Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tangaza Habari Njema ya Fazili Zenye Hatustahili

Tangaza Habari Njema ya Fazili Zenye Hatustahili

‘Toa ushahidi kamili kuhusu habari njema ya fazili zisizostahiliwa za Mungu.’MATENDO 20:24.

NYIMBO: 101, 84

1, 2. Namna gani mutume Paulo alionyesha kama alikuwa mwenye shukrani kwa ajili ya fazili za Mungu zenye hatustahili?

MUTUME Paulo alikuwa na sababu ya muzuri ya kusema waziwazi hivi: ‘Fazili [za Mungu] zisizostahiliwa zilizonielekea mimi hazikukuwa za bure.’ (Soma 1 Wakorintho 15:9, 10.) Mutume Paulo alijua waziwazi kama hakustahili rehema kubwa ya Mungu kwa sababu alikuwa anatesa Wakristo.

2 Wakati mutume Paulo alikaribia mwisho wa maisha yake, aliandikia Timotheo hivi: ‘Mimi namushukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenipa nguvu, kwa sababu aliniona kuwa muaminifu kwa kunigawia huduma [utumishi].’ (1 Timotheo 1:12-14) Ni huduma gani? Mutume Paulo aliambia wazee wa kutaniko la Efeso hivi: ‘Siifanye nafsi yangu kuwa kitu chenye samani [maana] sana kwangu, kama tu ningepata kumaliza mwendo wangu na huduma niliyopokea kutoka kwa Bwana Yesu, kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema ya fazili zisizostahiliwa za Mungu.’Matendo 20:24.

3. Mutume Paulo alipewa huduma gani ya pekee? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

3 Ni “habari njema” gani yenye mutume Paulo alihubiri, na namna gani habari hiyo ilionyesha fazili za Yehova zenye hatustahili? Mutume Paulo aliambia Wakristo wa Efeso hivi: ‘Mumesikia juu ya usimamizi-nyumba wa fazili zisizostahiliwa za Mungu ambao nilipewa kwa ajili yenu.’ (Waefeso 3:1, 2) Yesu alikuwa ameambia mutume Paulo ahubiri habari njema kwa watu wenye hawakukuwa Wayahudi. Sasa, iliwezekana kwa watu wa mataifa kuwa sehemu ya Ufalme ao serikali yenye kuongozwa na Masiya. (Soma Waefeso 3:5-8.) Mutume Paulo alihubiri kwa bidii na aliachia Wakristo wa leo mufano muzuri. Alionyesha kama fazili zenye hatustahili hazikukuwa “za bure” ao hazikukuwa na mafaa kwake.

UNACHOCHEWA NA FAZILI ZA MUNGU ZENYE HATUSTAHILI?

4, 5. Sababu gani tunaweza kusema kama “habari njema ya Ufalme” iko pia habari njema ya ‘fazili zisizostahiliwa za Mungu’?

4 Katika siku hizi za mwisho, watumishi wa Yehova wako na daraka la kuhubiri “habari njema ya Ufalme . . . katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote.” (Mathayo 24:14) Habari njema ya ufalme iko pia ‘habari njema ya fazili zisizostahiliwa za Mungu.’ Sababu gani tunasema hivyo? Baraka zote zenye tutapata kupitia Ufalme wa Mungu ni kwa sababu ya fazili zake. (Waefeso 1:3) Mutume Paulo alihubiri kwa bidii ili kuonyesha shukrani kwa ajili ya fazili za Yehova zenye hatustahili. Tunaiga mufano wa mutume Paulo?—Soma Waroma 1:14-16.

5 Katika habari yenye ilitangulia, tulijifunza namna fazili za Yehova zenye hatustahili zinatuletea sisi watenda-zambi faida katika njia nyingi. Kwa sababu tumepata faida nyingi sana, tuko na daraka la kufundisha wengine namna Yehova anaendelea kuonyesha upendo wake na namna wanaweza kupata faida za upendo huo. Ni katika njia gani tunaweza kusaidia wengine wakuwe wenye shukrani kwa ajili ya fazili za Mungu zenye hatustahili?

TANGAZA HABARI NJEMA YA ZABIHU YA UKOMBOZI

6, 7. Wakati tunafasiria watu maana ya zabihu ya ukombozi, namna gani tunaonyesha kama tunatangaza habari njema ya fazili za Mungu zenye hatustahili?

6 Leo, watu wengi hawasikie huzuni wakati wanafanya zambi; kwa hiyo, hawaelewe sababu gani wanadamu wako na lazima ya zabihu ya ukombozi. Hata hivyo, watu wengi zaidi wanatambua kama maisha yao hayawaletee furaha. Watu wengi hawajue zambi ni nini, iko na matokeo gani juu yetu, na tunapaswa kufanya nini ili kutoka katika utumwa wa zambi. Lakini, wakati wanazungumuza na Mashahidi wa Yehova, ndio wakati wanajua mambo hayo. Na wakati tu wanaelewa zambi ni nini, watu wenye kuwa na mioyo mizuri wanashukuru kujua kama Yehova alituma Mwana wake katika dunia ili kutukomboa kutoka katika kifo. Yehova alifanya hivyo kwa sababu ya upendo wake mukubwa na fazili zake zenye hatustahili.—1 Yohana 4:9, 10.

7 Ona maneno yenye mutume Paulo alisema juu ya Mwana mupendwa wa Yehova. Alisema hivi: ‘Kwa njia yake tuna kuachiliwa huru kwa njia ya fidia [zabihu ya ukombozi] kupitia damu ya huyo, ndiyo, musamaha wa makosa yetu, kulingana na utajiri wa fazili [za Yehova] zisizostahiliwa.’ (Waefeso 1:7) Zabihu ya Kristo ya ukombozi ni njia kubwa sana yenye Mungu ametumia ili kutuonyesha upendo na kama fazili Zake zenye hatustahili ni kubwa zaidi. Ni jambo lenye kutuliza kujua kama ikiwa tunaonyesha imani katika zabihu ya Yesu, zambi zetu zitasamehewa na tutakuwa na zamiri safi! (Waebrania 9:14) Kwa kweli, hiyo ni habari njema yenye tunapaswa kuhubiria wengine!

SAIDIA WATU WAKUWE MARAFIKI WA MUNGU

8. Sababu gani wanadamu watenda-zambi wako na lazima ya kupatanishwa na Mungu?

8 Ikiwa watu hawaonyeshe imani katika zabihu ya Yesu ya ukombozi, Mungu anawaona kuwa maadui wake. Kwa hiyo, tuko na daraka la kuwaambia kama wanaweza kuwa marafiki wa Mungu. Mutume Yohana aliandika hivi: ‘Yule anayemuamini Mwana ana uzima wa milele; yule asiyemutii Mwana hataona uzima, bali [lakini] gazabu [hasira] ya Mungu inakaa juu yake.’ (Yohana 3:36) Tuko na furaha kwa sababu zabihu ya Kristo ya ukombozi imetuwezesha tukuwe marafiki wa Mungu. Mutume Paulo alizungumuzia jambo hilo kwa kusema hivi: ‘Ninyi ambao hapo zamani mulikuwa mumetengwa, na nyinyi mulikuwa adui kwa sababu akili zenu zilikuwa zimekazwa juu ya matendo maovu, yeye sasa amewapatanisha tena kwa njia ya mwili wenye nyama wa huyo kupitia kifo chake.’—Wakolosai 1:21, 22.

Tuko na daraka la kuambia watu kama wanaweza kuwa marafiki wa Mungu

9, 10. (a) Kristo alipatia ndugu zake watiwa-mafuta kazi gani? (b) Namna gani “kondoo wengine” wanasaidia watiwa-mafuta?

9 Kristo amepatia ndugu zake watiwa-mafuta wenye kuwa duniani “huduma [kazi] ya upatanisho.” Paulo aliwaambia hivi: “Lakini mambo yote yametoka kwa Mungu, aliyetupatanisha sisi kwake mwenyewe kupitia Kristo na kutupa sisi huduma ya upatanisho, yaani, kwamba Mungu kupitia Kristo alikuwa akiupatanisha ulimwengu kwake mwenyewe, bila kuwahesabia makosa yao, naye alitukabizi [alitupatia] sisi lile neno la upatanisho. Kwa hiyo sisi ni mabalozi [ambasadere] walio badala ya Kristo, kana kwamba Mungu alikuwa akisihi kupitia sisi. Kama walio badala ya Kristo tunaomba: ‘Mupatanishwe pamoja na Mungu.’”—2 Wakorintho 5:18-20.

10 Ni pendeleo kwa ‘kondoo wengine’ kusaidia watiwa-mafuta katika kazi hiyo. (Yohana 10:16) Kama vile “wajumbe,” ao watu wenye kutumwa na Kristo, “kondoo wengine” wanafanya sehemu kubwa zaidi ya kazi ya kuhubiri, ni kusema, wanafundisha watu kweli na kuwasaidia wakuwe na urafiki wa sana pamoja na Yehova. Hiyo ni sehemu ya maana ya kazi ya kuhubiri habari njema ya fazili za Mungu zenye hatustahili.

FUNDISHA WATU KAMA MUNGU ANASIKIA SALA

11, 12. Wakati watu wanajifunza kama wanaweza kusali kwa Yehova, sababu gani hiyo ni habari njema kwao?

11 Watu wengi wanasali kwa sababu sala inafanya wajisikie muzuri, lakini hawaamini kabisa kama Mungu anasikia sala zao. Wako na lazima ya kujua kama Yehova ni ‘Musikiaji wa sala.’ Daudi, muandikaji mumoja wa zaburi aliandika hivi: ‘Ee musikiaji wa sala, kwako wewe watu wote wenye mwili watakuja. Mambo yenye makosa yamekuwa na nguvu kuliko mimi. Nayo makosa yetu, wewe mwenyewe utayafunika.’—Zaburi 65:2, 3.

Wakati tunafundisha watu namna ya kusali, tunawasaidia wakuwe marafiki wa Yehova

12 Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: ‘Mukiomba jambo lolote katika jina langu, nitalifanya.’ (Yohana 14:14) Hilo linamaanisha kama tunaweza kusali juu ya “jambo lolote” lenye kupatana na mapenzi ya Yehova. Mutume Yohana aliandika hivi: ‘Huu ndio uhakika ambao tunao kwake, kwamba, hata tukiomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.’ (1 Yohana 5:14) Ni muzuri kabisa kusaidia watu waelewe kama sala haiko jambo lenye kuwafanya tu wajisikie muzuri lakini ni njia ya kukaribia ‘kiti cha ufalme cha fazili zisizostahiliwa’ za Yehova! (Waebrania 4:16) Wakati tunafundisha watu namna ya kusali katika njia yenye kustahili, kwa Mutu mwenye kustahili, na juu ya mambo yenye kustahili, tunawasaidia wakuwe marafiki wa Yehova na wapate faraja ao kitulizo wakati wako katika mateso.—Zaburi 4:1; 145:18.

FAZILI ZENYE HATUSTAHILI KATIKA ULIMWENGU MUPYA

13, 14. (a) Watiwa-mafuta watakuwa na pendeleo gani la muzuri sana wakati unaokuja? (b) Ni kazi gani ya muzuri sana yenye watiwa-mafuta watafanyia wanadamu?

13 Yehova ataonyesha zaidi fazili zake zenye hatustahili hata ‘katika mufumo wa mambo [ulimwengu mupya] wenye kuja.’ Namna gani? Mungu atapatia wale 144000 wenye watatawala pamoja na Kristo pendeleo la muzuri sana. Mutume Paulo alifasiria pendeleo hilo wakati aliandika hivi: ‘Mungu, aliye tajiri katika rehema, kwa upendo wake mukubwa aliotupenda nao, alitufanya hai [wazima] pamoja na Kristo, tulipokuwa wafu katika makosa—kwa fazili zisizostahiliwa ninyi mumeokolewa. Naye alituinua pamoja na kutuketisha [kukaa] pamoja katika mahali pa kimbingu katika muungano na Kristo Yesu, ili katika mifumo ya mambo inayokuja uonyeshwe utajiri mwingi zaidi wa fazili zake zisizostahiliwa katika neema yake kutuelekea sisi katika muungano na Kristo Yesu.’—Waefeso 2:4-7.

14 Ni vigumu kuwazia mambo ya muzuri sana yenye Yehova ametayarishia Wakristo watiwa-mafuta wakati watatawala pamoja na Kristo mbinguni. (Luka 22:28-30; Wafilipi 3:20, 21; 1 Yohana 3:2) Kwa njia ya pekee, Yehova ‘ataonyesha utajiri mwingi zaidi wa fazili zake zisizostahiliwa’ kwa watiwa-mafuta. Watakuwa ‘Yerusalemu mupya,’ bibi arusi wa Kristo. (Ufunuo 3:12; 17:14; 21:2, 9, 10) Watatumika pamoja na Yesu ili “kuponya mataifa.” Watasaidia wanadamu watoke katika utumwa wa zambi na kifo na watawasaidia wakuwe wakamilifu.—Soma Ufunuo 22:1, 2, 17.

15, 16. Wakati unaokuja, namna gani Yehova ataonyesha “kondoo wengine” fazili zake zenye hatustahili?

15 Andiko la Waefeso 2:7 linasema kama Mungu ataonyesha fazili zenye hatustahili ‘katika mifumo ya mambo inayokuja.’ Wakati huo, kila mutu mwenye kuishi katika dunia atapata kabisa faida za ‘utajiri mwingi zaidi wa fazili zake zisizostahiliwa.’ (Luka 18:29, 30) Yehova ataonyesha fazili zake zenye hatustahili katika dunia kwa njia kubwa nyingi; moja kati ya njia hizo ni kufufua watu kutoka katika “Kaburi.” (Ayubu 14:13-15; Yohana 5:28, 29) Ni nani watafufuliwa? Wanaume na wanawake waaminifu wenye walikufa mbele ya kifo cha Kristo na wale wenye kuwa kati ya “kondoo wengine” wenye wanakufa waaminifu kwa Yehova katika siku za mwisho. Watu hao wote waaminifu watafufuliwa ili waendelee kumutumikia Yehova.

16 Mamilioni ya watu wenye walikufa bila kumujua Mungu, wao pia watafufuliwa. Yohana aliandika hivi: ‘Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme, na vitabu vya kukunjwa vikafunguliwa. Lakini kitabu kingine cha kukunjwa kikafunguliwa; hicho ni kitabu cha uzima. Na wafu wakahukumiwa kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao. Na bahari ikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake, na kifo na Kaburi vikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake, nao walihukumiwa kila mumoja kulingana na matendo yake.’ (Ufunuo 20:12, 13) Watu hao wenye watafufuliwa watapata nafasi ya kujifunza juu ya Yehova na kukubali utawala wake. Watajifunza na kutumikisha kanuni za Biblia na maagizo ya mupya yenye yatakuwa katika “vitabu vya kukunjwa.” Maagizo hayo ya mupya yatakuwa njia ingine yenye Yehova atatumia ili kuonyesha fazili zake zenye hatustahili.

ENDELEA KUHUBIRI HABARI NJEMA

17. Tunapaswa kukumbuka jambo gani wakati tunahubiri?

17 Ni jambo la maana sana leo kuhubiri habari njema ya Ufalme, kwa sababu mwisho unakaribia! (Marko 13:10) Tunapaswa kukumbuka kama wakati tunahubiri kusudi letu ni kumuletea Yehova heshima. Namna gani tunaweza kufanya hivyo? Tunapaswa kuambia watu kama baraka zote zenye tutapata katika dunia mupya ni kwa sababu tu ya fazili za Yehova zenye hatustahili.

Tutumike kwa bidii kama ‘wasimamizi-nyumba wazuri wa fazili zisizostahiliwa za Mungu.’—1 Petro 4:10 (Picha hii inapatana na fungu la 17-19)

18, 19. Namna gani tunatukuza fazili za Yehova zenye hatustahili?

18 Wakati tunahubiria watu, tunaweza kuwaelezea kama wakati Ufalme wa Kristo utaanza kutawala, watu watapata faida zote za zabihu ya ukombozi na watafikia ukamilifu polepole. Biblia inasema hivi: ‘Uumbaji wenyewe pia utawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu na kuwa na uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.’ (Waroma 8:21) Hilo litawezekana tu kupitia fazili za Yehova zenye hatustahili.

19 Tuko na pendeleo la kuambia watu wote juu ya ahadi yenye kufurahisha sana yenye kupatikana katika andiko la Ufunuo 21:4, 5: “[Mungu] atafuta [atapanguza] kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.” Na Yehova, mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme, anasema hivi: “Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Pia, anasema hivi: “Andika, kwa sababu maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.” Wakati tunahubiria wengine habari njema hiyo kwa bidii, tunatukuza kabisa fazili za Yehova zenye hatustahili!