Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 1

“Usihangaike, kwa Maana Niko Mungu Wako”

“Usihangaike, kwa Maana Niko Mungu Wako”

“Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe. Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako. Nitakutia nguvu, ndiyo, nitakusaidia.”​—ISA. 41:10.

WIMBO 7 Yehova, Nguvu Yetu

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. (a) Namna gani maneno ya Isaya 41:10 ilisaidia dada mumoja mwenye kuitwa Yoshiko? (b) Yehova alifanya ile maneno ichungwe kwa faida ya nani?

DADA mumoja muaminifu mwenye kuitwa Yoshiko alipata habari ya mubaya. Munganga wake alimuambia kama alikuwa anabakia na miezi kidogo ya kuishi. Alitenda namna gani? Yoshiko alikumbuka andiko la Biblia lenye alikuwa anapenda sana, ni kusema, Isaya 41:10. (Soma.) Kisha kwa utulivu, aliambia munganga wake kama hakuogopa, kwa sababu Yehova alikuwa anamukamata mukono. * Maneno yenye kutia moyo yenye kupatikana mu andiko hilo ilisaidia dada yetu mupendwa amutumainie Yehova kabisa. Andiko lilelile linaweza kutusaidia tuendelee kuwa wenye kutulia wakati tunapambana na magumu makali. Ili kuelewa namna linaweza kutusaidia, tuzungumuzie kwanza sababu gani Mungu aliongoza Isaya aandike ile maneno.

2 Mwanzoni, Yehova aliongoza Isaya aandike ile maneno ili kutia moyo Wayahudi wenye wangepelekwa Babiloni mu uhamisho. Lakini, Yehova alifanya ile maneno ichungwe, haiko tu kwa faida ya Wayahudi wenye walikuwa katika uhamisho, lakini pia kwa faida ya watu wake wote tangu wakati huo. (Isa. 40:8; Ro. 15:4) Leo, tunaishi mu “nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia,” na kuliko wakati mwingine wowote, tuko na lazima ya maneno yenye kutia moyo yenye kupatikana mu kitabu cha Isaya.​—2 Ti. 3:1.

3. (a) Ni uhakikisho gani wenye kupatikana mu Isaya 41:10, andiko lenye limechaguliwa kwa ajili ya mwaka wa 2019? (b) Juu ya nini tuko na lazima ya uhakikisho huo?

3 Mu habari hii tutazungumuzia uhakikisho tatu wenye Yehova anatupatia wenye kutia nguvu imani, wenye kupatikana mu Isaya 41:10: (1) Yehova atakuwa pamoja na sisi, (2) yeye ni Mungu wetu, na (3) atatusaidia. Tuko na lazima ya uhakikisho * huo kwa sababu kama vile Yoshiko, sisi pia tunapata magumu mu maisha. Tunapambana pia na magumu kwa sababu ya mambo ya mubaya yenye kutokea mu ulimwengu. Hata wamoja kati yetu wanateswa na serikali zenye nguvu na wanavumilia ile mateso. Tuzungumuzie basi uhakikisho huo tatu wenye kutia moyo.

“NIKO PAMOJA NA WEWE”

4. (a) Ni uhakikisho gani wa kwanza wenye tutazungumuzia? (Ona pia maelezo ya chini.) (b) Yehova anatumia maneno gani ili kutuambia namna anatuona? (c) Maneno ya Mungu inakusaidia namna gani?

4 Kwanza, Yehova anatutia moyo kupitia maneno hii: “Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe.” * Yehova anaonyesha kama iko pamoja na sisi kwa kutuhangaikia kabisa na kutuonyesha upendo wake. Ona namna anafasiria upendo wake kwetu na namna anatuona kabisa. Yehova anasema hivi: “Ulikuwa mwenye samani mbele ya macho yangu. Uliheshimiwa, na nimekupenda.” (Isa. 43:4) Hakuna kitu katika ulimwengu chenye kinaweza kufanya Yehova aache kupenda wale wenye kumutumikia; ushikamanifu wake kwetu hauwezi kutikisika hata kidogo. (Isa. 54:10) Upendo na urafiki wake vinatufanya tukuwe na uhodari kabisa. Atatulinda leo, kama vile tu alilinda rafiki yake Abramu (Abrahamu). Yehova alimuambia hivi: “Usiogope, Abramu. Mimi ni ngao kwako.”​—Mwa. 15:1.

Kwa musaada wa Yehova, tunaweza kushinda magumu yoyote yenye tunapambana nayo yenye kuwa kama maji mengi na yenye kuwa kama mwali wa moto (Picha hizi zinapatana na fungu la 5-6) *

5-6. (a) Namna gani tunajua kama Yehova anapenda kutusaidia wakati tuko na magumu? (b) Mufano wa dada Yoshiko unatufundisha nini?

5 Tunajua kama Yehova anapenda kutusaidia katika magumu yetu kwa sababu anaahidi watu wake hivi: “Wakati unapita katika maji, nitakuwa pamoja na wewe; na wakati unapita katika mito, haitakuzamisha. Wakati unatembea katika moto, hautaungua, wala mwali wa moto hautakuchoma.” (Isa. 43:2) Ile maneno iko na maana gani?

6 Yehova hatuahidi kama atatosha magumu yenye kufanya maisha ikuwe nguvu, lakini hataruhusu magumu yenye kuwa kama “mito” ituzamishe na majaribu yenye kuwa kama “mwali wa moto” ituangamize kabisa-kabisa. Anaahidi kama atakuwa pamoja na sisi, na kutusaidia ‘kupita katika’ ile magumu. Yehova atafanya nini? Atatusaidia kutuliza woga wetu ili tuendelee kuwa waaminifu-washikamanifu kwake, hata kama tunapambana na kifo. (Isa. 41:13) Yoshiko, mwenye tumekwisha kuzungumuzia alijionea jambo hilo. Mutoto wake mwanamuke anasema hivi: “Tulishangaa kuona namna Mama alikuwa mwenye kutulia kabisa. Tuliona kabisa kama Yehova alimupatia amani ya akili. Mupaka wakati Mama alikufa, alikuwa anazungumuza na wanganga na wagonjwa wengine juu ya Yehova na ahadi zake.” Mufano wa Yoshiko unatufundisha nini? Wakati tunatumainia uhakikisho huu wa Mungu: “Niko pamoja na wewe,” sisi pia tutakuwa na nguvu na uhodari wakati tunapambana na magumu.

“NIKO MUNGU WAKO”

7-8. (a) Ni uhakikisho gani wa pili wenye tutazungumuzia, na uko na maana gani? (b) Juu ya nini Yehova aliambia Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho ‘wasihangaike’? (c) Ni maneno gani yenye kupatikana mu Isaya 46:3, 4 yenye ilipaswa kutuliza mioyo ya watu wa Mungu?

7 Uhakikisho wa pili wenye Isaya aliandika ni huu: “Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako.” Ile maneno juu ya mahangaiko iko na maana gani? Mu andiko hili, neno la luga ya zamani lenye kutafsiriwa ‘kuhangaika,’ liko na wazo la “kuangalia-angalia nyuma kwa sababu ya kuogopa hatari fulani yenye inaweza kutokea” ao “kuogopa sana kama vile mutu mwenye kuwa mu hali ya hatari.”

8 Juu ya nini Yehova aliambia Wayahudi wenye wangeenda mu uhamisho Babiloni ‘wasihangaike’? Kwa sababu alijua kama wakaaji wa ile inchi wangeogopa. Ni nini ingewafanya waogope? Karibu na mwisho wa miaka 70 yenye Wayahudi wangefanya mu uhamisho, majeshi yenye nguvu ya Wamedi na Waajemi ingeshambulia Babiloni. Yehova angetumia ile majeshi ili kutosha watu wake mu uhamisho katika Babiloni. (Isa. 41:2-4) Wakati Wababiloni na watu wa mataifa ingine wenye walikuwa wanaishi wakati huo walijua kama maadui wao walikuwa wanakaribia, walijikaza kuendelea kuwa hodari kwa kuambiana hivi: “Ukuwe na nguvu.” Walifanya pia miungu mingine ya sanamu, na kutumainia kama itawalinda. (Isa. 41:5-7) Wakati huohuo, Yehova alituliza mioyo ya Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho kwa kuwaambia hivi: “Wewe, Ee Israeli, [tofauti na majirani wako] uko mutumishi wangu . . . Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako.” (Isa. 41:8-10) Ona kwamba Yehova alisema hivi: “Niko Mungu wako.” Kupitia ile maneno, Yehova alihakikishia waabudu wake washikamanifu kama hakukuwa amewasahau; alikuwa angali Mungu wao, na walikuwa wangali watu wake. Aliwaambia hivi: “Nitawachukua . . . na kuwaokoa.” Kwa kweli, ile maneno yenye kutia moyo ilitia nguvu Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho.​—Soma Isaya 46:3, 4.

9-10. Juu ya nini hatupaswe kuogopa? Leta mufano.

9 Kuliko wakati mwingine wowote, leo watu wenye kutuzunguka wako na mahangaiko sana kwa sababu hali za ulimwengu zinaendelea kuwa mubaya zaidi. Kwa kweli, sisi pia tunapatwa na magumu ileile. Lakini hatupaswe kuogopa. Yehova anatuambia hivi: “Niko Mungu wako.” Juu ya nini ile maneno inatupatia sababu kubwa ya kuendelea kuwa wenye kutulia?

10 Fikiria mufano huu: Watu wawili, Jim na Ben, wanasafiri mu ndege yenye kutikiswa-tikiswa na upepo mukali. Wakati upepo uko unatikisa-tikisa ndege, pilote anazungumuza kupitia kikuza-sauti na kusema hivi: “Mukaze mikaba (mishipi) yenu ya viti. Tutapita kwa wakati fulani mu eneo lenye kuwa na upepo mukali.” Jim anaogopa sana. Kisha pilote anasema tena: “Musihangaike. Mimi pilote wenu njo niko nasema.” Wakati Jim anasikia vile, anakataa kwa kutikisa kichwa. Anasema hivi: “Uhakikisho huo hauna maana.” Lakini, anaona kama Ben hahangaike hata kidogo. Jim anamuuliza hivi: “Juu ya nini hauogope?” Ben anaonyesha sura ya kicheko na kusema hivi: “Ni kwa sababu ninamujua muzuri sana pilote huyu. Ni baba yangu!” Kisha Ben anasema hivi: “Acha nikuelezee juu ya baba yangu. Niko hakika kama wakati utamujua na kujua uwezo wake, na wewe hautaogopa.”

11. Mufano wa watu wawili wenye kusafiri mu ndege, unaweza kutufundisha nini?

11 Mufano huo unaweza kutufundisha nini? Kama Ben, hatuogope kwa sababu tunamujua muzuri sana, Yehova, Baba yetu wa mbinguni. Tunajua kama atatuongoza kwa usalama ili tushinde magumu yenye kuwa kama upepo mukali yenye tunapata mu siku za mwisho za ulimwengu huu. (Isa. 35:4) Tunamutumainia Yehova, kwa hiyo tunaweza kubakia wenye kutulia wakati wengine katika ulimwengu wanazimia kwa sababu ya woga. (Isa. 30:15) Pia, tunatenda kama Ben wakati tunaelezea majirani wetu sababu za kumutumainia Mungu. Kwa hiyo, wao pia wanaweza kuwa hakika kwamba, hata kama wanapatwa na magumu ya namna gani, Yehova atawategemeza.

“NITAKUTIA NGUVU [NA] NITAKUSAIDIA”

12. (a) Ni uhakikisho gani wa tatu wenye tutazungumuzia? (b) Maneno “mukono” wa Yehova, inatukumbusha jambo gani?

12 Fikiria uhakikisho wa tatu wenye Isaya aliandika: “Nitakutia nguvu, ndiyo, nitakusaidia.” Isaya alikuwa amefasiria namna Yehova angetia nguvu watu wake; alisema hivi: “Yehova atakuja na nguvu, na mukono wake utatawala kwa ajili yake.” (Isa. 40:10) Mara mingi, Biblia inatumia neno “mukono” kwa njia ya mufano ili kumaanisha nguvu. Kwa hiyo, maneno “mukono [wa Yehova] utatawala” inatukumbusha kama Yehova ni Mufalme mwenye nguvu. Alitumia nguvu zake zenye haziwezi kushindwa ili kutegemeza na kupigania watumishi wake wa wakati wa zamani, na ataendelea kutia nguvu na kulinda wale wenye kumutumainia leo.​—Kum. 1:30, 31; Isa. 43:10, maelezo ya chini.

Hakuna silaha yenye itashinda mukono wenye nguvu wa Yehova wenye kutoa ulinzi (Picha hii inapatana na fungu la 12-16) *

13. (a) Yehova anatimiza ahadi yake ya kututia nguvu, zaidi sana wakati gani? (b) Ni ahadi gani yenye kututia nguvu kabisa na kutufanya tusiogope?

13 Yehova anatimiza ahadi yake ya ‘kututia nguvu,’ zaidi sana wakati maadui wanatutesa. Leo, mu sehemu fulani za dunia, maadui wetu wanajikaza sana kusimamisha kazi yetu ya kuhubiri ao kukataza tengenezo letu. Hata hivyo, ile mashambulizi haituhangaishe sana. Yehova ametupatia ahadi yenye inatutia nguvu kabisa na kutufanya tusiogope. Anatuahidi hivi: “Hakuna silaha yenye itafanywa juu yako yenye itafanikiwa.” (Isa. 54:17) Ile maneno inatukumbusha mambo tatu ya maana.

14. Juu ya nini hatushangae kuona maadui wa Mungu wanatushambulia?

14 Kwanza, kwa sababu sisi ni wanafunzi wa Kristo, tunajua kama watu watatuchukia. (Mt. 10:22) Yesu alitabiri kama wanafunzi wake watateswa sana mu siku za mwisho. (Mt. 24:9; Yoh. 15:20) Pili, unabii wa Isaya ulituonya mbele ya wakati kama, zaidi ya kutuchukia, maadui wetu watatumia silaha mbalimbali ili kutushambulia. Kati ya silaha hizo kuko udanganyifu wenye hauko wazi, uongo wa waziwazi, na mateso makali. (Mt. 5:11) Yehova hatazuia maadui wetu wasitumie silaha hizo ili kutupiganisha. (Efe. 6:12; Ufu. 12:17) Lakini hatupaswe kuogopa. Juu ya nini?

15-16. (a) Ni jambo gani la tatu lenye tunapaswa kukumbuka, na namna gani andiko la Isaya 25:4, 5 linaunga mukono jambo hilo? (b) Kulingana na Isaya 41:11, 12, wale wenye kutupiganisha watapatwa na nini?

15 Fikiria jambo la tatu lenye tunapaswa kukumbuka. Yehova alisema kama “hakuna silaha” yenye inatumiwa juu yetu yenye “itafanikiwa.” Kama vile ukuta unatulinda wakati wa zoruba ya mvua yenye kuleta uharibifu, ni vile Yehova anatulinda juu ya “mulipuko wa watu wenye kuonea.” (Soma Isaya 25:4, 5.) Maadui wetu hawataweza hata siku moja kutuangamiza kabisa-kabisa.​—Isa. 65:17.

16 Tena, Yehova anatusaidia tumutumainie zaidi kwa kutuelezea waziwazi mambo yenye itawapata wale wenye “kuwaka kasirani juu” yetu. (Soma Isaya 41:11, 12.) Hata maadui wetu watupiganishe namna gani ao vita ikuwe kali namna gani, matokeo ni ileile: Maadui wote wa watu wa Mungu “watafanywa kuwa bure na wataharibiwa.”

TUNAWEZA KUFANYA NINI ILI KUMUTUMAINIA YEHOVA ZAIDI?

Kusoma Biblia kwa ukawaida kunaweza kutusaidia tumutumainie Yehova zaidi (Picha hii inapatana na fungu la 17-18) *

17-18. (a) Namna gani kusoma Biblia kunaweza kutusaidia tumutumainie Mungu zaidi? Leta mufano. (b) Kufikiri sana juu ya andiko la mwaka wa 2019, kunaweza kutuletea faida gani?

17 Ili kumutumainia Yehova zaidi, tunapaswa kujikaza kumujua muzuri zaidi. Na njia moja ya kumujua Mungu muzuri kabisa ni kusoma Biblia kwa uangalifu na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma. Biblia inazungumuzia habari ya kweli juu ya namna Yehova alilinda watu wake wakati wa zamani. Ile habari inatusaidia tukuwe hakika kama Yehova atatuhangaikia leo.

18 Fikiria maneno ya muzuri sana ya mufano yenye Isaya anatumia ili kuonyesha namna Yehova anatulinda. Anazungumuzia Yehova kuwa muchungaji na watumishi wa Mungu kuwa wana-kondoo. Isaya anasema hivi juu ya Yehova: “Atakusanya wana-kondoo kwa mukono wake, na atawabeba kwenye kifua chake.” (Isa. 40:11) Wakati tunasikia kuwa mikono ya Yehova inatuzunguka, tunajisikia kuwa wenye kulindwa na wenye kutulia. Ili kutusaidia tuendelee kuwa wenye kutulia hata kama tunapatwa na magumu, mutumwa muaminifu na mwenye busara amechagua andiko la Isaya 41:10 ili likuwe andiko la mwaka wa 2019. Linasema hivi: “Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako.” Ufikiri sana juu ya ile maneno yenye kutia moyo. Itakutia nguvu wakati utapambana na magumu yenye kuwa mbele.

WIMBO 38 Atakupa Nguvu

^ fu. 5 Andiko la mwaka lenye lilichaguliwa kwa ajili ya mwaka wa 2019 linatupatia sababu tatu za kuendelea kuwa wenye kutulia hata kama mambo ya mubaya inatokea mu ulimwengu ao mu maisha yetu. Habari hii itazungumuzia sababu hizo na itatusaidia tusihangaike sana na tumutumainie Yehova zaidi. Fikiri sana juu ya andiko la mwaka. Uliweke katika akili yako kama unaweza. Litakusaidia kupambana na magumu yenye utapata wakati wenye kuja.

^ fu. 3 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Uhakikisho ni maneno ya kweli ao ahadi yenye kuonyesha kama jambo fulani litatokea kabisa-kabisa. Uhakikisho wenye Yehova anatupatia unaweza kutusaidia tusihangaike sana juu ya magumu yenye inaweza kutokea mu maisha yetu.

^ fu. 4 MAELEZO YA CHINI: Neno “Usiogope” linatumiwa mara tatu mu Isaya 41:10, 13, na 14. Andiko lilelile linasema pia “kwa maana niko pamoja na wewe,” “kwa maana niko Mungu wako,” na “nitakusaidia.” Juu ya nini Yehova alimuongoza Isaya kupitia roho yake ili aandike ile maneno? Ili kukazia jambo hili la maana: kama tu tunamutegemea Yehova hatuwezi kuendelea kuogopa sana.

^ fu. 52 MAFASIRIO YA PICHA: Watu wa familia wanapambana na magumu kwenye kazi, wanapambana na matatizo ya afya, wanapambana na magumu mu mahubiri, na kwenye masomo.

^ fu. 54 MAFASIRIO YA PICHA: Polisi wanashambulia ndugu na dada wenye wanafanya mukutano mu nyumba ya Shahidi fulani, lakini ndugu na dada hawaogope.

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Kufanya Ibada ya Familia kwa ukawaida kunatutia nguvu ili tuvumilie.