Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 42

Yehova Atakutumia Namna Gani?

Yehova Atakutumia Namna Gani?

“Mungu . . . anawachochea ninyi, na kuwapatia hamu na pia nguvu za kutenda.”​—FLP. 2:13.

WIMBO 104 Roho Takatifu​—Zawadi Kutoka kwa Mungu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Yehova anaweza kufanya nini ili kutimiza kusudi lake?

YEHOVA anaweza kuwa kitu chochote chenye kinahitajiwa ili kutimiza kusudi lake. Kwa mufano, Yehova amekuwa Mwalimu, Mufariji, na Mweneza-Injili, na ile ni mifano kidogo tu. (Isa. 48:17; 2 Ko. 7:6; Gal. 3:8) Lakini, mara mingi anatumia wanadamu ili kutimiza makusudi yake. (Mt. 24:14; 28:19, 20; 2 Ko. 1:3, 4) Pia, Yehova anaweza kupatia kila mumoja wetu hekima na nguvu yenye iko nayo lazima kusudi akuwe kitu chochote chenye iko nacho lazima ili kutimiza mapenzi yake. Kama vile watu fulani wenye elimu wanaonyesha, jina la Mungu liko na ile maana yote.

2. (a) Juu ya nini wakati fulani tunaweza kujiuliza ikiwa kwa kweli Yehova iko anatutumia? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

2 Sisi wote tunapenda Yehova atutumie ili kutimiza mapenzi yake, lakini watu fulani wanaweza kujiuliza ikiwa kwa kweli Yehova iko anawatumia. Juu ya nini? Juu wanajisikia kuwa hawawezi kufanya mambo mingi kwa sababu ya miaka yao, hali zao, ao uwezo wao. Na wengine wanaweza kuwaza kama mambo yenye wanafanya inatosha, na kama hawana lazima ya kufanya mambo mingi zaidi. Katika habari hii, tutazungumuzia namna Yehova anaweza kupatia kila mumoja wetu mambo yenye iko nayo lazima ili kutimiza kusudi lake. Kisha, tutazungumuzia habari za Biblia zenye kuonyesha namna Yehova alipatia watumishi wake, wanaume na wanamuke, hamu na nguvu za kutenda. Ku mwisho, tutazungumuzia namna tunaweza kumuacha Yehova atutumie.

NAMNA YEHOVA ANATUPATIA MAMBO YENYE TUKO NAYO LAZIMA

3. Andiko la Wafilipi 2:13 linaonyesha kama Yehova anaweza kutupatia hamu ya kutenda. Namna gani anafanya vile?

3 Soma Wafilipi 2:13. * Yehova anaweza kutupatia hamu ya kutenda. Anaweza kufanya vile namna gani? Pengine tunatambua kama kuko uhitaji fulani mu kutaniko letu. Ao wazee wanasoma barua fulani kutoka ku biro ya tawi yenye kuonyesha kama kuko lazima ya musaada mahali pengine. Hilo linaweza kufanya tujiulize hivi: ‘Ninaweza kufanya nini ili kusaidia?’ Ao pengine tumepewa mugao wa nguvu, na tunajiuliza ikiwa tunaweza kuufanya muzuri. Ao kisha kusoma andiko fulani mu Biblia, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Namna gani ninaweza kutumia andiko hili la Biblia ili kusaidia wengine?’ Yehova hatatulazimisha tufanye jambo fulani. Lakini wakati anaona kama tuko tunafikiria mambo yenye tunaweza kufanya, anaweza kutupatia hamu ya kufanya mambo yenye tulifikiria.

4. Namna gani Yehova anaweza kutupatia nguvu za kutenda?

4 Yehova anaweza pia kutupatia nguvu za kutenda. (Isa. 40:29) Namna gani? Anaweza kutupatia roho yake takatifu ili ifanye uwezo wetu wa kizalikio ukuwe muzuri zaidi. (Kut. 35:30-35) Kupitia tengenezo lake, Yehova anaweza kutufundisha namna ya kufanya kazi fulani. Kama siku moja unaona kama hauko hakika juu ya namna ya kufanya mugao fulani, omba musaada. Tena, usisite kumuomba Baba yetu mukarimu wa mbinguni “nguvu zenye kupita zile za kawaida.” (2 Ko. 4:7; Lu. 11:13) Biblia iko na mifano mingi yenye kuonyesha namna Yehova alipatia wanaume na wanamuke hamu na nguvu za kutenda. Wakati tunazungumuzia mifano fulani, jaribu kufikiria namna Yehova anaweza kukutumia ili kufanya mambo yenye kufanana na ile yenye walifanya.

NAMNA YEHOVA ALITUMIA WANAUME FULANI

5. Namna Yehova alitumia Musa na wakati wenye alimutumia ili kukomboa watu wake vinatufundisha nini?

5 Yehova alimufanya Musa kuwa mukombozi wa Waisraeli. Lakini, Yehova alimutumia wakati gani? Je, ilikuwa wakati Musa alijiona kama anastahili kisha ‘kufundishwa katika hekima yote ya Wamisri’? (Mdo. 7:22-25) Hapana, Yehova alimutumia Musa kisha kumusaidia akuwe mwanaume munyenyekevu, mwenye tabia ya upole. (Mdo. 7:30, 34-36) Yehova alimupatia Musa uhodari wa kuzungumuza na mutawala mwenye nguvu zaidi katika Misri. (Kut. 9:13-19) Namna Yehova alitumia Musa na wakati wenye alimutumia vinatufundisha nini? Yehova anatumia wale wenye wanaonyesha sifa kama zake na wenye wanamutegemea ili kupata nguvu.​—Flp. 4:13.

6. Namna Yehova alimutumia Barzilai ili kumusaidia Mufalme Daudi, inatufundisha nini?

6 Miaka mingi kisha pale, Yehova alimutumia Barzilai ili kumusaidia Mufalme Daudi. Daudi na wanaume wake walikuwa ‘wamesikia njaa na wamechoka na walikuwa na kiu’ wakati walikuwa wanamukimbia Absalomu, mwana wa Daudi. Muzee Barzilai pamoja na wanaume wengine, alitia uzima wake katika hatari ili kusaidia Daudi na wanaume wenye walikuwa pamoja naye. Barzilai hakusema kama Yehova hangemutumia tena, kwa sababu alikuwa mwenye kuzeeka. Lakini, alitumia kwa ukarimu vitu vyenye alikuwa navyo ili kusaidia watumishi wa Mungu wenye walikuwa na lazima ya musaada. (2 Sa. 17:27-29) Habari hiyo inatufundisha nini? Hata kama tuko na miaka ngapi, Yehova anaweza kututumia ili kutimiza mahitaji ya ndugu na dada zetu wenye wanakosa mambo ya lazima, ikuwe mu eneo letu ao mu inchi ingine. (Mez. 3:27, 28; 19:17) Hata kama hatuwezi kuwasaidia moja kwa moja, tunaweza kutoa michango ya kutegemeza kazi yetu ya mu dunia yote, ili kukuwe feza za kusaidia ndugu na dada zetu wakati kuko uhitaji na mahali kwenye kuko uhitaji.​—2 Ko. 8:14, 15; 9:11.

7. Namna gani Yehova alimutumia Simeoni, na juu ya nini jambo hilo linatutia moyo?

7 Yehova alimuahidi Simeoni, mwanaume muaminifu mwenye kuzeeka mwenye alikuwa anaishi Yerusalemu, kama hangekufa mbele amuone Masiya. Ahadi hiyo ilipaswa kumutia Simeoni moyo sana, juu alikuwa amengojea Masiya kwa miaka mingi. Yehova alimubariki Simeoni kwa sababu ya imani na uvumilivu wake. Siku moja, Simeoni ‘aliongozwa na roho’ ili kuja mu hekalu. Mule, alimuona mutoto Yesu, na Yehova alimutumia ili kutoa unabii juu ya mutoto huyo mwenye angekuwa Masiya. (Lu. 2:25-35) Hata kama inawezekana Simeoni alikufa mbele Yesu aanze utumishi wake ku dunia, alikuwa mwenye shukrani juu ya pendeleo lenye alipata, na atapata tena mambo ya muzuri wakati wenye kuja! Mu dunia mupya, mwanaume huyo muaminifu ataona namna utawala wa Yesu utaletea baraka familia zote za dunia. (Mwa. 22:18) Sisi pia tunaweza kuwa wenye shukrani juu ya pendeleo lolote lenye Yehova anatupatia katika utumishi wake.

8. Namna gani Yehova anaweza kututumia kama vile alimutumia Barnaba?

8 Wakati wa mitume, mwanaume mumoja mukarimu mwenye aliitwa Yosefu aliacha Yehova amutumie. (Mdo. 4:36, 37) Mitume walimuita Barnaba, maana yake “Mwana wa Faraja,” inawezekana walimupatia jina hilo juu alikuwa anajua kabisa kufariji wengine. Kwa mufano, kisha Sauli kuwa muamini, ndugu wengi waliogopa kumukaribia kwa sababu alikuwa ametesa makutaniko. Lakini, Barnaba alimufariji na kumusaidia Sauli, na Sauli alipaswa kuwa mwenye shukrani sana juu ya musaada huo. (Mdo. 9:21, 26-28) Kisha, wazee katika Yerusalemu waliona kama ilikuwa lazima watie moyo ndugu na dada wenye waliishi mbali sana katika Antiokia ya Siria. Walituma nani kule? Barnaba! Kwa kweli, walichagua muzuri. Biblia inasema kama Barnaba “akaanza kuwatia wote moyo waendelee kuwa waaminifu kwa Bwana kwa moyo wote.” (Mdo. 11:22-24) Leo vilevile, Yehova anaweza kutusaidia tukuwe ‘wana wa faraja’ kwa Wakristo wenzetu. Kwa mufano, anaweza kututumia ili kufariji wale wenye wamefiwa na wapendwa wao. Ao anaweza kutuchochea ili tutembelee ao kuita ku telefone ndugu ao dada fulani mwenye kuwa mugonjwa ao mwenye kushuka moyo na kumuambia maneno fulani ya kumutia moyo. Utamuacha Yehova akutumie kama vile alimutumia Barnaba?​—1 Te. 5:14.

9. Namna Yehova alimusaidia ndugu mumoja mwenye kuitwa Vasily akuwe muchungaji muzuri, inaweza kutufundisha nini?

9 Yehova alisaidia ndugu mumoja mwenye kuitwa Vasily akuwe muchungaji muzuri. Vasily aliwekwa kuwa muzee wa kutaniko wakati alikuwa na miaka 26. Aliogopa kwa sababu aliwaza kama hakukuwa na uwezo wa kusaidia kwa njia ya kiroho ndugu na dada wa kutaniko, zaidi sana wale wenye walikuwa na magumu. Lakini, alipata mazoezi ya muzuri kupitia wazee wa kutaniko wenye uzoefu na wakati alisoma Masomo ya Huduma ya Ufalme. Vasily alijikaza sana ili kuwa muchungaji muzuri. Kwa mufano, alifanya liste ya miradi ya kidogo-kidogo yenye alipaswa kufikia. Kadiri alikuwa anafikia kila muradi, woga wenye alikuwa nao ulipunguka polepole. Sasa anasema hivi: “Mambo yenye ilikuwa inaniogopesha zamani inaniletea furaha leo. Wakati Yehova ananisaidia nipate andiko lenye kufaa la kumufariji ndugu ao dada wa kutaniko, hilo linaniletea furaha sana.” Ndugu, kama munaacha Yehova awatumie kama vile Vasily alifanya, anaweza kuwapatia uwezo wa kutimiza madaraka makubwa zaidi mu kutaniko.

NAMNA YEHOVA ALITUMIA WANAMUKE FULANI

10. Abigaili alifanya nini, na mufano wake unakufundisha nini?

10 Daudi na wanaume wenye walikuwa washikamanifu kwake walikuwa wanamukimbia Mufalme Sauli, na walikuwa na lazima ya musaada. Wanaume wa Daudi walimuomba Nabali, tajiri mumoja Muisraeli, awapatie chakula kidogo, chenye angeweza kupata. Hawakusita kumuomba Nabali musaada juu walikuwa wamelinda mifugo yake katika jangwa. Lakini, Nabali alikataa kuwapatia kitu chochote kwa sababu alikuwa muchoyo. Daudi alikasirika sana na alitaka kuua Nabali na wanaume wote wa nyumba yake. (1 Sa. 25:3-13, 22) Lakini, Abigaili, bibi ya Nabali, mwenye alikuwa na sura ya muzuri, alikuwa na utambuzi sana. Alionyesha uhodari mukubwa, alianguka kwenye miguu ya Daudi na akamuomba asijiletee hatia ya damu kwa kulipiza kisasi. Kwa busara, alimushauria Daudi aache mambo mu mikono ya Yehova. Maneno ya unyenyekevu ya Abigaili na matendo yake ya busara ilimugusa Daudi moyo. Alitambua kama Yehova njo alimutuma Abigaili. (1 Sa. 25:23-28, 32-34) Abigaili alikuwa amekomalisha sifa zenye zilifanya Yehova amutumie. Vilevile, dada Wakristo wenye wanakomalisha sifa ya busara na utambuzi, Yehova anaweza kuwatumia ili kutia nguvu familia zao na ndugu na dada wengine mu kutaniko.​—Mez. 24:3; Tit. 2:3-5.

11. Watoto wanamuke wa Shalumu walifanya nini, na leo ni nani wanaiga mufano wao?

11 Miaka mingi kisha pale, watoto wanamuke wa Shalumu walikuwa kati ya watu wenye Yehova alitumia ili kutengeneza kuta za Yerusalemu. (Ne. 2:20; 3:12) Hata kama baba yao alikuwa mukubwa wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, watoto wanamuke wa Shalumu walikuwa tayari kufanya kazi ya nguvu na ya hatari. (Ne. 4:15-18) Walikuwa tofauti kabisa na wanaume wa maana kati ya Watekoa, wenye “hawakutaka kujishusha ili kushiriki” katika kazi hiyo! (Ne. 3:5) Wazia furaha yenye watoto wanamuke wa Shalumu walisikia wakati kazi ilimalizika kisha siku 52 tu! (Ne. 6:15) Leo, dada wenye roho ya kujitoa wanafurahi sana kusaidia katika aina hii ya pekee ya utumishi mutakatifu: kujenga na kutunza majengo yenye tunatumia juu ya ibada ya Yehova. Tuko na lazima ya dada hao wenye uwezo, wenye bidii, na washikamanifu ili kutimiza kazi hiyo.

12. Namna gani Yehova anaweza kututumia kama vile alimutumia Tabita?

12 Yehova alimuchochea Tabita azoee kutenda “mema na kutoa zawadi za rehema,” zaidi sana ili kusaidia wajane. (Mdo. 9:36) Kwa sababu alikuwa mukarimu sana na mwema, wengi walilia wakati alikufa. Lakini walifurahi sana wakati mutume Petro alimufufua. (Mdo. 9:39-41) Mufano wa Tabita unatufundisha nini? Ikuwe tuko vijana ao watu wazima, wanaume ao wanamuke, sisi wote tunaweza kufanya mambo fulani ili kusaidia ndugu na dada zetu.​—Ebr. 13:16.

13. Namna gani Yehova alitumia dada mumoja mwenye haya mwenye kuitwa Ruth, na Ruth alisema nini?

13 Dada mumoja mwenye haya mwenye kuitwa Ruth alipenda kuwa misionere. Wakati alikuwa kijana mudogo, alikuwa anapita haraka-haraka nyumba kwa nyumba na kutolea watu trakte. Alisema hivi: “Nilikuwa napenda kabisa kazi ya kuhubiri.” Lakini, ilikuwa nguvu sana kwake kuzungumuza na watu ku mulango na kuongea nao juu ya Ufalme wa Mungu. Hata kama Ruth alikuwa mwenye haya, alifikia kuwa painia wakati alikuwa na miaka 18. Mu mwaka wa 1946, alisoma Masomo ya Biblia ya Gileadi na kisha akatumikia mu Visiwa vya Hawaii na mu inchi ya Japani. Yehova alimutumia sana ili kueneza habari njema mu maeneo hiyo. Kisha kufanya kazi ya kuhubiri kwa miaka karibu 80, Ruth alisema hivi: “Yehova amenitia nguvu sikuzote. Amenisaidia kushinda haya yenye nilikuwa nayo. Ninaamini kabisa kama Yehova anaweza kutumia kila mutu mwenye anamutegemea.”

UMUACHE YEHOVA AKUTUMIE

14. Kulingana na Wakolosai 1:29, tunapaswa kufanya nini kama tunapenda Yehova atutumie?

14 Tangu zamani, Yehova amefanya watumishi wake watimize mambo mbalimbali. Atakufanya ukuwe nani? Inategemea sana namna utajikaza. (Soma Wakolosai 1:29.) Kama unamuacha Yehova akutumie, anaweza kukufanya ukuwe mweneza-injili mwenye bidii, mwalimu muzuri, mufariji muzuri, mufanyakazi mwenye ufundi, rafiki mwenye kutegemeza wengine, ao kitu kingine chochote chenye iko nacho lazima ili kutimiza mapenzi yake.

15. Kulingana na 1 Timoteo 4:12, 15, leo ndugu vijana wanapaswa kumuomba Yehova awasaidie kufanya nini?

15 Halafu ninyi ndugu vijana wenye munakaribia kuwa watu wazima? Kuko lazima kubwa ya wanaume wenye nguvu ili wasaidie kutaniko wakiwa watumishi wa huduma. Mu makutaniko mingi, wazee wako wengi kupita watumishi wa huduma. Ninyi ndugu vijana, je wamoja kati yenu wanaweza kukomalisha hamu ya kufanya mambo mingi mu kutaniko? Wakati fulani, ndugu wengine wanasema hivi: “Sina lazima ya madaraka, ninafurahia kubakia tu muhubiri wa kawaida.” Kama uko na ile mawazo, umuombe Yehova akusaidie ukuwe na hamu ya kutimiza sifa zenye zinaombwa ili ukuwe mutumishi wa huduma. Umuombe pia akupatie nguvu zenye uko nazo lazima ili ufanye mambo yote yenye unaweza katika utumishi wake. (Muh. 12:1) Tuko na lazima ya musaada wako!​—Soma 1 Timoteo 4:12, 15.

16. Tunapaswa kumuomba Yehova nini, na juu ya nini?

16 Yehova anaweza kukufanya ukuwe kitu chochote chenye iko nacho lazima ili kutimiza mapenzi yake. Kwa hiyo, umuombe akupatie hamu ya kufanya kazi yake, na kisha umuombe akupatie nguvu zenye uko nazo lazima. Ikuwe uko kijana ao mutu muzima, tumia wakati wako, nguvu yako, na mambo ingine yenye uko nayo kama vile ufundi wako na mali yako ili kumutukuza Yehova leo. (Muh. 9:10) Wakati unapewa nafasi ya muzuri ya kufanya mambo mingi katika kazi ya Yehova, usikatae mbiombio kwa sababu unawaza kama hautaweza. Ni pendeleo kabisa kufanya mambo yote yenye tunaweza ili kumuletea Baba yetu mwenye upendo utukufu wenye anastahili!

WIMBO 127 Napaswa Kuwa Mtu wa Namna Gani?

^ fu. 5 Unajisikia kuwa haufanye mambo mingi katika kazi ya Yehova? Unajiuliza ikiwa Yehova angali anakutumia? Ao unaona kama haiko lazima ufanye mambo mingi katika utumishi wa Yehova hata kama Yehova anapenda vile? Habari hii itazungumuzia njia mbalimbali zenye Yehova anatumia ili kukupatia hamu na nguvu ya kuwa kitu chochote chenye iko nacho lazima ili kutimiza kusudi lake.

^ fu. 3 Hata kama ni Wakristo wa wakati wa mitume njo Paulo aliandikia barua yake, kwa kweli, maneno yake inahusu watumishi wote wa Yehova.