Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Musisahau Ukaribishaji-Wageni’

‘Musisahau Ukaribishaji-Wageni’

‘Musisahau ukaribishaji-wageni.’​—WAEBRANIA 13:2.

NYIMBO: 12479

1, 2. (a) Wageni wengi wanapata magumu gani leo? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Mutume Paulo alitukumbusha jambo gani, na tutazungumuzia maulizo gani?

KUMEPITA miaka zaidi ya 30, Osei, [1] mwenye wakati huo hakukuwa Shahidi wa Yehova alitoka katika inchi yake ya Ghana na kuenda kuishi Ulaya. (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.) Alisema hivi: “Bila kukawia, nilitambua kama watu wengi hawakunihangaikia. Pia, hali ya hewa ilinisumbua. Wakati niliondoka kwenye uwanja wa ndege na kusikia baridi kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilianza kulia.” Kwa sababu ilikuwa vigumu kwa Osei kujifunza luga, alifanya zaidi ya mwaka moja ili kupata kazi ya muzuri. Na kwa sababu alikuwa mbali na inchi yake, alikuwa anakumbuka watu wa familia yake na alijisikia kuwa peke yake.

2 Fikiria namna ungependa watu wakutendee ikiwa ulikuwa katika hali kama hiyo. Kwa kweli, ungefurahia watu wenye wanakupenda wakukaribishe kwa furaha kwenye Jumba la Ufalme bila kuhangaikia inchi yako ao rangi yako ya ngozi. Biblia inaomba Wakristo wa kweli ‘wasisahau ukaribishaji-wageni.’ (Waebrania 13:2) Tuzungumuzie basi maulizo haya tatu: Yehova anaona wageni namna gani? Ni lazima tubadilishe namna yetu ya kuona wageni? Namna gani tunaweza kusaidia mutu fulani mwenye kutoka katika inchi ingine ajisikie kuwa anakaribishwa muzuri katika kutaniko letu?

MAWAZO YA YEHOVA JUU YA WAGENI

3, 4. Kulingana na andiko la Kutoka 23:9, namna gani Mungu alipenda Waisraeli watendee wageni, na sababu gani?

3 Kisha Yehova kukomboa watu wake kutoka katika utumwa wa Misri, aliwapatia sheria zenye ziliwafundisha kutendea muzuri wageni wenye walijiunga pamoja nao. (Kutoka 12:38, 49; 22:21) Kwa sababu maisha ya wageni hayako mepesi sikuzote, Yehova aliwahangaikia kwa upendo. Kwa mufano, ili wapate chakula, wangeokota masalio yenye wavunaji walikuwa wanaacha nyuma yao.​—Mambo ya Walawi 19:9, 10.

4 Yehova hakuamuru tu Waisraeli waheshimie wageni, lakini alipenda pia wakumbuke namna mutu anajisikiaka wakati iko mugeni. (Soma Kutoka 23:9.) Hata mbele Waisraeli wakuwe watumwa katika inchi ya Misri, Wamisri hawakuwapenda kwa sababu walikuwa tofauti nao. (Mwanzo 43:32; 46:34; Kutoka 1:11-14) Waisraeli walikuwa na maisha magumu kwa sababu walikuwa wageni. Yehova alipenda wakumbuke jambo hilo na watendee muzuri wageni wenye walikuwa wanaishi kati yao.​—Mambo ya Walawi 19:33, 34.

5. Ni nini itatusaidia kutendea wageni muzuri kama vile Yehova anawatendea?

5 Yehova hajabadilika. Kwa hiyo, wakati wageni wanakuja katika kutaniko letu, hatupaswe kusahau kama Yehova angali anatendea muzuri watu kama hao. (Kumbukumbu la Torati 10:17-19; Malaki 3:5, 6) Fikiria kidogo magumu yenye wageni wanaweza kuwa nayo. Kwa mufano, wanaweza kuwa na magumu ya kuelewa luga mupya na watu wanaweza kuwatendea mubaya. Tujikaze basi kuwasaidia na kuwatendea muzuri.​—1 Petro 3:8.

NI LAZIMA TUBADILISHE MAWAZO YETU JUU YA WAGENI?

6, 7. Ni nini ilionyesha kama Wakristo wa kwanza Wayahudi walijifunza kuachana na ubaguzi mukali?

6 Wakristo wa kwanza walijifunza kuachana na ubaguzi mukali wenye Wayahudi wengi walikuwa nao. Kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33, Wakristo Wayahudi wenye walikuwa wanaishi Yerusalemu walikaribisha na kuhangaikia kwa upendo wapya wenye walitoka katika inchi mbalimbali. (Matendo 2:5, 44-47) Hilo lilionyesha kama Wakristo Wayahudi walielewa maana ya “ukaribishaji-wageni,” ni kusema, kutendea wageni muzuri.

7 Lakini, jambo fulani lilitokea wakati huo. Wayahudi wenye kusema Kigiriki walikuwa wananungunika kuwa wajane wao walikuwa wanatendewa bila haki. (Matendo 6:1) Ili kumaliza tatizo hilo, mitume walichagua wanaume saba ili waende na wahakikishe kama watu wote wanatendewa kwa haki. Mitume walichagua wanaume wenye kuwa na majina ya Kigiriki, pengine walifanya hivyo ili kufanya wajane hao wajisikie muzuri.​—Matendo 6:2-6.

8, 9. (a) Ni maulizo gani yatatusaidia kujua ikiwa tuko na ubaguzi? (b) Tunapaswa kuachana kabisa na nini? (1 Petro 1:22)

8 Sisi wote tunachochewa sana na desturi zetu, hata kama tunatambua hilo ao hapana. (Waroma 12:2) Pia, tunaweza kusikia majirani wetu, wafanyakazi wenzetu, ao wanafunzi wenzetu wanasema mambo ya mubaya juu ya watu wa eneo lingine, kabila lingine, ao rangi ingine ya ngozi. Tunajiacha tuchochewe sana na mawazo hayo ya mubaya? Ao tunatenda namna gani wakati mutu fulani anachekelea inchi yetu ao jambo fulani la desturi zetu?

9 Wakati fulani mutume Petro alikuwa anabagua watu wenye hawakukuwa Wayahudi. Lakini hatua kwa hatua, alijifunza kuachana na mawazo hayo ya mubaya. (Matendo 10:28, 34, 35; Wagalatia 2:11-14) Vilevile, ikiwa tunaona ndani yetu hata alama kidogo ya ubaguzi ao majivuno juu ya rangi yetu ya ngozi, tunapaswa kujikaza sana ili kuachana kabisa na tabia hiyo. (Soma 1 Petro 1:22.) Ni nini inaweza kutusaidia kufanya hivyo? Hata kama tunatoka katika inchi gani tukumbuke kama sisi wote hatukamilike, na sisi wote hatustahili kuokolewa. (Waroma 3:9, 10, 21-24) Kwa hiyo, hatuna sababu ya kujiona kuwa watu wa maana kuliko wengine! (1 Wakorintho 4:7) Tunapaswa kuwa na mawazo kama ya mutume Paulo. Aliambia Wakristo wenzake kama wao “si wageni tena na wakaaji wageni” lakini walikuwa “washiriki [watu] wa nyumba ya Mungu.” (Waefeso 2:19) Ili tuweze kuvaa utu mupya, tunapaswa kujikaza sana ili kuachana kabisa na kila namna ya ubaguzi.​—Wakolosai 3:10, 11.

NAMNA YA KUONYESHA UKARIBISHAJI-WAGENI

10, 11. Namna gani Boazi aliiga mawazo ya Yehova juu ya wageni?

10 Boazi, mwanaume muaminifu, aliiga mawazo ya Yehova juu ya wageni. Namna gani? Wakati Boazi alienda kuangalia mashamba yake wakati wa mavuno, aliona Ruthu, mwanamuke mugeni mwenye alitoka katika inchi ya Moabu. Ruthu alikuwa anatumika kwa bidii ili kuokota mbegu. Kulingana na Sheria ya Musa, Ruthu alikuwa na haki ya kuokota masalio. Lakini wakati Boazi alisikia kama Ruthu aliomba ruhusa ili aokote masalio katika shamba lake, aliguswa moyo sana na alimuacha hata aokote masalio katika mafurushi ya mbegu.​—Soma Ruthu 2:5-7, 15, 16.

11 Mambo yenye yalifanyika kisha hapo yanaonyesha wazi kama Boazi alihangaikia Ruthu na hali yake ya kuwa mugeni. Aliomba Ruthu abakie katika kikundi cha vijana wanawake ili wanaume wenye walikuwa wanatumika katika shamba wasimutendee mubaya. Na hata alihakikisha kama Ruthu anapata chakula cha kutosha na maji, kama tu wafanyakazi wake mwenyewe. Boazi aliheshimia mwanamuke huyo mugeni masikini na alimutia moyo.​—Ruthu 2:8-10, 13, 14.

12. Kutendea wageni muzuri kunaweza kuwa na matokeo gani?

12 Boazi alimutendea Ruthu muzuri haiko kwa sababu tu alikuwa mushikamanifu kwa mama-mukwe wake, Naomi, lakini pia kwa sababu alianza kumutumikia Yehova na alitafuta ulinzi Wake. Wakati Boazi alitendea Ruthu muzuri, alikuwa anaiga upendo mushikamanifu wa Yehova. (Ruthu 2:12, 20; Methali 19:17) Vilevile leo, wakati tunatendea wageni muzuri, tunaweza kusaidia “watu wa namna zote” wajifunze kweli na waone kama Yehova anawapenda sana.​—1 Timotheo 2:3, 4.

Tunaonyesha ukaribishaji-wageni kwa watu wenye kutoka katika inchi zingine? (Picha hii inapatana na fungu la 13, 14)

13, 14. (a) Sababu gani tunapaswa kusalimia wageni kwenye Jumba la Ufalme? (b) Ni nini inaweza kukusaidia usisikie haya ya kuzungumuza na mutu fulani wa desturi ingine?

13 Tunaweza kutendea wageni muzuri wakati tunawasalimia kwa furaha kwenye Jumba la Ufalme. Watu wenye kutoka katika inchi zingine wenye wamehamia hivi karibuni katika inchi fulani wanaweza kusikia haya na kujitenga na watu wengine. Kwa sababu ya desturi ao hali yao ya maisha, wanaweza kujiona kuwa watu wa hali ya chini kuliko watu wa rangi ingine ya ngozi ao inchi ingine. Kwa hiyo, tunapaswa kuwasalimia kwanza na kuwatendea muzuri na kuonyesha kama tunapendezwa kabisa nao. Ikiwa programu JW Language inapatikana katika luga yako, inaweza kukusaidia ujifunze namna ya kuwasalimia katika luga yao.​—Soma Wafilipi 2:3, 4.

14 Unaweza kusikia haya ya kuzungumuza na mutu fulani wa desturi ingine. Ili kumaliza haya, unaweza kumuambia jambo fulani juu yako mwenyewe. Kisha unaweza kuona kama muko na mambo mengi yenye kufanana kuliko namna uliwazia. Ukumbuke kama kila desturi iko na mambo ya muzuri na uzaifu wake.

SAIDIA WOTE WAJISIKIE KUWA WAMEKARIBISHWA MUZURI

15. Ni nini itatusaidia kuelewa wale wenye wanajikaza kuzoea maisha katika inchi ya kigeni?

15 Ili kusaidia wengine wajisikie kuwa wamekaribishwa muzuri katika kutaniko, ujiulize hivi: ‘Ikiwa nilikuwa katika inchi ya kigeni, ningependa watu wanitendee namna gani?’ (Mathayo 7:12) Uwaonyeshe uvumilivu wale wenye wako wanajikaza kuzoea maisha katika inchi ya kigeni. Mwanzoni, tunaweza kushindwa kuelewa muzuri namna yao ya kuwaza ao kutenda. Lakini, kuliko kuwaomba wawaze na kutenda kama watu wa desturi yetu, tuwakubali tu vile wako.​—Soma Waroma 15:7.

16, 17. (a) Tunaweza kufanya nini ili tukaribie sana watu wa desturi zingine? (b) Ni musaada gani wenye kufaa tunaweza kutolea watu wa inchi ingine wenye wamehamia katika kutaniko letu?

16 Ikiwa tunapanga wakati wa kujifunza mambo fulani juu ya inchi ya wageni na desturi zao, inaweza kuwa vyepesi sana kwetu kuwajua. Wakati wa ibada yetu ya familia, tunaweza kutafuta habari fulani juu ya desturi za watu wa inchi zingine wenye wamehamia katika kutaniko ao eneo letu. Namna ingine ya kutusaidia kukaribia sana watu hao ni kuwaalika nyumbani kwetu ili kula pamoja nao. Yehova ‘amefungulia mataifa mulango wa kuingia katika imani,’ kwa hiyo, tunapaswa kuiga mufano wake na kufungulia mulango wageni wenye “katika imani ni jamaa zetu.”​—Matendo 14:27; Wagalatia 6:10; Ayubu 31:32.

Tunaonyesha ukaribishaji-wageni kwa watu wenye kutoka katika inchi zingine? (Picha hii inapatana na fungu la 16, 17)

17 Ikiwa tunapitisha wakati pamoja na watu wa familia fulani wenye walitoka katika inchi ingine, hilo litatusaidia kuwaelewa na kupendezwa na bidii yenye wanafanya ili wazoee desturi zetu. Tunaweza kuona kama wako na lazima ya musaada ili kujifunza luga na tunaweza kuwasaidia. Tunaweza pia kuwaongoza kwenye mashirika yenye yanaweza kuwasaidia wapate nyumba ao kazi ya muzuri. Musaada huo wenye kufaa unaweza kuwa wa maana sana kwa ndugu na dada zetu.​—Methali 3:27.

18. Leo, watu wenye wamehamia katika inchi zingine wanaweza kuiga mufano gani wa heshima na shukrani?

18 Kwa kweli, watu wenye wamehamia katika inchi zingine, wanapaswa kufanya yao yote ili wazoee desturi za inchi hizo. Ruthu alionyesha mufano muzuri katika jambo hilo. Kwanza, wakati aliomba ruhusa ya kuokota masalio, alionyesha kama aliheshimia desturi za inchi kwenye alihamia. (Ruthu 2:7) Hakuzarau haki hiyo na hakuona kuwa wengine walilazimika kumufanyia jambo fulani. Pili, hakukawia kuambia wengine kama alikuwa mwenye shukrani kwa sababu walimutendea muzuri. (Ruthu 2:13) Ikiwa watu wenye wamehamia katika inchi zingine wanatenda kama Ruthu, ndugu na dada zao na watu wengine wa inchi hizo wanaweza kabisa kuwaheshimia.

19. Sababu gani tunapaswa kufanya wageni wajisikie kuwa wamekaribishwa muzuri?

19 Tunafurahi sana kuona kama Yehova ameonyesha watu wote fazili zenye hawastahili na amewapatia nafasi ya kusikiliza habari njema. Katika inchi zao, pengine watu fulani hawangepata nafasi ya kujifunza Biblia ao kukusanyika pamoja na Mashahidi wa Yehova. Lakini sasa, kwa sababu wako na nafasi ya kukusanyika pamoja na sisi, tunapaswa kuwasaidia ili wasijisikie kuwa wageni. Pengine hatuna feza nyingi ao uwezo wa kusaidia wageni kwa njia yenye kufaa, lakini wakati tunawatendea muzuri, tunaiga mufano wa Yehova mwenye anapenda wageni. Kwa hiyo, kwa sababu tuko “waigaji wa Mungu,” tufanye yetu yote ili kukaribisha wageni kati yetu!​—Waefeso 5:1, 2.

^ [1] (fungu la 1) Jina limebadilishwa.