Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 4

Chakula cha Mangaribi cha Bwana Chenye Hakina Mambo Mingi, Kinatufundisha Nini Juu ya Mufalme wa Mbinguni

Chakula cha Mangaribi cha Bwana Chenye Hakina Mambo Mingi, Kinatufundisha Nini Juu ya Mufalme wa Mbinguni

“Huu unamaanisha mwili wangu. . . . Hii inamaanisha ‘damu yangu ya agano.’”​—MT. 26:26-28.

WIMBO 16 Msifuni Yah kwa Mwana Wake Mtiwa Mafuta

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. (a) Juu ya nini hatushangae kuona kama Yesu alituonyesha namna ya mwepesi ya kukumbuka kifo chake? (b) Tutazungumuzia sifa gani za Yesu?

UNAWEZA kueleza mambo yenye kufanyika kila mwaka kwenye Ukumbusho wa kifo cha Kristo? Kwa kweli, unaweza kukumbuka mambo ya musingi ya Chakula cha Mangaribi cha Bwana. Juu ya nini? Kwa sababu chakula hicho hakina mambo mingi. Lakini, ni tukio la maana sana. Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Juu ya nini chakula hicho hakina mambo mingi?’

2 Wakati wa utumishi wake hapa ku dunia, Yesu alijulikana kuwa mutu mwenye alifundisha kweli za maana kwa njia ya mwepesi, yenye kuwa wazi, na yenye haiko nguvu kuelewa. (Mt. 7:28, 29) Vilevile, alitutolea namna ya mwepesi lakini ya maana ya kufanya Ukumbusho * wa kifo chake. Tuzungumuzie basi kwa uangalifu chakula hicho cha Ukumbusho na mambo fulani yenye Yesu alisema na kufanya. Kisha tutaelewa zaidi namna Yesu ni munyenyekevu, mwenye uhodari, na mwenye upendo kabisa, na tutajifunza namna tunaweza kumuiga zaidi.

YESU NI MUNYENYEKEVU

Mukate na divai vyenye kutumiwa ku Ukumbusho vinatukumbusha kama Yesu alitoa uzima wake kwa ajili yetu na kama sasa yeye ni Mufalme wetu mwenye kutawala mbinguni (Picha hizi zinapatana na fungu la 3-5)

3. (a) Kulingana na Matayo 26:26-28, ni nini inaonyesha kama Yesu alianzisha tukio la Ukumbusho bila kutumia mambo mingi? (b) Vitu mbili vyenye alitumia vilifananisha nini?

3 Yesu alianzisha Ukumbusho wa kifo chake pamoja na mitume wake waaminifu 11. Alikamata chakula cha Pasaka chenye kilibakia, na akafanya Ukumbusho huo wenye haukukuwa na mambo mingi. (Soma Matayo 26:26-28.) Alitumia tu mukate wenye hauna chachu na divai; vile vitu vilikuwa tayari pale. Yesu aliambia mitume wake kama vile vitu mbili vilifananisha mwili wake mukamilifu na damu yake kamilifu, vyenye alikuwa karibu kutoa kwa ajili yao. Pengine mitume hawakushangaa kuona kama tukio hilo la mupya la maana halikukuwa na mambo mingi. Juu ya nini?

4. Namna gani shauri lenye Yesu alikuwa amemutolea Marta linatusaidia kuelewa juu ya nini Yesu alifanya chakula cha Ukumbusho kisikuwe na mambo mingi?

4 Fikiria jambo lenye lilitokea miezi fulani mbele ya pale, mu mwaka wa tatu wa utumishi wa Yesu, wakati alitembelea marafiki wake wa sana, ni kusema, Lazaro, Marta, na Maria. Katika ile hali yenye kutulia Yesu alianza kufundisha. Marta alikuwa pale, lakini alikengeushwa kwa sababu ya kutayarisha chakula chenye mambo mingi kwa ajili ya mugeni wake wa heshima. Wakati aliona jambo hilo, kwa upole, Yesu alimushauria Marta, kwa kumusaidia aelewe kama chakula chenye mambo mingi hakikukuwa cha lazima sikuzote. (Lu. 10:40-42) Kisha, saa kidogo mbele atoe uzima wake kuwa zabihu, Yesu alitumia shauri hilo lenye alikuwa ametoa. Alifanya chakula cha Ukumbusho kisikuwe na mambo mingi. Jambo hilo linatufundisha nini juu ya Yesu?

5. (a) Chakula cha kukumbuka kifo cha Yesu hakikukuwa na mambo mingi, hilo linaonyesha nini juu ya Yesu? (b) Namna gani hilo linapatana na andiko la Wafilipi 2:5-8?

5 Yesu alionyesha unyenyekevu mu mambo yote yenye alisema na kufanya. Kwa hiyo, hatuwezi kushangaa kuwa alionyesha unyenyekevu mukubwa katika ule usiku wa mwisho wa maisha yake ku dunia. (Mt. 11:29) Alijua kama alikuwa karibu kutoa zabihu kubwa zaidi katika historia ya wanadamu na kama Yehova angemufufua na kumupatia cheo chenye kuwa na utukufu mbinguni. Hata hivyo, hakujitafutia sifa kwa sababu hakuomba tukio la kukumbuka kifo chake likuwe na mambo mingi. Lakini, aliambia wanafunzi wake kama wanapaswa kumukumbuka mara moja mu mwaka kwa kufanya tukio hilo la chakula chenye hakina mambo mingi. (Yoh. 13:15; 1 Ko. 11:23-25) Chakula hicho chenye hakina mambo mingi lakini cha maana sana, kinaonyesha kama Yesu hakukuwa na majivuno. Tunafurahi kwa sababu unyenyekevu uko kati ya sifa zenye kupendeza sana za Mufalme wetu wa mbinguni.​—Soma Wafilipi 2:5-8.

6. Namna gani tunaweza kuiga unyenyekevu wa Yesu wakati tunapambana na majaribu?

6 Namna gani tunaweza kuiga unyenyekevu wa Yesu? Kwa kutia pa nafasi ya kwanza faida za wengine kuliko faida zetu wenyewe. (Flp. 2:3, 4) Fikiria tena usiku wa mwisho wa maisha ya Yesu ku dunia. Yesu alijua kama alikuwa karibu kufa kifo chenye kuwa na maumivu; lakini, alihangaikia sana mitume wake waaminifu, wenye walikuwa karibu kuhuzunika sana juu yake. Kwa hiyo, alitumia usiku wake wa mwisho ili kuwafundisha, kuwatia moyo, na kuwasaidia wasiogope. (Yoh. 14:25-31) Kwa unyenyekevu, Yesu alihangaikia sana hali ya muzuri ya wengine kuliko hali yake mwenyewe. Huo ni mufano muzuri sana wenye alituachia!

YESU IKO HODARI

7. Namna gani Yesu alionyesha uhodari mukubwa kisha tu kuanzisha Chakula cha Mangaribi cha Bwana?

7 Kisha tu Yesu kuanzisha Chakula cha Mangaribi cha Bwana, alionyesha uhodari mukubwa. Namna gani? Alikubali kufanya mapenzi ya Baba yake, hata kama alijua kwamba kufanya vile kungefanya auawe kwa kushitakiwa kosa la haya sana la kumutukana Mungu. (Mt. 26:65, 66; Lu. 22:41, 42) Yesu aliendelea kuonyesha uaminifu-mushikamanifu kwa ukamili ili kutukuza jina la Yehova, kutetea haki ya Mungu ya kutawala, na kufungua njia ili wanadamu wenye kutubu wapate uzima wa milele. Wakati huohuo, Yesu alitayarisha wanafunzi wake kwa ajili ya jambo lenye lilikaribia kuwapata.

8. (a) Yesu aliambia nini mitume wake waaminifu? (b) Mu miaka yenye ilifuata kisha kifo cha Yesu, ni nini inaonyesha kama wanafunzi wake waliiga mufano wake wa kuonyesha uhodari?

8 Yesu alionyesha pia uhodari kwa sababu hakukazia akili mahangaiko yoyote yenye pengine alikuwa nayo, lakini alikazia akili mahitaji ya mitume wake waaminifu. Chakula chenye hakikukuwa na mambo mingi chenye alianzisha kisha kumuambia Yuda aende, kingekumbusha wale wenye wangefikia kuwa wanafunzi wake watiwa-mafuta faida za damu ya Yesu yenye ilimwangwa na faida za kushiriki katika agano jipya. (1 Ko. 10:16, 17) Ili kuwasaidia wanafunzi wake waendelee kuwa waaminifu na wafikie kuwa pamoja naye mbinguni, Yesu aliwaambia jambo lenye yeye na Baba yake walipenda wafanye. (Yoh. 15:12-15) Pia, Yesu alielezea mitume majaribu yenye ingewapata. Kisha, ili kuwatia moyo wafuate mufano wake, aliwaambia hivi: “Musiogope!” (Yoh. 16:1-4a, 33) Miaka mingi kisha pale, wanafunzi wa Yesu walikuwa wangali wanafuata mufano wake wa kuonyesha roho ya kujitoa na kuonyesha uhodari. Walitegemezana mu majaribu mbalimbali yenye walipata, hata kama kufanya vile kungewaletea mateso.​—Ebr. 10:33, 34.

9. Tunaweza kufanya nini ili tuige uhodari wa Yesu?

9 Vilevile leo, tunafuata mufano wa Yesu wa kuonyesha uhodari. Kwa mufano, inaomba uhodari ili kusaidia ndugu na dada zetu wenye kuteswa kwa sababu ya imani yao. Wakati fulani, ndugu na dada zetu wanaweza kufungwa katika gereza bila haki. Wakati jambo hilo linatokea, tunapaswa kufanya nguvu yetu yote ili kuwasaidia, na hata kuwatetea. (Flp. 1:14; Ebr. 13:19) Pia, tunaonyesha uhodari kwa kuendelea kuhubiri “bila woga.” (Mdo. 14:3) Kama Yesu, tunaazimia kuhubiri ujumbe wa Ufalme, hata kama watu wanaweza kutupinga ao kututesa. Lakini, wakati fulani, tunaweza kuona kama tunakosa uhodari. Tunaweza kufanya nini?

10. Katika majuma fulani mbele ya Ukumbusho, tunapaswa kufanya nini, na juu ya nini?

10 Tunaweza kuwa na uhodari zaidi kwa kufikiri juu ya tumaini lenye zabihu ya bei ya ukombozi ya Kristo inatutolea. (Yoh. 3:16; Efe. 1:7) Katika majuma fulani mbele ya Ukumbusho, tuko na nafasi ya pekee ya kuonyesha shukrani zaidi juu ya bei ya ukombozi. Katika wakati huo, tufuate programu ya usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho na tuonyeshe heshima kabisa wakati tunafikiri sana juu ya mambo yenye ilitokea mbele na kisha kifo cha Yesu. Kisha, wakati tunakusanyika kwa ajili ya Chakula cha Mangaribi cha Bwana, tutaelewa muzuri zaidi maana ya mukate na divai vyenye kutumiwa ku Ukumbusho na zabihu ya pekee yenye vile vitu vinafananisha. Wakati tunaelewa mambo yenye Yehova na Yesu wametufanyia na kuelewa namna ile mambo inatuletea faida sisi na wapendwa wetu, tumaini letu kwa ajili ya wakati wenye kuja linakuwa nguvu zaidi, na hilo linatuchochea kuvumilia kwa uhodari mupaka mwisho.​—Ebr. 12:3.

11-12. Mupaka hapa, tumejifunza nini?

11 Mupaka hapa, tumejifunza kama Chakula cha Mangaribi cha Bwana kinatukumbusha kama bei ya ukombozi ni ya maana sana, lakini pia kinatukumbusha sifa za pekee za Yesu, kama vile unyenyekevu na uhodari. Tuko wenye shukrani sana kwa sababu Yesu, Kuhani wetu Mukubwa wa mbinguni mwenye anatuombea, anaendelea kuonyesha zile sifa! (Ebr. 7:24, 25) Ili kuonyesha shukrani yetu kwa moyo wetu wote, tunapaswa kukumbuka kwa uaminifu kifo cha Yesu, kama vile tu aliamuru. (Lu. 22:19, 20) Tunafanya vile katika siku yenye kulingana na tarehe 14 Mwezi wa Nisani, tarehe ya maana zaidi katika mwaka.

12 Kwa sababu Chakula cha Mangaribi cha Bwana hakikukuwa na mambo mingi, hilo linatuonyesha sifa ingine yenye ilimuchochea Yesu akufe kwa ajili yetu. Wakati alikuwa mwanadamu ku dunia, alijulikana kupitia ile sifa. Ni sifa gani?

YESU IKO NA UPENDO

13. Namna gani upendo wenye Yehova na Yesu wameonyesha unaelezwa mu andiko la Yohana 15:9 na 1 Yohana 4:8-10, na upendo wao unaletea nani faida?

13 Mu mambo yote yenye alifanya, Yesu alionyesha kwa ukamilifu upendo mukubwa wenye Yehova iko nao kwetu. (Soma Yohana 15:9; 1 Yohana 4:8-10.) Jambo la maana zaidi ni hii: Yesu alikubali kwa moyo wote kutoa uzima wake kwa ajili yetu. Ikuwe tuko watiwa-mafuta ao “kondoo wengine,” tunapata faida kupitia upendo wenye Yehova na Mwana wake walituonyesha kupitia ile zabihu. (Yoh. 10:16; 1 Yo. 2:2) Fikiria pia vitu vyenye vilitumiwa wakati wa Ukumbusho; vinaonyesha upendo wa Yesu na namna alihangaikia wanafunzi wake. Vinaonyesha vile namna gani?

Kwa upendo, Yesu alianzisha tukio la chakula cha Ukumbusho chenye hakikukuwa na mambo mingi; kwa hiyo ingewezekana kufanya tukio hilo kwa miaka mingi na mu hali mbalimbali (Picha hizi zinapatana na fungu la 14-16) *

14. Namna gani Yesu alionyesha wanafunzi wake upendo?

14 Yesu aliwaonyesha wanafunzi wake watiwa-mafuta upendo kwa sababu hakuanzisha tukio lenye kuwa na mambo mingi, lakini alianzisha tukio la mwepesi lenye wangepaswa kukumbuka. Kadiri wakati ulipita, wanafunzi hao watiwa-mafuta walipaswa kufanya Ukumbusho kila mwaka, na wangefanya vile mu hali mbalimbali, hata wakati wako katika gereza. (Ufu. 2:10) Waliweza kumutii Yesu? Ndiyo!

15-16. Wakristo fulani wamefanya nini ili waweze kufanya tukio la kukumbuka Chakula cha Mangaribi cha Bwana mu hali zenye kuwa nguvu?

15 Tangu wakati wa mitume mupaka leo, Wakristo wa kweli wamejikaza kukumbuka kifo cha Yesu. Wamefanya nguvu yao yote ili kufuata namna ya kufanya Chakula cha Mangaribi cha Bwana, wakati fulani wamefanya vile mu hali zenye kuwa nguvu. Fikiria mifano yenye kufuata. Wakati Ndugu Harold King alikuwa yeye mwenyewe mu chumba cha gereza katika inchi ya China, alipaswa kutafuta namna ya kufanya Ukumbusho. Kwa uficho, alitayarisha mukate na divai, kwa kutumia vitu vyenye alikuwa navyo. Pia, alihesabia siku kwa uangalifu ili ajue tarehe ya Ukumbusho. Wakati siku ya Ukumbusho ilifika, aliimba, alisali, na kutoa hotuba yenye kutegemea Maandiko, yeye mwenyewe mu chumba chake cha gereza.

16 Ona ingine mufano. Kikundi cha dada wenye walikuwa wamefungwa mu kambi ya mateso wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, walitia maisha yao mu hatari ili kufanya tukio la kukumbuka Chakula cha Mangaribi cha Bwana. Lakini, kwa sababu chakula hicho hakina mambo mingi, waliweza kufanya Ukumbusho kwa uficho. Walisema hivi: “Tulisimama pamoja na kuzunguka kiti chenye kuwa na kitambaa cha mweupe kwenye kulikuwa mukate na divai. Tuliwasha mushumaa ili kupata mwangaza mu chumba, kwa sababu mwangaza wa umeme ungefanya tuvumbuliwe. . . . Tulisema tena naziri zetu kwa Baba yetu kama tutatumia nguvu zetu zote ili kutetea jina lake takatifu.” Walionyesha imani yenye nguvu kabisa! Na Yesu alionyesha upendo mukubwa sana wakati alifanya tuweze kufanya Ukumbusho hata mu hali zenye kuwa nguvu!

17. Tunaweza kujiuliza maulizo gani?

17 Kadiri Ukumbusho unakaribia, ni muzuri tujiulize maulizo yenye kufuata: ‘Namna gani ninaweza kumuiga zaidi Yesu kwa kuonyesha upendo? Ninafikiria sana mahitaji ya Wakristo wenzangu kuliko namna ninafikiria mahitaji yangu? Ninaomba ndugu na dada zangu wafanye mambo yenye kupita uwezo wao, ao ninajua mipaka yao?’ Tumuige basi Yesu sikuzote na ‘tujitie pa nafasi ya wengine.’​—1 Pe. 3:8.

UIGE UNYENYEKEVU, UHODARI, NA UPENDO WA YESU

18-19. (a) Tunaweza kuwa hakika juu ya jambo gani? (b) Umeazimia kufanya nini?

18 Agizo la kukumbuka kifo cha Kristo halitaendelea kwa muda murefu. Wakati Yesu “atakuja” wakati wa taabu kubwa, atakusanya mabaki wake “wenye kuchaguliwa” ili waende mbinguni, na Ukumbusho hautafanywa tena.​—1 Ko. 11:26; Mt. 24:31.

19 Hata kama hatutafanya tena Ukumbusho, tunaweza kuwa hakika kwamba watu wa Yehova watafurahia kukumbuka chakula hicho chenye hakina mambo mingi kuwa alama yenye kuonyesha unyenyekevu, uhodari na upendo mukubwa wenye hakuna mwanadamu yeyote amekwisha kuonyesha. Wakati huo, wale wenye walihuzuria tukio hilo la pekee sana, bila shaka wataeleza juu ya tukio hilo kwa faida ya watu wote wenye wataishi wakati huo. Lakini, ili tukio hilo lituletee faida leo, tunapaswa kuazimia kuiga unyenyekevu, uhodari, na upendo wa Yesu. Kama tunafanya vile, tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatubariki.​—2 Pe. 1:10, 11.

WIMBO 13 Kristo, Kielelezo Chetu

^ fu. 5 Hivi karibuni, tutahuzuria tukio la Chakula cha Mangaribi cha Bwana ili kukumbuka kifo cha Yesu Kristo. Chakula hicho chenye hakina mambo mingi kinatufundisha mambo mingi juu ya uvumilivu, uhodari, na upendo wa Yesu. Mu habari hii, tutazungumuzia namna tunaweza kuiga sifa za maana sana zenye alionyesha.

^ fu. 2 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Ukumbusho ni mupango wa kufanya jambo fulani la pekee ili kukumbuka na kuheshimia tukio fulani la maana ao mutu fulani wa maana.

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Picha zenye kuonyesha namna watumishi waaminifu wa Mungu wanafanya Ukumbusho katika kutaniko la wakati wa mitume; mwisho-mwisho wa miaka ya 1800; mu kambi ya mateso ya Wanazi; na mu siku zetu Ukumbusho unafanywa mu Jumba la Ufalme lenye halina kuta mu inchi moja yenye kuwa na joto katika Amerika ya Kusini.