Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tufundishe Kweli

Tufundishe Kweli

“Ee Yehova, . . . chanzo kabisa cha neno lako ni kweli.”​—ZB. 119:159, 160.

NYIMBO: 29, 53

1, 2. (a) Ni kazi gani yenye ilikuwa ya maana sana mu maisha ya Yesu, na juu ya nini? (b) Juu tuko “wafanyakazi pamoja na Mungu,” tunapaswa kufanya nini ili tupate matokeo ya muzuri?

YESU KRISTO alikuwa seremala na kisha akakuwa mutumishi ao muhubiri. (Mk. 6:3; Ro. 15:8) Alifanya kazi hizo mbili kwa ukamilifu. Wakati alikuwa seremala, alijifunza namna ya kutumia vyombo vyake ili kufanya vitu mbalimbali vya mbao. Na wakati alikuwa muhubiri, alitumia ujuzi mingi wa Maandiko wenye alikuwa nao ili kusaidia watu wa kawaida ili waelewe kweli ya Neno la Mungu. (Mt. 7:28; Lu. 24:32, 45) Wakati Yesu alikuwa na miaka 30, aliacha kazi ya useremala na akakuwa muhubiri kwa sababu alijua kama hiyo ndiyo ilikuwa kazi ya maana sana yenye angefanya. Alisema kama kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu ilikuwa sababu moja kati ya sababu zenye zilifanya Mungu amutume mu dunia. (Mt. 20:28; Lu. 3:23; 4:43) Yesu alitia kazi ya kuhubiri habari njema pa nafasi ya kwanza mu maisha yake, na alipenda wengine wafanye vile.​—Mt. 9:35-38.

2 Wengi kati yetu hawako waseremala, lakini sisi wote tuko wahubiri wenye kufundisha wengine habari njema. Kazi hiyo iko ya maana sana, juu tunaifanya pamoja na Mungu. Tunaitwa “wafanyakazi pamoja na Mungu.” (1 Ko. 3:9; 2 Ko. 6:4) Tunakubali maneno ya muandikaji wa zaburi mwenye alisema hivi: “Chanzo kabisa cha neno lako ni kweli.” (Zb. 119:159, 160) Neno la Yehova ni kweli. Ndiyo maana tunapenda kuhakikisha kama ‘tunatumia sawasawa neno la kweli’ mu kazi yetu ya kuhubiri. (Soma 2 Timoteo 2:15.) Kwa hiyo, tunaendelea kujikaza ili tukuwe na ufundi zaidi wa kutumia Biblia, chombo chetu kikubwa cha kufundisha watu juu ya Yehova, Yesu, na Ufalme. Ili tupate matokeo ya muzuri mu kazi yetu ya kuhubiri, tengenezo la Yehova limetupatia vyombo vingine vya kutusaidia, na tunapaswa kujua namna ya kuvitumia pia. Vyombo hivyo viko kati ya Vyombo vyetu vya Kufundishia.

3. Tunapaswa kukaza akili yetu juu ya jambo gani mu kazi yetu ya kuhubiri, na namna gani Matendo 13:48 inatusaidia kufanya vile?

3 Unaweza kujiuliza juu ya nini tunaita vyombo hivyo Vyombo vya Kufundishia lakini hatuviite Vyombo vya Kuhubiria. Juu “kuhubiri” maana yake kutangaza ujumbe, lakini “kufundisha” maana yake kufasiria ujumbe huo ili mutu aelewe mambo yenye anasikia na kisha achochewe kutenda kulingana na mambo yenye anajifunza. Katika wakati mufupi wenye kubakia wa ulimwengu huu, tunapaswa kukaza akili yetu juu ya kuanzisha mafunzo ya Biblia na kufundisha watu kweli ili wakuwe wanafunzi wa Kristo. Maana yake tunapaswa kutafuta kwa bidii wale wote wenye kuwa na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele” na kuwasaidia waanze kumutumikia Yehova.​—Soma Matendo 13:44-48.

4. Namna gani tunaweza kupata wale wenye kuwa na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele”?

4 Namna gani tunaweza kupata wale wenye kuwa na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele”? Njia moja yenye Wakristo wa kwanza walitumia ili wapate watu kama hao ilikuwa kuhubiri. Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Katika muji ao kijiji chochote kwenye mutaingia, mutafute ni nani mwenye kustahili.” (Mt. 10:11) Tunapaswa kufanya vilevile leo. Kwa kweli, kama watu hawana moyo muzuri, ni wenye kiburi, ao hawahangaikie mambo ya Mungu, hatuwezi kutazamia kama watasikiliza habari njema. Tunatafuta watu wenye kuwa na moyo muzuri, wenye kuwa wanyenyekevu, na wenye kupenda kabisa kujua kweli. Tunaweza kulinganisha kazi yetu ya kutafuta watu na mambo yenye Yesu alipaswa kufanya wakati alikuwa seremala. Mbele ya kutengeneza kitu fulani kama vile meza ao kiti, mulango, nira ao kitu kingine, alipaswa kwanza kutafuta mbao zenye kufaa. Kisha angekamata kisanduku chake cha vyombo, angetumia ufundi wake, na kutengeneza kitu hicho. Vilevile leo, tunatafuta kwanza watu wenye kuwa na moyo muzuri, na kisha tunaweza kutumia sasa vyombo vyetu na ufundi wetu ili kuwasaidia wakuwe wanafunzi.​—Mt. 28:19, 20.

5. Tunapaswa kujua nini juu ya Vyombo vyetu vya Kufundishia? Leta mufano. (Ona picha ku mwanzo wa habari hii.)

5 Katika sanduku la vyombo, kila chombo kiko na kazi yake. Kwa mufano, wazia vyombo vyenye Yesu alikuwa anatumia wakati alikuwa seremala. * (Ona maelezo ya chini.) Alikuwa na lazima ya vyombo vya kupima, kutia alama, kukata, kutoboa matundu, na kupatia mbao umbo fulani, na pia vyombo vya kusawazisha vipande vya mbao na kuviunganisha pamoja. Vilevile, kila chombo kati ya Vyombo vyetu vya Kufundishia kiko na kazi yake. Tuone basi namna ya kutumia vyombo hivyo vya maana.

VYOMBO VYENYE KUJULISHA WATU SISI NI NANI

6, 7. (a) Namna gani umetumia karte za jw.org? (b) Juu ya nini tunatumia mialiko ya kualika watu kwenye mikutano ya kutaniko?

6 Karte za Jw.Org. Karte hizo ni za kidogo-kidogo lakini ni vyombo vyenye kuleta matokeo ya muzuri vyenye vinajulisha watu sisi ni nani na kuwaongoza ku site yetu ya Enternete jw.org. Kwenye site yetu ya Enternete wanaweza kujifunza mambo mingi juu yetu na kuomba hata funzo la Biblia. Kufikia sasa watu zaidi ya 400 000 wameomba funzo la Biblia kwenye jw.org, na mamia wanafanya vile kila siku! Unaweza kutembea na karte kidogo ili uzitumie wakati unazungumuza na watu wenye unakutana nao muchana wote.

7 Mialiko. Kwenye mwaliko wenye kuchapishwa wa kualika watu ku mikutano yetu kuko maneno haya: “Unaalikwa Kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova.” Kisha mualiko unasema kama unaweza kufanya vile “kwenye mikutano yetu” “ao Shahidi fulani atakufundisha Biblia.” Kwa hiyo, mialiko inajulisha watu sisi ni nani na pia inaalika wale wenye “wanatambua uhitaji wao wa kiroho” wajifunze Biblia pamoja na sisi. (Mt. 5:3) Kwa kweli, watu wanaalikwa kuja kwenye mikutano yetu hata kama wanakubali kujifunza Biblia ao hapana. Wakati wanakuja kwenye mikutano yetu, wataona kama wanaweza kujifunza mambo mingi juu ya Biblia.

8. Juu ya nini ni jambo la maana watu wakuje ku mikutano yetu, hata mara moja? Leta mufano.

8 Ni jambo la maana sana tuendelee kualika watu ili wakuje ku mikutano yetu hata mara moja. Juu ya nini? Juu wakati wanakuja ku mikutano, wataona kama Mashahidi wa Yehova wanafundishaka kweli yenye kuwa katika Biblia na wanasaidia watu wafikie kumujua Mungu, lakini dini za uongo hazifanye vile. (Isa. 65:13) Kwa mufano, bwana mumoja mwenye kuitwa Ray na bibi yake Linda, wenye kuishi mu inchi ya Amerika, waliona tofauti hiyo kumepita miaka fulani. Walikuwa wanamuamini Mungu na walipenda kumujua muzuri zaidi. Kwa hiyo, waliamua kutembelea makanisa yote yenye yalikuwa mu muji wao na kutafuta mambo mbili mbele waingie katika kanisa moja. Kwanza, walipaswa kujifunza jambo fulani katika kanisa hilo, na pili, watu wa kanisa hilo walipaswa kuvaa kwa njia yenye kuonyesha kama wao ni watu wenye kumutumikia Mungu. Juu kulikuwa makanisa mingi sana, iliomba miaka mingi ili wafanye vile. Lakini, walivunjika moyo sana. Walikuwa hawajajifunza hata jambo moja, na watu wa makanisa hayo walikuwa wanavaa mubaya sana. Kisha kutembelea kanisa la mwisho lenye walikuwa wanafikiria, Linda alienda ku kazi na Ray naye alirudia ku nyumba. Wakati alikuwa anarudia ku nyumba, alitembeza motokari yake mupaka kwenye Jumba moja la Ufalme. Aliwaza hivi: ‘Acha niingie ndani nione ni nini inafanyika mule.’ Kwa kweli, alijionea jambo lenye kufurahisha sana mu Jumba la Ufalme! Kila mutu alikuwa mwema na mwenye urafiki na mwenye kuvaa muzuri sana. Ray alikaa ku viti vya mbele na alifurahia mambo yenye alijifunza! Hilo linatukumbusha mambo yenye mutume Paulo alisema juu ya mutu mwenye anakuja ku mikutano kwa mara ya kwanza na kusema hivi: “Kwa kweli Mungu iko katikati yenu.” (1 Ko. 14:23-25) Kisha pale, Ray alianza kuja ku mukutano kila Siku ya Yenga. Kisha akaanza kuja ku kila mukutano wa katikati ya juma. Linda naye akaanza kuja ku mikutano, na hata kama walikuwa na miaka zaidi ya 70 walijifunza Biblia na wakabatizwa.

VYOMBO VYA KUANZISHA MAZUNGUMUZO

9, 10. (a) Juu ya nini ni mwepesi kutumia trakte? (b) Fasiria namna ya kutumia trakte Ufalme wa Mungu Ni Nini?

9 Trakte. Tuko na trakte munane kati ya Vyombo vyetu vya Kufundishia. Ziko mwepesi kutumia, na zinaleta matokeo ya muzuri sana wakati wa kuanzisha mazungumuzo. Tangu wakati trakte za kwanza kati ya trakte hizo zilitolewa katika mwaka wa 2013, miliare tano hivi ya trakte hizo zimechapishwa! Trakte hizo zote zimepangwa kwa namna moja. Kwa hiyo, wakati unajua namna ya kutumia trakte moja, unaweza kutumia zingine zote! Namna gani unaweza kutumia trakte ili kuanzisha mazungumuzo na mutu fulani?

10 Pengine unapenda kutumia trakte Ufalme wa Mungu Ni Nini? Onyesha mutu ulizo lenye kuwa mbele ya trakte na umuulize hivi: “Ulishaka kujiuliza Ufalme wa Mungu ni nini? Unawaza ni . . . ?” Kisha umuulize ni jibu gani lenye anaweza kuchagua kati ya majibu tatu yenye kuonyeshwa. Usiseme kama jibu lake ni la muzuri ao la mubaya, ufungue tu trakte kwenye sehemu “Ona Jibu la Biblia” yenye kuwa ndani ya trakte na usome maandiko yenye kuwa ndani, Danieli 2:44 na Isaya 9:6. Ku mwisho wa mazungumuzo, umuulize ulizo lenye kuwa nyuma ya trakte lenye kuwa katika sehemu yenye kichwa “Pengine Unajiuliza”: “Maisha ya watu yatakuwa namna gani wakati Ufalme wa Mungu utaanza kutawala?” Unaweza kujibu ulizo hilo wakati utazungumuza naye tena. Wakati munakutana tena, unaweza kutumia somo la 7 la broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu! Broshua hiyo iko kati ya vyombo vyetu vya kuanzisha mafunzo ya Biblia.

VYOMBO VYENYE KUSAIDIA WATU WAPENDEZWE NA BIBLIA

11. Magazeti yetu yako na kusudi gani, na tunapaswa kujua nini juu ya magazeti hayo?

11 Magazeti. Munara wa Mulinzi na Amuka! ndiyo magazeti yenye kuchapishwa na kutafsiriwa zaidi katika dunia! Watu wa inchi mbalimbali wanasoma magazeti hayo, kwa hiyo, vichwa vya habari vyenye kuwa ku jalada viko na kusudi la kuchochea watu wa kila mahali wapendezwe. Tunapaswa kutumia magazeti hayo ili kusaidia watu wakaze akili yao juu ya jambo la maana zaidi mu maisha leo. Lakini, tunapaswa kwanza kujua kila gazeti linatayarishwa kwa ajili ya watu wa namna gani.

12. (a) Amuka! inatayarishwa kwa ajili ya watu gani, na iko na kusudi gani? (b) Ni mambo gani ya kufurahisha yenye umejionea hivi karibuni wakati ulitumia chombo hiki?

12 Amuka! iko na kusudi la kusaidia watu wenye wanajua mambo kidogo sana juu ya Biblia ao wenye hawajue jambo lolote juu ya Biblia. Pengine hawajue hata jambo lolote juu ya mafundisho ya Kikristo, pengine hawatumainie hata kidogo dini, ao pengine hawajue kama Biblia inaweza kuwasaidia mu maisha yao. Kusudi kubwa la Amuka! ni kusaidia musomaji aamini kabisa kama Mungu iko. (Ro. 1:20; Ebr. 11:6) Inasaidia pia musomaji aamini kama Biblia ‘iko kwa kweli . . . neno la Mungu.’ (1 Te. 2:13) Amuka! tatu za mwaka wa 2018 ziko na tungo hizi: “Njia ya Maisha Yenye Furaha,” “Siri 12 ili Kuwa na Familia Yenye Furaha,” na “Musaada kwa Wale Wenye Wamefiwa na Wapendwa Wao.”

13. (a) Gazeti Munara wa Mulinzi la watu wote linatayarishwa kwa ajili ya watu wa namna gani? (b) Ni mambo gani ya kufurahisha yenye umejionea hivi karibuni wakati ulitumia chombo hiki?

13 Kusudi kubwa la gazeti Munara wa Mulinzi la watu wote ni kufasiria mafundisho ya Biblia watu wenye tayari wanaheshimia Mungu na Biblia kwa kadiri fulani. Pengine wanajua mambo fulani juu ya Biblia, lakini hawaelewe muzuri kabisa mambo yenye Biblia inafundisha. (Ro. 10:2; 1 Ti. 2:3, 4) Magazeti tatu ya mwaka wa 2018 yanajibu maulizo haya: “Biblia Ingali Yenye Faida Leo?,” “Maisha Yako ya Wakati Wenye Kuja Yatakuwa Namna Gani?,” na “Mungu Anakuhangaikia?

VYOMBO VYENYE KUCHOCHEA WATU WAPENDEZWE

14. (a) Video ine zenye tuko nazo katika Vyombo vyetu vya Kufundishia ziko na kusudi gani? (b) Ni mambo gani ya kufurahisha yenye umejionea wakati ulionyesha watu video hizo?

14 Video. Wakati wa Yesu, seremala alikuwa tu na vyombo vya kutumia na mikono. Lakini leo, seremala wako pia na vyombo vyenye kutumia umeme, kama vile misumeno, vyombo vya kutoboa matundu, na vyombo ya kufanya mbao ikuwe laini. Wakati tunahubiri leo, zaidi ya vichapo vyenye kuchapishwa, tuko na video za muzuri za kuonyesha watu. Video ine zenye kuwa kati ya vyombo vyetu ni: Sababu Gani Ujifunze Biblia?, Tunajifunzaka Biblia na Watu Namna Gani?, Kwa Kawaida Tunafanya Nini Kwenye Jumba la Ufalme?, na Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Namna Gani? Tunaweza kuonyesha watu video hizo zenye kuwa fupi kwa karibu dakika mbili na zinaleta matokeo ya muzuri wakati tunatembelea watu kwa mara ya kwanza. Tunaweza kutumia video za murefu wakati tunarudilia watu na tunaweza kuzionyesha watu wenye kuwa na wakati zaidi. Video hizo ni vyombo vya muzuri sana juu zinachochea watu wajifunze Biblia na wakuje ku mikutano yetu.

15. Wakati watu wanaangalia video zetu mu luga yao, hilo linaweza kuleta matokeo gani? Leta mifano.

15 Kwa mufano, dada mumoja alikutana na mwanamuke mumoja mwenye alikuwa ametoka Mikronesia na luga ya kizalikio ya mwanamuke huyo ilikuwa Kiyapese. Dada huyo alimuonyesha mu luga ya Kiyapese video Sababu Gani Ujifunze Biblia? Wakati video ilianza, mwanamuke huyo alisema hivi: “Hii ni luga yangu. Siamini kabisa! Kupitia namna yake ya kutamka maneno, ninaweza kujua kama alitoka ku kisiwa changu. Anazungumuza luga yangu!” Kisha hapo, alisema kama atasoma na kuangalia kila kitu chenye kuwa katika luga yake ku jw.org. (Linganisha na Matendo 2:8, 11.) Mufano mwingine ni wa dada fulani wa inchi ya Amerika mwenye mutoto wa ndugu yake mukubwa anaishi mu kontinenti ingine. Alimutumia njia ya kumupeleka mara moja ku video hiyo mu luga yake. Mutoto huyo aliangalia video hiyo na akamuandikia ujumbe huu ku Enternete: “Sehemu yenye kuzungumuzia nguvu ya mubaya yenye inaongoza dunia ilichochea akili yangu. Niliomba funzo la Biblia.” Hilo ni jambo la kupendeza sana kwa sababu anaishi katika inchi kwenye kazi yetu imewekewa vizuizi!

VYOMBO VYENYE KUTUSAIDIA KUFUNDISHA KWELI

16. Fasiria kusudi la broshua: (a) Umusikilize Mungu ili Uishi Milele. (b) Habari Njema Inayotoka kwa Mungu! (c) Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?

16 Broshua. Namna gani tunaweza kufundisha kweli mutu fulani mwenye hajue kusoma muzuri ao mutu mwenye hana kichapo chochote chenye kuzungumuzia Biblia mu luga yake? Tunaweza kutumia broshua Umusikilize Mungu ili Uishi Milele. * (Ona maelezo ya chini.) Chombo cha muzuri sana cha kutumia juu ya kuanzisha mafunzo ya Biblia ni broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu! Unaweza kuonyesha mutu somo 14 zenye kupatikana nyuma ya broshua na kumuuliza ni habari gani yenye kumupendeza sana. Kisha muanze kujifunza habari hiyo. Umejaribu kufanya vile wakati unarudilia watu? Broshua ya tatu yenye kuwa kati ya vyombo vyetu ni broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo? Iko na kusudi la kufundisha wanafunzi wa Biblia juu ya tengenezo letu. Ili kujua namna ya kutumia broshua hiyo wakati wa kila funzo la Biblia, ona Utumishi na Maisha ya Mukristo​—Buku la Mukutano la Mwezi wa 3, 2017.

17. (a) Kila kitabu cha funzo kiko na kusudi gani? (b) Wale wote wenye wanabatizwa wanapaswa kufanya nini, na juu ya nini?

17 Vitabu. Kisha kuanza kujifunza na mutu mu broshua fulani, wakati wowote unaweza kubadilisha kichapo na kuanza kutumia kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Chombo hicho kinaweza kusaidia watu wajifunze mambo mengi zaidi juu ya mafundisho ya musingi ya Biblia. Kama mwanafunzi iko anafanya maendeleo na anamaliza kitabu hicho, unaweza kuendelea kujifunza naye kitabu Mubaki “Katika Upendo wa Mungu.” Chombo hicho kitasaidia mwanafunzi ajue namna ya kutumia kanuni za Biblia mu maisha yake ya kila siku. Ukumbuke kama, hata kisha kubatizwa, wapya wanapaswa kuendelea kujifunza mupaka wakati watamaliza vitabu hivyo viwili. Hilo litawasaidia wakuwe na imani yenye nguvu katika Yehova na kubakia washikamanifu kwake.​—Soma Wakolosai 2:6, 7.

18. (a) Andiko la 1 Timoteo 4:16 linatutia moyo sisi walimu wa kweli tufanye nini, na hilo litakuwa na matokeo gani? (b) Kusudi letu ni gani wakati tunatumia Vyombo vyetu vya Kufundishia?

18 Sisi Mashahidi wa Yehova, tuko na daraka la kufundisha watu “ujumbe wa kweli ya habari njema” wenye unaweza kuwasaidia wapate uzima wa milele. (Kol. 1:5; soma 1 Timoteo 4:16.) Ili kutusaidia kufanya vile, tuko na Vyombo vya Kufundishia vyenye tuko navyo lazima. (Ona kisanduku “ Vyombo vya Kufundishia.”) Tujikaze basi kutumia vyombo hivyo muzuri kabisa. Kila mumoja wetu anaweza kuamua ikiwa atatumia chombo gani kati ya vyombo hivyo na wakati gani. Lakini, ukumbuke kama kusudi letu haiko kutolea tu watu vichapo, na hatupatie vichapo watu wenye hawapendezwe na ujumbe wetu. Kusudi letu ni kusaidia watu wenye kuwa na moyo muzuri, wenye kuwa wanyenyekevu, na wenye kupenda kabisa kumujua Mungu wakuwe wanafunzi; watu wenye kuwa na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele.”​—Mdo. 13:48; Mt. 28:19, 20.

^ fu. 5 Ona habari “Seremala” na pia kisanduku “Sanduku la Vifaa vya Seremala” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 8, 2010.

^ fu. 16 Kama mutu hajue kusoma, unaweza kumusaidia afuatane na wewe mu broshua Umusikilize Mungu, yenye kuwa na picha za mingi kuliko maneno.