Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 2

Umusifu Yehova Katika Kutaniko

Umusifu Yehova Katika Kutaniko

“Katikati ya kutaniko nitakusifu.”​—ZB. 22:22.

WIMBO 59 Msifuni Yah Pamoja Nami

KIFUPI CHA HABARI *

1. Daudi alijisikia namna gani juu ya Yehova, na hilo lilimuchochea afanye nini?

MUFALME DAUDI aliandika hivi: “Yehova ni mukubwa na anastahili kusifiwa sana.” (Zb. 145:3) Alimupenda Yehova, na upendo huo ulimuchochea kumusifu “katikati ya kutaniko.” (Zb. 22:22; 40:5) Bila shaka, unamupenda Yehova na unakubaliana na hii maneno ya Daudi: “Usifiwe, Ee Yehova Mungu wa Israeli baba yetu, kwa umilele wote.”​—1 Ny. 29:10-13.

2. (a) Tunaweza kufanya nini ili kumusifu Yehova? (b) Ndugu na dada fulani wako na tatizo gani, na tutazungumuzia nini?

2 Leo, kutoa majibu wakati wa mikutano ya Kikristo ni njia moja ya kumusifu Yehova. Lakini, ndugu na dada zetu fulani wako na tatizo kabisa. Wanapenda kutoa majibu wakati wa mikutano, lakini woga unawazuia kufanya vile. Tunaweza kufanya nini ili tushinde woga huo? Na ni mashauri gani yenye kufaa yenye inaweza kutusaidia sisi wote ili tutoe majibu yenye kutia moyo? Mbele tujibu ile maulizo, tuzungumuzie kwanza sababu ine za maana zenye kuonyesha juu ya nini tunatoa majibu ku mikutano.

JUU YA NINI TUNATOA MAJIBU KU MIKUTANO?

3-5. (a) Kulingana na andiko la Waebrania 13:15, juu ya nini tunatoa majibu ku mikutano? (b) Sisi wote tunapaswa kutoa majibu ya namna ileile? Fasiria.

3 Yehova ametupatia sisi wote pendeleo la kumusifu. (Zb. 119:108) Majibu yenye tunatoa ku mikutano ni sehemu ya “zabihu [yetu] ya sifa,” na hakuna mutu mwenye anaweza kutoa ile zabihu pa nafasi yetu. (Soma Waebrania 13:15.) Je, Yehova anatuomba sisi wote tutoe zabihu, ao majibu ya namna ileile? Hapana!

4 Yehova anajua kama tuko na uwezo na hali mbalimbali na anapendezwa sana na zabihu zenye tunaweza kumutolea. Fikiria zabihu za namna mbalimbali zenye alikubali Waisraeli wamutolee. Waisraeli fulani walikuwa na uwezo wa kutoa mwana-kondoo ao mbuzi. Lakini Muisraeli mwenye alikuwa maskini angeweza kutoa “njiwa-tetere wawili ao njiwa wawili wadogo.” Na kama Muisraeli hakukuwa na uwezo wa kupata ndege wawili, Yehova alikubali “sehemu moja ya kumi (1/10) ya kipimo cha efa moja ya unga muzuri.” (Law. 5:7, 11) Unga ulikuwa wa bei chini, lakini Yehova aliona ile zabihu kuwa ya maana, kama tu ile zabihu ilikuwa “unga muzuri.”

5 Mungu wetu mwenye fazili hajabadilika mupaka leo. Wakati tunatoa majibu, hatuombe sisi wote tukuwe wenye kusema muzuri kama Apolo ao wenye kujua kushawishi kama Paulo. (Mdo. 18:24; 26:28) Yehova anapenda tutoe majibu ya muzuri kabisa, kulingana na uwezo wetu. Kumbuka mujane mwenye alitoa feza mbili za vichele. Yehova alimuona kuwa wa maana kwa sababu alitoa yote yenye alikuwa nayo.​—Lu. 21:1-4.

Kutoa majibu kunatuletea faida na pia wale wenye kutusikiliza (Picha hii inapatana na fungu la 6-7) *

6. (a) Kulingana na andiko la Waebrania 10:24, 25, majibu yenye tunasikia ku mikutano inaweza kutufanya tujisikie namna gani? (b) Unaweza kufanya nini ili kuonyesha shukrani kwa ajili ya majibu yenye inakutia moyo?

6 Tunatiana moyo kupitia majibu yetu. (Soma Waebrania 10:24, 25.) Sisi wote tunafurahia kusikia majibu ya namna mbalimbali ku mikutano yetu. Tunafurahia maneno ya mutoto yenye kuwa mwepesi na yenye kutoka moyoni. Tunaguswa moyo wakati tunasikia sauti yenye furaha ya mutu mwenye anatoa maelezo juu ya kweli fulani yenye ametoka tu kuvumbua. Na tunafurahia wale wenye wanajikaza ‘kuwa na uhodari’ ili watoe majibu, hata kama ni wenye haya ao wameanza tu kujifunza luga yetu. (1 Te. 2:2; maelezo ya chini.) Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha shukrani kwa wale wenye wanajikaza kufanya vile? Kisha mikutano, tunaweza kuwashukuru kwa majibu yao yenye kutia moyo. Njia ingine ya kuwaonyesha shukrani ni kwa kutoa majibu sisi wenyewe. Kama tunafanya vile sisi wenyewe tutatiwa moyo ku mikutano, na tutatia wengine moyo.​—Ro. 1:11, 12.

7. Tunapata faida gani wakati tunatoa majibu?

7 Sisi wenyewe tunapata faida wakati tunatoa majibu. (Isa. 48:17) Ni faida gani? Kwanza, kama tunapanga mbele ya wakati kutoa majibu, hilo linatuchochea zaidi kutayarisha muzuri mikutano. Wakati tunatayarisha muzuri, tunaelewa muzuri zaidi Neno la Mungu. Na wakati tunaelewa muzuri zaidi Neno la Mungu, inakuwa mwepesi kwetu kutumia mu maisha yetu mambo yenye tunajifunza. Pili, inawezekana kabisa tutafurahia zaidi mikutano kwa sababu tunashiriki katika mazungumuzo. Tatu, kwa sababu inaomba kujikaza sana ili kutoa majibu, mara mingi kisha mikutano tunakumbuka kwa muda murefu mambo yenye tulizungumuzia.

8-9. (a) Kama vile andiko la Malaki 3:16 linaonyesha, unawaza Yehova anajisikia namna gani wakati tunatoa majibu? (b) Watu fulani wanaweza kuogopa kufanya nini?

8 Tunamupendeza Yehova wakati tunazungumuza juu ya imani yetu. Tunaweza kuwa hakika kama Yehova anatusikiliza na anapendezwa sana na bidii yenye tunafanya ili kutoa majibu ku mikutano. (Soma Malaki 3:16.) Anaonyesha kama anapendezwa na bidii yetu kwa kutubariki wakati tunajikaza sana ili kumupendeza.​—Mal. 3:10.

9 Kwa kweli, tuko na sababu za muzuri za kutoa majibu ku mikutano. Lakini, watu fulani wanaweza kuogopa kutia mukono juu. Kama na wewe unaogopaka, usivunjike moyo. Tuzungumuzie basi kanuni fulani za Biblia, mifano fulani, na mashauri fulani yenye kufaa yenye inaweza kutusaidia sisi wote tujikaze kutoa majibu zaidi ku mikutano.

MAMBO YA KUFANYA ILI USIOGOPE

10. (a) Juu ya nini wengi kati yetu wanaogopaka kutoa majibu? (b) Kama unaogopaka kutoa majibu, pengine ile inaweza kuwa alama yenye kuonyesha nini?

10 Unasikiaka moyo wako unapiga-piga kila wakati unafikiria kutia mukono juu ili kutoa majibu? Kama ni vile, haiko wewe tu. Kusema kweli, wengi kati yetu wanasikiaka woga kwa kadiri fulani wakati wanatoa majibu. Mbele upiganishe woga huo, unapaswa kujua ni juu ya nini unaogopaka. Unaogopa kuwa utasahau mambo yenye unapenda kusema ao kama utasema mambo yenye makosa? Unaogopa kuwa maelezo yako haitakuwa ya muzuri kama ya wengine? Kwa kweli, kuogopa vile inaweza kuwa alama ya muzuri. Inaonyesha kama uko munyenyekevu na kama unaona wengine kuwa wazuri zaidi kukupita. Yehova anapenda ile sifa. (Zb. 138:6; Flp. 2:3) Lakini, Yehova anapenda pia umusifu na kutia moyo ndugu na dada zako ku mikutano. (1 Te. 5:11) Anakupenda na atakupatia uhodari wenye uko nao lazima.

11. Maandiko inatukumbusha mambo gani yenye inaweza kutusaidia?

11 Fikiria mambo fulani yenye Biblia inatukumbusha. Inasema kama sisi wote tunakoseaka mu mambo yenye tunasema na namna tunaisema. (Yak. 3:2) Yehova hatuombe tukuwe wakamilifu, na ndugu na dada zetu nao hawatuombe tukuwe wakamilifu. (Zb. 103:12-14) Wao ni familia yetu ya kiroho, na wanatupenda. (Mk. 10:29, 30; Yoh. 13:35) Wanaelewa kama wakati fulani hatuseme mambo yenye tulipenda kusema kabisa mu majibu yetu.

12-13. Mufano wa Nehemia na wa Yona unatufundisha nini?

12 Fikiria mifano fulani yenye kuwa mu Biblia yenye inaweza kukusaidia kushinda woga wako. Kumbuka mufano wa Nehemia. Alikuwa anatumika katika makao ya mufalme mwenye nguvu. Nehemia alikuwa na huzuni kwa sababu alikuwa amesikia kama kuta na milango ya Yerusalemu vilikuwa vimeharibika. (Ne. 1:1-4) Wazia namna moyo wake ulipiga-piga wakati mufalme alimuomba aseme juu ya nini hakukuwa na furaha! Palepale Nehemia alisali na kisha akajibu. Matokeo ni kwamba, mufalme alifanya mambo mingi ili kusaidia watu wa Mungu. (Ne. 2:1-8) Fikiria pia mufano wa Yona. Wakati Yehova alimuomba azungumuze na wakaaji wa Ninawi, Yona aliogopa sana mupaka akakimbilia katika eneo lingine. (Yon. 1:1-3) Lakini kwa musaada wa Yehova, Yona alitimiza mugao wake. Na maneno yenye alisema ilisaidia sana watu wa Ninawi. (Yon. 3:5-10) Mufano wa Nehemia unatufundisha kama ni jambo la maana kusali mbele ya kujibu. Na mufano wa Yona unatufundisha kama Yehova anaweza kutusaidia tumutumikie hata kama tunaogopa sana. Kwa kweli, hakuna kutaniko lenye linaweza kuogopesha kama vile watu wa Ninawi.

13 Ni mashauri gani yenye kufaa yenye inaweza kukusaidia kutoa majibu yenye kutia moyo ku mikutano? Tuzungumuzie basi mashauri fulani.

14. Juu ya nini tunapaswa kutayarisha muzuri mikutano yetu, na tunaweza kufanya vile wakati gani?

14 Utayarishe kila mukutano. Wakati unafanya mipango mbele ya wakati na kutayarisha muzuri, hautaogopa kutoa majibu. (Mez. 21:5) Kwa kweli, kila mutu iko na programu yake ya kutayarisha mikutano. Eloise, dada mujane mwenye kuwa na miaka zaidi ya 80, anaanza kutayarisha funzo la Munara wa Mulinzi ku mwanzo-mwanzo wa juma. Anasema hivi: “Ninafurahia mikutano zaidi kama ninajifunza mbele ya wakati.” Joy, dada mwenye kufanya kazi ya kimwili yenye kumukamata wakati wote, anapanga wakati Siku ya Posho ili kujifunza Munara wa Mulinzi. Anasema hivi: “Ni mwepesi kukumbuka kama ninajifunza muda mufupi mbele ya mikutano.” Ike, muzee wa kutaniko mwenye kuwa na mambo mingi ya kufanya na mwenye kuwa pia painia, anasema hivi: “Ninaona kama ni muzuri zaidi kwangu kujifunza kwa vipindi vifupi-vifupi vya wakati katika juma lote kuliko kujifunza siku moja kwa wakati murefu.”

15. Unaweza kufanya nini ili utayarishe muzuri mikutano?

15 Unaweza kufanya nini ili kutayarisha muzuri mikutano? Kila wakati mbele ya kuanza kujifunza, umuombe Yehova akupatie roho takatifu. (Lu. 11:13; 1 Yo. 5:14) Kisha, tumia dakika fulani ili kuchunguza habari yote: chunguza kichwa cha habari, vichwa vidogo-vidogo, picha, na visanduku. Sasa wakati uko unajifunza kila fungu, ujikaze kusoma maandiko mengi kati ya maandiko yenye kutajwa. Ufikiri sana juu ya habari yenye unajifunza, na ukazie zaidi mahali kwenye unapenda kutoa majibu. Wakati unatayarisha muzuri, utapata faida zaidi na hautaona kuwa ni nguvu kutoa majibu.​—2 Ko. 9:6.

16. Yehova ametupatia vifaa gani, na namna gani unavitumia?

16 Kama inawezekana, tumia programu na site zetu za Enternete zenye kuwa mu luga yenye unajua. Kupitia tengenezo lake, Yehova ametupatia programu na site za Enternete ili kutusaidia kutayarisha mikutano. Programu JW Library® inatusaidia kuchukua vichapo vya kujifunza katika vyombo vyetu vya kielektroniki kama vile tablete, ao telefone. Kisha tunaweza kujifunza ao hata kusoma ao kusikiliza habari fulani kila wakati na kila mahali. Watu fulani wanatumia programu hiyo ili kujifunza wakati wa mapumuziko ku kazi ao ku masomo, ao wakati wako wanasafiri. Watchtower Library na Watchtower MAKTABA KWENYE ENTERNETE, vinafanya ikuwe mwepesi sana kutafuta mawazo makubwa mu habari yenye tunapenda kujifunza kwa uangalifu zaidi.

Unatayarishaka mikutano wakati gani? (Picha hizi zinapatana na fungu la 14-16) *

17. (a) Juu ya nini ni muzuri kutayarisha majibu mbalimbali? (b) Ulijifunza nini wakati uliangalia video Ukuwe Rafiki ya Yehova​—Tayarisha Majibu Yako?

17 Kama inawezekana, tayarisha majibu mbalimbali kwa ajili ya kila habari ya kujifunza. Juu ya nini? Juu pengine hautatajwa kila mara wakati unatia mukono juu. Inawezekana wengine watatia mukono juu wakati huohuo, na kiongozi anaweza kuchagua mumoja kati yao. Ili mikutano imalizike kwa wakati, kiongozi anaweza kuomba watu kidogo watoe majibu juu ya wazo fulani. Kwa hiyo, usikwazike ao kuvunjika moyo kama hakutaje ku mwanzo-mwanzo wa funzo. Kama unatayarisha majibu mbalimbali, utakuwa na nafasi za mingi zaidi za kutoa majibu. Kusoma andiko ni kati ya majibu yenye unaweza kutayarisha. Lakini, kama inawezekana, ujitayarishe ili kutoa majibu mu maneno yako mwenyewe. *

18. Juu ya nini ni muzuri kutoa majibu ya mufupi?

18 Utoe majibu ya mafupi. Mara mingi, majibu ya mufupi na ya mwepesi njo yenye inatiaka moyo zaidi. Kwa hiyo, ukuwe na muradi wa kutoa majibu ya mufupi. Ujikaze kutoa majibu kwa segonde 30 hivi. (Mez. 10:19; 15:23) Kama umetoa majibu ku mikutano kwa miaka mingi, uko na daraka la maana, ni kusema, unapaswa kuonyesha mufano muzuri kwa kutoa majibu ya mufupi. Kama unazungumuzia mambo mingi yenye kufanya dakika fulani, wengine wanaweza kuogopa, na kufikiri kama hawawezi kufikia uwezo wako wa kujibu. Tena, kutoa majibu ya mufupi kunaruhusu watu wengi zaidi watoe majibu wakati wa mikutano. Zaidi sana, kama wewe njo unapewa nafasi ya kutoa jibu la kwanza, utoe jibu la mwepesi, na lenye kujibu ulizo moja kwa moja. Usijaribu kuzungumuzia mawazo yote ya fungu. Kisha wazo kubwa la fungu kuzungumuziwa, unaweza kutoa maelezo juu ya mawazo ingine.​—Ona kisanduku “ Ninaweza Kutoa Majibu Juu ya Mambo Gani?

19. Namna gani kiongozi anaweza kukusaidia, lakini unapaswa kufanya nini?

19 Uambie kiongozi kama unapenda kujibu kwenye fungu fulani. Kama unaamua kufanya vile, unapaswa kuzungumuza na kiongozi mbele mukutano uanze. Wakati mutafika kwenye ile fungu, utie haraka mukono wako juu sana ili kiongozi aone mukono wako.

20. Juu ya nini mikutano ya kutaniko iko kama vile kuchangia chakula pamoja na marafiki?

20 Uone mikutano ya kutaniko kama vile kuchangia chakula pamoja na marafiki wazuri. Wazia kuwa marafiki fulani wa kutaniko wanapanga mutumie chakula pamoja na wanakuomba ulete chakula fulani cha mwepesi. Unaweza kufanya nini? Unaweza kuwa na wasiwasi kidogo, lakini inawezekana kabisa kama utajikaza sana ili kuleta kitu fulani chenye watu wote watafurahia. Yehova, mwenye kutualika, ametutayarishia meza yenye kujaa vitu vya muzuri ku mikutano yetu. (Zb. 23:5; Mt. 24:45) Na anafurahi wakati tunaleta zawadi ya kidogo, ya muzuri zaidi kulingana na uwezo wetu. Kwa hiyo, tayarisha muzuri na ukuwe huru kutoa majibu kadiri unaweza. Kama unafanya vile, utakula ku meza ya Yehova na utaleta pia zawadi ili kuchangia pamoja na kutaniko.

WIMBO 2 Jina Lako Ni Yehova

^ fu. 5 Kama Daudi, muandikaji mumoja wa zaburi, sisi wote tunamupenda Yehova na tunafurahia kumusifu. Tuko na nafasi ya pekee ya kuonyesha upendo wetu kwa Mungu wakati tunakutana pamoja na ndugu na dada wa kutaniko letu ili kuabudu. Lakini, wamoja kati yetu wanaona kuwa haiko mwepesi kutoa majibu ku mikutano yetu. Kama unapambana na ile tatizo, habari hii itakusaidia kujua ni nini inakufanya uogope na kujikaza ili kushinda woga huo.

^ fu. 63 MAFASIRIO YA PICHA: Watu wa kutaniko wako wenye furaha wakati wanatoa majibu wakati wa mazungumuzo ya Munara wa Mulinzi.

^ fu. 65 MAFASIRIO YA PICHA: Watu fulani wa kutaniko wenye walionyeshwa ku picha yenye kutangulia wenye walikuwa wanatoa majibu wakati wa Funzo la Munara wa Mulinzi. Hata kama kila mumoja kati yao iko na hali yake, wote wanapanga wakati wa kujifunza habari yenye itazungumuziwa ku mikutano.