Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Muvalio Wako Unamutukuza Mungu?

Muvalio Wako Unamutukuza Mungu?

‘Mufanye mambo yote kwa utukufu wa Mungu.’—1 WAKORINTHO 10:31.

NYIMBO: 34, 61

1, 2. Sababu gani Mashahidi wa Yehova wanafuata kanuni zenye kufaa juu ya muvalio? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

GAZETI moja katika inchi ya Uholanzi (Pays-Bas) lilieleza namna viongozi wa dini walivaa kwenye mukutano wao mumoja. Lilisema hivi: “Wengi walivaa nguo za ovyoovyo, zaidi sana wakati wa joto.” Lakini gazeti lilelile lilisema kama Mashahidi wa Yehova hawakuvaa hivyo kwenye mukusanyiko wao. Lilisema kama vijana wanaume na wanaume wazima walivaa koti na kravate na vijana wanawake na wanawake wazima walivaa jupes zenye zilikuwa na urefu wenye kufaa, lakini za sasa. Mara nyingi watu wanasifu Mashahidi wa Yehova juu ya muvalio wao. Mutume Paulo alisema kama nguo zenye Wakristo wanavaa zinapaswa kuonyesha “kiasi na utimamu wa akili [akili ya muzuri],” wenye kufaa watumishi wa Mungu. (1 Timotheo 2:9, 10) Hata kama Paulo alikuwa anazungumuzia wanawake, kanuni hiyo inatumika pia kwa wanaume Wakristo.

2 Kwa sababu tuko watu wa Yehova, kanuni za muzuri juu ya muvalio ni za maana kwetu, na Mungu mwenye tunaabudu anaziona kuwa za maana. (Mwanzo 3:21) Biblia inaonyesha wazi kama Yehova, Mutawala wa Ulimwengu Wote, ameweka kanuni juu ya namna anapenda watumishi wake wavae. Kwa hiyo, nguo zenye tunachagua kuvaa hazipaswe tu kutupendeza sisi wenyewe, lakini jambo la maana zaidi, zinapaswa kupendeza Yehova, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi.

3. Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli juu ya muvalio inaweza kutufundisha nini?

3 Sheria ya Musa ilikuwa na amri mbalimbali zenye zililinda Waisraeli ili wasijiingize katika mwenendo mubaya wa watu wa mataifa yenye yalikuwa yanawazunguka. Sheria hiyo ilionyesha kama Yehova anachukia sana nguo zenye hazikuonyesha waziwazi tofauti kati ya mwanaume na mwanamuke. Leo pia, kuko nguo za namna hiyo. (Soma Kumbukumbu la Torati 22:5.) Sheria hiyo inatuonyesha kama Yehova anachukia nguo zenye kufanya mwanaume aonekana kuwa mwanamuke, ao mwanamuke aonekane kuwa mwanaume, ao zenye kufanya ikuwe vigumu kuona tofauti kati ya mwanaume na mwanamuke.

4. Ni nini inaweza kusaidia Wakristo wakamate maamuzi ya muzuri juu ya muvalio?

4 Kanuni za Biblia zinaweza kutusaidia tukamate maamuzi ya muzuri juu ya muvalio wetu. Kanuni hizo zinatumika kwa watu wa inchi zote, desturi zote, na hali zote za hewa. Hatuna lazima ya liste ndefu yenye kuonyesha nguo zenye tunapaswa kuvaa na zenye hatupaswe kuvaa. Tunapaswa tu kufuata kanuni za Maandiko, lakini kanuni hizo zinaturuhusu kuvaa nguo zenye tunapenda. Tuzungumuzie basi kanuni fulani za Biblia zenye zinaweza kutusaidia kujua “mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu,” wakati tunachagua nguo zenye tutavaa.—Waroma 12:1, 2.

TUNAONYESHA KUWA TUKO WATUMISHI WA MUNGU

5, 6. Muvalio wetu unaweza kuwa na matokeo gani juu ya wengine?

5 Roho ya Mungu ilimuongoza mutume Paulo kuandika kanuni ya maana yenye kupatikana katika 2 Wakorintho 6:4. (Soma.) Namna tunaonekana inaonyesha sisi ni watu wa namna gani, na hilo linafanya watu wengi wakuwe na wazo fulani juu yetu. (1 Samweli 16:7) Sisi watumishi wa Mungu, hatupaswe kuvaa nguo kwa sababu tu inafanya tujisikie muzuri ao kwa sababu tunaipenda. Wakati tunatumikisha kanuni za Biblia, zinapaswa kutusaidia kuepuka kuvaa nguo zenye kubana sana mwili, zenye kuacha mwili wazi ao zenye kuamusha tamaa ya ngono. Ni kusema kama hatupaswe kuvaa nguo yenye kuonyesha wazi sehemu za siri za mwili. Hatupaswe kufanya mutu yeyote ajisikie mubaya ao alazimike kuangalia pembeni kwa sababu ya muvalio wetu.

Wakati tunaonekana muzuri, tuko safi, tunajipamba muzuri na tunavaa nguo zenye kiasi, watu wanaweza kutuheshimia sana kwa sababu tuko watumishi wa Yehova, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi

6 Wakati tunaonekana muzuri, tuko safi, tunajipamba muzuri na tunavaa nguo zenye kiasi, watu wanaweza kutuheshimia sana kwa sababu tuko watumishi wa Yehova, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi. Pia, wanaweza kupendezwa zaidi na Mungu mwenye tunaabudu, wataheshimia zaidi tengenezo letu, na wanaweza kabisa kusikiliza ujumbe wetu wenye kuokoa uzima.

7, 8. Tunapaswa kuvaa nguo zenye kufaa zaidi sana wakati gani?

7 Tunapaswa kuvaa kwa njia yenye kuletea Yehova heshima na ujumbe wenye tunahubiri; kwa sababu muvalio wetu unaweza kuchukiza ao kupendeza Mungu wetu mutakatifu, ndugu na dada zetu, na watu wa eneo letu. (Waroma 13:8-10) Tunapaswa kuchunguza muvalio wetu zaidi sana wakati tunaenda kwenye mikutano yetu ya Kikristo ao katika mahubiri. Tunapaswa kuvaa kwa njia yenye kuonyesha kama tuko watumishi wa Mungu. (1 Timotheo 2:10) Kwa kweli, nguo fulani zinaweza kuwa zenye kufaa mahali fulani lakini hazifae mahali pengine. Kwa hiyo, hata kama tunaishi wapi, kwa sababu tuko Mashahidi wa Yehova, tunapaswa kuepuka kukwaza wengine kupitia muvalio wetu.

Muvalio wako utafanya wengine waheshimie Mungu mwenye unatumikia? (Picha hii inapatana na fungu la 7, 8)

8 Soma 1 Wakorintho 10:31. Wakati tunaenda kwenye mikusanyiko, nguo zetu zinapaswa kuwa zenye kufaa na zenye kiasi. Hatupaswe kuiga mivalio yenye kupita mipaka yenye kuenea katika ulimwengu huu. Hata mbele ao kisha mukusanyiko, na hata wakati tunafika kwenye hoteli ao wakati tunaondoka, tunapaswa kuhakikisha kama hatuvae nguo za ovyoovyo. Wakati tunavaa muzuri, hatutasikia haya ya kuambia watu kama tuko Mashahidi wa Yehova, na tutakuwa tayari kuhubiri wakati wowote.

9, 10. Sababu gani andiko la Wafilipi 2:4 linaweza kutusaidia kuchagua nguo zetu?

9 Soma Wafilipi 2:4. Sababu gani tunapaswa kufikiria matokeo yenye muvalio wetu unaweza kuwa nayo juu ya ndugu na dada zetu? Sababu moja ni kwamba watu wa Mungu wanajikaza sana ili kufuata shauri hili: ‘Muue viungo vya mwili wenu vilivyo duniani kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngono, tamaa yenye mazara [tamaa ya mubaya].’ (Wakolosai 3:2, 5) Ndugu na dada zetu fulani waliachana na mwenendo wa uasherati, na pengine wangali wanapiganisha tamaa za mubaya. Ikiwa hatuko waangalifu, muvalio wetu unaweza kufanya ikuwe vigumu zaidi kwao kufuata mashauri ya Biblia na kupiganisha tamaa hizo. (1 Wakorintho 6:9, 10) Hatupendi kufanya ikuwe vigumu kwa ndugu na dada zetu kupiganisha tamaa za mubaya.

10 Wakati tuko pamoja na ndugu na dada zetu, tunaepuka kuambukizwa na watu wenye kuchochea mwenendo muchafu. Namna tunavaa inapaswa kufanya hali hiyo ikuwe safi zaidi, ikuwe tuko kwenye mukutano ao mahali pengine. Tuko na uhuru wa kuchagua nguo zenye tutavaa. Lakini tuko pia na daraka la kuvaa nguo zenye zitafanya ikuwe vyepesi kwa wengine kulinda mawazo yao, maneno, na mwenendo wao kuwa safi mbele za Mungu. (1 Petro 1:15, 16) Upendo wa kweli ‘haujiendeshe bila adabu, hautafute faida zake wenyewe.’—1 Wakorintho 13:4, 5.

NGUO ZENYE KUFAA KWA WAKATI NA MAHALI PENYE KUFAA

11, 12. Namna gani andiko la Mhubiri 3:1, 17 linatusaidia kuwa wenye kiasi?

11 Wakati watumishi wa Mungu wanachagua nguo za kuvaa, wanajua kama “kuna wakati wa kila jambo na kuhusu kila kazi.” (Mhubiri 3:1, 17) Muvalio wetu unaweza kutegemea hali za hewa, majira, na hali zingine mbalimbali. Lakini kanuni za Yehova hazibadilike hata siku moja.—Malaki 3:6.

Kanuni za Yehova hazibadilike hata siku moja

12 Wakati wa joto, ni vigumu zaidi kuhakikisha ikiwa tunavaa nguo zenye kuleta heshima na zenye kiasi. Tunafurahisha ndugu na dada zetu wakati tunaepuka kuvaa nguo zenye kuonyesha sehemu za siri za mwili kwa sababu ni zenye kutubana ao zenye kuachilia sana mwili. (Ayubu 31:1) Pia, wakati tunaenda kuogelea kwenye bahari ao kwenye kisima, nguo zetu za kuogelea zinapaswa kuwa zenye kiasi. (Methali 11:2, 20) Hata kama watu wengi katika dunia wanavaa nguo za kuogelea zenye kuacha wazi sehemu za siri za mwili, tunapaswa kuhakikisha kuwa nguo zetu za kuogelea zinamutukuza Yehova, Mungu wetu mutakatifu.

13. Sababu gani shauri lenye kupatikana katika andiko la 1 Wakorintho 10:32, 33 linaweza kutusaidia kuchagua nguo zetu?

13 Kuko kanuni ingine ya maana sana yenye inaweza kutusaidia kuchagua nguo zetu. Tunapaswa kuwa waangalifu ili tusikwaze zamiri ya wengine. (Soma 1 Wakorintho 10:32, 33.) Tunapaswa kuepuka nguo zenye zinaweza kukwaza ndugu na dada zetu na pia watu wenye hawatumikie Yehova. Mutume Paulo aliandika hivi: ‘Kila mumoja wetu na amupendeze jirani yake katika yaliyo mema kwa ajili ya kujengwa kwake.’ Paulo alionyesha sababu. Alisema hivi: “Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe.” (Waroma 15:2, 3) Kama Yesu, tunapaswa kuona kuwa jambo la maana sana kwetu ni kufanya mapenzi ya Mungu na kusaidia wengine kuliko kujipendeza sisi wenyewe. Kwa hiyo, hatutavaa nguo zenye tunapenda tu lakini zenye zinaweza kufanya watu wakatae kusikiliza ujumbe wetu.

14. Namna gani wazazi wanaweza kufundisha watoto wao wamutukuze Mungu kupitia muvalio wao?

14 Wazazi Wakristo wako na daraka la kufundisha watoto wao kufuata kanuni za Biblia. Hilo linamaanisha pia kuhakikisha kama wao na watoto wao wanafurahisha Mungu kwa kuvaa na kujipamba kwa kiasi. (Methali 22:6; 27:11) Namna gani wazazi wanaweza kufundisha watoto wao kuheshimia Mungu wetu mutakatifu na kanuni zake? Wazazi wanapaswa kuwa mufano muzuri kwa watoto wao. Na wanapaswa kufundisha watoto wao kwa upendo namna na mahali kwenye wanaweza kupata nguo zenye kufaa. Watoto hawapaswe kuchagua nguo kwa sababu tu wanazipenda, lakini jambo la maana sana, wanapaswa kuchagua nguo zenye kumutukuza Yehova, Mungu mwenye wanatumikia.

TUMIA UHURU WAKO KWA HEKIMA

15. Ni nini inaweza kutusaidia tukamate maamuzi ya muzuri?

15 Biblia inatoa muongozo wenye kufaa ambao unaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya hekima yenye yatamutukuza Mungu. Lakini kila mutu iko na aina ya nguo zenye anapendaka. Nguo zenye tunapenda na zenye tuko na uwezo wa kuuza zinaweza kuwa tofauti na za wengine. Lakini sikuzote, nguo zetu zinapaswa kuonekana muzuri, safi, zenye kiasi, zenye kupatana na hali, na mahali kwenye tunaishi.

16. Sababu gani ni jambo la maana tujikaze kuvaa muzuri?

16 Haiko vyepesi kupata kila wakati nguo zenye kiasi na zenye kufaa. Nguo zenye kuuzishwa nafasi nyingi ni zile zenye watu wengi wanapenda. Kwa hiyo, inaweza kuomba wakati na bidii ili kupata nguo kama vile jupes, kanzu, ao kuchagua koti na pantalons zenye kiasi na zenye hazibane sana mwili. Lakini ndugu na dada wataona na kufurahia bidii yenye tunafanya ili kuvaa nguo zenye kupendeza na zenye kufaa. Na furaha yenye tunapata wakati tunamutukuza Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo ni ya maana zaidi kuliko jambo lolote lenye tunajinyima ili tuvae kwa njia yenye kumuletea utukufu.

17. Ni nini inaweza kusaidia ndugu ajue ikiwa atakomalisha ndevu ao kuzikata?

17 Ni jambo lenye kufaa ndugu wakomalishe ndevu? Sheria ya Musa iliomba wanaume wakomalishe ndevu. Lakini, Wakristo hawaongozwe na Sheria ya Musa na hawalazimishwe kuifuata. (Mambo ya Walawi 19:27; 21:5; Wagalatia 3:24, 25) Katika desturi fulani, ndevu zenye kutunzwa muzuri zinakubaliwa na zinaleta heshima, na haziwezi kuzuia hata kidogo watu kusikiliza ujumbe wetu. Kwa kweli, ndugu fulani wenye kuwa na madaraka wako na ndevu. Hata hivyo, ndugu fulani wanaweza kuamua kukata ndevu. (1 Wakorintho 8:9, 13; 10:32) Katika desturi zingine ao maeneo mengine, wanaume hawazoee kuacha ndevu, na ndevu hazikubalike kwa Mashahidi wa Yehova. Katika desturi hizo, kukomalisha ndevu kunaweza kufanya ndugu akose kumuletea Mungu utukufu na akuwe mwenye ‘kulaumika.’—1 Timotheo 3:2, 7; Waroma 15:1-3.

18, 19. Andiko la Mika 6:8 linatusaidia namna gani?

18 Tuko wenye shukrani sana kwa Yehova kwa sababu hatupatie liste ya nguo na namna za kujipamba zenye zinakubalika na zenye hazikubalike. Lakini, amepatia kila mutu uhuru wa kukamata maamuzi yenye hekima yenye kutegemea kanuni za Biblia. Kwa hiyo, hata wakati tunachagua nguo na namna tutajipamba, tunaweza kuonyesha kama tunapenda kuwa na kiasi kwa sababu tuko watumishi wa Mungu.—Mika 6:8.

19 Tunakubali kwa unyenyekevu kama Yehova ni safi na ni mutakatifu na kama kanuni zake zinatutolea muongozo muzuri zaidi. Ikiwa tunataka kuwa wenye kiasi na wanyenyekevu, tutafuata kanuni zake katika maisha yetu. Kuwa na kiasi kutatusaidia pia tusikwaze wengine na tuheshimie mawazo yao.

20. Muvalio wetu na namna tunajipamba vinaweza kuwa na matokeo gani juu ya wengine?

20 Muvalio wetu unapaswa kuonyesha waziwazi kama tuko watumishi wa Yehova. Kanuni za Yehova ni za juu sana, na tunafurahi kabisa kuzifuata. Ndugu na dada wengi wanastahili pongezi kwa sababu ya mwenendo wao muzuri na namna wanaonekana. Hilo linafanya watu wenye mioyo mizuri wapendezwe na ujumbe wa Biblia wenye kuokoa uzima na wanamuletea Yehova furaha na utukufu. Wakati tunakamata maamuzi ya muzuri juu ya muvalio wetu, tutaendelea kumuletea utukufu Yule mwenye kuvaa “utukufu na fahari [heshima].”—Zaburi 104:1, 2.