tunafundishaka watu kupitia programu ya kujifunza Biblia na kupitia mikutano yetu. Mwanamuke huyo alikubali kujifunza Biblia, na alienda kwenye mikutano siku yenye ilifuata, na alihuzuria mukusanyiko wa muzunguko wenye ulifanywa muda kidogo kisha pale. Kisha mwaka moja, alibatizwa. Ujiulize hivi: ‘Watu wenye ninarudilia wanapendezwa na mambo gani? Ninaweza kuzungumuzia programu ya kujifunza Biblia na watu kwa njia yenye kufanya wapendezwe nayo?’

14. Namna gani unaweza kupatanisha habari na mahitaji ya kila mwanafunzi?

14 Kisha kuanza kujifunza Biblia na mutu fulani, utayarishe kila funzo lenye utaongoza, kwa kufikiria hali ya mwanafunzi na mambo yenye inamupendeza. Wakati unatayarisha, uamue ni maandiko gani utasoma, ni video gani utaonyesha, na ni mifano gani utatumia ili kufasiria kweli za Biblia. Ujiulize hivi: ‘Ni mambo gani itapendeza zaidi mwanafunzi na kumugusa moyo?’ (Mez. 16:23) Katika Albania, mwanamuke mwenye alikuwa anajifunza na painia mwenye kuitwa Flora alisema hivi kwa mukazo: “Siwezi kukubali hata kidogo fundisho la ufufuo.” Flora hakujaribu kukaza ule mwanamuke akubali fundisho hilo palepale. Anasema hivi: “Nilitambua kama mbele aamini ufufuo, alipaswa kwanza kumujua Mungu mwenye anatoa ahadi ya ufufuo.” Kuanzia pale na kuendelea, kila wakati Flora alijifunza na ule mwanamuke, alikuwa anakazia upendo wa Yehova, hekima yake na nguvu zake. Kisha muda fulani, mwanafunzi wake akakuwa tayari kuamini ufufuo. Sasa iko Shahidi wa Yehova mwenye bidii.

UWAONE KAMA WANAWEZA KUWA WANAFUNZI WA YESU

15. Kulingana na Matendo 17:16-18, ni tabia gani zilimuchukiza Paulo katika Atene, lakini juu ya nini aliendelea kuhubiria watu wa Atene?

15 Soma Matendo 17:16-18. Paulo hakuwaza kama watu wa Atene hawawezi kuwa wanafunzi wa Yesu, hata kama muji wao ulikuwa unajaa sanamu, mambo ya uasherati na filozofia za wapagani. Na hakuacha kuwahubiria hata kama walimutukana. Paulo mwenyewe alifikia kuwa Mukristo hata kama alikuwa “mutu mwenye kumutukana Mungu na mutesaji na mutu mwenye zarau.” (1 Ti. 1:13) Yesu aliona kama Paulo angeweza kuwa mwanafunzi wake, Paulo vilevile aliona kama watu wa Atene wangeweza kuwa wanafunzi wa Yesu. Na alikuwa na sababu ya muzuri ya kuamini vile.​—Mdo. 9:13-15; 17:34.

16-17. Ni nini inaonyesha kama watu wa namna zote wanaweza kuwa wanafunzi wa Kristo? Leta mufano.

16 Katika wakati wa mitume, watu wa namna zote walifikia kuwa wanafunzi wa Yesu. Wakati Paulo aliandikia Wakristo wenye walikuwa wanaishi katika muji wa Ugiriki wa Korinto, alisema kama, wakati fulani, watu fulani katika kutaniko hilo walikuwa watenda-mabaya ao walikuwa na mwenendo mubaya wenye kuchukiza. Na kisha aliongeza hivi: “Wengine wenu mulikuwa vile. Lakini mumesafishwa mukakuwa safi.” (1 Ko. 6:9-11) Ingekuwa wewe, ungeona kama watu hao wanaweza kubadilika na kuwa wanafunzi wa Yesu?

17 Leo, watu wengi wako tayari kufanya mabadiliko yenye inaombwa ili kuwa wanafunzi wa Yesu. Kwa mufano, katika Australia, painia mumoja wa pekee mwenye kuitwa Yukina alielewa kama watu wa namna zote wanaweza kukubali ujumbe wa Biblia. Siku moja, wakati alikuwa ku biro fulani yenye kusimamia mambo ya udongo na nyumba, aliona mwanamuke mumoja kijana mwenye kuwa na chanjo mingi ku mwili wake na mwenye kuvaa nguo kubwa-kubwa. Yukina anasema hivi: “Kwanza nilisita kumukaribia, lakini kisha nilianza kuzungumuza naye. Nilitambua kama alikuwa anapendezwa sana na ujumbe wa Biblia kwa sababu chanjo zake fulani zilikuwa maandiko ya Zaburi!” Mwanamuke huyo alianza kujifunza Biblia na kuhuzuria mikutano. *

18. Juu ya nini hatupaswe kuhukumu watu?

18 Je, Yesu aliona kama mashamba imekomaa kwa ajili ya mavuno kwa sababu alitazamia kama watu wengi wangemufuata? Hapana kabisa. Maandiko ilikuwa imetabiri kama ni watu kidogo njo wangemuamini. (Yoh. 12:37, 38) Na Yesu alikuwa na uwezo wa ajabu wa kusoma mioyo ya watu. (Mt. 9:4) Hata kama alikaza akili yake juu ya wale kidogo wenye wangeamini, alihubiria kila mutu kwa bidii. Sisi hatuwezi kusoma mioyo ya watu, njo maana, tunapaswa kuepuka kuhukumu watu wa eneo letu ao mutu mumoja-mumoja! Lakini, tunapaswa kuona kama watu wanaweza kuwa wanafunzi wa Yesu. Marc, misionere mwenye anatumikia katika Burkina Faso, alisema hivi: “Watu wenye ninawazaka kama watafanya maendeleo mara mingi wanaachaka kujifunza. Lakini watu wenye ninaonaka kama hawatafanya maendeleo njo wanafanyaka maendeleo ya muzuri. Kwa hiyo, nimeelewa kama ni muzuri zaidi kuacha roho ya Yehova ituongoze.”

19. Tunapaswa kuwa na mawazo gani juu ya watu wa eneo letu?

19 Ku mwanzo, unaweza kuwaza kama hakuna watu wengi katika eneo wenye wako kama nafaka yenye kuwa tayari kwa ajili ya kuvunwa. Lakini ukumbuke mambo yenye Yesu aliambia wanafunzi wake. Mashamba iko meupe, ni kusema, iko tayari kwa ajili ya kuvunwa. Watu wanaweza kubadilika na kuwa wanafunzi wa Kristo. Yehova anaona watu wa eneo letu kuwa wanaweza kuwa wanafunzi na anawaona kuwa “vitu vyenye samani.” (Hag. 2:7) Kama tunaona watu namna Yehova na Yesu wanawaona, tutajikaza kujua hali zao na mambo yenye kuwapendeza. Hatutakuwa na mawazo ya mubaya juu yao, lakini tutawaona kama wanaweza kuwa ndugu na dada zetu.

WIMBO 57 Kuwahubiria Watu wa Namna Zote

^ fu. 5 Mawazo yenye tuko nayo juu ya watu wa eneo letu iko na matokeo gani juu ya namna yetu ya kuhubiri na kufundisha? Habari hii inazungumuzia namna Yesu na mutume Paulo waliona wasikilizaji wao na namna gani tunaweza kuwaiga kwa kufikiria mambo yenye watu wenye tunakutana nao wanaamini, mambo yenye wanapendezwa nayo, na kuona kila mumoja wao kama anaweza kuwa mwanafunzi wa Yesu.

^ fu. 17 Habari zenye kichwa “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” zinazungumuzia mifano mingi yenye kuonyesha namna watu wanaweza kubadilika. Habari hizo zilitolewa katika Munara wa Mulinzi mupaka mwaka wa 2017. Zinaendelea sasa kutolewa ku jw.org®. Fungua sehemu HABARI JUU YETU > USHUHUDA WA MASHAHIDI WA YEHOVA.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati bibi na bwana fulani wanahubiri nyumba kwa nyumba, wanaangalia (1) nyumba yenye kutunzwa muzuri, yenye kupambwa na maua; (2) nyumba kwenye familia yenye kuwa na watoto wadogo wanaishi; (3) nyumba yenye haitunzwe muzuri inje na ndani; na (4) nyumba ya mutu fulani mwenye kupenda mambo ya dini. Unawaza ni katika nyumba gani unaweza kupata mutu mwenye anaweza kuwa kabisa mwanafunzi wa Yesu?