Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Usiache ‘Mikono Yako Iregee’

Usiache ‘Mikono Yako Iregee’

‘Mikono yako isiregee.’—SEFANIA 3:16.

NYIMBO: 81, 32

1, 2. (a) Watu wengi wanapatwa na magumu gani leo, na hilo linaleta matokeo gani? (b) Andiko la Isaya 41:10, 13 linatoa tumaini gani lenye kuwa hakika?

 DADA mumoja painia wa kawaida mwenye kuolewa na muzee alisema hivi: “Hata kama ninaendelea kuwa na programu ya muzuri ya kiroho, nimepiganisha mahangaiko kwa miaka mingi. Mahangaiko hayo yanafanya nikose usingizi, yanaharibisha afya yangu, yanabadilisha namna yangu ya kutendea wengine, na wakati fulani yananifanya nikuwe karibu kuvunjika moyo.”

2 Unaweza kumuelewa dada huyo? Jambo la kuhuzunisha ni hili: Tunapata magumu mengi kwa sababu tunaishi katika ulimwengu wa Shetani. Na kama vile nanga inasimamishaka mashua nafasi moja, mahangaiko yanaweza kutufanya tujisikie kuwa tunabeba muzigo muzito ao wenye kuvunjika moyo. (Methali 12:25) Ni nini inaweza kukuletea mahangaiko? Pengine uko na huzuni kwa sababu mutu fulani mwenye unapenda amekufa ao unavumilia ugonjwa hatari ao unateswa kwa sababu ya imani yako. Ao pengine unajikaza kuhangaikia familia yako katika hali ngumu ya kukosa feza. Kadiri wakati unapita, mahangaiko katika moyo wako yanaweza kukufanya ukuwe zaifu na hata upoteze furaha yako. Lakini, unaweza kuwa hakika kama Mungu ni tayari kukusaidia kabisa.—Soma Isaya 41:10, 13.

3, 4. (a) Namna gani Biblia inatumia neno ‘mukono’? (b) Ni nini inaweza kufanya mikono yetu iregee?

3 Mara nyingi Biblia inatumia sehemu za mwili ili kuzungumuzia sifa mbalimbali za mutu ao matendo yake. Kwa mufano, mukono unazungumuziwa mara nyingi sana. Wakati Biblia inasema kama mikono ya mutu fulani inatiwa nguvu, ni kusema kama mutu huyo ametiwa moyo, ni mwenye nguvu, na iko tayari kutenda. (1 Samweli 23:16; Ezra 1:6) Hilo linaweza pia kumaanisha kama mutu huyo ana mawazo ya muzuri na ana tumaini la wakati unaokuja.

4 Wakati mwengine Biblia inaweza kuzungumuzia mutu mwenye anaregeza mikono yake. Hilo linamaanisha mutu mwenye kuvunjika moyo ao mwenye kupoteza tumaini. (2 Mambo ya Nyakati 15:7; Waebrania 12:12) Wakati uko na mahangaiko ao unachoka ao unajisikia kuwa urafiki wako pamoja na Yehova unaanza kuwa zaifu sana, unaweza kuwa karibu kuvunjika moyo. Ni nini inaweza kukutia moyo? Ni nini inaweza kukuchochea na kukutia nguvu ili uvumilie na usipoteze furaha?

MUKONO WA YEHOVA HAUKO MUFUPI SANA ILI USHINDWE KUOKOA

5. (a) Wakati tuko na magumu, tunaweza kujisikia namna gani, lakini tunapaswa kukumbuka nini? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

5 Soma Sefania 3:16, 17. Wakati tuko na magumu, hatupaswe kuogopa na kuvunjika moyo, ao kuacha mikono yetu iregee. Yehova, Baba yetu mwenye upendo, anatuomba tumutupie mahangaiko yetu yote. (1 Petro 5:7) Yehova anatuhangaikia kama vile alihangaikia Waisraeli. Aliwaambia kama mukono wa wake ‘haujakuwa mufupi mno [sana] kwamba usiweze kuokoa.’ Sikuzote, Yehova ni tayari kuokoa watumishi wake washikamanifu. (Isaya 59:1) Katika habari hii, tutazungumuzia mifano tatu ya muzuri sana yenye kupatikana katika Biblia. Mifano hiyo inaonyesha kama Yehova anapenda sana kutia watu wake nguvu ili wafanye mapenzi yake hata kama wako na magumu makali, na ana uwezo wa kufanya hivyo. Tuone basi namna mifano hiyo inaweza kukutia nguvu.

6, 7. Ushindi wa Waisraeli juu ya Waamaleki unaweza kutufundisha nini?

6 Muda mufupi kisha tu Waisraeli kukombolewa katika utumwa wa Misri, Waamaleki waliwashambulia. Musa aliambia Yoshua, mwanaume mwenye ujasiri, aongoze Waisraeli katika vita. Kisha Musa alienda pamoja na Haruni na Huru kwenye kilima chenye kilikuwa karibu. Huko, wangeweza kuona uwanja wa vita. Wanaume hao watatu walikimbilia kwenye kilima kwa sababu waliogopa? Hapana kabisa!

7 Musa alifuata mupango wenye ulisaidia Waisraeli wapate ushindi juu ya Waamaleki. Alikamata fimbo ya Mungu wa kweli katika mikono yake na akainyoosha juu mbinguni. Wakati Musa alifanya hivyo, Yehova alipatia Waisraeli nguvu ya kupigana na Waamaleki. Lakini, wakati mikono ya Musa ilikuwa mizito na kuanza kuregea, Waamaleki walianza kupata ushindi. Haruni na Huru walifanya haraka ili kusaidia Musa. ‘Walichukua jiwe wakaliweka chini yake, naye akalikalia; naye Haruni na Huru wakaitegemeza mikono yake, mumoja upande huu na yule mwingine upande ule, hivi kwamba mikono yake ikakuwa imara mupaka jua lilipotua [kushuka].’ Kwa kweli, Waisraeli walipata ushindi katika vita hiyo kwa sababu ya mukono wa Mungu wenye nguvu.—Kutoka 17:8-13.

8. (a) Asa alifanya nini wakati Waethiopia waliogopesha Yuda? (b) Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Asa?

8 Yehova alikuwa pia tayari kutumia mukono wake wenye nguvu ili kusaidia watu wake katika siku za Mufalme Asa. Biblia inazungumuzia majeshi mengi, lakini jeshi kubwa sana lilikuwa la Zera Muethiopia, mwenye alikuwa na maaskari 1000000 wenye uzoefu. Jeshi la Waethiopia lilikuwa kubwa karibu mara mbili kupita jeshi la Asa. Lakini, Asa alihangaika, aliogopa, ao kuvunjika moyo? Aliacha mikono yake iregee? Hapana! Bila kukawia, alimuomba Yehova musaada. Kulingana na ufundi wa kijeshi wa kupigana vita, haingewezekana kabisa kupata ushindi katika vita juu ya Waethiopia. “Lakini kwa Mungu mambo yote yanawezekana.” (Mathayo 19:26) Mungu alitumia uwezo wake na “akawashinda Waethiopia mbele ya Asa,” mwenye ‘moyo wake ulikuwa mukamilifu kwa Yehova siku zake zote.’—2 Mambo ya Nyakati 14:8-13; 1 Wafalme 15:14.

9. (a) Ni nini haikuzuia Nehemia kujenga tena kuta za Yerusalemu? (b) Namna gani Mungu alijibu sala ya Nehemia?

9 Wakati Nehemia alienda Yerusalemu, aliona nini? Aliona kuwa maadui wenye walitoka katika inchi za kigeni walikuwa wanaogopesha Wayahudi, na hilo lilifanya Wayahudi waache kujenga kuta za Yerusalemu. Muji haukukuwa na ulinzi, na Wayahudi walivunjika moyo. Nehemia alijisikia namna gani? Alivunjika moyo pia na kuacha mikono yake iregee? Hapana! Kama vile Musa, Asa, na watumishi wengine waaminifu wa Yehova, Nehemia alimutegemea Yehova sikuzote. Pia, katika hali hiyo, Nehemia alisali Yehova amusaidie, na Yehova alijibu sala yake. Mungu alitumia ‘uwezo wake mukubwa’ na ‘mukono wake wenye nguvu’ ili kutia nguvu Wayahudi. (Soma Nehemia 1:10; 2:17-20; 6:9.) Unaamini kuwa Yehova anatumia ‘uwezo wake mukubwa’ na ‘mukono wake wenye nguvu’ leo ili kutia nguvu watumishi wake?

YEHOVA ATATIA NGUVU MIKONO YAKO

10, 11. (a) Namna gani Shetani anajikaza ili kufanya mikono yetu iregee? (b) Yehova anatumia nini ili kututia nguvu? (c) Mafundisho yenye Yehova anatutolea yamekuletea faida gani?

10 Tujue kama Shetani hataacha hata kidogo mikono yake iregee. Ataendelea kutushambulia ili kufanya tuache kumutumikia Mungu. Anatumia serikali, viongozi wa dini, na waasi-imani ili kutuogopesha na kueneza uongo juu yetu. Kusudi lake ni nini? Anapenda tuache kuhubiri habari njema ya Ufalme. Lakini Yehova anapenda kutusaidia na ana uwezo wa kufanya hivyo, anatupatia roho yake takatifu ili kututia nguvu. (1 Mambo ya Nyakati 29:12) Ni jambo la maana sana tumuombe Mungu roho yake ili tuweze kupiganisha Shetani na ulimwengu wake muovu. (Zaburi 18:39; 1 Wakorintho 10:13) Pia, tuko wenye shukrani kwa Mungu kwa ajili ya musaada wenye tunapata katika Neno lake. Fikiria pia habari nyingi zenye tunajifunza katika vichapo vyetu kila mwezi. Maneno ya andiko la Zekaria 8:9, 13 (soma) yalisemwa wakati hekalu la Yerusalemu lilikuwa linajengwa upya, lakini maneno hayo yanaweza kutusaidia leo.

Ni jambo la maana sana tumuombe Mungu roho yake ili tuweze kupiganisha Shetani na ulimwengu wake muovu

11 Pia, Yehova anatutia nguvu kupitia mafundisho yenye tunapata kwenye mikutano yetu ya Kikristo, kwenye mikusanyiko, na kwenye masomo mbalimbali ya kiteokrasi. Mafundisho hayo yanaweza kutusaidia tutumikie Mungu na nia ya muzuri, tujiwekee miradi, na tutimize madaraka yetu mbalimbali ya Kikristo. (Zaburi 119:32) Unapenda kabisa kupata nguvu kupitia mafundisho ya Yehova?

12. Tunapaswa kufanya nini ili tuendelee kuwa na nguvu?

12 Yehova alisaidia watu wake wapate ushindi juu ya Waamaleki na Waethiopia, na alipatia Nehemia na Wayahudi nguvu ya kujenga kuta za Yerusalemu. Sisi pia, Mungu atatupatia nguvu ya kuendelea kuhubiri hata kama tuko na mahangaiko, hata kama kuko watu wenye wanatupinga na hawapendezwe na ujumbe wetu. (1 Petro 5:10) Yehova hatafanya miujiza ili kumaliza magumu yetu. Lakini, tunapaswa kufanya mambo fulani. Ni mambo gani? Tunapaswa kusoma Neno la Mungu kila siku, kutayarisha na kuenda kwenye mikutano yetu kila juma, kuendelea kufanya funzo letu la pekee na ibada ya familia, na kumutegemea Yehova katika sala. Tusiache kitu chochote kitukengeushe ili tusikaze akili juu ya mambo yenye Yehova ametutolea ili kututia nguvu na kututia moyo. Ukiona kama mikono yako imeregea katika jambo moja kati ya mambo hayo, umuombe Yehova akusaidie. Kisha, uone namna roho ya Mungu ‘inatenda ndani yako [inakutia nguvu] ili ukuwe na nia na kutenda pia.’ (Wafilipi 2:13) Lakini, unaweza pia kutia nguvu mikono ya wengine?

UTIE NGUVU MIKONO YENYE INAWEZA KUREGEA

13, 14. (a) Namna gani ndugu mumoja alitiwa nguvu kisha kufiwa na bibi yake? (b) Namna gani tunaweza kutia wengine nguvu?

13 Katika dunia yote, Yehova anatupatia familia ya ndugu na dada wenye kutuhangaikia na wenye wanaweza kututia moyo. Mutume Paulo aliandika hivi: ‘Muinyooshe mikono inayoregea na magoti yaliyo zaifu, nanyi muendelee kuifanyia miguu yenu mapito [njia] yaliyonyooka.’ (Waebrania 12:12, 13) Ndugu na dada wengi wa wakati wa mitume walipata musaada kama huo kupitia ndugu na dada zao. Ni vile pia leo. Fikiria mufano fulani. Ndugu mumoja alifiwa na bibi yake na alivumilia hali zingine zenye kuhuzunisha. Kisha hapo alisema hivi: “Nilijifunza kama hatuwezi kuchagua majaribu yenye yatatupata, hatuwezi kuchagua wakati yatatupata ao mara ngapi yatatupata. Sala na funzo langu la pekee vimekuwa kama vile nguo yenye mutu anavaa ili asizame ndani ya maji. Na musaada wa ndugu na dada zangu wa kiroho umenitia moyo sana. Nimetambua kama ni jambo la maana mutu afanye urafiki wa muzuri pamoja na Yehova mbele hali ngumu zimufikie.”

Kila mutu katika kutaniko anaweza kutia wengine moyo (Picha hii inapatana na fungu la 14)

14 Haruni na Huru walisaidia kutia nguvu mikono ya Musa wakati walimutegemeza katika vita juu ya Waamaleki. Leo, sisi pia tunaweza kutafuta namna za kutegemeza wengine na kuwasaidia. Ndugu na dada zetu fulani wanateseka kwa sababu ya uzee, magonjwa, wanateswa na watu wa familia yao, wanajisikia kuwa pekee yao, ao mutu fulani mwenye walipenda amekufa. Tunaweza pia kutia nguvu vijana wenye mara nyingi wanakazwa wafanye mambo ya mubaya ao watafute maisha ya muzuri katika ulimwengu huu. (1 Wathesalonike 3:1-3; 5:11, 14) Tafuta namna za kuonyesha wengine kuwa unapendezwa nao wakati muko kwenye Jumba la Ufalme, katika mahubiri, wakati munakula pamoja nao, ao wakati unazungumuza nao kwenye telefone.

15. Maneno yenye kujenga yanaweza kuwa na matokeo gani juu ya ndugu na dada zetu?

15 Kisha Asa kupata ushindi mukubwa juu ya jeshi kubwa la Waethiopia, nabii Azaria alimutia moyo yeye na watu wake. Aliwaambia hivi: ‘Nanyi mukuwe hodari na musiache mikono yenu iregee, kwa sababu kuna sawabu [malipo] kwa ajili ya kazi yenu.’ (2 Mambo ya Nyakati 15:7) Maneno hayo yalimuchochea Asa afanye mabadiliko mengi ili kurudisha ibada ya kweli. Vilevile, maneno yako yenye kujenga yanaweza kutia wengine moyo na kuwasaidia waendelee kutumikia Yehova. (Methali 15:23) Na usisahau hata kidogo kama wakati unatoa maelezo yenye kutia moyo kwenye mikutano yetu, unatia nguvu ndugu na dada zako.

Nehemia hakuangalia tu wengine wakati walikuwa wanafanya kazi. Yeye pia alisaidia kujenga kuta za Yerusalemu

16. Namna gani wazee wanaweza kuiga mufano wa Nehemia? Toa mifano yenye kuonyesha namna ndugu na dada wamekusaidia.

16 Kupitia musaada wa Yehova, Nehemia na Wayahudi wenzake walitia nguvu mikono yao. Walimaliza kujenga kuta za Yerusalemu katika siku 52 tu! (Nehemia 2:18; 6:15, 16) Nehemia hakuangalia tu wengine wakati walikuwa wanafanya kazi hiyo. Yeye pia alisaidia kujenga kuta za Yerusalemu. (Nehemia 5:16) Vilevile, wazee wengi wa kutaniko wanaiga mufano wa Nehemia wakati wanasaidia katika mipango ya ujenzi ao kusafisha na kutengeneza Jumba la Ufalme. Pia, wanaume hao wenye upendo wanatia nguvu ndugu na dada wenye ‘wanahangaika moyoni’ wakati wanawatembelea na wakati wanahubiri pamoja nao.—Soma Isaya 35:3, 4.

USIACHE ‘MIKONO YAKO IREGEE’

17, 18. Wakati tuko na magumu ao mahangaiko, tunaweza kuwa hakika na jambo gani?

17 Wakati tunatumika pamoja na ndugu na dada zetu, hilo linafanya umoja wetu ukuwe wenye nguvu. Pia, hilo linatusaidia kufanya nao urafiki wa muda murefu na tunatumainia zaidi baraka zenye Ufalme wa Mungu utatuletea hivi karibuni. Wakati tunatia nguvu mikono ya wengine, tunawasaidia kuvumilia hali ngumu na kuwa na tumaini kwa ajili ya wakati unaokuja. Zaidi ya hilo, wakati tunasaidia wengine, hilo linatia nguvu mikono yetu na linatusaidia kukazia akili wakati unaokuja.

18 Wakati tunafikiria namna Yehova alisaidia na kulinda watumishi wake waaminifu wakati wa zamani, imani na tumaini letu kwake vinatiwa nguvu. Kwa hiyo, wakati uko na magumu na mahangaiko, usiache ‘mikono yako iregee’! Ukuwe hakika kama wakati unasali Yehova akusaidie, mukono wake wenye uwezo utakutia nguvu na kukuongoza upate baraka za Ufalme za hivi karibuni.—Zaburi 73:23, 24.