Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wazazi, Musaidie Watoto Wenu Wakuwe na Imani Yenye Nguvu

Wazazi, Musaidie Watoto Wenu Wakuwe na Imani Yenye Nguvu

“Enyi vijana, nanyi mabikira [vijana wanawake] pia . . . Na walisifu jina la Yehova.”—ZABURI 148:12, 13.

NYIMBO: 88, 115

1, 2. (a) Sababu gani haiko vyepesi kwa wazazi kufundisha watoto wao wakuwe na imani kwa Yehova, na ni njia gani moja tu yenye wazazi wanaweza kutumia ili kufanya hivyo? (b) Tutazungumuzia mambo gani ine katika habari hii?

 WAZAZI fulani katika inchi ya Ufaransa walisema hivi: “Tunamuamini Yehova, lakini hilo halimaanishe kama watoto wetu watamuamini pia. Mutu hariti imani kutoka kwa wazazi wake. Watoto wetu wanapata imani hatua kwa hatua.” Ndugu mumoja katika inchi ya Australia aliandika hivi: “Kusaidia watoto wakuwe na imani ndani ya moyo wao, pengine ndilo tatizo kubwa zaidi lenye utapambana nalo.” Aliongeza hivi: “Unaweza kufikiri kama jibu la ulizo fulani lenye ulipatia mutoto wako lilimufurahisha kabisa. Kisha wakati fulani, unaona kama anauliza tena ulizo hilohilo! Majibu yenye kufurahisha mutoto wako leo, pengine hayatamufurahisha kesho.” Wakati watoto wanaendelea kukomaa, wazazi wengi wanaona kama wanapaswa kuwafasiria tena zaidi mambo yaleyale. Na wanaona kama wanapaswa kutumia njia mbalimbali ili kufundisha watoto wao wamupende Yehova.

2 Ikiwa uko muzazi, pengine wakati fulani unajiuliza kama utaweza kabisa kufundisha watoto wako wamupende Yehova na waendelee kumutumikia hata wakati watakomaa. Kwa kweli, hakuna mutu kati yetu mwenye anaweza kufanya hivyo kwa nguvu zake mwenyewe. (Yeremia 10:23) Ndiyo sababu tunapaswa kutegemea musaada wa Yehova. Ametolea wazazi maagizo mengi. Namna gani unaweza kusaidia watoto wako? (1) Ujikaze kuwajua muzuri. (2) Uwafundishe juu ya Yehova mambo yenye kuwa ndani ya moyo wako. (3) Utumie mifano. (4) Umuombe Yehova roho yake takatifu na uvumilie watoto wako.

UJUE MUZURI WATOTO WAKO

3. Ni katika njia gani wazazi wanaweza kuiga namna Yesu alifundisha wanafunzi wake?

3 Mara nyingi, Yesu aliuliza wanafunzi wake mambo yenye waliamini. (Mathayo 16:13-15) Unaweza kuiga mufano wake. Wakati unazungumuza na watoto wako ao wakati unafanya jambo fulani pamoja nao, uwaulize mambo yenye wanawaza na uwaache wajieleze kabisa. Wanaonekana kuwa na mashaka fulani? Ndugu mumoja wa miaka 15 katika inchi ya Australia alisema hivi: “Mara nyingi baba anazungumuza na mimi juu ya imani yangu na ananisaidia kufikiri. Ananiuliza hivi: ‘Biblia inasema nini?’ ‘Unaamini mambo Biblia inasema?’ ‘Sababu gani unaamini mambo hayo?’ Anapenda nijibie kwa kutumia maneno yangu mwenyewe kuliko kurudilia tu maneno yake ao maneno ya Mama. Wakati niliendelea kukomaa, nilipaswa kufasiria zaidi majibu yangu.”

4. Sababu gani ni jambo la maana ukuwe na uvumilivu na kujibia maulizo ya watoto wako? Toa mufano.

4 Ikiwa watoto wako hawaamini mara moja jambo fulani lenye Biblia inafundisha, ukuwe na uvumilivu. Uwasaidie wapate majibu ya maulizo yao. Baba mumoja alisema hivi: “Usizarau maulizo ya mutoto wako. Usikatae maulizo hayo kwa sababu unawaza kuwa haiko ya maana sana, na usiache kuzungumuzia habari fulani kwa sababu tu inaweza kukufanya ujisikie mubaya.” Kwa kweli, ni muzuri watoto wako wakuulize maulizo, kwa sababu hilo linaonyesha kama wanapenda kujua. Hata Yesu aliuliza maulizo wakati alikuwa kijana. (Soma Luka 2:46.) Kijana mumoja katika inchi ya Denmaki alisema hivi: “Wakati nilisema kama nilikuwa ninajiuliza ikiwa tuko katika dini ya kweli, wazazi wangu hawakunikaripia, hata kama walikuwa na wasiwasi juu yangu. Walitumia Biblia ili kujibia maulizo yangu yote.”

Uzungumuze na watoto wako juu ya Yehova kila siku wakati munafanya mambo fulani pamoja

5. Wazazi wanapaswa kufanya nini, hata kama watoto wanaonekana kuwa wako na imani kwa Yehova?

5 Ujikaze kujua muzuri watoto wako. Usifikiri kama wako na imani kwa Yehova kwa sababu tu wanaendaka katika mahubiri na kwenye mikutano. Wako na mawazo gani kabisa juu ya Yehova na juu ya Biblia? Ujikaze sana ili ujue ikiwa kuna jambo fulani lenye kufanya ikuwe vigumu kwao kubakia waaminifu kwa Yehova. Uzungumuze na watoto wako juu ya Yehova kila siku wakati munafanya mambo fulani pamoja. Usali kwa ajili ya watoto wako, wakati uko pamoja nao na wakati uko peke yako.

UWAFUNDISHE JUU YA YEHOVA MAMBO YENYE KUWA NDANI YA MOYO WAKO

6. Wakati wazazi wanaendelea kujifunza mambo mengi juu ya Yehova na juu ya Biblia, namna gani hilo linawasaidia kufundisha watoto wao?

6 Watu walifurahia kumusikiliza Yesu kwa sababu alimupenda Yehova na alijua muzuri Maandiko. Pia, waliona kuwa Yesu aliwapenda. Kwa hiyo, walimusikiliza kwa uangalifu. (Luka 24:32; Yohana 7:46) Vilevile, wakati watoto wako wanaona kuwa unamupenda Yehova, hilo litawasaidia wao pia wamupende. (Soma Kumbukumbu la Torati 6:5-8; Luka 6:45.) Kwa hiyo, uendelee kujifunza Biblia kwa uangalifu na usome vichapo vyetu kwa ukawaida. Ujikaze kujua mengi juu ya vitu vyenye Yehova aliumba. (Mathayo 6:26, 28) Ikiwa unajua mambo mengi juu ya Yehova, unaweza pia kufundisha watoto wako mambo mengi juu yake.—Luka 6:40.

Uzungumuze na watoto wako mambo yenye unajifunza juu ya Yehova

7, 8. Unaweza kufanya nini kila wakati unajifunza jambo fulani juu ya Yehova? Namna gani wazazi fulani wamefanya hivyo?

7 Wakati unajifunza jambo fulani juu ya Yehova, uzungumuze na watoto wako juu ya jambo hilo. Ufanye hivyo wakati wowote wenye muko pamoja, haiko tu wakati munatayarisha mikutano ao wakati wa ibada ya familia. Ni vile wazazi fulani wanafanya katika inchi ya Amerika. Wanazungumuza na watoto wao juu ya Yehova wakati wanaona kitu fulani cha muzuri katika uumbaji ao wakati wanakula pamoja chakula kitamu. Wanasema hivi: “Tunakumbusha watoto wetu kama kila kitu chenye Yehova ametupatia alikiumba kwa upendo na alikifikiria kwa uangalifu.” Bibi na bwana fulani katika inchi ya Afrika Kusini wanafurahia kuzungumuza juu ya uumbaji wakati wanatumika katika bustani yao pamoja na watoto wao wawili wanawake. Kwa mufano, wanaweza kuwaonyesha kama inashangaza sana kuona namna mbegu inafikia kuwa mumea. Wazazi hao wanasema hivi: “Tunajikaza kusaidia watoto wetu waheshimie sana uzima na wauone kuwa wa ajabu.”

8 Baba mumoja katika inchi ya Australia alienda na mutoto wake, wa miaka kumi hivi, kwenye nyumba ya makumbusho (musée). Baba huyo aliamua kutumia nafasi hiyo ili kusaidia mutoto wake atie nguvu imani yake na aone mambo yenye kuhakikisha kama Yehova ni Muumbaji wetu. Alisema hivi: “Tuliona viumbe fulani vya baharini vya zamani vyenye kuitwa ammonoids na trilobites. Tulishangaa kuona kama wanyama hao wenye wamekwisha kupotea walikuwa wazuri, wa ajabu, na hawakukosa kitu, na walikuwa kama wanyama wengine wenye tunaona leo. Sasa, kama uzima uligeuka kutoka aina nyepesi ya uzima na kufikia kuwa aina ya ajabu, sababu gani viumbe hao wa zamani walikuwa tayari wa ajabu sana? Hilo lilinishangaza sana na nilizungumuzia jambo hilo pamoja na mutoto wangu.”

TUMIA MIFANO

9. Sababu gani ni muzuri kutumia mifano? Mama mumoja alitumia mufano gani?

9 Yesu alitumia mifano kila mara. Alifundisha watu mambo ya maana sana kwa kutumia hadisi fulani ao kwa kutoa mufano. (Mathayo 13:34, 35) Wakati unatumia mifano, unasaidia watoto wako watumie uwezo wao wa kuona mambo katika akili. Hilo litawasaidia wafikirie mambo yenye unawafundisha, waelewe muzuri mambo hayo, na wayakumbuke. Pia, watapenda kujifunza mambo mengi. Kwa mufano, mama mumoja katika inchi ya Japani alipenda watoto wake wanaume wawili waelewe kama namna Yehova aliumba anga-hewa ya dunia inaonyesha kama anatuhangaikia sana. Mumoja alikuwa na miaka munane na mwengine alikuwa na miaka kumi. Kwa hiyo, alitumia mufano fulani wenye wangeweza kuelewa kulingana na miaka yao. Alipatia watoto hao maziwa, sukari, na kahawa (café). Kisha aliomba kila mutoto afanye kahawa katika kopo yake. Mama huyo alisema hivi: “Walifanya hivyo kwa uangalifu sana.” Aliongeza hivi: “Wakati niliwauliza sababu gani walifanya hivyo kwa uangalifu sana, walisema kama walipenda kahawa ikuwe kama vile nilipenda. Niliwafasiria kama Mungu alichanga kwa uangalifu sana gaze katika anga-hewa kwa njia yenye kufaa kwa ajili yetu.” Watoto hao walifurahia sana kujifunza jambo hilo na hawakulisahau hata kidogo!

Unaweza kutumia mifano myepesi ili kuonyesha watoto wako kama kuna Muumbaji (Picha hii inapatana na fungu la 10)

10, 11. (a) Unaweza kutumia mufano gani ili kuonyesha watoto wako kama kuna Muumbaji? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Umekwisha kutumia mifano gani?

10 Unaweza kutumia mufano gani ili kuonyesha watoto wako kama kuna Muumbaji? Unaweza kupika vitumbua pamoja na mutoto wako kwa kutumia maagizo fulani ya upishi. Umufasirie sababu gani ni muzuri kufuata kabisa maagizo hayo. Kisha umupatie mutoto wako tofaa (pomme) ao tunda lingine, na kisha umuulize hivi: Unajua kama tunda hili lilitengenezwa kwa kufuata maagizo fulani?” Kisha ukate tofaa hilo katika vipande mbili, na umupatie mbegu moja. Umufasirie kama mbegu hiyo iko kama vile maagizo ya upishi. Iko na maagizo fulani yenye kuonyesha namna ya kufanya tofaa. Lakini maagizo hayo ni ya ajabu sana kuliko maagizo ya kufanya kitumbua. Unaweza kumuuliza hivi: “Mutu fulani aliandika maagizo ya kufuata ili kufanya kitumbua. Sasa, ni nani aliandika maagizo juu ya namna ya kufanya tofaa?” Ikiwa watoto wako ni wenye kukomaa, unaweza kuwaambia kama hata maagizo juu ya kufanya mutofaa wenye unaweza kutoa matunda mengi zaidi yanapatikana katika ADN. Unaweza pia kuwaonyesha picha fulani na mifano yenye kupatikana kwenye ukurasa wa 10 mupaka wa 20 wa broshua yetu Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai.

11 Wazazi wengi wanasoma pamoja na watoto wao habari zenye kichwa “Kitu Hiki Kilijifanya Chenyewe?” zenye kupatikana katika Amuka! Ikiwa watoto wao wangali wadogo sana, wazazi wanaweza kuwaelezea habari hizo kwa njia nyepesi. Kwa mufano, bibi na bwana fulani katika inchi ya Denmaki walilinganisha avion na ndege. Walisema hivi: “Avion ziko tu kama vile ndege. Lakini, avion zinaweza kutaga mayai na kutotoa avion ndogo-ndogo? Ndege ziko na lazima ya viwanja vya pekee kwenye zinaweza kushukia? Na namna gani unaweza kulinganisha mulio wa avion na wimbo wa ndege? Ni nani mwenye kuwa na akili sana; mutu mwenye alitengeneza avion ao Muumbaji wa ndege?” Wakati unafikiri pamoja na watoto wako na kuwauliza maulizo, unawasaidia watumie ‘uwezo wao wa kufikiri’ na kutia nguvu imani yao kwa Yehova.—Methali 2:10-12.

12. Namna gani unaweza kutumia mifano ili kufundisha watoto wako kama mambo yote yenye Biblia inasema ni ya kweli?

12 Unaweza kutumia mifano ili kuonyesha watoto wako kama mambo yote yenye Biblia inasema ni ya kweli. Kwa mufano, unaweza kusoma Ayubu 26:7. (Soma.) Usiambie tu watoto wako kama habari yenye kupatikana katika andiko hilo ilitoka kabisa kwa Yehova. Lakini, uwasaidie watumie uwezo wao wa kuona mambo katika akili. Unaweza kusema kama pengine watu wa wakati wa Ayubu hawakuamini kama dunia haikamatwe na kitu fulani katika anga. Walijua kama kila kitu, kama vile kabumbu ao jiwe, linapaswa kukaa kwenye kitu fulani. Wakati huo, hakuna mutu mwenye alikuwa amehakikisha kama hakuna kitu fulani chenye kukamata dunia katika anga, kwa sababu hakukuwa darubini (chombo cha kusaidia kuona vitu vyenye kuwa mbali katika anga) ao vyombo vingine vya kusafiri kwenye anga za juu. Jambo la kujifunza ni hili: hata kama Biblia iliandikwa zamani sana, inasema kweli sikuzote kwa sababu inatoka kwa Mungu.—Nehemia 9:6.

UWAFUNDISHE SABABU GANI NI MUZURI KUFUATA MUONGOZO WA BIBLIA

13, 14. Namna gani wazazi wanaweza kufundisha watoto wao watii mambo yenye Biblia inasema?

13 Pia, ni jambo la maana ufundishe watoto wako kama watakuwa na furaha zaidi ikiwa wanatii mambo yenye Biblia inasema. (Soma Zaburi 1:1-3.) Kwa mufano, unaweza kuwaomba watoto wako wawazie kuwa wanaenda kuishi kwenye kisiwa fulani. Wanapaswa kuchagua watu wenye wataishi pamoja nao kwenye kisiwa hicho. Kisha, unaweza kuwauliza hivi: “Ikiwa munapenda watu wote waishi kwa amani, mutachagua kuenda na watu wa namna gani?” Kisha, unaweza kusoma Wagalatia 5:19-23 ili kujua ni watu wa namna gani wenye Yehova anapenda waishi katika dunia mupya.

14 Ikiwa unafanya hivyo, unaweza kufundisha watoto wako mambo mbili ya maana. Kwanza, Yehova anaendelea kutufundisha namna ya kupata furaha katika maisha yetu leo, na namna ya kuishi kwa amani pamoja na wengine. Pili, anaendelea kutufundisha namna ya kuishi katika dunia mupya. (Isaya 54:13; Yohana 17:3) Unaweza pia kuonyesha watoto wako namna Biblia imesaidia ndugu na dada zetu. Kwa mufano, tafuta katika vichapo vyetu habari yenye kuzungumuzia maisha ya mutu fulani, pengine katika habari zenye kichwa “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” zenye kuwa katika Munara wa Mulinzi. Ao uliza ndugu ao dada fulani katika kutaniko lenu akuelezee wewe na watoto wako namna Biblia ilimusaidia afanye mabadiliko makubwa ili amupendeze Yehova.—Waebrania 4:12.

15. Ni nini itakusaidia ufundishe watoto wako?

15 Utumie uwezo wako wa kuona mambo katika akili ili mambo yenye unafundisha watoto wako yakuwe yenye kuwapendeza na kuwafurahisha. Ufikirie njia mbalimbali zenye unaweza kutumia ili kuwasaidia wafurahie kujifunza mambo juu ya Yehova na wamukaribie zaidi. Na uendelee kufanya hivyo wakati wanaendelea kukomaa. Baba mumoja alisema hivi: “Usichoke hata kidogo kutumia njia za mupya ili kufasiria habari za zamani.”

UMUOMBE YEHOVA ROHO TAKATIFU NA UVUMILIE WATOTO WAKO

16. Wakati wazazi wanafundisha watoto wao, sababu gani ni jambo la maana wakuwe na uvumilivu? Namna gani wazazi fulani wameonyesha uvumilivu?

16 Roho takatifu ya Yehova inaweza kusaidia watoto wako wakuwe na imani yenye nguvu. (Wagalatia 5:22, 23) Lakini inaomba wakati ili imani yao ikuwe yenye nguvu. Kwa hiyo, uvumilie watoto wako, na uendelee kuwafundisha. Baba mumoja katika inchi ya Japani mwenye kuwa na watoto wawili, mwanaume na mwanamuke, alisema hivi: “Mimi na bibi yangu tunahangaikia sana watoto wetu. Tangu wakati walikuwa wadogo sana, nilijifunza pamoja nao kwa dakika 15 kila siku, kutosha siku zenye tulikuwa na mikutano ya Kikristo. Ilikuwa vyepesi sana kwetu na kwa watoto wetu kufanya dakika hizo kumi na tano.” Mwangalizi mumoja wa muzunguko aliandika hivi: “Wakati nilikuwa kijana, nilikuwa na mashaka ao maulizo mengi zaidi yenye sikuweza kuuliza. Kisha wakati fulani, nilipata majibu mengi ya maulizo yangu kwenye mikutano ao wakati wa ibada ya familia ao wakati wa funzo la pekee. Ndiyo sababu ni jambo la maana wazazi wasiache kufundisha watoto wao.”

Ili ukuwe mwalimu muzuri, unapaswa kupenda Neno la Mungu (Picha hii inapatana na fungu la 17)

17. Sababu gani ni jambo la maana wazazi watie nguvu imani yao wenyewe? Namna gani baba na mama mumoja katika inchi ya Bermuda wanasaidia watoto wao wanawake wakuwe na imani kwa Yehova?

17 Kwa kweli, watoto wako wanaweza kujifunza mambo mengi wakati wanaona kama uko na imani yenye nguvu kwa Yehova. Wataangalia mambo yenye unafanya. Kwa hiyo, uendelee kutia nguvu imani yako mwenyewe. Acha watoto wako watambue kama unaona Yehova kuwa mutu wa kweli kabisa. Kwa mufano, wakati baba na mama mumoja katika inchi ya Bermuda wanahangaika juu ya jambo fulani, wanasali kwa Yehova pamoja na watoto wao wanawake na kumuomba awaongoze. Pia, wanatia moyo watoto wao wakuwe wanasali wao wenyewe. Wazazi hao wanasema hivi: “Tuliambia pia mutoto wetu mukubwa mwanamuke kama amutegemee kabisa Yehova, aendelee kufanya mengi katika kazi ya Ufalme, na asihangaike sana. Wakati anaona matokeo, anaelewa kama Yehova anaendelea kutusaidia. Hilo limemusaidia sana akuwe na imani yenye nguvu kwa Mungu na katika Biblia.”

18. Wazazi hawapaswe kusahau nini?

18 Wazazi, musisahau hata kidogo kama hamuwezi kukaza watoto wenu wakuwe na imani. Munapanda mbegu na kuimwangia maji, lakini ni Yehova tu ndiye anaikomalisha. (1 Wakorintho 3:6) Kwa hiyo, mutumike kwa bidii ili kufundisha watoto wenu wapendwa juu ya Yehova, na mumuombe roho yake takatifu iwasaidie wakuwe na imani. Munaweza kuwa hakika kama Yehova atabariki kazi yenu ya bidii.—Waefeso 6:4.