Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 41

Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza

Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza

“Munaonyeshwa kuwa ninyi ni barua ya kristo yenye tuliandika tukiwa watumishi.”​—2 KO. 3:3.

WIMBO 78 “Kufundisha Neno la Mungu”

KIFUPI CHA HABARI *

Ndugu na dada wa kutaniko lote wanafurahiaka sana kuona mwanafunzi wa Biblia anafikia kubatizwa. (Ona fungu la 1)

1. Andiko la 2 Wakorinto 3:1-3 linasema nini yenye inatusaidia kuelewa kama ni pendeleo kujifunza na watu na kuwasaidia wafikie kubatizwa? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

UNAJISIKIAKA namna gani wakati unaona mutu wa mu eneo lenu mwenye alikuwa anajifunza Biblia anafikia kubatizwa? Bila shaka ile inakufurahishaka sana. (Mt. 28:19) Na kama ni wewe njo ulikuwa unajifunza naye Biblia, unasikiaka furaha sana wakati unaona namna anabatizwa! (1 Te. 2:19, 20) Wanafunzi wa mupya wenye wametoka tu kubatizwa, ni “barua za pendekezo,” haiko tu kwa wale wenye walijifunza nao Biblia, lakini kwa kutaniko lote.​—Soma 2 Wakorinto 3:1-3.

2. (a) Tunapaswa kufikiria ulizo gani la maana na juu ya nini? (b) Funzo la Biblia ni nini? (Ona maelezo ya chini.)

2 Inafurahisha kujua kama mu miaka ine yenye ilipita, Mashahidi wa Yehova wa mu dunia yote waliongoza mafunzo ya Biblia * 10 000 000 hivi kila mwezi. Na mu ile miaka, watu zaidi ya 280 000 walikuwa wanabatizwa kila mwaka. Tunaweza kufanya nini ili kusaidia watu wengi zaidi wenye kujifunza Biblia wafikie kubatizwa? Yehova angali anavumilia watu na kuwaachia wakati wa kujifunza Biblia ili wafikie kuwa wanafunzi wa Kristo. Kwa hiyo, tunapaswa kufanya yote yenye tunaweza ili kuwasaidia wafikie kubatizwa haraka kadiri inawezekana. Wakati wenye unabakia ni wa kidogo sana!​—1 Ko. 7:29a; 1 Pe. 4:7.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Kwa sababu kazi ya kufanya wanafunzi ni ya maana sana leo, Baraza Lenye Kuongoza liliuliza biro mbalimbali za tawi mambo yenye wahubiri wanapaswa kufanya ili kusaidia wanafunzi wa Biblia wafanye maendeleo na wafikie kubatizwa. Mu hii habari na mu habari yenye kufuata tutaona mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia uzoefu wa mapainia, wamisionere, na waangalizi wa muzunguko. * (Mez. 11:14; 15:22) Walionyesha mambo yenye walimu na wanafunzi wa Biblia wanapaswa kufanya ili funzo likuwe na matokeo ya muzuri. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo tano yenye kila mwanafunzi wa Biblia anapaswa kufanya ili afikie kubatizwa.

MUKUWE MUNAJIFUNZA KILA JUMA

Umuulize mwanafunzi wako ikiwa kuko fasi kwenye munaweza kuwa munakaa ili kujifunza (Ona fungu la 4-6)

4. Kuongoza mafunzo ya Biblia kwa dakika kidogo tu kuko na tatizo gani?

4 Ndugu na dada wengi wako wanaongoza mafunzo ya Biblia kwa dakika kidogo tu. Wakati fulani wanafanyaka vile ku mulango wa musikilizaji na pengine hawazungumuzake kila juma. Hata kama ile ni njia ya muzuri ya kusaidia mutu apendezwe na Biblia, tunapaswa kumuchochea ili apende zaidi mambo yenye Biblia inafundisha. Kwa hiyo, wahubiri fulani wanazoea kuomba namba ya telefone ya mutu mwenye kupendezwa na mbele siku yao ya kujifunza ifike, wanaweza kumuita ao kumuandikia ujumbe ili kuzungumuzia mawazo fulani ya Biblia. Wanaweza hata kuendelea na ile mazungumuzo kwa miezi fulani. Lakini mwanafunzi hawezi kufanya maendeleo na kufikia kujitoa kwa Yehova na kubatizwa, kama hajikaze sana na kama ile njo tu wakati wenye anatumia ili kujifunza Neno la Mungu.

5. Mu Luka 14:27-33, Yesu alizungumuzia mufano gani wenye unaweza kutusaidia mu kazi yetu ya kufanya wanafunzi?

5 Wakati fulani, Yesu alitumia mufano ili kuonyesha mambo yenye mutu anapaswa kufanya ili kuwa mwanafunzi wake. Alizungumuzia mutu mwenye anapenda kujenga munara na mufalme mwenye anapenda kuenda ku vita. Alisema kama mutu mwenye anapenda kujenga munara, anapaswa ‘kukaa kwanza na kuhesabia garama’ ili kuona kama atamaliza kujenga ule munara. Na mufalme anapaswa ‘kukaa kwanza na kufanya shauri’ ili kuona kama maaskari wake watapata ushindi. (Soma Luka 14:27-33.) Vilevile, Yesu alijua kama mutu mwenye anapenda kuwa mwanafunzi wake, anapaswa kufikiri sana juu ya mambo yenye anapaswa kufanya ili kumufuata. Njo maana tunapaswa kutia moyo wanafunzi wetu wa Biblia wakubali tukuwe tunajifunza nao kila juma. Tunaweza kufanya vile namna gani?

6. Tunaweza kufanya nini ili kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia wafanye maendeleo?

6 Kwanza, ongeza wakati wenye unatumia ili kujifunza na mwanafunzi wako. Pengine kuliko kuzungumuzia andiko moja tu, munaweza kuzungumuzia maandiko mbili kila wakati unamutembelea. Saa mwanafunzi wako atazoea, umuulize ikiwa munaweza kuongeza wakati wenye muko munatumia ili kujifunza. Kama ulikuwa unaongoza funzo la Biblia kwenye mulango, umuulize ikiwa munaweza kukaa fasi fulani ili kujifunza. Jibu la mwanafunzi wako litaonyesha kama anaona funzo la Biblia kuwa la maana ao hapana. Ku mwisho, ili kumusaidia afanye maendeleo haraka, unaweza kumuuliza ikiwa atapenda mukuwe munajifunza mara mbili mu juma. Lakini zaidi ya kujifunza mara moja ao mara mbili kila juma, kuko mambo ingine yenye anapaswa kufanya.

ANAPASWA KUJITAYARISHA KWA AJILI YA KILA FUNZO

Ujitayarishe muzuri mbele ujifunze na mwanafunzi wako na umuonyeshe namna ya kujitayarisha (Ona fungu la 7-9)

7. Namna gani mwalimu anaweza kujitayarisha muzuri kila mara mbele aende kuongoza funzo?

7 Kwa sababu uko mwalimu, unapaswa kujitayarisha muzuri kila mara mbele ya kuenda kujifunza na mwanafunzi. Unaweza kuanza kwa kusoma habari yote na kusoma maandiko yenye kuwa mu ile habari. Ujikaze kuelewa muzuri mawazo makubwa. Fikiria kichwa cha habari, vichwa vidogo-vidogo, maulizo ya funzo, maandiko yenye kuwa na neno “soma,” picha, na video yoyote yenye inaweza kusaidia kuelewa ile habari. Kisha ufikirie hali ya mwanafunzi wako, na uone namna unaweza kumufasiria ile habari mu njia yenye kuwa mwepesi na yenye kuwa wazi. Kama unafanya vile, ile itamusaidia asikuwe na magumu ya kuelewa ile habari na akuwe tayari kutumikisha mambo yenye anajifunza.​—Ne. 8:8; Mez. 15:28a.

8. Maneno ya mutume Paulo yenye kuwa mu Wakolosai 1:9, 10, inatufundisha nini kuhusu kusali kwa ajili ya wanafunzi wetu?

8 Wakati uko unatayarisha, usali kwa ajili ya mwanafunzi wako. Umuombe Yehova akusaidie utumie Biblia mu njia yenye itagusa moyo wa mwanafunzi wako. (Soma Wakolosai 1:9, 10.) Ujikaze kufikiria mbele ya wakati mambo yenye mwanafunzi wako anaweza kuwa na magumu ya kuelewa ao kuamini. Ukumbuke kama kusudi lako ni kumusaidia afanye maendeleo ili afikie kubatizwa.

9. Unaweza kufanya nini ili kusaidia mwanafunzi akuwe anajitayarisha kwa ajili ya funzo? Fasiria.

9 Tunatumaini kama ikiwa unazoea kujifunza na mwanafunzi wako kwa ukawaida, atakuwa mwenye shukrani kwa ajili ya mambo yenye Yehova na Yesu wamefanya, na atapenda kujua mambo mingi zaidi. (Mt. 5:3, 6) Ili mwanafunzi apate faida kabisa wakati iko anajifunza, anapaswa kukaza akili juu ya mambo yenye iko anajifunza. Ili afikie kufanya vile, umusaidie aelewe kama ni jambo la maana ajitayarishe kila mara mbele mujifunze, ni kusema, anapaswa kusoma habari yote mbele ya wakati na kufikiria namna anaweza kuitumikisha mu maisha yake. Namna gani mwalimu anaweza kumusaidia? Mwalimu anaweza kutayarisha sehemu fulani ya funzo pamoja na mwanafunzi ili kumuonyesha namna ya kufanya vile. * Umufasirie namna anaweza kupata majibu ya maulizo ya funzo na kama anapaswa kutia alama maneno ao misemwa yenye kuwa na mawazo makubwa, juu ile njo itamusaidia akumbuke majibu. Kisha, umuombe akuwe anatoa majibu mu maneno yake mwenyewe. Kama anazoea kufanya vile, itakuwa mwepesi kwako kujua ikiwa iko anaelewa mambo yenye muko munajifunza. Lakini unapaswa kutia mwanafunzi wako moyo afanye jambo lingine.

UMUSAIDIE AJUE NAMNA YA KUZUNGUMUZA NA YEHOVA KILA SIKU

Usaidie mwanafunzi wako ajue namna ya kuzungumuza na Yehova (Ona fungu la 10-11)

10. Juu ya nini ni jambo la maana kusoma Biblia kila siku, na mutu anapaswa kufanya nini ili mambo yenye iko anasoma imuletee faida kabisa?

10 Zaidi ya kujifunza Biblia kila juma, mwanafunzi atapata faida kama anazoea kufanya mambo fulani yeye mwenyewe kila siku. Anapaswa kuzungumuza na Yehova. Anaweza kufanya vile namna gani? Kwa kumusikiliza na kuongea naye. Anaweza kumusikiliza Yehova kwa kusoma Biblia kila siku. (Yos. 1:8; Zb. 1:1-3) Umuonyeshe namna ya kutumia “Programu ya Usomaji wa Biblia” yenye kuwa ku jw.org. * Lakini ili mambo yenye iko anasoma imuletee faida kabisa, umutie moyo akuwe anafikiri sana juu ya mambo yenye Biblia inafundisha kuhusu Yehova na juu ya namna anaweza kutumikisha mu maisha yake mambo yenye iko anajifunza.​—Mdo. 17:11; Yak. 1:25.

11. Nini njo inaweza kumusaidia mwanafunzi ajue muzuri namna ya kusali, na juu ya nini ni jambo la maana akuwe anasali kwa Yehova kwa ukawaida?

11 Utie moyo mwanafunzi wako akuwe anaongea na Yehova kwa kusali kila siku. Utoe sala zenye kutoka ku moyo ku mwanzo na ku mwisho wa kila funzo, na utaje mwanafunzi wako mu zile sala. Wakati atakuwa anasikiliza sala zako, atajifunza namna ya kuambia Yehova mambo yenye kuwa mu moyo wake na atajifunza kufanya vile kupitia jina la Yesu Kristo. (Mt. 6:9; Yoh. 15:16) Kwa kweli, kusoma Biblia kila siku, ni kusema, kumusikiliza Yehova, na kusali, ni kusema, kuongea na Yehova, kutasaidia mwanafunzi wako amukaribie Yehova zaidi! (Yak. 4:8) Kama mwanafunzi wako anafanya vile kila siku, ile itamusaidia afanye maendeleo ili afikie kujitoa kwa Yehova na kubatizwa. Nini ingine inaweza kumusaidia?

UMUSAIDIE AKUWE NA URAFIKI WA KARIBU PAMOJA NA YEHOVA

12. Namna gani mwalimu anaweza kumusaidia mwanafunzi wake akuwe na urafiki wa karibu pamoja na Yehova?

12 Mambo yenye mwanafunzi iko anajifunza mu Biblia haipaswe tu kubakia mu akili yake, lakini inapaswa kugusa moyo wake. Juu ya nini? Juu mu moyo njo munatokaka tamaa zetu na hisia zetu. Na moyo wetu njo unaweza kutuchochea tutumikishe mambo yenye tuko tunajifunza. Yesu alijua kufundisha, na watu walikuwa wanaelewa mafundisho yake. Hata vile, watu hawakumufuata juu tu walielewa mafundisho yake, lakini walimufuata kwa sababu mafundisho yake iligusa mioyo yao. (Lu. 24:15, 27, 32) Mwanafunzi wako anapaswa kumuona Yehova kuwa Mutu wa kweli kabisa; Mutu mwenye anaweza kufanya naye urafiki. Anapaswa kumuona kuwa Baba yake, Mungu wake, na Rafiki yake. (Zb. 25:4, 5) Wakati muko munajifunza, umusaidie aone sifa za Mungu. (Kut. 34:5, 6; 1 Pe. 5:6, 7) Mu kila habari yenye muko munazungumuzia, umusaidie aelewe Yehova ni Mutu wa namna gani. Umusaidie aone kama Yehova ni Mungu mwenye upendo, mwenye fazili, na mwenye huruma. Yesu alisema kama “amri kubwa zaidi na ya kwanza” ni “kumupenda Yehova Mungu wako.” (Mt. 22:37, 38) Umusaidie mwanafunzi wako amupende kabisa Yehova.

13. Mwalimu anaweza kufanya nini ili asaidie mwanafunzi ajifunze juu ya sifa za Yehova?

13 Wakati uko unazungumuza na mwanafunzi wako, umufasirie namna unapendaka kabisa Yehova. Ile itasaidia mwanafunzi wako aone kama yeye pia anapaswa kufanya urafiki pamoja na Yehova na kumupenda sana. (Zb. 73:28) Kwa mufano, kama mu kichapo cha funzo ao mu andiko fulani muko jambo lenye linagusaka sana moyo wako kuhusu upendo wa Yehova, hekima yake, haki yake, ao nguvu yake, umuelezee mwanafunzi wako juu ya jambo hilo. Na kisha umuambie kama ile ni kati ya mambo yenye inafanya umupende sana Baba yetu wa mbinguni. Kuko jambo lingine lenye mwanafunzi wa Biblia anapaswa kufanya ili afanye maendeleo na afikie kubatizwa.

UMUTIE MOYO AKUWE ANAHUZURIA MIKUTANO

Usaidie mwanafunzi wako asikawie kuanza kuhuzuria mikutano! (Ona fungu la 14-15)

14. Kulingana na Waebrania 10:24, 25, nini njo inaweza kusaidia mwanafunzi afanye maendeleo haraka?

14 Sisi wote tunapenda wanafunzi wetu wa Biblia wafanye maendeleo na kufikia kubatizwa. Kwa hiyo, tunaweza kuwatia moyo waanze kuhuzuria mikutano. Walimu wenye ufundi wanasema kama wanafunzi wenye wanahuzuriaka mikutano wakati tu wanaanza kujifunza, wanafanyaka maendeleo haraka sana. (Zb. 111:1) Walimu fulani wanaambia wanafunzi wao kama zaidi ya funzo lao la Biblia, watajifunza mambo mingi zaidi kuhusu Biblia wakati wanahuzuria mikutano. Soma Waebrania 10:24, 25 pamoja na mwanafunzi wako, na umuambie faida zenye atapata kama anahuzuria mikutano. Umuonyeshe video Kwa Kawaida Tunafanya Nini Kwenye Jumba la Ufalme? * Saidia mwanafunzi wako asikuwe anakosa hata mukutano moja.

15. Tunapaswa kufanya nini ili kutia moyo mwanafunzi wa Biblia ahuzurie mikutano kwa ukawaida?

15 Unaweza kufanya nini kama mwanafunzi wako hajahuzuriaka mukutano ao hahuzuriake mikutano kwa ukawaida? Kwa uchangamufu, umuambie jambo fulani lenye ulifurahia ku mukutano wenye umepita. Wakati anaona namna unafurahia mikutano, ile inaweza kumuchochea akuwe na hamu ya kuhuzuria. Umupatie Buku la Mukutano ao Munara wa Mulinzi na umuonyeshe mambo yenye mutazungumuzia ku mukutano wenye kufuata, kisha umuulize ni sehemu gani yenye anafurahia zaidi. Mambo yenye mwanafunzi wako atasikia na kuona wakati atahuzuria mukutano kwa mara ya kwanza, inapita mambo yote yenye alishakaona ao kusikia mu dini zingine. (1 Ko. 14:24, 25) Anaweza kuiga mifano ya watu wenye atakutana nao ku mikutano, na wanaweza kumusaidia ili afanye maendeleo na afikie kubatizwa.

16. Tunapaswa kufanya nini ili kusaidia wanafunzi wa Biblia wafanye maendeleo na kufikia kubatizwa, na tutajifunza nini mu habari yenye kufuata?

16 Tunapaswa kufanya nini ili kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia wafanye maendeleo na kufikia kubatizwa? Tunapaswa kusaidia kila mwanafunzi wa Biblia aone funzo la Biblia kuwa jambo la maana, kwa kumutia moyo akuwe anajifunza kila juma na akuwe anatayarisha mbele ya wakati. Pia, tunapaswa kumutia moyo akuwe anazungumuza na Yehova kila siku na akuwe na urafiki wa karibu pamoja naye. Tena, tunapaswa kumutia moyo akuwe anahuzuria mikutano. (Ku ukurasa wa 12, ona kisanduku “ Mambo Yenye Wanafunzi wa Biblia Wanapaswa Kufanya ili Wafikie Kubatizwa.”) Lakini, kuko mambo ingine tano yenye walimu wa Biblia wanapaswa kufanya ili wasaidie wanafunzi wao wafikie kubatizwa. Tutaona ile mambo mu habari yenye kufuata.

WIMBO 76 Unahisije?

^ fu. 5 Kufundisha mutu maana yake kumusaidia afikiri na atende mu njia ya mupya. Andiko letu la mwaka wa 2020, Matayo 28:19, lilitukumbusha kama ni jambo la maana kujifunza na watu Biblia ili wafikie kubatizwa na kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo. Mu hii habari na mu habari yenye kufuata, tutaona mambo yenye inaweza kutusaidia ili tufanye muzuri zaidi ile kazi ya kufundisha.

^ fu. 2 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Kama unajifunzaka na mutu kwa ukawaida ili kumusaidia aelewe mafundisho ya musingi ya Biblia, uko unaongoza funzo la Biblia. Unaweza kuripoti funzo kama ulishazungumuza na ule mutu mara mbili kisha kumuonyesha namna tunajifunzaka na watu Biblia, na ikiwa unaona kama ataendelea kujifunza.

^ fu. 3 Hizi habari mbili ziko pia na mawazo fulani yenye ilizungumuziwa mu habari zenye kichwa “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo,” zenye zilitolewa mu Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 7, 2004 mupaka Mwezi wa 5, 2005.

^ fu. 9 Ku jw.org, angalia video ya dakika ine yenye kichwa Tuonyeshe Wanafunzi Wetu Namna ya Kujitayarisha. Fungua sehemu MAKTABA > VIDEO > MIKUTANO NA KAZI YETU YA MAHUBIRI > TUKOMALISHE UFUNDI WETU.

^ fu. 10 Fungua sehemu MAKTABA > VITABU NA BROSHUA.

^ fu. 14 Ku jw.org, fungua sehemu MAFUNDISHO YA BIBLIA > VYOMBO VYA KUSAIDIA KUJIFUNZA BIBLIA > UJIFUNZE KWENYE MIKUTANO YETU YA WATU WOTE.