Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 2

Mambo Yenye Tunajifunza Kupitia “Mwanafunzi Mwenye Yesu Alipenda”

Mambo Yenye Tunajifunza Kupitia “Mwanafunzi Mwenye Yesu Alipenda”

“Tuendelee kupendana, kwa sababu upendo unatoka kwa Mungu.”​—1 YO. 4:7.

WIMBO 105 “Mungu Ni Upendo”

KIFUPI CHA HABARI *

1. Upendo wa Mungu unatufanya tujisikie namna gani?

MUTUME Yohana aliandika hivi: “Mungu ni upendo.” (1 Yo. 4:8) Ile maneno kidogo inatukumbusha kweli hii ya maana: Kama vile uzima unatoka kwa Mungu, upendo pia unatoka kwake. Yehova anatupenda. Upendo wake unatufanya tujisikie kuwa salama, wenye furaha, na wenye kutosheka.

2. Kulingana na Matayo 22:37-40, amri mbili kubwa ni gani, na juu ya nini inaweza kuwa nguvu kutii amri ya pili?

2 Kwa Mukristo, kuonyesha upendo ni amri. Haiko jambo lenye anaweza kufanya ikiwa tu anapenda. (Soma Matayo 22:37-40.) Wakati tunamujua Yehova muzuri, inakuwa mwepesi kutii amri ya kwanza. Ni mwepesi kumupenda Yehova kwa sababu yeye ni mukamilifu, anatuhangaikiaka na anatutendeaka muzuri. Lakini inaweza kuwa nguvu kutii amri ya pili. Juu ya nini? Juu ndugu na dada zetu, wenye wako kati ya majirani wetu wa karibu, ni watu wenye hawakamilike. Wakati fulani, wanaweza kusema ao kufanya mambo yenye haitufurahishe. Yehova alijua kama haitakuwa mwepesi kwetu kutii amri ya pili. Njo maana aliongoza waandikaji fulani wa Biblia waandike mashauri yenye inaonyesha juu ya nini tunapaswa kupendana na namna tunaweza kufanya vile. Yohana iko kati ya wale waandikaji.​—1 Yo. 3:11, 12.

3. Yohana alikazia nini?

3 Katika maandishi yake, Yohana alikazia kama Wakristo wanapaswa kuonyesha upendo. Ile inaonekana mu Injili yenye aliandika. Alizungumuzia sana upendo kuliko waandikaji wa Injili zingine tatu. Yohana alikuwa na miaka mia moja hivi wakati aliandika Injili yake na barua zake tatu. Ile maandishi yenye iliongozwa na roho ya Mungu inaonyesha kama upendo njo unapaswa kuchochea mambo yote yenye tunafanya. (1 Yo. 4:10, 11) Lakini, iliombaka wakati ili Yohana afikie kuelewa vile.

4. Wakati Yohana alikuwa kijana, je, kila mara alikuwa anaonyesha upendo?

4 Wakati Yohana alikuwa kijana, haiko kila mara njo alikuwa anaonyesha upendo. Kwa mufano, wakati fulani, Yesu na wanafunzi wake walipita Samaria wakati walikuwa wanaenda Yerusalemu. Watu wa kijiji fulani cha Samaria walikataa kuwakaribisha. Yohana alitenda namna gani? Yeye pamoja na ndugu yake Yakobo waliuliza Yesu ikiwa wanaweza kuita moto ushuke kutoka mbinguni ili kuharibu watu wote wa kile kijiji! (Lu. 9:52-56) Wakati ingine, Yohana alishindwa kuonyesha mitume wenzake upendo. Inawezekana yeye na ndugu yake Yakobo, walimuchochea mama yao amuombe Yesu awapatie vyeo vya juu katika Ufalme. Wakati mitume wengine walijua mambo yenye Yakobo na Yohana walifanya, walikasirika sana! (Mt. 20:20, 21, 24) Lakini, hata kama wakati fulani Yohana alishindwa kuonyesha upendo, Yesu alimupenda.​—Yoh. 21:7.

5. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

5 Mu hii habari, tutazungumuzia mufano wa Yohana na mambo fulani yenye aliandika kuhusu upendo. Kufanya vile kutatusaidia tujue namna tunaweza kuonyesha ndugu na dada zetu upendo. Tutazungumuzia pia jambo la maana lenye vichwa vya familia wanapaswa kufanya ili kuonyesha kama wanapenda watu wa familia zao.

ONYESHA UPENDO KUPITIA MATENDO

Yehova alionyesha kama anatupenda kwa kutuma Mwana wake ku dunia ili akufe kwa ajili yetu (Ona fungu la 6-7)

6. Yehova alifanya nini ili kuonyesha kama anatupenda?

6 Mara mingi tunawazaka kama kupenda mutu ni kumufurahia na kumuambia maneno ya muzuri. Lakini kama tunapenda kabisa mutu fulani, tunapaswa kuonyesha jambo hilo kupitia matendo yetu. (Linganisha na Yakobo 2:17, 26.) Kwa mufano, Yehova anatupenda. (1 Yo. 4:19) Na anaonyesha kama anatupenda kupitia maneno ya muzuri yenye aliandikisha katika Neno lake. (Zb. 25:10; Ro. 8:38, 39) Lakini, jambo lenye linatuhakikishia kama anatupenda haiko tu maneno yenye anatuambia, lakini pia mambo yenye anatufanyia. Yohana aliandika hivi: “Kwa jambo hili upendo wa Mungu ulifunuliwa kwetu, kwamba Mungu alimutuma Mwana wake muzaliwa-pekee katika ulimwengu ili tupate uzima kupitia yeye.” (1 Yo. 4:9) Yehova alimutuma Mwana wake mupendwa ili ateseke na kufa kwa ajili yetu. (Yoh. 3:16) Bila shaka, Yehova anatupenda kabisa.

7. Yesu alifanya nini ili kuonyesha kama anatupenda?

7 Yesu alihakikishia wanafunzi wake kama alikuwa anawapenda. (Yoh. 13:1; 15:15) Alionyesha kama anawapenda kabisa kupitia maneno na pia matendo yake. Alisema hivi: “Hakuna mwenye iko na upendo mukubwa kuliko huu, kwamba mutu atoe uzima wake kwa ajili ya marafiki wake.” (Yoh. 15:13) Kufikiria mambo yenye Yehova na Yesu wametufanyia, kunapaswa kutuchochea tufanye nini?

8. 1 Yohana 3:18 inasema kama tunapaswa kufanya nini?

8 Tunaonyesha kama tunapenda Yehova na Yesu wakati tunawatii. (Yoh. 14:15; 1 Yo. 5:3) Yesu alituambia waziwazi kama tunapaswa kupendana. (Yoh. 13:34, 35) Tunapaswa kuonyesha ndugu na dada zetu kama tunawapenda kupitia matendo yetu, haiko tu kupitia maneno. (Soma 1 Yohana 3:18.) Ni mambo gani fulani yenye tunaweza kufanya ili kuonyesha kama tunawapenda?

PENDA NDUGU NA DADA ZAKO

9. Upendo ulichochea Yohana kufanya nini?

Yohana angependa, angebakia na baba yake mu kazi ya kuvua samaki na angepata feza mingi. Lakini kuliko kufanya vile, alitumia maisha yake ili kusaidia wengine wajifunze kweli kuhusu Yehova na Yesu. Maisha yenye Yohana alichagua haikukuwa mwepesi. Aliteswa, na ku mwisho wa karne ya kwanza wakati alikuwa amezeeka, alifungwa. (Mdo. 3:1; 4:1-3; 5:18; Ufu. 1:9) Wakati alikuwa katika kifungo kwa sababu ya kuhubiri habari njema kumuhusu Yesu, Yohana alionyesha kama alikuwa anapenda wengine. Kwa mufano, wakati alikuwa mu kisiwa cha Patmo, aliandika kitabu cha Ufunuo na akakitumia makutaniko ili waweze kujua mambo yenye ‘yangepaswa kutendeka karibuni.’ (Ufu. 1:1) Kisha, Yohana aliandika Injili yake kuhusu maisha na utumishi wa Yesu. Inaonekana alifanya vile kisha kufunguliwa kutoka mu kisiwa cha Patmo. Aliandika pia barua tatu ili kutia moyo ndugu na dada zake na kuwatia nguvu. Unaweza kufanya nini ili kuiga roho ya kujitoa yenye Yohana alionyesha?

10. Unaweza kufanya nini ili kuonyesha kama unapenda wengine?

10 Namna unachagua kutumia maisha yako inaweza kuonyesha kama unapenda wengine. Mu ulimwengu huu wa Shetani, watu wanaweza kukuchochea utumie wakati na nguvu yako ili kutafuta faida yako mwenyewe kwa kujikaza kupata feza mingi ao kujulikana. Kuliko kufanya vile, wahubiri wenye kujitoa mu dunia yote wanatumia wakati mingi kadiri wanaweza ili kuhubiri habari njema na kusaidia watu wamukaribie Yehova. Na hata wamoja wanajikaza sana mu kazi ya kuhubiri na kufundisha wakiwa watumishi wa wakati wote.

Tunaonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu na watu wa familia yetu kupitia mambo yenye tunawafanyia (Ona fungu la 11, 17) *

11. Namna gani Wakristo wengi waaminifu wanaonyesha kama wanamupenda Yehova na ndugu na dada zao?

11 Wakristo wengi waaminifu wanapaswa kutumika saa mingi ili wapate mahitaji yao na ya familia zao. Hata vile, wanajikaza kutegemeza tengenezo la Mungu kulingana na uwezo wao. Kwa mufano, wamoja wanasaidia kutoa misaada wakati wa misiba, wengine wanasaidia mu kazi za ujenzi, na kila mutu anaweza kutoa michango ili kutegemeza kazi ya mu dunia yote. Wanafanya ile yote kwa sababu wanamupenda Mungu na jirani. Kila juma, tunaonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu kwa kuhuzuria mikutano na kutoa maelezo. Hata kama pengine tumechoka, tunajikaza kufika ku mikutano. Hata kama pengine tunaogopaka kujibia, tunajikaza kufanya vile. Na hata kama tuko tunapambana na magumu fulani, tunajikaza kutia wengine moyo mbele na kisha mukutano. (Ebr. 10:24, 25) Tunafurahia sana mambo yenye ndugu na dada zetu wanafanya!

12. Yohana alifanya nini ingine ili kuonyesha kama anapenda ndugu na dada zake?

12 Yohana alionyesha kama anapenda ndugu na dada zake kwa kuwapongeza lakini pia kwa kuwatolea mashauri. Kwa mufano, mu barua zake, alipongeza ndugu na dada zake kwa sababu ya imani yao na kwa sababu ya mambo ya muzuri yenye walikuwa wanafanya. Lakini, aliwatolea pia mashauri mazito juu ya zambi. (1 Yo. 1:8–2:1, 13, 14) Vilevile, tunapaswa kupongeza ndugu na dada zetu kwa sababu ya mambo ya muzuri yenye wako wanafanya. Lakini kama ndugu ao dada anaanza kuwa na mawazo ao tabia fulani ya mubaya, tunaonyesha kama tunamupenda kwa kumutolea mashauri kwa upole. Inaomba uhodari ili kushauria rafiki. Lakini Biblia inasema kama rafiki wa kweli iko tayari kunoa, ao kurekebisha rafiki yake.​—Mez. 27:17.

13. Tunapaswa kuepuka kufanya nini?

13 Wakati fulani, tunaonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu kwa kuepuka kufanya mambo fulani. Kwa mufano, tunaepuka kukwazika haraka juu ya mambo yenye wanasema. Fikiria mambo yenye ilifanyika ku mwisho-mwisho wa maisha ya Yesu ku dunia. Aliambia wanafunzi wake kama, ili kupata uzima wa milele, walipaswa kula mwili wake na kunywa damu yake. (Yoh. 6:53-57) Wanafunzi wengi walikwazika kwa sababu ya ile maneno na walimuacha. Lakini, marafiki wake wa kweli, kama vile Yohana, hawakufanya vile. Walishikamana naye. Hawakuelewa maneno yenye Yesu alisema, na inawezekana wao pia walishangaa. Lakini, marafiki washikamanifu wa Yesu hawakuwaza kama alikosea na hawakukwazika juu ya mambo yenye alisema. Kuliko kufanya vile, walimutumainia kwa sababu walijua kama anasemaka kweli. (Yoh. 6:60, 66-69) Kwa hiyo, sisi pia hatupaswe kukwazika haraka juu ya mambo yenye marafiki wetu wanasema! Kuliko kufanya vile, tunapaswa kuwaachia nafasi ya kujifasiria.​—Mez. 18:13; Muh. 7:9.

14. Juu ya nini hatupaswe kuchukia ndugu na dada zetu?

14 Pia, Yohana alitushauria kama hatupaswe kuchukia ndugu na dada zetu. Kama hatufuate ile shauri, Shetani anaweza kutuchochea. (1 Yo. 2:11; 3:15) Ile ilifikia Wakristo fulani ku mwisho wa karne ya kwanza K.K.Y. Shetani alikuwa anafanya yake yote ili kupanda mbegu za chuki na migawanyiko kati ya watu wa Mungu. Wakati Yohana aliandika barua zake, watu fulani wenye kuchochea roho ya chuki na migawanyiko kama Shetani walikuwa wameingia mu kutaniko. Kwa mufano, Diotrefe alikuwa analeta migawanyiko mu kutaniko fulani. (3 Yo. 9, 10) Hakukuwa anaheshimia wazee wenye kusafiri wenye walikuwa wanatumwa na baraza lenye kuongoza. Alijaribu hata kutupa inje ya kutaniko wale wenye walikuwa wanakaribisha watu wenye yeye hakukuwa anapenda. Alikuwa na kiburi kabisa! Hata leo, Shetani angali anafanya yake yote ili kuleta migawanyiko kati ya watu wa Mungu. Hatupaswe hata kidogo kuchukia ndugu na dada zetu.

PENDA FAMILIA YAKO

Yesu aliomba Yohana ahangaikie mahitaji ya kimwili na ya kiroho ya mama yake. Leo, vichwa vya familia wanapaswa pia kuhangaikia mahitaji ya kimwili na ya kiroho ya familia zao (Ona fungu la 15-16)

15. Kichwa cha familia anapaswa kukumbuka nini?

15 Kichwa cha familia anaonyesha kama anapenda watu wa familia yake kwa kuwatimizia mahitaji yao ya kimwili. (1 Ti. 5:8) Lakini, anapaswa kukumbuka kama wako pia na lazima ya mambo ya kiroho. (Mt. 5:3) Fikiria mufano wenye Yesu aliachia vichwa vya familia. Kulingana na Injili ya Yohana, wakati Yesu alikuwa karibu kufa ku muti wa mateso, alikuwa angali anafikiria familia yake. Yohana alikuwa anasimama karibu na Maria, mama ya Yesu, pale kwenye Yesu alikuwa ametundikwa. Hata kama Yesu alikuwa na maumivu ya mingi sana, aliomba Yohana achunge Maria. (Yoh. 19:26, 27) Yesu alikuwa na ndugu na dada wenye wangehangaikia mahitaji ya kimwili ya Maria. Lakini, inaonekana kama ile wakati, walikuwa hawajamuamini Yesu. Kwa hiyo, Yesu alikamata mipango ili Yohana ahangaikie mahitaji ya kimwili na ya kiroho ya Maria.

16. Yohana alikuwa na madaraka gani?

16 Yohana alikuwa na madaraka mingi. Alikuwa mutume, kwa hiyo, alipaswa kuhubiri kwa bidii. Pia, inawezekana alikuwa na familia, kwa hiyo, alipaswa kuhangaikia mahitaji ya kimwili na ya kiroho ya familia yake. (1 Ko. 9:5) Mufano wake unaweza kufundisha nini vichwa vya familia leo?

17. Juu ya nini kichwa cha familia anapaswa kuhangaikia mahitaji ya kiroho ya watu wa familia yake?

17 Ndugu mwenye kuwa kichwa cha familia anaweza kuwa na madaraka ya mingi. Kwa mufano, ku kazi anapaswa kutumika kwa bidii ili namna yake ya kutumika ichochee wengine wamusifu Yehova. (Efe. 6:5, 6; Tit. 2:9, 10) Na anaweza kuwa na madaraka ingine mu kutaniko. Kwa mufano, pengine anapaswa kufanya kazi za uchungaji na kusaidia wengine wahubiri kwa bidii. Na tena, anapaswa kujifunza Biblia kwa ukawaida pamoja na bibi na watoto wake. Kama anafanya vile, watafurahia sana namna iko anajikaza ili kuwasaidia wakuwe na afya ya muzuri, wakuwe na furaha, na waendelee kumutumikia Yehova.​—Efe. 5:28, 29; 6:4.

“MUBAKI KATIKA UPENDO WANGU”

18. Yohana alikuwa hakika na jambo gani?

18 Yohana aliishi miaka mingi, na alijionea mambo mingi yenye kufurahisha. Na alipambana na magumu mingi yenye ingeregeza imani yake. Lakini, kila mara alijikaza kutii amri za Yesu, kama vile amri ya kupenda ndugu na dada zake. Ile ilisaidia Yohana akuwe hakika kama Yehova na Yesu walimupenda na kama wangemupatia nguvu ya kuvumilia magumu yote yenye angepata. (Yoh. 14:15-17; 15:9, 10; 1 Yo. 4:16) Shetani na ulimwengu wake hawangeweza kumufanya Yohana aache kupenda ndugu na dada zake na kuonyesha ule upendo kupitia maneno na matendo.

19. 1 Yohana 4:7 inatutia moyo tufanye nini, na juu ya nini?

19 Kama Yohana, tunaishi mu ulimwengu wenye unatawaliwa na Shetani, mutawala mwenye chuki. (1 Yo. 3:1, 10) Nia yake ni kutufanya tuache kupenda ndugu na dada zetu. Lakini, hawezi kutuchochea kufanya vile ikiwa hatumupatie nafasi. Tuazimie basi kupenda ndugu na dada zetu, na kuonyesha upendo wetu kupitia maneno na matendo. Kama tunafanya vile, tutafurahia kuwa mu familia ya Yehova, na tutakuwa na furaha mu maisha yetu.​—Soma 1 Yohana 4:7.

WIMBO 88 Nijulishe Njia Zako

^ fu. 5 Inaonekana kabisa kama mutume Yohana njo mwenye Biblia inaita “mwanafunzi mwenye Yesu alipenda.” (Yoh. 21:7) Ile inaonyesha kama, hata kama alikuwa kijana, inawezekana kabisa alikuwa na sifa mingi za muzuri. Miaka mingi kisha, wakati alikuwa amezeeka, Yehova alimutumia ili kuandika mambo mingi kuhusu upendo. Mu hii habari, tutazungumuzia mawazo fulani yenye Yohana aliandika na tutazungumuzia mambo yenye mufano wake unaweza kutufundisha.

^ fu. 59 MAFASIRIO YA PICHA: Kichwa cha familia mwenye kuwa na mambo mingi ya kufanya anasaidia kisha musiba kutokea, anategemeza kazi ya mu dunia yote kwa kutoa michango, na anaalika wengine ili wajiunge pamoja naye na bibi yake na watoto wake ku ibada yao ya familia.