Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 41

Endelea Kuwa Muaminifu Wakati wa “Taabu Kubwa”

Endelea Kuwa Muaminifu Wakati wa “Taabu Kubwa”

“Mumupende Yehova, ninyi wote wenye kuwa washikamanifu kwake! Yehova analinda waaminifu.”​—ZB. 31:23.

WIMBO 129 Tutaendelea Kuvumilia

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. (a) Viongozi wa ulimwengu watatangaza nini hivi karibuni? (b) Ni maulizo gani yenye inapaswa kujibiwa?

WAZIA viongozi wa ulimwengu wametoka tu kufanya tangazo lenye lilitabiriwa la “amani na usalama.” Pengine wanajisifu kwa kusema kama ulimwengu unakuwa sasa na amani kabisa. Viongozi wa ulimwengu watapenda tuwaze kama wako na uwezo wa kumaliza magumu yote ya wanadamu. Lakini hawataweza hata kidogo kuzuia mambo yenye itatokea kisha pale! Juu ya nini? Juu kulingana na unabii wa Biblia, “uharibifu wa kushitukia utakuja juu yao mara moja, . . . na hawataponyoka hata kidogo.”​—1 Te. 5:3.

2 Kuko maulizo ya maana yenye inapaswa kujibiwa: Ni mambo gani itatokea wakati wa “taabu kubwa”? Yehova atatuomba tufanye nini wakati huo? Na namna gani tunaweza kujitayarisha leo ili tuendelee kuwa waaminifu wakati wa taabu kubwa?​—Mt. 24:21.

NI MAMBO GANI ITATOKEA WAKATI WA “TAABU KUBWA”?

3. Kulingana na Ufunuo 17:5, 15-18, namna gani Mungu ataharibu “Babiloni Mukubwa”?

3 Soma Ufunuo 17:5, 15-18. “Babiloni Mukubwa” ataharibiwa! Kama vile tumeona, viongozi wa ulimwengu hawataweza kuzuia mambo yenye itatokea wakati huo. Juu ya nini? Juu “Mungu [atatia] jambo hilo ndani ya mioyo yao ili kutimiza wazo lake.” Ni wazo gani? Ni kuharibu dini zote za uongo, kutia ndani dini zenye kujiita kuwa za Kikristo. * Mungu atatia wazo lake mu mioyo ya “pembe kumi (10)” za “munyama wa pori mwenye rangi nyekundu yenye kungaa.” Pembe kumi zinafananisha serikali zote za ulimwengu zenye zinaunga mukono “munyama wa pori,” ni kusema, Umoja wa Mataifa. (Ufu. 17:3, 11-13; 18:8) Wakati serikali za ulimwengu zitageukia dini za uongo, huo utakuwa mwanzo wa taabu kubwa. Litakuwa tukio la kushitukia na lenye kuogopesha lenye litagusa kila mutu ku dunia.

4. (a) Pengine viongozi wa ulimwengu watatoa sababu gani ili kufasiria juu ya nini walishambulia dini za uongo? (b) Pengine watu wenye walikuwa katika dini hizo watafanya nini?

4 Hatujue ikiwa viongozi wa ulimwengu watatoa sababu gani ili kufasiria juu ya nini walimushambulia Babiloni Mukubwa. Pengine watasema kama dini za ulimwengu njo zinafanya kusikuwe amani na kama zinajiingiza sikuzote mu mambo ya politike. Ao pengine watasema kama dini hizo zimejirundikia utajiri na vitu mingi. (Ufu. 18:3, 7) Inaonekana kama ni jambo lenye kupatana na akili kusema kuwa watu wote wenye kuwa katika dini hizo hawataharibiwa wakati wa shambulizi hilo. Lakini, inaonekana kuwa viongozi wa ulimwengu wataharibu dini zote. Kisha dini hizo zote kuharibiwa, wale wenye walikuwa katika dini hizo watatambua kama viongozi wao wa dini waliwadanganya na inawezekana wataanza kukana kabisa dini hizo.

5. Yehova ameahidi nini juu ya taabu kubwa, na juu ya nini?

5 Biblia haionyeshe ikiwa uharibifu wa Babiloni Mukubwa utafanya muda gani, lakini tunajua kama hautafanya muda murefu. (Ufu. 18:10, 21) Yehova ameahidi kama ‘atafupisha siku hizo’ za taabu kubwa ili “wale wenye amechagua” waokoke na ili dini ya kweli isiharibiwe. (Mk. 13:19, 20) Lakini, Yehova atatuomba tufanye nini kuanzia wakati Babiloni Mukubwa ataharibiwa mupaka vita ya Armagedoni?

ENDELEA KUSHIKAMANA NA IBADA SAFI

6. Juu ya nini haitoshe tu kuvunja uhusiano wowote na dini za uongo?

6 Kama vile tuliona katika habari yenye ilitangulia, Yehova anaomba waabudu wake wajitenge na Babiloni Mukubwa. Lakini, kufanya vile kunatia ndani mambo mingi zaidi ya kuvunja uhusiano wowote na dini za uongo. Tunapaswa kuazimia kushikamana na dini ya kweli, ni kusema, ibada safi ya Yehova. Tunaweza kufanya vile katika njia mbili. Tuone njia hizo.

Tusiache hata kidogo kukutana pamoja, hata wakati wa magumu (Picha hii inapatana na fungu la 7) *

7. (a) Namna gani tunaweza kushikamana na kanuni za Yehova za haki juu ya mwenendo muzuri? (b) Namna gani andiko la Waebrania 10:24, 25 linakazia kama ni jambo la maana kukutana pamoja, zaidi sana leo?

7 Njia ya kwanza, tunapaswa kushikamana na kanuni za Yehova za haki juu ya mwenendo muzuri. Hatupaswe kukubali kanuni za mwenendo za ulimwengu. Kwa mufano, hatukubali matendo ya uasherati ya aina zote, ndoa ya mwanaume na mwanaume na mwanamuke na mwanamuke, na matendo ingine ya wanaume kulala na wanaume na wanamuke kulala na wanamuke. (Mt. 19:4, 5; Ro. 1:26, 27) Njia ya pili, tunapaswa kuendelea kumuabudu Mungu pamoja na Wakristo wenzetu. Tunafanya vile nafasi yoyote kwenye tunaweza, ikuwe mu Majumba ya Ufalme ao, wakati ni lazima, tunafanya vile mu nyumba za ndugu ao hata kwa uficho. Hata jambo gani litokee, hatuwezi kuacha programu yetu ya kukutana pamoja ili kumuabudu Mungu. Kwa kweli, tunapaswa kukutana pamoja “zaidi sana kwa kadiri [tunaona] siku ile kuwa inakaribia.”​—Soma Waebrania 10:24, 25.

8. Inawezekana tutahubiri ujumbe gani wakati wenye kuja?

8 Wakati wa taabu kubwa, inawezekana ujumbe wenye tunahubiri utabadilika. Leo, tuko tunahubiri habari njema ya Ufalme na tuko tunajikaza kufanya wanafunzi. Lakini wakati huo, pengine tutahubiri ujumbe muzito sana wenye Biblia inafananisha na mvua ya majiwe. (Ufu. 16:21) Pengine tutahubiria watu kama ulimwengu wa Shetani unakaribia sana kuharibiwa. Wakati wenye kuja, tutajua muzuri ni ujumbe gani tutahubiri na namna tutahubiri ujumbe huo. Je, tutatumia njia zilezile za kuhubiri zenye tumetumia kwa miaka zaidi ya mia moja ili kutimiza utumishi wetu? Ao tutatumia njia zingine za kuhubiri? Hatujue. Hata ikuwe tutatumia njia gani, inaonekana kama tutakuwa na pendeleo la kuhubiri bila woga ujumbe wa hukumu ya Yehova!​—Eze. 2:3-5.

9. Pengine viongozi wa ulimwengu watatenda namna gani wakati watasikia ujumbe wetu, lakini tunaweza kuwa hakika na jambo gani?

9 Inawezekana kabisa kama ujumbe wetu utafanya viongozi wa ulimwengu wakasirike na watajaribu kutunyamazisha lote. Kama vile tunamutegemea Yehova leo ili atusaidie katika kazi yetu, tutakuwa na lazima ya kumutegemea wakati huo pia. Tunaweza kuwa hakika kama Mungu wetu atatupatia nguvu ya kutimiza mapenzi yake.​—Mik. 3:8.

UJITAYARISHE KWA AJILI YA SHAMBULIZI LENYE LITAFIKIA WATU WA MUNGU

10. Kulingana na unabii wa Biblia mu Luka 21:25-28, watu wengi watatenda namna gani juu ya mambo yenye itatokea wakati wa taabu kubwa?

10 Soma Luka 21:25-28. Wakati wa taabu kubwa, watu watavunjika moyo wakati wataona mambo yote yenye waliwaza kama itadumu inaanza kuanguka. Watakuwa na “uchungu,” kwa sababu wataogopa kama wanaweza kuuawa katika wakati huo mubaya sana wa historia ya wanadamu. (Sef. 1:14, 15) Wakati huo, inaonekana kuwa maisha itakuwa nguvu sana hata kwa watumishi wa Yehova. Pengine tutapata magumu fulani juu hatuko sehemu ya ulimwengu. Pengine tutakosa mambo fulani ya lazima.

11. (a) Juu ya nini viongozi wa ulimwengu watakazia Mashahidi wa Yehova uangalifu? (b) Juu ya nini hatupaswe kuogopa taabu kubwa?

11 Wakati fulani, watu wenye dini zao ziliharibiwa wanaweza kukasirika wakati wataona kama Mashahidi wa Yehova wanaendelea na dini yao. Kwa kweli, watu wataambia wengine namna wamekasirika sana, watafanya vile hata kupitia Enternete. Viongozi wa ulimwengu na Shetani, kiongozi wao, watatuchukia sana wakati wataona kama dini yetu tu njo inabakia. Wataona kama hawajatimiza kusudi lao la kutosha dini zote ku dunia. Kwa hiyo, watatukazia uangalifu. Wakati huo, mataifa itageuka kuwa Gogu wa Magogu. * Itajiunga pamoja ili kushambulia vikali watu wa Yehova. (Eze. 38:2, 14-16) Pengine tunaweza kuanza kuogopa juu ya mambo yenye itatokea wakati wa taabu kubwa, zaidi sana kwa sababu hatujue mambo yote. Lakini, tuko hakika na jambo hili: Hatupaswe kuogopa taabu kubwa. Yehova atatupatia maagizo yenye itatusaidia tuokoke. (Zb. 34:19) ‘Tutasimama wima na kuinua vichwa vyetu,’ kwa sababu tutatambua kama ‘ukombozi wetu unakaribia.’ *

12. Namna gani “mutumwa muaminifu na mwenye busara” ameanza kututayarisha juu ya mambo yenye itatokea wakati wenye kuja?

12 “Mutumwa muaminifu na mwenye busara” ameanza kututayarisha ili tuendelee kuwa waaminifu wakati wa taabu kubwa. (Mt. 24:45) Amefanya vile katika njia mingi, lakini tuone njia moja: mikusanyiko yetu ya eneo ya mwaka wa 2016-2018 yenye ilifika kwa wakati wenye kufaa. Mikusanyiko hiyo imetutia moyo tukomalishe sifa zenye tuko nazo lazima kadiri tunakaribia siku ya Yehova. Tuzungumuzie basi kwa kifupi sifa hizo.

ENDELEA KUTIA NGUVU USHIKAMANIFU WAKO, UVUMILIVU WAKO, NA UHODARI WAKO

Ujitayarishe leo ili kuokoka “taabu kubwa” (Picha hii inapatana na fungu la 13-16) *

13. Namna gani tunaweza kutia nguvu ushikamanifu wetu kwa Yehova, na juu ya nini tunapaswa kufanya vile leo?

13 Ushikamanifu: Mukusanyiko wa eneo wa 2016 ulikuwa na kichwa “Endelea Kuwa Mushikamanifu kwa Yehova!” Mukusanyiko huo ulitufundisha kama, ili tukuwe washikamanifu kwa Yehova, tunapaswa kuwa na urafiki wenye nguvu pamoja naye. Tulikumbushwa kama ili tumukaribie Yehova, tunapaswa kusali kwa moyo wote na kujifunza Neno lake kwa bidii. Kufanya vile kunatusaidia tupate nguvu ya kushinda hata majaribu ya nguvu sana. Kadiri ulimwengu wa Shetani uko unakaribia mwisho wake, tunaweza kutazamia kama ushikamanifu wetu kwa Mungu na kwa Ufalme wake utajaribiwa hata zaidi. Inawezekana watu wataendelea kutuchekelea. (2 Pe. 3:3, 4) Wanaweza kufanya vile zaidi sana juu hatuunge mukono sehemu yoyote ya ulimwengu huu wa Shetani. Tunapaswa kutia nguvu ushikamanifu wetu leo ili tuendelee kuwa washikamanifu wakati wa taabu kubwa.

14. (a) Kutakuwa badiliko gani kuhusu ndugu wenye wanaongoza kazi ku dunia? (b) Juu ya nini itakuwa lazima tukuwe washikamanifu wakati huo?

14 Wakati wa taabu kubwa, kutakuwa badiliko kuhusu ndugu wenye wanaongoza kazi ku dunia. Wakati fulani, watiwa-mafuta wote wenye wangali ku dunia watapelekwa mbinguni ili wakuwe pamoja na Yesu na malaika wake ili kupigana vita ya Armagedoni. (Mt. 24:31; Ufu. 2:26, 27) Maana yake, ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza hawatakuwa tena pamoja na sisi hapa ku dunia. Lakini, kundi kubwa la watu wataendelea kupangwa muzuri. Ndugu fulani wenye kustahili kati ya kondoo wengine wataongoza kazi. Tutakuwa na lazima ya kuonyesha ushikamanifu wetu kwa kuunga mukono ndugu hao na kufuata muongozo wao wenye kutoka kwa Mungu. Kama tunafanya vile, tutaokolewa!

15. Namna gani tunaweza kutia nguvu uvumilivu wetu, na juu ya nini ni jambo la maana tufanye vile leo?

15 Uvumilivu: Mukusanyiko wa eneo wa mwaka wa 2017 ulikuwa na kichwa “Usiache Hata Kidogo!” Mukusanyiko huo ulitusaidia tutie nguvu uwezo wetu wa kuvumilia majaribu. Tulijifunza kama uvumilivu wetu hautegemee kuwa katika hali za muzuri. Tunaweza kutia nguvu uvumilivu wetu kwa kumutegemea Yehova. (Ro. 12:12) Tusisahau hata kidogo ahadi hii ya Yesu: “Ule mwenye anavumilia mupaka mwisho ataokolewa.” (Mt. 24:13, maelezo ya chini) Ahadi hiyo inamaanisha kama tunapaswa kuendelea kuwa waaminifu hata tupate magumu gani. Wakati tunavumilia kila jaribu leo, tunaweza kuwa na nguvu zaidi mbele taabu kubwa ianze.

16. Ni nini inatufanya tukuwe hodari, na namna gani tunaweza kutia nguvu uhodari wetu leo?

16 Uhodari: Mukusanyiko wa eneo wa mwaka wa 2018 ulikuwa na kichwa “Ukuwe Hodari!” Mukusanyiko huo ulitukumbusha kama haiko uwezo wetu mbalimbali njo unatufanya tukuwe hodari. Kama vile tulisema juu ya uvumilivu, tunapaswa kumutegemea Yehova ili tukuwe na uhodari wa kweli. Ni nini inaweza kutusaidia tumutegemee Yehova zaidi? Kusoma Neno lake kila siku na kufikiri sana juu ya namna Yehova aliokoa watu wake zamani. (Zb. 68:20; 2 Pe. 2:9) Wakati viongozi wa ulimwengu watatushambulia wakati wa taabu kubwa, itaomba tukuwe hodari na kumutegemea Yehova zaidi kuliko zamani. (Zb. 112:7, 8; Ebr. 13:6) Kama tunamutegemea Yehova leo, tutakuwa na uhodari wenye tuko nao lazima ili kupambana na shambulizi la Gogu. *

UNGOJEE UKOMBOZI WAKO KWA HAMU

Hivi karibuni, Yesu na majeshi yake ya mbinguni watapanda farasi ili kupigana vita ya Armagedoni na kuharibu maadui wa Mungu! (Picha hii inapatana na fungu la 17)

17. Juu ya nini hatupaswe kuogopa vita ya Armagedoni? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

17 Kama vile tulisema mu habari yenye ilitangulia, wengi kati yetu wameishi maisha yao yote katika siku za mwisho. Lakini tuko pia na tumaini la kuokoka taabu kubwa. Vita ya Armagedoni njo utakuwa mwisho kabisa wa mupangilio huu wa mambo. Lakini, hatuna sababu ya kuogopa. Juu ya nini? Juu vita hiyo ni vita ya Mungu. (Mez. 1:33; Eze. 38:18-20; Zek. 14:3) Wakati Yehova atatoa amri, Yesu Kristo ataongoza majeshi ya Mungu ili kupigana. Atakuwa pamoja na watiwa-mafuta wenye walifufuliwa na makumi ya maelfu ya malaika. Wote pamoja, watapigana na Shetani, pepo wake wachafu, na majeshi yao ya ku dunia.​—Da. 12:1; Ufu. 6:2; 17:14.

18. (a) Yehova ametuhakikishia nini? (b) Namna gani andiko la Ufunuo 7:9, 13-17 linakusaidia ukuwe hakika kama utaokoka?

18 Yehova ametuhakikishia hivi: “Hakuna silaha yenye itafanywa juu yako yenye itafanikiwa.” (Isa. 54:17) “Kundi kubwa la watu” waaminifu wenye kumuabudu Yehova ‘watatoka katika ile taabu kubwa’ wakiwa wazima! Kisha, wataendelea kumutolea utumishi mutakatifu. (Soma Ufunuo 7:9, 13-17.) Biblia inatusaidia tukuwe hakika kama tutaokoka wakati wenye kuja! Tunajua kama “Yehova analinda waaminifu.” (Zb. 31:23) Watu wote wenye wanamupenda Yehova na kumusifu watafurahi wakati atatakasa jina lake takatifu.​—Eze. 38:23.

19. Ni tumaini gani la muzuri sana lenye kuwa mbele yetu?

19 Wazia namna andiko la 2 Timoteo 3:2-5 linaweza kusemwa kama lingezungumuzia watu wenye wataishi mu ulimwengu mupya wenye hawatachochewa na Shetani. (Ona kisanduku “ Tabia za Watu Wakati Huo.”) Ndugu George Gangas, * mwenye alitumikia katika Baraza Lenye Kuongoza, alifasiria jambo hilo kwa kusema hivi: “Ulimwengu utakuwa muzuri sana wakati kila mutu atakuwa ndugu ao dada! Hivi karibuni, utakuwa na pendeleo la kuishi mu ulimwengu mupya. Utaishi siku mingi kama vile Yehova anaishi. Tutaishi milele.” Hilo ni tumaini la muzuri sana!

WIMBO 122 Iweni Imara, Thabiti!

^ fu. 5 Tunajua kama “taabu kubwa” itafikia wanadamu wote hivi karibuni. Wakati huo, watumishi wa Yehova watakuwa katika hali gani? Yehova atatuomba tufanye nini wakati huo? Tunapaswa kukomalisha zaidi sifa gani leo ili tuendelee kuwa waaminifu wakati wa taabu kubwa? Tutapata majibu katika habari hii.

^ fu. 3 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Dini zenye kujiita kuwa za Kikristo ni dini zenye zinasema kama zinamufuata Kristo lakini hazimuabudu Yehova kulingana na kanuni zake.

^ fu. 11 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Maneno Gogu wa Magogu (na kifupi chake, Gogu) inamaanisha muungano wa mataifa yenye itashambulia waabudu wa Yehova wakati wa taabu kubwa.

^ fu. 11 Ili kupata habari zaidi juu ya matukio yote yenye itatokea mbele ya vita ya Armagedoni, ona sura ya 21 ya kitabu Ufalme wa Mungu Unatawala! Ili kupata habari zaidi juu ya shambulizi la Gogu wa Magogu na namna Yehova atapigania watu wake wakati wa Armagedoni, ona sura ya 17 na ya 18 ya kitabu Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!

^ fu. 16 Mukusanyiko wa eneo wa mwaka wa 2019 wenye kichwa “Upendo Haushindwe Hata Kidogo!” unatuhakikishia kama tunaweza kuendelea kujisikia salama kwa sababu Yehova anatulinda kwa upendo.​—1 Ko. 13:8.

^ fu. 19 Ona habari ‘Matendo Yake Yamfuata’ katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 12, 1994.

^ fu. 65 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati wa taabu kubwa, kikundi kidogo cha Mashahidi wanaonyesha uhodari kwa kukutana mu pori ili kufanya mukutano wa kutaniko.

^ fu. 67 MAFASIRIO YA PICHA: Kundi kubwa la watu waaminifu wenye kumuabudu Yehova watatoka katika taabu kubwa na wako wazima na wenye furaha!