Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 42

Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Pili

Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Pili

“Endelea kuwa muangalifu juu yako mwenyewe na kuhusu kufundisha kwako.”​—1 TI. 4:16.

WIMBO 77 Nuru Katika Ulimwengu Wenye Giza

KIFUPI CHA HABARI *

1. Ni nini inatusaidia kujua kama kazi ya kuhubiri ni kazi yenye inasaidia watu waokolewe?

KAZI ya kuhubiri ni kazi yenye inasaidia watu waokolewe! Ni nini inatusaidia kujua vile? Wakati Yesu alipatia wanafunzi wake amri yenye kuwa mu Matayo 28:19, 20, alisema hivi: “Muende, . . . mufanye wanafunzi . . . , na muwabatize.” Juu ya nini ubatizo ni jambo la maana sana? Juu mutu mwenye anapenda kuokolewa anapaswa kubatizwa. Mutu mwenye anapenda kubatizwa, anapaswa kuamini kama Yesu alikufa kwa ajili yetu na kufufuliwa, na kama ni ile tu njo inatuwezesha kuokolewa. Njo maana mutume Petro aliambia Wakristo wenzake hivi: “Ubatizo unawaokoa ninyi sasa . . . kupitia ufufuo wa Yesu Kristo.” (1 Pe. 3:21) Kwa hiyo, wakati mwanafunzi mupya anabatizwa, anaweza sasa kutumaini kama ataokolewa.

2. Kulingana na 2 Timoteo 4:1, 2, sisi walimu wa Biblia, tunapaswa kufanya nini?

2 Ili kufanya wanafunzi, tunapaswa kukomalisha “ufundi wa kufundisha.” (Soma 2 Timoteo 4:1, 2.) Juu ya nini? Juu Yesu alitupatia hii amri: “Muende, . . . mufanye wanafunzi . . . , na muwafundishe.” Mutume Paulo alisema kama ni jambo la maana ‘kuendelea’ kufanya ile kazi, “kwa maana kwa kufanya vile utajiokoa wewe mwenyewe na utaokoa pia wale wenye wanakusikiliza.” Kwa hiyo, Paulo alikuwa na sababu ya muzuri ya kusema hivi: “Endelea kuwa muangalifu . . . kuhusu kufundisha kwako.” (1 Ti. 4:16) Inaomba kufundisha watu ili wakuwe wanafunzi. Njo maana tunapaswa kujikaza sana kukomalisha ufundi wa kufundisha.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Mu dunia muzima tuko tunafundisha watu wengi sana mafundisho ya Biblia. Lakini kama vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, tunapaswa kujua mambo yenye tunaweza kufanya ili kuwasaidia wafikie kubatizwa na wakuwe wanafunzi wa Yesu Kristo. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo ingine tano yenye kila mwalimu anapaswa kufanya ili kusaidia mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo na afikie kubatizwa.

UACHE BIBLIA IFUNDISHE

Uombe mwalimu mwenye uzoefu akusaidie ujue namna unaweza kuacha Biblia ifundishe (Ona fungu la 4-6) *

4. Juu ya nini mwalimu anapaswa kuonyesha sifa ya kujizuia wakati iko anaongoza funzo la Biblia? (Ona maelezo ya chini.)

4 Tunapenda mambo yenye kuwa mu Biblia yenye tunafundishaka watu. Njo maana tunaweza kushawishiwa kusema mingi wakati tuko tunazungumuzia ile mambo. Lakini ikuwe tuko tunaongoza Funzo la Munara wa Mulinzi, Funzo la Biblia la Kutaniko, ao tuko tunajifunza na mutu Biblia, tunapaswa kuepuka kusema mingi. Ili kuacha Biblia ifundishe, mwalimu anapaswa kuonyesha sifa ya kujizuia na kuepuka kufasiria mambo yote yenye anajua kuhusu andiko fulani la Biblia ao habari fulani. * (Yoh. 16:12) Fikiria ujuzi wenye ulikuwa nao wakati ulibatizwa na ujuzi wenye uko nao sasa. Inawezekana kama wakati ulibatizwa ulikuwa unajua tu mafundisho ya musingi. (Ebr. 6:1) Iliomba wakati mingi, juu ukuwe na ujuzi wenye uko nao sasa. Kwa hiyo, wakati uko unajifunza na mwanafunzi mupya usijaribu kumufundisha kwa wakati mumoja mambo yote yenye unajua.

5. (a) Kulingana na 1 Watesalonike 2:13, tunapaswa kusaidia mwanafunzi ajue nini? (b) Tunaweza kufanya nini ili kusaidia mwanafunzi akuwe anatoa mawazo yake juu ya mambo yenye iko anajifunza?

5 Tunapenda mwanafunzi wetu ajue kama mambo yenye iko anajifunza inatoka mu Biblia. (Soma 1 Watesalonike 2:13.) Ni nini itatusaidia kufanya vile? Umutie moyo mwanafunzi atoe mawazo yake kuhusu mambo yenye iko anajifunza. Kuliko kumufasiria maandiko yote ya Biblia, umuombe akufasirie pia maandiko fulani. Umusaidie mwanafunzi aone namna anaweza kutumikisha mafundisho ya Biblia mu maisha yake. Umuulize maulizo yenye itamuchochea aseme mawazo yake kuhusu maandiko yenye anasoma. (Lu. 10:25-28) Kwa mufano, umuulize hivi: “Kulingana na hii andiko unaona kama Yehova iko na sifa gani?” “Namna gani hii mafundisho ya Biblia inaweza kukusaidia?” “Unajisikia namna gani juu ya mambo yenye unatoka kujifunza?” (Mez. 20:5) Ikuwe mwanafunzi wa Biblia anajua mambo mingi ao hapana, jambo la maana ni hili: anapaswa kupenda mambo yenye iko anajifunza, na anapaswa kuwa tayari kuitumikisha.

6. Juu ya nini ni muzuri kuomba muhubiri mwenye uzoefu akusindikize wakati unaenda kujifunza na mwanafunzi wa Biblia?

6 Wakati fulani, unaombaka wahubiri wenye uzoefu wakusindikize wakati unaenda kuongoza funzo la Biblia? Kama unafanyaka vile, uwaombe wakuambie ikiwa uko unaongoza funzo muzuri, ao ikiwa uko unaacha Biblia ifundishe. Unapaswa kuwa munyenyekevu kama unapenda kukomalisha ufundi wako wa kufundisha. (Linganisha na Matendo 18:24-26.) Pia uombe muhubiri mwenye uzoefu akuambie ikiwa anawaza kama mwanafunzi iko anaelewa mambo yenye iko anajifunza. Kama jambo fulani litakuzuia kujifunza na mwanafunzi wako kwa juma moja ao mbili, umuombe ule muhubiri ajifunze naye. Ile itasaidia mwanafunzi aendelee kujifunza kwa ukawaida na aone kama kujifunza ni jambo la maana. Usiwaze kama juu tu ni mwanafunzi wako, mutu mwingine hapaswe kujifunza naye. Ni muzuri uepuke kuwaza vile, juu na wewe unapenda mwanafunzi wako ajifunze mambo mingi, na afanye maendeleo.

UONYESHE KAMA UNAPENDA NA KUAMINI MAMBO YENYE UKO UNAFUNDISHA

Elezea mwanafunzi wako mifano ya ndugu na dada wenye walifanya mabadiliko mu maisha yao ili aone namna anaweza kutumikisha mambo yenye iko anajifunza (Ona fungu la 7-9) *

7. Ni nini itasaidia mwanafunzi wa Biblia afurahie mambo yenye iko anajifunza?

7 Ni jambo la maana mwanafunzi wa Biblia aone kama unapenda na kuamini mafundisho ya Biblia. (1 Te. 1:5) Kama anaona vile, inawezekana yeye pia atafurahia mambo yenye iko anajifunza. Unaweza kumuambia namna kutumikisha mashauri ya Biblia kumekusaidia mu maisha yako. Ile inaweza kumusaidia aone kama mashauri yenye kuwa mu Biblia inaweza kumusaidia yeye pia.

8. Unaweza kufanya nini ingine ili kusaidia mwanafunzi wako, na juu ya nini ni jambo la maana kufanya vile?

8 Wakati muko munajifunza Biblia, umuelezee mwanafunzi wako mifano ya ndugu na dada wenye walipambana na matatizo kama yake, na waliishinda. Mu kutaniko lenu muko ndugu ao dada mwenye mufano wake unaweza kusaidia mwanafunzi wako? Kama ni vile, umuombe akusindikize wakati unaenda kujifunza na ule mwanafunzi. Ao ku jw.org, kwenye sehemu “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu,” * unaweza kupata habari mbalimbali na video zenye zinaweza kusaidia mwanafunzi wako aone kama ni jambo la maana kutumikisha kanuni za Biblia mu maisha yake.

9. Namna gani unaweza kusaidia mwanafunzi wako wa Biblia aambie watu wa familia na marafiki mambo yenye iko anajifunza?

9 Kama mwanafunzi wako wa Biblia alishakaoa ao kuolewa, bibi ao bwana yake iko anajifunza? Kama haiko anajifunza, umuombe ajiunge na ninyi wakati wa funzo. Umutie moyo mwanafunzi wako akuwe anaambia watu wa familia na marafiki wake mambo yenye iko anajifunza. (Yoh. 1:40-45) Ili kufanya vile unaweza kumuuliza hivi: “Namna gani unaweza kufasiria mutu fulani wa familia yako mambo yenye tumejifunza?” ao “Ni andiko gani la Biblia lenye unaweza kutumia ili kusaidia rafiki yako fulani aamini mambo yenye umejifunza?” Kama unafanya vile, utakuwa unazoeza mwanafunzi wako ili afikie kuwa mwalimu. Kisha, wakati atatimiza sifa zenye kuombwa ili kuwa muhubiri, ataanza kuhubiri pamoja na kutaniko. Unaweza kuomba mwanafunzi wako akuambie ikiwa anajua mutu fulani mwenye anaweza kupenda kujifunza Biblia. Kama anajua, bila kukawia umutafute ule mutu na uanzishe naye funzo la Biblia. Umuonyeshe video Tunajifunzaka Biblia na Watu Namna Gani? *

UMUTIE MOYO MWANAFUNZI WAKO AJIKAZE KUWA NA MARAFIKI MU KUTANIKO

Utie moyo mwanafunzi wako akuwe na marafiki mu kutaniko (Ona fungu la 10-11) *

10. Kulingana na 1 Watesalonike 2:7, 8, namna gani mwalimu anaweza kuiga mufano wa Paulo?

10 Walimu wa Biblia wanapaswa kuhangaikia kabisa wanafunzi wao. Wanapaswa kuwaona kuwa ndugu na dada wa kesho. (Soma 1 Watesalonike 2:7, 8.) Haiko mwepesi kwao kuachana na marafiki wao wa zamani na kufanya mabadiliko ili kumutumikia Yehova. Tunapaswa kuwasaidia wapate marafiki wazuri mu kutaniko. Ujikaze ukuwe rafiki ya mwanafunzi wako kwa kupitisha wakati pamoja naye hata kama haiko saa ya kujifunza. Unaweza kumuita ku telefone, kumuandikia ujumbe ao kumutembelea siku yenye haiko siku yenu ya kujifunza. Ile itaonyesha kama unamuhangaikia kabisa.

11. Tunapenda wanafunzi wa Biblia wapate nini mu kutaniko, na juu ya nini?

11 Mezali moja inasemaka kama, “Kijiji chote njo kinakomalishaka mutoto.” Sisi pia tunaweza kusema kama, “Kutaniko lote njo linasaidiaka mwanafunzi wa Biblia afikie kuwa mwanafunzi wa Yesu.” Njo maana walimu wazuri wanasaidia wanafunzi wao wajuane na ndugu na dada mu kutaniko. Wale ndugu na dada wanaweza kusaidia mwanafunzi amukaribie Yehova zaidi. Kama mwanafunzi anapitisha wakati pamoja nao, wanaweza kumusaidia atie nguvu urafiki wake pamoja na Yehova, na wanaweza kumusaidia wakati wa magumu. Tunapenda kila mwanafunzi wa Biblia aone kama iko wa maana mu kutaniko na kama iko mu familia yetu ya kiroho. Na tunapenda afurahie upendo wenye kuwa kati ya ndugu na dada mu familia yetu ya kiroho. Ile itafanya ikuwe mwepesi kwake kuachana na marafiki wenye hawamusaidie amupende Yehova. (Mez. 13:20) Atajua kama ikiwa marafiki wake wa zamani wanamukataa anaweza kupata marafiki wazuri mu tengenezo la Yehova.​—Mk. 10:29, 30; 1 Pe. 4:4.

UKAZIE KAMA NI JAMBO LA MAANA KUJITOA KWA YEHOVA NA KUBATIZWA

Kuko mambo fulani yenye mwanafunzi wa Biblia anapaswa kufanya ili afikie kubatizwa! (Ona fungu la 12-13)

12. Juu ya nini tunapaswa kuambia mwanafunzi wetu kama ni jambo la maana ajitoe kwa Yehova na kubatizwa?

12 Kila mara uambie mwanafunzi wako kama ni jambo la maana ajitoe kwa Yehova na kubatizwa. Kusema kweli, wakati tunajifunza na mutu Biblia, nia yetu ni kumusaidia afikie kubatizwa na akuwe mwanafunzi wa Yesu. Kama ulishajifunza na mwanafunzi wako kwa miezi fulani, na zaidi sana kama alishaanza kukusanyika, anapaswa kuelewa kama nia yetu ni kumusaidia afikie kuwa Shahidi wa Yehova.

13. Mwanafunzi anapaswa kufanya nini ili afikie kubatizwa?

13 Kuko mambo fulani yenye mwanafunzi wa Biblia anapaswa kufanya ili afikie kubatizwa. Anapaswa kwanza kumujua Yehova, kumupenda, na kumuamini. (Yoh. 3:16; 17:3) Kisha anapaswa kuanza kufanya urafiki pamoja na Yehova na pamoja na ndugu na dada mu kutaniko. (Ebr. 10:24, 25; Yak. 4:8) Tena, anapaswa kujikaza kuachana na tabia za mubaya na anapaswa kutubu zambi zake. (Mdo. 3:19) Pia, anapaswa kuanza kuambia wengine mambo yenye anaamini sasa. (2 Ko. 4:13) Anapaswa kujitoa kwa Yehova, na ili kuonyesha kama amefanya vile, anapaswa kubatizwa. (1 Pe. 3:21; 4:2) Na ile inakuwaka siku ya furaha sana! Wakati mwanafunzi iko anajikaza kufanya mambo mbalimbali, usikuwe unakosa kumupongeza na kumutia moyo aendelee kufanya vile.

UCHUNGUZE MAENDELEO YA MWANAFUNZI WAKO MARA KWA MARA

14. Namna gani mwalimu anaweza kuchunguza maendeleo ya mwanafunzi?

14 Tunapaswa kuwa wavumilivu wakati tuko tunasaidia mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo ili afikie kujitoa kwa Yehova na kubatizwa. Lakini pia tunapswa kuchunguza ikiwa anapenda kabisa kumutumikia Yehova. Kwa hiyo, ujiulize hivi: Kuko mambo yenye kuonyesha kama mwanafunzi wangu iko anajikaza kutii amri za Yesu, ao anapenda tu kujifunza mambo yenye Biblia inafundisha?

15. Ni nini inaweza kusaidia mwalimu ajue ikiwa mwanafunzi iko anafanya maendeleo?

15 Uchunguze kwa ukawaida maendeleo yenye mwanafunzi wako iko anafanya. Kwa mufano, iko anaonyesha kama anamupenda Yehova? Iko na kawaida ya kusali kwa Yehova? (Zb. 116:1, 2) Anapendaka kusoma Biblia? (Zb. 119:97) Iko anakusanyika kwa ukawaida? (Zb. 22:22) Amefanya mabadiliko yenye kuonyesha kama iko anatumikisha mambo yenye iko anajifunza? (Zb. 119:112) Ameanza kuambia watu wa familia na marafiki mambo yenye iko anajifunza? (Zb. 9:1) Na zaidi ya yote, anapenda kuwa Shahidi wa Yehova? (Zb. 40:8) Kama mwanafunzi haiko anafanya maendeleo hata kidogo, ujikaze ujue sababu yenye kumuzuia kufanya maendeleo. Kisha uzungumuze naye kwa upole lakini waziwazi. *

16. Ni nini inaweza kukusaidia ujue ikiwa unapaswa kuacha kujifunza Biblia na mutu fulani?

16 Mara kwa mara uchunguze ikiwa unaweza kuendelea kujifunza na mwanafunzi wako. Ujiulize hivi: ‘Mwanafunzi wangu anatayarishaka funzo? Anapendaka kukusanyika? Alishaachana na tabia za mubaya? Alishatoka mu dini ya uongo?’ Kama jibu ni hapana, kuendelea kujifunza naye ni sawa vile kufundisha mutu kuogelea, lakini ule mutu hapendake kulowana. Kama mwanafunzi hafurahie kabisa mambo yenye iko anajifunza, na hapendi kufanya mabadiliko, unawaza kama ni muzuri kuendelea kujifunza naye?

17. Kulingana na 1 Timoteo 4:16, walimu wa Biblia wanapaswa kufanya nini?

17 Tunaona kazi yetu ya kufanya wanafunzi kuwa ya maana sana. Na tunapenda kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia wafanye maendeleo na kufikia kubatizwa. Njo maana ni muzuri tuache Biblia ifundishe na tuonyeshe kama tunapenda na kuamini mambo yenye tunafundisha. Pia, tunapaswa kutia moyo mwanafunzi akuwe na marafiki mu kutaniko. Tena, tunapaswa kukazia kama ni jambo la maana kujitoa kwa Yehova na kubatizwa. Na tunapaswa kuchunguza mara kwa mara ikiwa mwanafunzi iko anafanya maendeleo. (Ku ukurasa wa 13, ona kisanduku “ Mambo Yenye Mwalimu Anapaswa Kufanya ili Kusaidia Mwanafunzi Afikie Kubatizwa.”) Tunafurahi sana juu tuko na pendeleo la kufanya hii kazi yenye inasaidia watu waokolewe. Tujikaze basi kufanya yote yenye tunaweza ili kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia wafanye maendeleo na wafikie kubatizwa.

WIMBO 79 Wafundishe Kusimama Imara

^ fu. 5 Wakati tunaongoza mafunzo ya Biblia, tuko na pendeleo la kusaidia watu wajue namna Yehova anapenda wafikiri na kutenda. Mu hii habari tutazungumuzia mambo ingine yenye inaweza kutusaidia tukomalishe ufundi wetu wa kufundisha.

^ fu. 4 Ona habari yenye kichwa “Epuka Mitego Hii Wakati Unaongoza Funzo la Biblia” yenye ilitolewa mu Buku la Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo ya Mwezi wa 9, 2016.

^ fu. 8 Fungua sehemu HABARI JUU YETU > USHUHUDA WA MASHAHIDI WA YEHOVA.

^ fu. 9 Ku jw.org fungua sehemu MAKTABA > VIDEO > MIKUTANO NA KAZI YETU YA MAHUBIRI > VYOMBO KWA AJILI YA MAHUBIRI.

^ fu. 15 Ona habari yenye kichwa “Kumupenda Yehova na Kuwa Mwenye Shukrani Kutakuchochea Ubatizwe” na habari yenye kichwa “Uko Tayari Kubatizwa?” zenye zilitolewa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 3, 2020.

^ fu. 77 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati fulani kisha dada mumoja kuongoza funzo, dada mwenye uzoefu anamusaidia ajue namna ya kuepuka kusema mingi wakati iko anaongoza funzo.

^ fu. 79 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati wa funzo, mwanafunzi anajifunza namna ya kuwa bibi muzuri. Kisha anamuambia bwana yake mambo yenye alijifunza.

^ fu. 81 MAFASIRIO YA PICHA: Ule mwanafunzi na bwana yake wako ku nyumba ya ndugu na dada fulani wenye ule mwanafunzi alikutana nao ku Jumba la Ufalme.