Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Endelea Kuwa na Amani ya Akili Hata Kama Hali Zinabadilika

Endelea Kuwa na Amani ya Akili Hata Kama Hali Zinabadilika

“Nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu.”​—ZB. 131:2.

NYIMBO: 128, 129

1, 2. (a) Mabadiliko yenye hatukutazamia yanaweza kufanya tujisikie namna gani? (Ona picha ku mwanzo wa habari hii.) (b) Kulingana na Zaburi ya 131, ni nini inaweza kutusaidia tukuwe na amani ya akili?

KISHA Lloyd na Alexandra kutumikia ku Beteli miaka zaidi ya 25, walipewa mugao wa kutumikia mu kutaniko. Ku mwanzo, walihuzunika. Lloyd anasema hivi: “Nilikuwa ninajisikia kama vile Beteli na kazi yangu ku Beteli ndio ulikuwa utambulisho wangu. Mu akili yangu, nilikuwa ninaelewa sababu gani mabadiliko hayo yalifanywa, lakini katika majuma na miezi yenye ilifuata, mara mingi nilijisikia kuwa nimekataliwa.” Wakati fulani, Lloyd alikuwa na mawazo ya muzuri juu ya mabadiliko hayo, na wakati mwingine alikuwa anajisikia kuwa mwenye kuvunjika moyo.

2 Wakati fulani, kutakuwa mabadiliko mu maisha yetu yenye hatukuwazia na yanaweza kutufanya tuhangaike sana. (Mez. 12:25) Wakati ni nguvu kukubali mabadiliko ao kujipatanisha nayo, tunaweza kufanya nini ili tuendelee kuwa wenye kutulia? (Soma Zaburi 131:1-3.) Tuone basi namna watumishi wa Yehova wa wakati wa zamani na wa leo, waliweza kuwa na amani ya akili hata wakati maisha yao yalibadilika bila kutazamia.

NAMNA “AMANI YA MUNGU” INATUSAIDIA

3. Namna gani maisha ya Yosefu yalibadilika bila kutazamia?

3 Fikiria mufano wa Yosefu. Yakobo alikuwa anamupenda Yosefu sana kati ya watoto wake wote. Hilo lilifanya ndugu zake wamusikilie wivu sana. Wakati Yosefu alikuwa na miaka 17, walimuuzisha ili akuwe mutumwa. (Mwa. 37:2-4, 23-28) Kwa miaka 13 hivi, aliteseka mu Misri, kwanza alikuwa mutumwa na kisha akakuwa mufungwa. Yosefu alikuwa mbali sana na baba yake, mwenye alikuwa anapenda sana. Hali yake ingeweza kumufanya ajisikie kuwa mwenye kukosa tumaini na mwenye huzuni, lakini hakujisikia vile. Ni nini ilimusaidia?

4. (a) Yosefu alifanya nini wakati alikuwa mu gereza? (b) Namna gani Yehova alijibu sala za Yosefu?

4 Wakati Yosefu alikuwa anateseka mu gereza, inawezekana kabisa alikaza akili juu ya namna Yehova alikuwa anamusaidia. (Mwa. 39:21; Zb. 105:17-19) Pengine alifikiria pia ndoto za unabii zenye aliota wakati alikuwa kijana mudogo na hilo lilimufanya akuwe hakika kama Yehova alikuwa pamoja naye. (Mwa. 37:5-11) Inawezekana alikuwa anasali mara nyingi na kumuambia Yehova kila jambo lenye lilikuwa mu moyo wake. (Zb. 145:18) Na Yehova alijibu sala za Yosefu kwa kumuhakikishia kama atakuwa “pamoja naye” hata kutokee nini.​—Mdo. 7:9, 10. * (Ona maelezo ya chini.)

5. Namna gani “amani ya Mungu” inaweza kutufanya tuazimie zaidi kumutumikia Yehova?

5 Hata kama hali yetu ni ya nguvu namna gani, tunaweza kuwa na “amani ya Mungu” yenye kulinda ‘nguvu zetu za akili’ na kutufanya tujisikie kuwa wenye kutulia. (Soma Wafilipi 4:6, 7.) Wakati tuko na mahangaiko, “amani ya Mungu” inaweza kututia nguvu ili tuendelee kumutumikia Yehova na tusichoke. Tujifunze basi juu ya mifano fulani ya ndugu na dada wa siku zetu wenye wamejionea jambo hilo.

UMUOMBE YEHOVA AKUSAIDIE ILI UKUWE NA AMANI TENA

6, 7. Namna gani sala zetu zinaweza kutusaidia kuwa tena na amani ya akili? Leta mufano.

6 Wakati Ryan na Juliette walisikia kama mugao wao wa kuwa mapainia wa muda ulifikia mwisho, walivunjika moyo. Ryan anasema hivi: “Mara moja tulimuambia Yehova jambo hilo mu sala. Tulijua kama hiyo ilikuwa nafasi ya pekee ya kuonyesha kama tunamutumainia. Watu wengi mu kutaniko letu walikuwa wapya katika kweli, kwa hiyo tulisali kwa Yehova ili atusaidie kuonyesha mufano muzuri kabisa wa imani.”

7 Namna gani Yehova alijibu sala yao? Ryan anasema hivi: “Kisha tu kusali, mawazo ya mubaya na mahangaiko yenye tulikuwa nayo yaliisha. Amani ya Mungu ilikuwa inalinda mioyo yetu na nguvu zetu za akili. Tulitambua kama Yehova angeendelea kututumikisha ikiwa tuliendelea kuwa na mawazo yenye kufaa.”

8-10. (a) Namna gani roho ya Mungu inaweza kutusaidia wakati tuko na mahangaiko? (b) Namna gani Yehova anaweza kutusaidia wakati tunakaza akili yetu juu ya kumutumikia?

8 Roho ya Mungu inaweza kutusaidia tujisikie kuwa wenye kutulia, na inaweza pia kutusaidia kupata maandiko ya Biblia yenye yatatusaidia kuelewa jambo lenye kuwa la maana zaidi mu maisha. (Soma Yohana 14:26, 27.) Fikiria mambo yenye yalimupata Philip na Mary, bibi na bwana wenye walikuwa wametumikia ku Beteli miaka karibu 25. Katika kipindi cha miezi ine, mama ya Philip na mama ya Mary walikufa na mutu mwingine wa jamaa yao alikufa pia, na walipaswa kuhangaikia baba ya Mary mwenye kuwa na ugonjwa fulani wa akili.

9 Philip anasema hivi: “Niliwaza kama nilikuwa ninavumilia kwa kadiri fulani, lakini kulikuwa jambo fulani lenye nilikosa. Niliona andiko la Wakolosai 1:11 katika habari fulani ya kujifunza ya Munara wa Mulinzi. Kusema kweli, nilikuwa ninavumilia lakini sikukuwa ninavumilia kwa ukamili. Nilipaswa ‘kuvumilia kwa ukamili kwa subira na furaha.’ Andiko hilo lilinikumbusha kama furaha yangu mu maisha haitegemee hali zangu, lakini inategemea namna roho ya Mungu inatumika mu maisha yangu.”

10 Kwa sababu Philip na Mary waliendelea kukaza akili juu ya kumutumikia Yehova, aliwabariki katika njia nyingi. Kisha tu kutoka ku Beteli, wote wawili walipata wanafunzi wa Biblia wenye walifanya maendeleo ya muzuri na wenye walipenda kujifunza zaidi ya mara moja katika juma. Mary anasema hivi: “Walituletea furaha na hiyo ilikuwa njia ya Yehova ya kutuambia kama mambo yote yatakuwa muzuri.”

FANYA JAMBO FULANI LENYE YEHOVA ANAWEZA KUBARIKI

Namna gani tunaweza kumuiga Yosefu hata kutokee nini mu maisha yetu? (Picha hii inapatana na fungu la 11-13)

11, 12. (a) Namna gani Yosefu alifanya jambo fulani lenye Yehova angeweza kubariki? (b) Namna gani Yehova alimubariki Yosefu?

11 Wakati maisha yanabadilika bila kutazamia, tunaweza kuhangaika sana na kuanza kufikiria tu magumu yetu. Jambo hilo lingeweza kumufikia Yosefu. Lakini, aliamua kufanya mambo yote yenye angeweza kufanya katika hali yake. Kama vile Yosefu alikuwa amemutumikia Potifa kwa bidii, wakati alikuwa mu gereza, alifanya pia kwa bidii kila kazi yenye ofisa mukubwa wa gereza alimupatia.​—Mwa. 39:21-23.

12 Siku moja, Yosefu alipewa mugao wa kuhangaikia wafungwa wawili wenye walikuwa wametumikia katika makao ya Farao. Yosefu alionyesha wema wanaume hao, na wakajisikia huru kumuambia mahangaiko yao na ndoto zao zenye kusumbua zenye walikuwa wameota usiku. (Mwa. 40:5-8) Wakati Yosefu alikuwa anazungumuza nao, hakujua kama mazungumuzo hayo yangemusaidia apate uhuru. Miaka mbili kisha pale, alifunguliwa kutoka mu gereza na akakuwa mutawala mukubwa mu inchi ya Misri. Ni Farao tu ndiye alikuwa na mamlaka zaidi kumupita Yosefu!​—Mwa. 41:1, 14-16, 39-41.

13. Hata kama tuko mu hali gani, namna gani tunaweza kutenda mu njia yenye Yehova atabariki?

13 Kama Yosefu, tunaweza kujikuta mu hali fulani yenye hatuna uwezo wa kubadilisha. Lakini, kama tunaonyesha uvumilivu na kufanya mambo yote yenye tunaweza, Yehova atatubariki. (Zb. 37:5) Hata wakati tunajisikia kuwa wenye kuvurugika na wenye kuhangaika, “hatuachwe bila tumaini.” (2 Ko. 4:8; maelezo ya chini) Yehova atakuwa pamoja na sisi, zaidi sana kama tunaendelea kukaza akili juu ya kazi yetu ya kuhubiri.

ENDELEA KUKAZA AKILI JUU YA KAZI YAKO YA KUHUBIRI

14-16. Filipo mueneza-injili aliendelea kukaza akili juu ya kazi yake ya kuhubiri hata kama maisha yake yalibadilika. Namna gani?

14 Filipo mueneza-injili ni mufano muzuri wa mutu mwenye aliendelea kukaza akili juu ya kazi yake ya kuhubiri, hata wakati maisha yake yalibadilika. Wakati fulani, alifurahia mugao mupya mu muji wa Yerusalemu. (Mdo. 6:1-6) Hata hivyo, mambo yote yalibadilika. Kisha Stefano kuuawa, * kulitokea upinzani mukali juu ya Wakristo na walitoka Yerusalemu na kukimbia. Kwa sababu Filipo alipenda kuendelea kufanya mengi mu kazi ya Yehova, alienda mu muji wa Samaria, kwenye watu walikuwa na lazima ya kusikia habari njema.​—Mt. 10:5; Mdo. 8:1, 5.

15 Filipo alikuwa tayari kuenda kila mahali kwenye roho ya Mungu ilimuongoza. Kwa hiyo, Yehova alimutumia ili kuhubiri mahali kwenye watu walikuwa hawajasikia habari njema. Wayahudi wengine walikuwa wanazarau Wasamaria na walikuwa wanawatendea mubaya. Lakini, Filipo hakukuwa na ubaguzi, na alifurahia kuwahubiria habari njema. Na Wasamaria walimusikiliza “kwa umoja”!​—Mdo. 8:6-8.

16 Kisha, roho ya Mungu ilimuongoza Filipo aende kuhubiri mu miji ya Ashdodi na Kaisaria, kwenye kulikuwa Watu wengi wa Mataifa. (Mdo. 8:39, 40) Kisha maisha yake yalibadilika tena. Alibakia nafasi moja na akakuwa na familia. Lakini, hata kama maisha ya Filipo yalibadilika, aliendelea kuwa na mengi ya kufanya mu kazi yake ya kuhubiri, na Yehova aliendelea kumubariki yeye na familia yake.​—Mdo. 21:8, 9.

17, 18. Wakati maisha yetu yanabadilika mu njia fulani, namna gani kukaza akili juu ya kazi ya kuhubiri kunaweza kutusaidia?

17 Ndugu na dada wengi wenye kuwa katika utumishi wa wakati wote wanasema kama kuendelea kukaza akili juu ya kazi yao ya kuhubiri kunawasaidia waendelee kuwa na furaha na mawazo ya muzuri hata wakati hali zao zinabadilika. Kwa mufano, wakati Osborne na Polite, bibi na bwana wenye kuishi mu inchi ya Afrika ya Kusini walitoka ku Beteli, waliwaza kama itakuwa mwepesi kupata mahali pa kuishi na kazi yenye haiwakamate wakati wote. Lakini Osborne anasema hivi: “Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, hatukupata kazi haraka kama vile tulikuwa tunatumainia.” Polite anasema hivi: “Tulifanya miezi tatu bila kupata kazi, na hatukukuwa tumeweka feza zozote. Ilikuwa shida sana.”

18 Ni nini ilisaidia Osborne na Polite katika hali hiyo yenye kuleta mahangaiko? Osborne anasema hivi: “Kuhubiri pamoja na kutaniko kulitusaidia sana ili akili zetu zisitange-tange na ili tuendelee kuwa na mawazo ya muzuri.” Kuliko kubakia tu ku nyumba wakiwa na mahangaiko, waliamua kuendelea kufanya mengi mu kazi ya kuhubiri. Kufanya vile kuliwaletea furaha kubwa! Na Osborne anaongeza hivi: “Tuliendelea kutafuta kazi sana, na tulifikia kupata kazi.”

TUMAINIA YEHOVA KABISA

19-21. (a) Ni nini itatusaidia tuendelee kuwa na amani ya akili? (b) Tunaweza kupata faida gani wakati tunajipatanisha na badiliko fulani lenye hatukuwazia?

19 Kama vile tumeona, ikiwa tunafanya mambo yote yenye tunaweza mu hali zetu na kumutumainia Yehova kabisa, tutaendelea kuwa na amani ya akili hata kutokee nini. (Soma Mika 7:7.) Kisha wakati fulani, tunaweza kutambua kama namna tulijipatanisha na mabadiliko ilitia nguvu urafiki wetu pamoja na Yehova. Polite anasema kama kutoka ku Beteli kulimusaidia ajue maana ya kumutegemea Yehova hata wakati maisha yanaonekana kuwa nguvu sana. Anasema hivi: “Urafiki wangu pamoja na Yehova umekuwa wenye nguvu zaidi.”

20 Mary, mwenye tumekwisha kutaja, anaendelea kumuhangaikia baba yake mwenye kuzeeka na anaendelea kufanya kazi ya upainia. Anasema hivi: “Nimejifunza kama wakati niko na mahangaiko, ninapaswa kutua, kusali, na kutulia. Kuacha mambo mu mikono ya Yehova, pengine ndilo jambo kubwa zaidi lenye nimejifunza, na itakuwa lazima sana kufanya vile wakati wenye kuja.”

21 Lloyd na Alexandra wanasema kama mabadiliko yenye yalitokea mu maisha yao yalijaribu imani yao mu njia zenye hawakuwazia. Lakini wanaona kama kujaribiwa mu njia hizo kumewasaidia kabisa. Sasa wanajua kama imani yao ni yenye nguvu zaidi; inaweza kuwasaidia wapate kitulizo wakati wako na magumu, na wanaona kama wamekuwa watu wazuri zaidi.

Mabadiliko yenye hatukuwazia yanaweza kuleta baraka zenye hatukuwazia! (Picha hizi zinapatana na fungu la 19-21)

22. Kama tunafanya mambo yote yenye tunaweza kufanya mu hali zetu, tunaweza kuwa hakika juu ya jambo gani?

22 Katika ulimwengu huu, maisha yetu yanaweza kubadilika bila kutazamia. Tunaweza kupewa mugao mupya mu kazi ya Yehova, tunaweza kugonjwa, ao tunaweza kulazimika kuhangaikia familia yetu mu njia ya mupya. Lakini, hata jambo gani litokee, ukuwe hakika kama Yehova anakuhangaikia na atakusaidia kwa wakati wenye kufaa. (Ebr. 4:16; 1 Pe. 5:6, 7) Kwa sasa, fanya mambo yote yenye unaweza kufanya katika hali yako. Sali kwa Yehova, Baba yako, na ujifunze kumutegemea kabisa. Kama unafanya vile, utakuwa na amani ya akili yenye kutoka kwa Yehova, hata hali zako zibadilike namna gani.

^ fu. 4 Miaka fulani kisha pale, Yosefu alimupatia mwana wake muzaliwa wa kwanza jina la Manase kwa sababu, alisema hivi: “Mungu amenifanya nisahau taabu yangu yote.” Alielewa kama mwana wake alikuwa zawadi yenye Yehova alimupatia ili kumufariji.​—Mwa. 41:51, maelezo ya chini.

^ fu. 14 Ona habari “Ulijua?” katika gazeti hili.