Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Watu wako na lazima ya kusikia onyo kadiri “upepo mukali” wa Mungu unakaribia!

Hukumu za Mungu​—Sikuzote Anaonya Watu Wakati wa Kutosha?

Hukumu za Mungu​—Sikuzote Anaonya Watu Wakati wa Kutosha?

MUTU mwenye kutabiri hali ya hewa anachunguza picha ya rada (picha yenye kuonyesha hali ya hewa). Anaona upepo hatari wenye unakaribia kuja juu ya eneo fulani lenye watu wengi. Juu anahangaikia usalama wa watu, anaonya watu bila kuchoka mbele ikuwe kuchelewa sana.

Vilevile, leo Yehova iko anaonya wakaaji wa dunia juu ya “upepo mukali” wenye kuwa hatari kuliko jambo lolote lenye tunaweza kusikia katika habari kuhusu hali ya hewa. Iko anafanya vile namna gani? Na juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama anapatia watu wakati wa kutosha ili wafanye jambo fulani? Ili kupata majibu, tuzungumuzie kwanza maonyo fulani yenye Yehova alitoa wakati wa zamani.

MUNGU ALIONYA WATU MBELE YA WAKATI

Wakati wa zamani, Yehova alionya watu juu ya “upepo mukali,” ao hukumu zake, zenye angeleta juu ya wale wenye walikataa kutii amri zake. (Mez. 10:25; Yer. 30:23) Kila mara mbele alete hukumu, alionya mbele ya wakati watu wenye walikosa utii na aliwaagiza wafanye mabadiliko yenye ilipatana na mapenzi yake. (2 Fa. 17:12-15; Ne. 9:29, 30) Ili kusaidia watu wafanye mabadiliko yenye iliombwa, mara mingi alitumia watumishi wake washikamanifu ku dunia ili watangaze hukumu zake na kusaidia watu waone kama ilikuwa lazima watende haraka.​—Amo. 3:7.

Noa iko kati ya watu hao waaminifu wenye Mungu alitumia ili kutangaza hukumu zake. Kwa miaka mingi, alionya bila woga watu wa wakati wake wenye walikuwa na mwenendo muchafu na wenye jeuri kuhusu Garika yenye ingekuja juu ya dunia yote. (Mwa. 6:9-13, 17) Aliwaambia mambo yenye walipaswa kufanya ili waokoke. Alihubiri sana na kwa hiyo, aliitwa baadaye “muhubiri wa haki.”​—2 Pe. 2:5.

Hata kama Noa alijikaza sana, watu wenye waliishi mbele ya Garika hawakusikiliza ujumbe wake wenye ulitoka kwa Mungu. Walionyesha kama hawakukuwa na imani kabisa. Kwa hiyo, walikufa wakati Garika ‘ilikuja na kuwaharibu wote.’ (Mt. 24:39; Ebr. 11:7) Wakati mwisho wao ulikaribia, hawangesema hata kidogo kama Mungu hakuwaonya.

Wakati mwingine, Yehova alionya watu muda mufupi mbele hukumu yake yenye kuwa kama “upepo mukali” ianze. Hata hivyo, alihakikisha kama wale wenye wangepatwa na hukumu hiyo walipewa wakati wa kutosha ili kufanya mabadiliko. Kwa mufano, wakati alileta Mapigo Kumi juu ya Misri ya zamani, alionya watu mbele ya wakati. Yehova alituma Musa na Haruni ili waonye Farao na watumishi wake juu ya pigo la saba, ni kusema, mvua ya majiwe yenye ilileta uharibifu mukubwa. Kwa sababu mvua ya majiwe ingeanza siku yenye ilifuata, je, Mungu aliwapatia wakati wa kutosha ili wapate nafasi ya kujificha na waokoke pigo hilo? Biblia inasema hivi: “Kila mutu kati ya watumishi wa Farao mwenye aliogopa neno la Yehova akaleta haraka watumishi wake mwenyewe na mifugo yake katika nyumba, lakini kila mutu mwenye hakuweka katika moyo wake neno la Yehova aliacha watumishi wake na mifugo yake katika eneo la mashamba.” (Kut. 9:18-21) Ni wazi kama Yehova alionya watu wakati wa kutosha, kwa hiyo, wale wenye walitenda haraka hawakupatwa na matokeo ya mubaya sana ya pigo hilo.

Vilevile, Farao na watumishi wake walionywa mbele pigo la kumi lianze. Lakini, walikuwa wapumbavu juu walikataa onyo hilo. (Kut. 4:22, 23) Kwa hiyo, wana wao wazaliwa wa kwanza walikufa. Hilo lilikuwa jambo la kuhuzunisha sana! (Kut. 11:4-10; 12:29) Walikuwa na nafasi ya kutii onyo hilo mbele ikuwe kuchelewa? Ndiyo! Bila kukawia, Musa alionya Waisraeli juu ya pigo la kumi lenye lilikuwa karibu kutokea na aliwapatia maagizo juu ya namna ya kuokoa familia zao. (Kut. 12:21-28) Ni watu ngapi njo walitii onyo lenye Musa aliwatolea? Inakadiriwa kama, watu milioni tatu, kutia ndani Waisraeli na “kikundi kikubwa cha watu wenye kuchangamana” wenye hawakukuwa Waisraeli na Wamisri, waliokoka hukumu ya Mungu na walitoka Misri.​—Kut. 12:38; maelezo ya chini.

Kama vile ile mifano inaonyesha, sikuzote Yehova alipatia watu wakati wa kutosha ili watii maonyo yake. (Kum. 32:4) Juu ya nini Mungu alifanya vile? Mutume Petro alisema kama Yehova “hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.” (2 Pe. 3:9) Kwa kweli, Mungu alihangaikia watu. Alipenda watubu na kufanya mabadiliko yenye iliombwa mbele hukumu yake ifike.​—Isa. 48:17, 18; Ro. 2:4.

TUTII ONYO LA MUNGU LEO

Leo pia, watu wote wanapaswa kutii onyo la maana lenye linatolewa mu dunia yote. Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alionya watu kama mupangilio huu wa mambo utafikia kuharibiwa wakati wa “taabu kubwa.” (Mt. 24:21) Juu ya hukumu ya wakati wenye kuja, alitoa unabii mbalimbali wenye kuonyesha mambo yenye wanafunzi wake wangeona na mambo yenye ingewapata kadiri wakati huo ungekaribia. Kwa hiyo, Yesu alitaja matukio makubwa yenye tuko tunaona inatokea mu dunia yote leo.​—Mt. 24:3-12; Lu. 21:10-13.

Kupatana na unabii huo, leo Yehova anaomba kila mutu akubali utawala wake wenye upendo. Anapenda watu wenye kutii wakuwe na maisha ya muzuri leo na wapate baraka katika ulimwengu wake mupya wenye haki wakati wenye kuja. (2 Pe. 3:13) Ili kusaidia watu waamini ahadi zake, Yehova anatolea watu ujumbe wenye kuokoa uzima. Ujumbe huo ni “habari njema ya Ufalme,” yenye Yesu alitabiri kama “itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote.” (Mt. 24:14) Mungu amepanga waabudu wake wa kweli watoe “ushahidi,” huo ao ujumbe wake, na sasa wako wanafanya vile mu inchi 240 hivi. Yehova anapenda watu wengi kadiri inawezekana watii onyo hilo na waokoke hukumu yake ya haki yenye iko kama “upepo mukali.”​—Sef. 1:14, 15; 2:2, 3.

Kwa hiyo, ulizo la maana haiko kujiuliza ikiwa Yehova anapatiaka watu wakati wa kutosha ili watii maonyo yake. Ushuhuda unaonyesha kama anafanyaka vile sikuzote. Lakini, ulizo la maana ni hili: Watu watatii maonyo ya Mungu wakati haijakuwa kuchelewa? Sisi wajumbe wa Mungu tuendelee basi kusaidia watu wengi kadiri inawezekana ili waokoke mwisho wa mupangilio huu wa mambo.