Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Sababu gani maadui wa Yesu walifanya kunawa mikono kuwa tatizo?

Kunawa mikono ilikuwa moja kati ya mambo yenye yalifanya maadui wa Yesu wamuchambue yeye na wanafunzi wake. Sheria ya Musa ilieleza mambo yenye yangeweza kuchafua mutu. Kwa mufano, vitu vyenye kutoka katika mwili, ukoma, ao kugusa maiti ya mutu ao ya munyama. Sheria ilitoa pia maagizo juu ya namna mutu angefanywa tena kuwa safi. Hilo lingefanywa kupitia zabihu, kunawa, ao kunyunyiza maji.—Mambo ya Walawi, sura ya 11-15; Hesabu, sura ya 19.

Walimu wa dini ya Wayahudi, ni kusema, marabi, waliongeza sheria zao wenyewe juu ya sheria hizo. Kitabu kimoja kinasema kama marabi walitunga sheria zingine nyingi juu ya mambo yenye yangefanya mutu asikuwe safi na namna mutu huyo angefanya wengine wasikuwe safi. Marabi walitunga pia sheria juu ya aina ya vyombo vyenye vingechafuka na vyenye havingechafuka na desturi yenye watu walipaswa kufuata ili wakuwe safi tena.

Maadui wa Yesu walimuuliza hivi: ‘Kwa nini wanafunzi wako hawajiendeshe kulingana na mapokeo [desturi] ya watu wa zamani, bali [lakini] wanakula mulo [chakula] wao kwa mikono iliyo najisi [yenye haiko safi]?’ (Marko 7:5) Mafarisayo hao hawakukuwa wanazungumuzia usafi wa kawaida, ni kusema, kunawa mikono mbele ya kula chakula. Mafarisayo walikuwa wameweka sheria yenye kusema kama mbele mutu akule chakula, maji yalipaswa kumwangwa kwenye mikono yake kulingana na desturi. Kitabu chenye kutajwa hapo juu kinaongeza kama marabi walikuwa “pia wanabishana juu ya vyombo vyenye vilipaswa kutumiwa ili kumwanga maji, aina ya maji yenye kufaa ili kusafisha mikono, ni nani mwenye alipaswa kumwanga maji kwenye mikono, na maji yalipaswa kufika mupaka sehemu gani ya mikono.”

Yesu alitenda namna gani juu ya sheria zote hizo zenye zilifanywa na watu? Aliambia viongozi wa dini ya Wayahudi hivi: “Isaya kwa kufaa alitoa unabii juu yenu wanafiki, kama ilivyoandikwa, ‘Watu hawa wananiheshimu mimi kwa midomo yao, bali mioyo yao iko mbali na mimi [Yehova]. Wao wananiabudu bure, kwa sababu wao wanafundisha amri za wanadamu kuwa mafundisho.’ Munaiacha amri ya Mungu, na kuyashika sana mapokeo ya wanadamu.”—Marko 7:6-8.