Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 2

Unaweza Kuwa “Chanzo cha Faraja Nyingi”

Unaweza Kuwa “Chanzo cha Faraja Nyingi”

‘Hawa ndio wafanyakazi wenzangu kwa ajili ya Ufalme wa Mungu, na wamekuwa chanzo cha faraja nyingi kwangu.’​—KOL. 4:11.

WIMBO 90 Tianeni Moyo

KIFUPI CHA HABARI *

1. Ni magumu gani yenye kuleta mahangaiko yenye watumishi wengi waaminifu wa Yehova wako wanapata?

KATIKA dunia yote, watumishi wengi wa Yehova wako wanapata magumu yenye inawafanya wakuwe na mahangaiko na hata huzuni. Umetambua jambo hilo mu kutaniko lenu? Wakristo fulani wako na ugonjwa wa nguvu ao wanahuzunika juu ya kifo cha mutu mwenye wanapenda. Wengine wako na huzuni sana kwa sababu mutu wa familia yao ao rafiki yao wa sana ameacha kweli. Na wengine wako wanateseka juu ya matokeo ya misiba ya asili. Ndugu na dada hao wote wako na lazima ya kufarijiwa. Namna gani tunaweza kuwasaidia?

2. Juu ya nini wakati fulani mutume Paulo alikuwa na lazima ya kufarijiwa?

2 Mara mingi uzima wa mutume Paulo ulikuwa mu hatari. (2 Ko. 11:23-28) Pia, alipaswa kuvumilia “mwiba katika mwili,” pengine tatizo fulani la afya. (2 Ko. 12:7) Na alipaswa kuvumilia hali ya kuvunjika moyo wakati Dema, ndugu mumoja mwenye alitumika naye wakati fulani, alimuacha “kwa sababu [Dema] alipenda mupangilio wa mambo wa sasa.” (2 Ti. 4:10) Hata kama Paulo alikuwa Mukristo mutiwa-mafuta mwenye uhodari na mwenye alisaidia sana wengine, wakati fulani alijisikia kuwa mwenye kuvunjika moyo.​—Ro. 9:1, 2.

3. Ni nani walimufariji Paulo na kumutia moyo?

3 Paulo alipata kitia-moyo na faraja yenye alikuwa nayo lazima. Namna gani? Kwa kweli, Yehova alitumia roho yake takatifu ili kumutia nguvu. (2 Ko. 4:7; Flp. 4:13) Yehova alitumia pia Wakristo wenzake ili kumufariji. Paulo alisema kama wafanyakazi wenzake fulani walikuwa “chanzo cha faraja nyingi.” (Kol. 4:11) Kati ya wale wenye alitaja majina yao kulikuwa Aristarko, Tikiko, na Marko. Walimutia Paulo nguvu, na hilo lilimusaidia avumilie magumu. Ni sifa gani zilisaidia Wakristo hao watatu wakuwe wenye kufariji sana? Namna gani tunaweza kufuata mufano wao muzuri wakati tunajikaza kufarijiana na kutiana moyo?

UKUWE MUSHIKAMANIFU KAMA ARISTARKO

Kama Aristarko, tunaweza kuwa marafiki washikamanifu kwa kushikamana na ndugu na dada zetu “nyakati za taabu” (Ona fungu la 4-5) *

4. Namna gani Aristarko alijionyesha kuwa rafiki mushikamanifu kwa Paulo?

4 Aristarko, Mukristo kutoka mu muji wa Tesalonike, wenye ulikuwa katika Makedonia, alijionyesha kuwa rafiki mushikamanifu kwa Paulo. Biblia inamutaja Aristarko kwa mara ya kwanza wakati Paulo alitembelea Efeso katika safari yake ya tatu ya umisionere. Wakati Aristarko alimusindikiza Paulo, alikamatwa na kikundi cha watu wenye jeuri. (Mdo. 19:29) Wakati aliachiliwa, hakumuacha Paulo ili kuepuka hatari lakini alishikamana naye. Miezi fulani kisha pale, katika Ugiriki, Aristarko alikuwa angali pamoja na Paulo hata kama wapinzani waliendelea kutafuta kumuua Paulo. (Mdo. 20:2-4) Mu mwaka wa 58 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, wakati Paulo alipelekwa Roma akiwa mufungwa, Aristarko alimusindikiza katika safari hiyo ya murefu, na walivumilia pamoja magumu ya kuvunjikiwa mashua. (Mdo. 27:1, 2, 41) Wakati walifika Roma, inaonekana alipitisha wakati fulani pamoja na Paulo mu gereza. (Kol. 4:10) Njo maana haishangaze kuona kama Paulo alijisikia kuwa mwenye kutiwa moyo na mwenye kufarijiwa na rafiki kama huyo mushikamanifu!

5. Kulingana na Mezali 17:17, namna gani tunaweza kuwa marafiki washikamanifu?

5 Kama Aristarko, tunaweza kuwa marafiki washikamanifu kwa kushikamana na ndugu na dada zetu hapana tu wakati muzuri lakini pia “nyakati za taabu.” (Soma Mezali 17:17.) Hata wakati magumu inaisha, ndugu na dada yetu anaweza kuwa angali na lazima ya kufarijiwa. Frances, * mwenye baba yake na mama yake walikufa katika muda wa miezi tatu kwa sababu ya kansere, anasema hivi: “Ninawaza kama magumu ya nguvu inatufanya tuteseke kwa muda murefu. Niko mwenye shukrani kwa marafiki washikamanifu wenye wanakumbuka kama ningali na maumivu, hata kama kumepita wakati fulani tangu wazazi wangu walikufa.”

6. Kama tuko washikamanifu, tutafanya nini?

6 Rafiki washikamanifu wanajitoa kabisa ili kusaidia ndugu na dada zao. Kwa mufano, munganga alimuambia ndugu mumoja mwenye kuitwa Peter kama alikuwa na ugonjwa mubaya wenye ungefikia kumuua. Bibi yake, Kathryn, anasema hivi: “Ndugu mumoja na bibi yake wa kutaniko letu walitusindikiza kwa munganga kwenye ugonjwa wa Peter ulivumbuliwa. Palepale waliamua kama hawatatuacha tuvumilie ile magumu sisi wenyewe, na wamekuwa pamoja na sisi kila wakati wenye tumekuwa na lazima yao.” Inafariji kabisa kuwa na marafiki wa kweli, wenye wanaweza kutusaidia kuvumilia magumu!

UKUWE MWENYE KUTUMAINIKA KAMA TIKIKO

Kama Tikiko, tunaweza kuwa marafiki wenye kutumainika wakati wengine wanapambana na magumu (Ona fungu la 7-9) *

7-8. Kulingana na Wakolosai 4:7-9, namna gani Tikiko alijionyesha kuwa mwenye kutumainika?

Tikiko, Mukristo kutoka jimbo la Roma la Asia, alikuwa kabisa rafiki mwenye kutumainika kwa Paulo. (Mdo. 20:4) Mu mwaka wa 55 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, Paulo alifanya mupango wa kukusanya michango ili kusaidia Wakristo wa Yudea, na inawezekana aliacha Tikiko ashugulikie mugao huo wa maana. (2 Ko. 8:18-20) Kisha, wakati Paulo alikuwa anafungwa katika Roma kwa mara ya kwanza, Paulo alimutumia Tikiko kuwa mujumbe wake. Alipelekea makutaniko ya Asia barua za Paulo na ujumbe wake wa kitia-moyo.​—Kol. 4:7-9.

Tikiko aliendelea kuwa rafiki mwenye kutumainika wa Paulo. (Tit. 3:12) Haiko Wakristo wote wa wakati huo njo walikuwa wenye kutumainika kama Tikiko. Karibu mwaka wa 65 kisha kuzaliwa kwa Yesu, wakati Paulo alifungwa kwa mara ya pili, aliandika kama wanaume wengi Wakristo katika jimbo la Asia waliepuka kupitisha wakati pamoja naye, inawezekana juu ya kuogopa wapinzani. (2 Ti. 1:15) Lakini, Paulo angeweza kumutumainia Tikiko na alimupatia mugao mwingine. (2 Ti. 4:12) Kwa kweli, Paulo alifurahia kuwa na rafiki muzuri kama Tikiko.

9. Namna gani tunaweza kumuiga Tikiko?

9 Tunaweza kumuiga Tikiko kwa kuwa marafiki wenye kutumainika. Kwa mufano, hatuahidi tu kama tutasaidia ndugu na dada zetu wenye kuwa na lazima ya musaada lakini tunafanya pia mambo fulani ili kuwasaidia. (Mt. 5:37; Lu. 16:10) Wakati wale wenye kuwa na lazima ya musaada wanajua kama tutawasaidia, wanajisikia kuwa wenye kufarijika kabisa. Dada mumoja anafasiria sababu. Anasema hivi: “Unajisikia kuwa mwenye kutulia kwa sababu unajua kama mutu mwenye aliahidi kukusaidia atafanya vile kwa wakati wenye kufaa.”

10. Kulingana na Mezali 18:24, wale wenye kupambana na magumu fulani ao hali ya kuvunjika moyo wanaweza kupata faraja wapi?

10 Wale wenye kupambana na magumu fulani ao hali ya kuvunjika moyo, mara mingi wanapata faraja kwa kumuelezea rafiki mwenye kutumainika magumu yao. (Soma Mezali 18:24.) Bijay, mwenye alivunjika moyo wakati mutoto wake mwanaume alitengwa na kutaniko, anasema hivi: “Nilikuwa na lazima ya kumuambia mutu fulani mwenye ninatumainia namna nilikuwa ninajisikia.” Carlos alipoteza pendeleo fulani lenye alipenda sana katika kutaniko kwa sababu alifanya kosa fulani. Anasema hivi: “Nilikuwa na lazima ya watu wenye ningeongea nao waziwazi bila kuogopa kama watanihukumu-hukumu.” Carlos aliona kama anaweza kuongea na wazee, na walimusaidia kushinda tatizo lake. Alifarijiwa pia kwa kujua kama wazee walikuwa na busara na wangechunga siri.

11. Tunapaswa kufanya nini ili tukuwe marafiki wenye kutumainika wenye wengine wanaweza kufunulia siri?

11 Ili tukuwe marafiki wenye kutumainika wenye wengine wanaweza kufunulia siri, tunapaswa kuwa na sifa ya uvumilivu. Wakati bwana ya Zhanna alimuacha, Zhanna alipata faraja kwa kuambia marafiki wa sana namna alikuwa anajisikia. Anasema hivi: “Walinisikiliza kwa uvumilivu hata kama inawezekana nilikuwa ninasema mambo ileile tena na tena.” Na wewe unaweza kuonyesha kama uko rafiki muzuri kwa kusikiliza wengine muzuri.

UKUWE TAYARI KUTUMIKIA WENGINE KAMA MARKO

Matendo ya wema ya Marko ilimusaidia Paulo avumilie, na sisi tunaweza kusaidia ndugu na dada zetu wakati wa musiba (Ona fungu la 12-14) *

12. Marko alikuwa nani, na namna gani alionyesha roho ya kujitoa?

12 Marko alikuwa Mukristo Muyahudi kutoka Yerusalemu. Binamu yake Barnaba alikuwa misionere mwenye kujulikana sana. (Kol. 4:10) Inaonekana kuwa familia ya Marko ilikuwa tajiri, lakini Marko hakutia vitu vya kimwili pa nafasi ya kwanza mu maisha yake. Mu maisha yake yote, Marko alionyesha roho ya kujitoa. Alifurahia kutumikia wengine. Kwa mufano, kwa wakati mbalimbali alitumika pamoja na mutume Paulo na mutume Petro wakati walikuwa wanatimiza migao yao; inawezekana Marko alikuwa anawasaidia kupata vitu vya kimwili vyenye walikuwa navyo lazima. (Mdo. 13:2-5; 1 Pe. 5:13) Paulo alisema kama Marko alikuwa mumoja wa ‘wafanyakazi wenzake kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,’ na “musaada wenye kutia nguvu” kwake.​—Kol. 4:10, 11, maelezo ya chini.

13. Namna gani andiko la 2 Timoteo 4:11 linaonyesha kama Paulo alifurahia namna Marko alitumika kwa uaminifu?

13 Marko alifikia kuwa mumoja kati ya marafiki wa sana wa Paulo. Kwa mufano, wakati Paulo alikuwa anafungwa kwa mara ya mwisho katika Roma, karibu mwaka wa 65 kisha kuzaliwa kwa Yesu, alimuandikia Timoteo barua yake ya pili. Katika barua hiyo, Paulo alimuomba Timoteo akuje Roma pamoja na Marko. (2 Ti. 4:11) Bila shaka, Paulo alifurahia namna Marko alitumika pamoja na yeye kwa uaminifu zamani, njo maana alipenda Marko akuwe pamoja na yeye katika wakati huo wa maana. Marko alimusaidia Paulo mu njia fulani za maana, pengine alikuwa anamusaidia kupata chakula na vitabu vya kukunjwa na wino. Inawezekana namna Marko alimusaidia Paulo na kumutia moyo ilimusaidia avumilie siku za mwisho za maisha yake mupaka wakati aliuawa.

14-15. Andiko la Matayo 7:12 linatufundisha nini juu ya namna tunaweza kusaidia wengine katika njia zenye kufaa?

14 Soma Matayo 7:12. Wakati tunapambana na magumu, tunakuwa wenye shukrani sana kwa wale wenye wanafanya mambo fulani ili kutusaidia! Ryan, mwenye baba yake alikufa kwa kushitukia katika aksidenti ya mubaya sana, anasema hivi: “Kuko mambo mingi yenye tunazoea kufanya kila siku yenye inaonekana kuwa nguvu kufanya wakati tuko na magumu. Hata musaada wenye kufaa, wenye kuonekana kuwa kidogo, unaweza kusaidia sana.”

15 Kama tuko waangalifu na watazamaji, inawezekana tutapata namna zenye kufaa za kusaidia wengine. Kwa mufano, dada mumoja alifanya mipango ya kusaidia Peter na Kathryn, wenye tumekwisha kuzungumuzia, kila wakati walikuwa na lazima ya kuonana na munganga. Peter na Kathryn hawangeweza kutembeza tena motokari, kwa hiyo alifanya programu ili kila ndugu ao dada mwenye alijitolea kuwatembeza akuwe na siku yake ya kufanya vile. Je, mupango huo ulisaidia? Kathryn anasema hivi: “Tulisikia kama vile muzigo muzito umetoka ku mabega yetu.” Sikuzote, ukumbuke kama unaweza kufariji wengine sana wakati unafanya hata mambo ya kidogo-kidogo ili kuwasaidia.

16. Mufano wa Marko unatufundisha somo gani la maana juu ya kufariji wengine?

16 Marko, mwanafunzi Mukristo mwenye aliishi wakati wa mitume, alikuwa na mambo mingi ya kufanya. Alikuwa na mambo ya maana ya kufanya katika kazi ya Yehova, kutia ndani kuandika Injili yenye kuitwa kwa jina lake. Hata hivyo, Marko alitafuta wakati wa kumufariji Paulo, na Paulo alijisikia huru kumuomba Marko musaada. Angela, mwenye alipaswa kuvumilia huzuni yenye alipata wakati mutu mumoja wa familia yake aliuawa, alikuwa mwenye shukrani sana kwa wale wenye walikuwa tayari kumufariji. Anasema hivi: “Wakati marafiki wanapenda kabisa kusaidia, iko mwepesi kuzungumuza nao. Wanaonekana kuwa tayari kusaidia na hawasite kufanya vile.” Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Ninajulikana kuwa mutu mwenye kuwa tayari kufariji ndugu na dada zangu katika njia zenye kufaa?’

UAZIMIE KUFARIJI WENGINE

17. Namna gani kufikiri juu ya andiko la 2 Wakorinto 1:3, 4 kunaweza kutuchochea tufariji wengine?

17 Ni mwepesi sana kujua ndugu na dada wenye kuwa na lazima ya faraja. Tunaweza hata kutumia maneno yenye kutia moyo yenye wengine wametumia ili kutufariji. Nino, dada mumoja mwenye alifiwa na tate (nkambo) yake mwanamuke, anasema hivi: “Yehova anaweza kututumia ili kufariji wengine kama tunajiacha atutumie.” (Soma 2 Wakorinto 1:3, 4.) Frances, mwenye tumekwisha kuzungumuzia, anasema hivi: “Maneno ya 2 Wakorinto 1:4 ni ya kweli kabisa. Tunaweza kufariji wengine kupitia faraja yenye tunapata.”

18. (a) Juu ya nini watu fulani wanaweza kuogopa kufariji wengine? (b) Namna gani tunaweza kufariji wengine kabisa? Leta mufano.

18 Tunapaswa kutafuta njia za kufariji wengine hata kama tuko na woga. Kwa mufano, tunaweza kuogopa kwamba hatujue mambo ya kusema ao ya kufanya ili kufariji mutu fulani mwenye kuwa na magumu. Muzee mumoja wa kutaniko mwenye kuitwa Paul anakumbuka namna wengine walijikaza sana ili kumufariji wakati baba yake alikufa. Anasema hivi: “Niliona kama haikukuwa mwepesi kwao kuja na kuzungumuza na mimi. Hawakujua waseme nini. Lakini, nilifurahia nia yenye walikuwa nayo ya kunifariji na kunitia moyo.” Vilevile, kisha tetemeko kubwa la inchi, ndugu mumoja mwenye kuitwa Tajon alisema hivi: “Sikumbuke kabisa kila ujumbe wenye watu walinitumia mu siku zenye zilifuata tetemeko la inchi, lakini ninakumbuka kama walihangaika sana ili kujua ikiwa nilikuwa salama.” Tunaweza kufariji wengine kabisa kama tunaonyesha kuwa tunawahangaikia.

19. Juu ya nini unaazimia kuwa “chanzo cha faraja nyingi”?

19 Kadiri tunaendelea kukaribia mwisho wa mupangilio huu wa mambo, hali za ulimwengu zitaendelea kuharibika na maisha itakuwa nguvu zaidi. (2 Ti. 3:13) Na magumu yenye tunajiletea kwa sababu ya zambi yenye tuliriti na hali yetu ya kukosa kukamilika inaonyesha pia kama tutaendelea kuwa na lazima ya faraja. Sababu moja yenye ilimusaidia mutume Paulo avumilie kwa uaminifu mupaka mwisho wa maisha yake, ni faraja yenye Wakristo wenzake walimutolea. Tukuwe basi washikamanifu kama Aristarko, wenye kutumainika kama Tikiko, na tayari kutumikia wengine kama Marko. Kama tunafanya vile, tunaweza kusaidia ndugu na dada zetu wabakie imara katika imani.​—1 Te. 3:2, 3.

^ fu. 5 Mutume Paulo alipata magumu mingi katika maisha yake. Wakati wa magumu, wafanyakazi fulani wenzake walimufariji sana. Tutazungumuzia sifa tatu zenye zilisaidia wafanyakazi hao wakuwe na uwezo wa kufariji wengine. Tutazungumuzia pia ni katika njia gani tunaweza kufuata mufano wao.

^ fu. 5 Majina fulani imebadilishwa katika habari hii.

WIMBO 111 Sababu za Kuwa na Shangwe

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Aristarko na Paulo wanavumilia pamoja magumu ya kuvunjikiwa mashua.

^ fu. 58 MAFASIRIO YA PICHA: Tikiko alipewa mugao wa kupelekea makutaniko barua za Paulo.

^ fu. 60 MAFASIRIO YA PICHA: Marko alimusaidia Paulo katika njia zenye kufaa.