Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unaona Lazima ya Kufanya Maendeleo ya Kiroho?

Unaona Lazima ya Kufanya Maendeleo ya Kiroho?

“Endelea kufanya bidii katika kusoma mbele ya watu wote, katika kuhimiza [kuchochea], katika kufundisha.”1 TIMOTHEO 4:13.

NYIMBO: 45, 70

1, 2. (a) Namna gani andiko la Isaya 60:22 linatimia katika siku hizi za mwisho? (b) Leo, kuko lazima gani katika sehemu ya duniani ya tengenezo la Yehova?

‘MUDOGO atakuwa elfu, na munyonge [asiyekuwa na nguvu] atakuwa taifa lenye nguvu.’ (Isaya 60:22) Maneno hayo yanaendelea kutimia leo katika siku hizi za mwisho. Kwa kweli, katika mwaka wa 2015, watumishi wa Yehova 8220105 walihubiri habari njema ya Ufalme katika dunia yote! Juu ya kuongezeka kwa watumishi wake, Mungu alisema hivi: “Mimi mwenyewe, Yehova, nitaharakisha jambo hilo kwa wakati wake.” Kwa hiyo, kadiri wakati unaendelea kupita, sisi wote tutakuwa na kazi nyingi ya kufanya. Tunafanya nguvu yetu yote ili kuhubiri na kufundisha habari njema? Ndugu na dada wengi wanafanya kazi ya upainia musaidizi ao wa kawaida. Wengine wamehamia katika maeneo mengine ili kusaidia katika kazi ya kuhubiri habari njema, na wengine wanatumika kwa bidii katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme.

2 Kila mwaka, makutaniko mapya karibu 2000 yanaanzishwa. Makutaniko hayo yako na lazima ya wazee na watumishi wa huduma. Kila mwaka, maelfu ya watumishi wa huduma wanapaswa kutimiza sifa zenye kuombwa ili wakuwe wazee na maelfu ya ndugu wengine wanapaswa kutimiza sifa zenye kuombwa ili wakuwe watumishi wa huduma. Kwa kweli, kuna “mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana,” na haiko ndugu wenyewe tu lakini dada pia.—1 Wakorintho 15:58.

UNAPASWA KUFANYA NINI ILI UFANYE MAENDELEO YA KIROHO

3, 4. Kufanya maendeleo ya kiroho kunamaanisha nini kwako?

3 Soma 1 Timotheo 3:1. Mutume Paulo alipongeza ndugu wenye walikuwa ‘wanajitahidi [kujikaza] kufikia’ kuwa waangalizi. Ili mutu afikie kitu fulani chenye kuwa mbali, anapaswa kujikaza sana ao pengine kunyoosha mukono wake ili kukikamata. Sasa wazia ndugu mwenye anapenda kutimiza sifa zenye kuombwa ili akuwe mutumishi wa huduma. Anatambua kama anapaswa kujikaza sana ili akomalishe zaidi sifa za Kikristo. Kisha, wakati anakuwa mutumishi wa huduma, anaendelea kujikaza kutimiza sifa zenye kuombwa ili akuwe muzee.

4 Ndugu na dada fulani wanaendelea kufanya mabadiliko katika maisha yao kwa sababu wanapenda kufanya mengi zaidi katika kazi ya Yehova. Kwa mufano, wanaweza kupenda kufanya kazi ya upainia, kutumika kwenye Beteli, ao kusaidia katika kazi ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Tuzungumuzie basi namna Biblia inaweza kusaidia kila mumoja wetu ili afanye maendeleo.

FANYA MAENDELEO YA KIROHO

5. Namna gani vijana wanaweza kutumia nguvu zao katika kazi ya Ufalme?

5 Vijana wanaweza kufanya mengi katika kazi ya Yehova kwa sababu wako na nguvu na afya ya muzuri. (Soma Methali 20:29.) Vijana fulani wenye kutumika kwenye Beteli wanasaidia katika kazi ya kuchapa na kuunganisha Biblia na vichapo vyetu. Ndugu na dada wengi wanajenga ao kutengeneza Majumba ya Ufalme. Ndugu na dada fulani wanajitoa ili kusaidia wakati musiba wa asili unatokea. Na mapainia wengi vijana wanajifunza luga ingine ao wanahamia katika eneo lingine ili kuhubiri habari njema.

6-8. (a) Namna gani kijana mumoja alibadilisha mawazo yake juu ya kazi ya Mungu, na alipata matokeo gani? (b) Namna gani unaweza ‘kuonja na kuona ya kuwa Yehova ni mwema’?

6 Tunapenda Yehova na tunapenda kumutumikia kwa nguvu zetu zote. Hata hivyo, tunaweza kujisikia kama ndugu mumoja mwenye kuitwa Aaron. Alipenda kufurahia kazi ya Mungu, lakini hakukuwa na furaha. Hata kama Aaron alikuwa amehuzuria mikutano na kuhubiri tangu alikuwa kijana, alisema hivi: “Niliona mikutano na kazi ya kuhubiri kuwa mambo yenye kuchokesha.” Sasa, alifanya nini?

7 Aaron alijikaza sana kusoma Biblia kwa ukawaida, kutayarisha mikutano, na kutoa maelezo kwenye mikutano hiyo. Pia, alianza kusali kwa ukawaida. Mambo hayo yote yalimusaidia afanye maendeleo ya kiroho. Alifikia kumujua Yehova muzuri zaidi na akaanza kumupenda sana. Kwa hiyo, Aaron akakuwa na furaha zaidi. Alifanya kazi ya upainia, alisaidia wengine wakati walipatwa na misiba ya asili, na alihamia katika inchi ingine ili kuhubiri. Sasa Aaron ni muzee wa kutaniko na anatumikia kwenye Beteli. Anajisikia namna gani juu ya maisha yake? Aaron alisema hivi: ‘Nimeonja na kuona kuwa Yehova ni mwema.’ Kwa sababu ya baraka zake, ninajisikia kuwa na deni lake na ninachochewa kufanya mengi katika kazi yake, na hilo linaniletea baraka zaidi.”

8 Muandikaji mumoja wa zaburi alisema hivi: ‘Muonje muone ya kuwa Yehova ni mwema.’ Aliongeza hivi: ‘Wale wanaomutafuta Yehova, hawatakosa chochote chema [kizuri].’ (Soma Zaburi 34:8-10.) Kwa kweli, wakati tunatumikia Yehova kwa nguvu zetu zote, tunajisikia wenye furaha kabisa kwa sababu tunajua kama tunafanya mambo yenye kumupendeza. Naye atatimiza ahadi yake ya kutuhangaikia.

USICHOKE

9, 10. Sababu gani unaona kama kungojea kwa uvumilivu ni jambo la maana?

9 Tunaweza kuwa na tamaa ya kufanya mengi katika kazi ya Yehova. Lakini, tutafanya nini ikiwa tumengojea kwa wakati murefu hali zetu zibadilike ao pendeleo fulani katika kutaniko? Inaweza kuwa muzuri tuvumilie. (Mika 7:7) Na hata kama Yehova anaweza kuruhusu hali yetu iendelee, tunaweza kuwa hakika kama atatutegemeza sikuzote. Mufano wa Abrahamu unaweza kutufundisha jambo fulani. Yehova alimuahidi kama angekuwa na mutoto, lakini alipaswa kungojea kwa miaka mingi mupaka siku Isaka alizaliwa. Katika wakati huo, Abrahamu alivumilia na hakupoteza hata kidogo imani yake kwa Yehova.—Mwanzo 15:3, 4; 21:5; Waebrania 6:12-15.

10 Kwa kweli, haiko vyepesi kungojea. (Methali 13:12) Lakini ikiwa tunaendelea kufikiri juu ya hali yetu na juu ya namna tunavunjika moyo, tutajisikia mubaya sana. Kuliko kufanya hivyo, tunaweza kutumia wakati huo ili kukomalisha zaidi sifa zenye tutakuwa nazo lazima ili kutimiza mapendeleo fulani katika kutaniko.

Kufikiri sana juu ya mambo yenye unasoma kunaweza kukusaidia ukuwe na hekima, na ufanye maamuzi ya muzuri

11. Ni sifa gani za kiroho zenye tunaweza kujikaza sana kukomalisha, na sababu gani sifa hizo ni za maana?

11 Komalisha sifa na uwezo mbalimbali wenye uko nao lazima. Kusoma Biblia na kufikiri sana juu ya mambo yenye unasoma kunaweza kukusaidia ukuwe na hekima, ujifunze kufikiri na kutumia akili, na kufanya maamuzi ya muzuri. Kwa kweli, ndugu wako na lazima ya sifa na uwezo wa namna hiyo ili kuhangaikia kutaniko. (Methali 1:1-4; Tito 1:7-9) Wakati tunajifunza Biblia, tunaweza kujua mawazo ya Yehova juu ya mambo mbalimbali. Kisha, kila siku tunaweza kutumia mambo yenye tunajifunza ili kukamata maamuzi yenye kumupendeza. Kwa mufano, tutajua namna ya kutendea wengine, namna ya kutumia feza, na namna ya kuchagua manguo na mambo ya kujifurahisha.

12. Namna gani ndugu na dada katika kutaniko wanaweza kuonyesha kuwa ni wenye kutumainika?

12 Tumika kwa bidii kila kazi yenye unapewa. Wakati watu wa Mungu walikuwa wanajenga upya hekalu, Nehemia alikuwa na lazima ya wanaume wenye angepatia daraka la kusimamia kazi mbalimbali. Alichagua wale wenye walikuwa na sifa za muzuri. Alijua kama wanaume hao walikuwa wanapenda Mungu na kama wangetumika kwa bidii kila kazi yenye wangepewa. (Nehemia 7:2; 13:12, 13) Vilevile leo, wale wenye kuwa waaminifu na wenye kutumika kwa bidii watakuwa na sifa za muzuri na wanaweza kupewa madaraka zaidi. (1 Wakorintho 4:2) Kwa hiyo, sisi wote, ni kusema, ndugu ao dada, tunapaswa sikuzote kufanya kwa bidii kila kazi yenye tunapewa.—Soma 1 Timotheo 5:25.

13. Namna gani unaweza kufuata mufano wa Yosefu wakati wengine wanakutendea mubaya?

13 Tegemea Yehova. Unaweza kufanya nini ikiwa wengine wanakutendea mubaya? Unaweza kuwaambia namna unajisikia. Lakini kama unaendelea kujitetea na kukazia kama hauna kosa, unaweza kufanya hali ikuwe mubaya zaidi. Mufano wa Yosefu unaweza kutufundisha mambo mengi. Ndugu zake walimutendea mubaya. Watu walimusemea uongo, na akafungwa katika gereza kwa sababu ya kosa lenye hakufanya. Lakini Yosefu alimutegemea Yehova. Alifikiri juu ya ahadi za Yehova, na alibakia muaminifu. (Zaburi 105:19) Katika wakati huo wa magumu, alikomalisha sifa nyingi za muzuri zenye zilimusaidia wakati alipewa kazi ya maana ya kufanya. (Mwanzo 41:37-44; 45:4-8) Ikiwa wengine wamekutendea mubaya, usali kwa Yehova akupatie hekima. Atakusaidia ubakie kimya na uzungumuze nao kwa heshima.—Soma 1 Petro 5:10.

FANYA MAENDELEO KATIKA KAZI YA KUHUBIRI

14, 15. (a) Sababu gani tunapaswa ‘kuangalia daima’ namna yetu ya kuhubiri? (b) Namna gani unaweza kufanya mabadiliko kulingana na hali? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii na kisanduku “ Uko Tayari Kupima Njia Ingine?”)

14 Mutume Paulo alimuambia Timotheo afanye maendeleo katika namna yake ya kufasiria Maandiko. Alimuambia hivi: “Jiangalie daima [sikuzote] wewe mwenyewe na kufundisha kwako.” (1 Timotheo 4:13, 16) Timotheo alikuwa amefanya kazi ya kuhubiri kwa miaka mingi. Sasa, sababu gani alipaswa kufanya maendeleo? Timotheo alijua kama watu wanabadilika na hali zinabadilika pia. Kwa sababu alipenda watu waendelee kumusikiliza, alipaswa kufanya maendeleo na kubadilisha namna yake ya kufundisha. Wakati tunaendelea kuhubiri leo, tunapaswa pia kufanya hivyo.

15 Katika maeneo fulani, hatupate watu wengi nyumbani wakati tunahubiri nyumba kwa nyumba. Katika maeneo mengine, watu wanaweza kuwa nyumbani, lakini hatuwezi kuonana nao, pengine kwa sababu hatuwezi kufika katika nyumba kwenye wanaishi. Ikiwa hali iko hivyo katika eneo lenu, unaweza kupima njia ingine ili kupata watu?

16. Namna gani kuhubiri mahali pa watu wengi kunaweza kuwa na matokeo ya muzuri?

16 Ndugu na dada wengi wanafurahia kuhubiria watu mahali pa watu wengi. Kwa mufano, wanaenda kwenye nafasi za kungojea treni ao bisi, kwenye masoko, na kwenye bustani za watu wote (parcs) ili kutafuta watu wa kuhubiria. Shahidi wa Yehova anaweza kuanzisha mazungumuzo na mutu juu ya habari fulani ya hivi karibuni yenye ilitangazwa katika vyombo vya habari. Ao Shahidi anaweza kusema jambo fulani la muzuri juu ya watoto wa mutu huyo ao kumuuliza ulizo juu ya kazi yake. Ikiwa mutu huyo anaonekana kuwa anafurahia mazungumuzo, muhubiri anaweza kusema jambo fulani juu ya Biblia na kumuuliza mawazo yake. Mara nyingi, watu wanapenda kujua mengi juu ya Biblia.

17, 18. (a) Ni nini inaweza kukusaidia usiogope kuhubiri mahali pa watu wengi? (b) Sababu gani unaona kama maneno yenye Daudi alisema juu ya kumusifu Yehova yanaweza kukusaidia wakati unahubiri?

17 Pengine unaona kuwa ni vigumu kuanzisha mazungumuzo kwenye barabara pamoja na watu wenye haujue. Eddie, painia mumoja katika New York City, alikuwa na magumu hayo. Lakini alipata jambo fulani lenye lilimusaidia kumaliza uoga. Anasema hivi: “Wakati wa ibada yetu ya familia, mimi na bibi yangu tunatafuta habari ili kujua namna ya kujibia vizuia-mazungumuzo na mawazo yenye watu wanatoa. Pia tunaomba mashauri kwa Mashahidi wengine.” Sasa, Eddie anafurahia kuhubiri mahali pa watu wengi.

18 Wakati tunafurahia sana kazi ya kuhubiri na tunakomalisha ufundi wetu wa kuhubiria watu habari njema, wengine wataona maendeleo yetu. (Soma 1 Timotheo 4:15.) Ikiwa tunafanya hivyo, tunaweza hata kusaidia mutu fulani akuwe mutumishi wa Yehova. Daudi alisema hivi: ‘Nitamubariki Yehova nyakati zote; daima sifa yake itakuwa katika kinywa changu. Nafsi yangu itajisifu katika Yehova; wapole watasikia na kushangilia.’—Zaburi 34:1, 2.

ENDELEA KUMUSIFU YEHOVA KWA KUFANYA MAENDELEO YA KIROHO

19. Sababu gani mutumishi muaminifu wa Yehova anaweza kuwa na furaha hata kama hali yake haimuruhusu kufanya mambo mengi?

19 Daudi alisema tena hivi: “Kazi zako zote zitakusifu, Ee Yehova, na washikamanifu wako watakusifu. Wataongea juu ya utukufu wa ufalme wako, nao watasema juu ya nguvu zako, kuwajulisha wana wa binadamu matendo yake yenye nguvu na utukufu wa fahari ya ufalme wake.” (Zaburi 145:10-12) Wale wote wenye kumupenda Yehova na wenye kuwa washikamanifu kwake wanapenda sana kuhubiria wengine juu yake. Lakini, itakuwa namna gani ikiwa kwa sababu ya ugonjwa ao uzee, hauwezi tena kupitisha wakati mwingi wenye ungependa kupitisha katika kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba? Sikuzote ukumbuke kama unamusifu Yehova kila wakati unahubiria wanganga na watu wengine wenye kutumika katika hopitali. Ikiwa unafungwa katika gereza kwa sababu ya imani yako, unaweza kuwa na nafasi ya kuzungumuza na wengine juu ya Yehova, na kufurahisha moyo wake. (Methali 27:11) Pia, Yehova anafurahi sana ikiwa unaendelea kumutumikia hata kama wengine katika familia yako hawamutumikie. (1 Petro 3:1-4) Hata kama uko katika hali ngumu zaidi, unaweza kumusifu Yehova, kuendelea kumukaribia zaidi, na kufanya maendeleo ya kiroho.

20, 21. Ikiwa umepewa kazi nyingi ya kufanya katika kutaniko la Yehova, namna gani unaweza kuwa baraka kwa wengine?

20 Yehova atakubariki kabisa ikiwa unaendelea kumukaribia zaidi na kumutumikia kwa nguvu zako zote. Pengine ikiwa unafanya mabadiliko fulani katika maisha ao katika programu yako, utapata nafasi nyingi zaidi za kusaidia watu wajifunze juu ya ahadi za muzuri sana za Mungu. Unaweza pia kusaidia ndugu na dada zako hata zaidi. Na ufikirie namna ndugu na dada watakupenda zaidi wakati wanaona namna unatumikia kutaniko kwa bidii.

21 Hata kama tumemutumikia Yehova kwa miaka mingi ao hapana, sisi wote tunaweza kuendelea kumukaribia zaidi na kufanya maendeleo ya kiroho. Katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia namna tunaweza kusaidia wengine wafanye maendeleo ya kiroho.