Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Neno la Mungu liko hai”

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Andiko la Waebrania 4:12 linasema kama “neno la Mungu liko hai [liko na uzima] nalo lina nguvu.” Neno hilo ni nini?

 

Kila mara tunazungumuzia andiko la Waebrania 4:12 katika vichapo vyetu ili kuonyesha kama Biblia iko na nguvu ya kubadilisha maisha ya watu, na hilo ni kweli. Lakini, ni muzuri tuelewe jambo lenye mutume Paulo alikuwa anazungumuzia wakati aliandika maneno ya Waebrania 4:12. Alikuwa anatia moyo Wakristo Waebrania watende kupatana na makusudi ya Mungu. Mengi kati ya makusudi hayo yalipatikana katika maandiko matakatifu. Ili kuzungumuzia jambo hilo, mutume Paulo alitumia mufano wa Waisraeli wenye Mungu alikomboa kutoka Misri. Walikuwa na tumaini la kuenda katika inchi ya ahadi ‘inchi inayotiririka maziwa na asali,’ kwenye wangefurahia pumuziko la kweli.—Kutoka 3:8; Kumbukumbu la Torati 12:9, 10.

Hilo lilikuwa kusudi la Mungu. Lakini, Waisraeli hawakufuata muongozo wa Yehova na hawakuonyesha imani, kwa hiyo, wengi kati yao hawakuingia katika pumuziko hilo. (Hesabu 14:30; Yoshua 14:6-10) Hata hivyo, mutume Paulo aliongeza kama kulikuwa kungali ‘ahadi ya kuingia katika pumuziko la [Mungu].’ (Waebrania 3:16-19; 4:1) Kwa kweli, “ahadi” hiyo ni sehemu ya mambo yenye Mungu amefunua juu ya kusudi lake. Kama vile Wakristo Waebrania, tunaweza kusoma habari juu ya kusudi hilo na kutenda kupatana nalo. Ili kukazia kama ahadi hiyo inategemea Maandiko, mutume Paulo alitaja maneno fulani ya andiko la Mwanzo 2:2 na Zaburi 95:11.

Inagusa sana mioyo yetu kujua kama ‘ahadi imebaki ya kuingia katika pumuziko la [Mungu].’ Tunatumaini kama inawezekana kabisa kuingia katika pumuziko la Mungu kama vile Biblia inafundisha, na tumekamata hatua ya kuingia katika pumuziko hilo. Hatufanye hivyo kwa kujaribu kufuata Sheria ya Musa ao kwa kufanya mambo ya muzuri ili tu tukubaliwe na Yehova. Lakini, kwa sababu ya imani yetu kwa Mungu, tumetenda kwa furaha kupatana na kusudi lake na tunaendelea kufanya hivyo. Mamilioni ya watu katika dunia yote wameanza pia kujifunza Biblia na kujua mambo yenye Mungu amefunua juu ya kusudi lake. Hilo limechochea wengi kati yao wafanye mabadiliko katika maisha yao, waonyeshe imani, na wabatizwe. Namna wanaendelea kufanya mabadiliko inaonyesha kabisa kama “neno la Mungu liko hai nalo lina nguvu.” Mambo yenye Mungu amefunua katika Biblia juu ya kusudi lake yametusaidia kufanya mabadiliko katika maisha, na yataendelea kuwa na nguvu katika maisha yetu.