Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ndugu Rutherford anatoa hotuba ku mukusanyiko wa Cedar Point, Ohio, mwaka wa 1919

1919​—Kumepita Sasa Miaka Mia Moja

1919​—Kumepita Sasa Miaka Mia Moja

KUFIKIA mwaka wa 1919, Vita Kubwa (yenye kisha iliitwa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu), ilikuwa imeisha; vita hiyo ilifanya zaidi ya miaka ine. Ku mwisho wa mwaka wa 1918, mataifa iliacha kupigana, na tarehe 18 Mwezi wa 1, 1919, Mukutano wa Amani wa Paris ulianza. Jambo moja kati ya mambo yenye mukutano huo ulitimiza ni Makubaliano ya Versailles, yenye ilimaliza vita kati ya Majeshi ya Muungano na Ujerumani. Makubaliano hiyo ilitiwa sinyatire tarehe 28 Mwezi wa 6, 1919.

Makubaliano hiyo ilianzisha pia shirika mupya lenye liliitwa Ushirika wa Mataifa. Shirika hilo lilikuwa na kusudi la “kuendelesha uhusiano muzuri kati ya mataifa na kuleta amani na usalama kati ya mataifa.” Dini za mingi zenye kujiita kuwa za Kikristo ziliunga mukono Ushirika huo. Baraza la Muungano wa Makanisa ya Kristo katika Amerika liliunga mukono Ushirika wa Mataifa kwa kusema kama “lilikuwa tengenezo la politike lenye liliwakilisha Ufalme wa Mungu ku dunia.” Baraza hilo liliunga mukono Ushirika wa Mataifa kwa kutuma wajumbe kwenye Mukutano wa Amani wa Paris. Mumoja kati ya wajumbe hao alisema kama mukutano huo “ulikuwa mwanzo wa kipindi cha mupya katika historia ya ulimwengu.”

Kipindi cha mupya kilikuwa kinaanza, lakini haiko wanaume wenye walikuwa katika mukutano huo wa amani njo wangeanzisha kipindi hicho. Katika mwaka wa 1919, kipindi cha mupya katika kazi yetu ya kuhubiri kilianza wakati Yehova alipatia watu wake nguvu za kuhubiri zaidi kuliko zamani. Lakini mbele kipindi hicho kianze, badiliko kubwa lilipaswa kufanywa kuhusu Wanafunzi wa Biblia.

UAMUZI WA NGUVU

Joseph F. Rutherford

Uchaguzi wa kila mwaka wa viongozi wa Watch Tower Bible and Tract Society ulipangwa kufanywa Siku ya Posho tarehe 4 Mwezi wa 1, 1919. Wakati huo, Joseph Rutherford, mwenye alikuwa anaongoza kati ya watu wa Yehova, alikuwa amefungwa bila haki katika Atlanta, Georgia, Inchi ya Amerika, pamoja na wengine saba. Lakini ulizo lilikuwa hili: Ndugu wenye walikuwa wamefungwa wenye walikuwa maofisa walipaswa kuchaguliwa tena? Ao watu wengine walipaswa kuchaguliwa pa nafasi yao?

Evander Coward

Wakati Ndugu Rutherford alikuwa mu chumba chake cha gereza, alikuwa na mahangaiko juu ya namna tengenezo lingekuwa wakati wenye kuja. Alijua kama ndugu fulani walikuwa wanawaza kama ilikuwa muzuri wachague ndugu mwingine akuwe musimamizi. Kwa hiyo, aliandikia barua wale wenye walikuwa katika mukutano na akapendekeza ndugu Evander Coward akuwe musimamizi. Rutherford alisema kama Coward ni ndugu “mutulivu,” “mwenye busara,” na “mwenye kujitoa kwa Bwana.” Lakini ndugu wengi walikuwa na mawazo tofauti, walipenda uchaguzi huo usifanywe wakati huo lakini ufanywe kisha miezi sita. Wanasheria wenye walikuwa wametetea ndugu wenye walikuwa katika gereza walikubali. Wakati walikuwa wanazungumuzia jambo la kufanya, ndugu fulani walikasirika sana.

Richard Barber

Kisha jambo fulani lilitokea lenye Richard Barber alisema kama lilikuwa kama vile ‘kumwanga maji juu ya moto wenye kuwaka.’ Mumoja kati ya ndugu wenye walikuwa pale alisema hivi: “Sijue muzuri mambo yenye sheria inaomba, lakini ninajua maana ya kuwa mushikamanifu. Mungu anatuomba tukuwe washikamanifu. Njia ya muzuri zaidi ya kuonyesha ushikamanifu wetu kwa Mungu ni kufanya uchaguzi na kumuchagua tena Ndugu Rutherford akuwe musimamizi.”​—Zb. 18:25.

Alexander Macmillan

Siku moja Alexandre Macmillan mwenye alikuwa pia katika gereza alikumbuka kama siku yenye ilifuata uchaguzi, Ndugu Rutherford aligonga ku ukuta wa chumba chake cha gereza na kusema hivi: “Leta mukono wako inje.” Kisha, Ndugu Rutherford alimupatia telegramu. Macmillan aliona ujumbe mufupi wa telegramu hiyo na alijua maana yake palepale. Ujumbe huo ulisema hivi: “RUTHERFORD WISE VAN BARBER ANDERSON BULLY NA SPILL MUSIMAMIZI NA MAOFISA TATU WA KWANZA TUNAWAPENDA NINYI WOTE.” Ujumbe huo ulimaanisha kama viongozi wote walikuwa wamechaguliwa tena na kama Joseph Rutherford, na William Van Amburgh walibakia maofisa. Kwa hiyo, Ndugu Rutherford angeendelea kuwa musimamizi.

WANAACHILIWA!

Wakati ndugu hao munane walikuwa wanafungwa, Wanafunzi waaminifu wa Biblia waliomba watu watie sinyatire juu ya ombi lenye walipaswa kutumia serikali ili kuomba ndugu hao waachiliwe. Ndugu na dada hao wenye uhodari walipata sinyatire zaidi ya 700 000. Siku ya Tatu tarehe 26 Mwezi wa 3, 1919, mbele ombi hilo litumwe, Ndugu Rutherford na ndugu wengine wenye madaraka waliachiliwa.

Katika hotuba yenye alitolea wale wenye walimukaribisha wakati alitoka mu gereza, Ndugu Rutherford alisema hivi: “Niko hakika kama jaribu hili lenye tulipata sisi wote linatutayarisha tu kwa ajili ya wakati wa magumu zaidi. . . . Kusudi la pigano lenu haikukuwa kutosha ndugu zenu katika gereza. Haiko njo kusudi kabisa la mambo yote yenye mulifanya. . . . Pigano lenu lilikuwa na kusudi la kutoa ushahidi juu ya ile Kweli, na wale wenye walipigana pigano hilo wamepata baraka ya muzuri sana.”

Mambo yenye ilitokea wakati ndugu zetu walikuwa wanasamba inaweza kuonyesha kama Yehova alikuwa anaongoza mambo. Tarehe 14 Mwezi wa 5, 1919, tribinali ya kusikiliza tena mashitaka ilitoa uamuzi huu: “Washitakiwa katika kesi hii hawakupewa . . . hukumu yenye haina upendeleo yenye walikuwa na haki ya kupewa, na kwa hiyo hukumu hiyo imevunjwa.” Ndugu walikuwa wameshitakiwa makosa mazito, na hukumu hizo zingebakia mu dosye zao kama wangesamehewa tu ao kama hukumu zao zingepunguzwa tu. Hakuna mambo ingine yenye walishitakiwa tena. Kwa hiyo, Muamuzi Rutherford aliendelea kutumia uzoefu wake wa mambo ya sheria ili kutetea watu wa Yehova ku Tribinali Kubwa ya inchi ya Amerika, na alifanya vile mara mingi kisha kuachiliwa kwake.

WALIAZIMIA KUHUBIRI

Ndugu Macmillan alikumbuka hivi: “Hatukupaswa kuwa wavivu na kukunja mikono yetu ili kungojea Bwana atupeleke mbinguni. Tulitambua kama tulipaswa kufanya jambo fulani ili tujue mapenzi ya Bwana ilikuwa nini kabisa.”

Lakini ndugu kwenye makao makubwa hawangeweza kuendelea kufanya kazi yenye walikuwa wamefanya kwa miaka mingi. Juu ya nini? Juu wakati ndugu walikuwa wamefungwa, mabamba yote ya kuchapishia yenye ilikuwa inatumiwa ili kuchapisha vichapo ilikuwa imeharibiwa. Hilo lilivunja moyo, na ndugu na dada fulani walijiuliza ikiwa kazi ya kuhubiri ilikuwa imeisha.

Kulikuwa kungali watu wenye kupendezwa na ujumbe wa Ufalme wenye Wanafunzi wa Biblia walikuwa wanahubiri? Ili kujibu ulizo hilo, Ndugu Rutherford aliamua kutoa hotuba. Iliomba kualika watu wote. Ndugu Macmillan alisema hivi: “Kama hakuna mutu mwenye alikuja kwenye mukutano huo, tungejua kama kazi ya kuhubiri imeisha.”

Tangazo la gazeti la hotuba ya Ndugu Rutherford katika Los Angeles, California, mwaka wa 1919. Hotuba hiyo ilikuwa na kichwa “Tumaini kwa Ajili ya Wanadamu Wenye Kutaabika”

Kwa hiyo, Siku ya Yenga tarehe 4 Mwezi wa 5, 1919, hata kama Ndugu Rutherford alikuwa na ugonjwa wa nguvu sana, alitoa katika Los Angeles, California, hotuba yenye kichwa “Tumaini kwa Ajili ya Wanadamu Wenye Kutaabika.” Watu karibu 3 500 walikuja kusikiliza hotuba hiyo, na mamia ingine ya watu walirudishwa juu hawakupata nafasi. Siku yenye ilifuata, watu wengine 1 500 walikuja kusikiliza hotuba hiyo. Ndugu walipata jibu: watu walikuwa wanapendezwa!

Jambo lenye ndugu walifanya kisha pale lilikuwa na matokeo juu ya namna kazi ya kuhubiri ya Mashahidi wa Yehova inafanywa mupaka leo.

WALIJITAYARISHA KWA AJILI YA ONGEZEKO LA WAKATI WENYE ULIKUWA MBELE

Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 8, 1919, ulitangaza kama mukusanyiko mukubwa ungefanywa Cedar Point, Ohio ku mwanzo-mwanzo wa Mwezi wa 9. Clarence Beaty, Mwanafunzi kijana wa Biblia wa Missouri, alikumbuka hivi: “Kila mutu aliona kama alipaswa tu kuwa pale.” Ndugu na dada zaidi ya 6 000 walihuzuria mukusanyiko huo, walikuwa wengi zaidi kuliko namna waliwazia. Wanafunzi zaidi ya 200 walibatizwa mu Ziwa Erie lenye lilikuwa karibu, na jambo hilo pia lilifanya mukusanyiko huo ukuwe wenye kufurahisha sana.

Jalada la gazeti la kwanza L’Âge d’Or, la tarehe 1 Mwezi wa 10, 1919

Tarehe 5 Mwezi wa 9, 1919, siku ya tano ya mukusanyiko huo, katika hotuba yake yenye kichwa “Hotuba kwa Wafanyakazi Wenzi,” Ndugu Rutherford alitangaza kutolewa kwa gazeti mupya lenye kichwa L’Âge d’Or. * Gazeti hilo “lingekuwa na habari za sasa za maana sana, na kutoa mafasirio yenye kutegemea Maandiko yenye kuonyesha juu ya nini matukio makubwa [ilikuwa] inatendeka.”

Wanafunzi wote wa Biblia walitiwa moyo wahubiri kwa bidii kwa kutumia gazeti hilo mupya. Barua yenye ilifasiria namna kazi hiyo ilipaswa kufanywa ilisema hivi: “Kila mutu mwenye kujitoa kwa Mungu [mwenye kubatizwa] akumbuke kama ni pendeleo kubwa kufanya utumishi huu, na afanye mambo yote yenye anaweza leo ili kutolea ulimwengu ushahidi huu mukubwa.” Watu wengi walikubali mwaliko huo wa kuhubiri! Kufikia Mwezi wa 12, wahubiri wa Ufalme wenye bidii walikuwa wamepata watu zaidi ya 50 000 wenye walijiandikisha ili kupata gazeti hilo mupya kila mwezi.

Ndugu katika Brooklyn, New York, na motokari wenye kubeba mizigo ya gazeti L’Âge d’Or

Kufikia mwisho wa mwaka wa 1919, watu wa Yehova walikuwa wamepangwa muzuri na walikuwa wametiwa nguvu. Tena, unabii mbalimbali wa maana juu ya siku za mwisho ulikuwa umetimia. Kujaribiwa na kusafishwa kwa watu wa Mungu, kwenye kulitabiriwa mu Malaki 3:1-4, kulikuwa kumemalizika. Watu wa Yehova walikuwa wamekombolewa kutoka katika utekwa wa mufano wa “Babiloni Mukubwa,” na Yesu alikuwa amemuweka “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” * (Ufu. 18:2, 4; Mt. 24:45) Sasa wanafunzi wa Biblia walikuwa tayari ili kufanya kazi yenye Yehova alipenda wafanye.

^ fu. 22 Gazeti L’Âge d’Or liliitwa Consolation katika mwaka wa 1937 na Amuka! mu mwaka wa 1946.